Check out the new design

কুরআনুল কারীমের অর্থসমূহের অনুবাদ - সোয়াহিলি ভাষায় অনুবাদ- আব্দুল্লাহ মুহাম্মদ ও নাসির খামীস * - অনুবাদসমূহের সূচী


অর্থসমূহের অনুবাদ সূরা: আয-যুখরুফ   আয়াত:

Az-Zukhruf

حمٓ
“Hā, Mīm” maelezo yametangulia mwanzoni mwa sura ya Al-Baqarah juu ya herufi zilizokatwa na kutengwa.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ
Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Ameapa kwa Qur’ani ambayo matamshi yake na maana yake yako waziwazi.
আরবি তাফসীরসমূহ:
إِنَّا جَعَلۡنَٰهُ قُرۡءَٰنًا عَرَبِيّٗا لَّعَلَّكُمۡ تَعۡقِلُونَ
Hakika sisi tumeiteremsha Qur’ani kwa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kwa lugha ya Kiarabu , huenda nyinyi mkaelewa na mkazingatia maana yake na hoja zake.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَإِنَّهُۥ فِيٓ أُمِّ ٱلۡكِتَٰبِ لَدَيۡنَا لَعَلِيٌّ حَكِيمٌ
Nayo , kwa hakika, katika Ubao Uliohifadhiwa kwetu sisi ina cheo na heshima za juu, iko thabiti, haina tafauti ndani yake wala kugongana.
আরবি তাফসীরসমূহ:
أَفَنَضۡرِبُ عَنكُمُ ٱلذِّكۡرَ صَفۡحًا أَن كُنتُمۡ قَوۡمٗا مُّسۡرِفِينَ
Je tuwape nyinyi mgongo na tuache kuwateremshia Qur’ani kwa ajili ya kupuuza kwenu, kutofuata na kupita mipaka kwenu katika kukataa kuiamini?
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَكَمۡ أَرۡسَلۡنَا مِن نَّبِيّٖ فِي ٱلۡأَوَّلِينَ
Tumewatumiliza Manabii wengi katika kame za mwanzo zilizopita kabla ya watu wako, ewe Nabii.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَمَا يَأۡتِيهِم مِّن نَّبِيٍّ إِلَّا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ
Hawajiwi na Nabii yoyote isipokuwa huwa wakimcheza shere kama vile watu wako walivyokucheza shere, basi tukawaangamiza wale waliowakanusha Mitume wetu, nao walikuwa ni wenye nguvu kali na ushujaa wa kivita kuliko watu wako, ewe Mtume.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَأَهۡلَكۡنَآ أَشَدَّ مِنۡهُم بَطۡشٗا وَمَضَىٰ مَثَلُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Na yashapita mateso ya wa mwanzo kwa kuangamizwa kwa sababu ya ukanushaji wao, ujeuri wao na kuwacheza shere Mitume wao. Katika haya pana maliwazo kwa Nabii, rehema na amani zimshukie.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَلَئِن سَأَلۡتَهُم مَّنۡ خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ لَيَقُولُنَّ خَلَقَهُنَّ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡعَلِيمُ
Na unapowauliza, ewe Mtume, hawa washirikina miongoni mwa watu wako, «Ni nani aliyeumba mbingu na ardhi? Wanasema , «Aliyeziumba ni Yule Aliye Mshindi katika mamlaka Yake, Aliye Mjuzi wa hizo na vitu vilivyomo ndani yake, hakuna chochote kinachofichamana Kwake.
আরবি তাফসীরসমূহ:
ٱلَّذِي جَعَلَ لَكُمُ ٱلۡأَرۡضَ مَهۡدٗا وَجَعَلَ لَكُمۡ فِيهَا سُبُلٗا لَّعَلَّكُمۡ تَهۡتَدُونَ
Aliyewafanyia ardhi kuwa ni (kama) tandiko na mkeka, Akawasahilishia humo njia za maisha yenu na biashara zenu, ili mjiongoze kwa njia hizo kwenye maslahi yenu ya kidini na ya kidunia.
আরবি তাফসীরসমূহ:
 
অর্থসমূহের অনুবাদ সূরা: আয-যুখরুফ
সূরাসমূহের সূচী পৃষ্ঠার নাম্বার
 
কুরআনুল কারীমের অর্থসমূহের অনুবাদ - সোয়াহিলি ভাষায় অনুবাদ- আব্দুল্লাহ মুহাম্মদ ও নাসির খামীস - অনুবাদসমূহের সূচী

ড. আব্দুল্লাহ মুহাম্মদ আবূ বকর এবং শায়েখ নাসির খামীস অনূদিত।

বন্ধ