Check out the new design

কুরআনুল কারীমের অর্থসমূহের অনুবাদ - সোয়াহিলি ভাষায় অনুবাদ- আলী মুহসিন আল-বারওয়ানী * - অনুবাদসমূহের সূচী

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

অর্থসমূহের অনুবাদ সূরা: আল-মাআরিজ   আয়াত:
يُبَصَّرُونَهُمۡۚ يَوَدُّ ٱلۡمُجۡرِمُ لَوۡ يَفۡتَدِي مِنۡ عَذَابِ يَوۡمِئِذِۭ بِبَنِيهِ
Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe, [11]
[11] Watakuwa wakijuulishana wao kwa wao mpaka wajuane baraabara, na ilhali hapana amuulizae mwenzie kitu. Kafiri atatamani lau ange pata kujikomboa nafsi yake na adhabu hiyo Siku ya Kiyama kwa kumtoa mwanawe awe ni fidia yake,
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَصَٰحِبَتِهِۦ وَأَخِيهِ
Na mkewe, na nduguye, [12]
[12] Au mkewe, au nduguye,
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَفَصِيلَتِهِ ٱلَّتِي تُـٔۡوِيهِ
Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu, [13]
[13] Au jamaa zake aliyo khusiana nao,
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَمَن فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗا ثُمَّ يُنجِيهِ
Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye. [14]
[14] Na wote waliomo duniani, apate kuokoka yeye tu!
আরবি তাফসীরসমূহ:
كَلَّآۖ إِنَّهَا لَظَىٰ
La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa, [15]
[15] Ewe mkosefu! Wacha hayo unayo yatamani ya kutaka kujikomboa kwa fidia! Hakika huo moto, unawaka kweli!
আরবি তাফসীরসমূহ:
نَزَّاعَةٗ لِّلشَّوَىٰ
Unao babua ngozi ya kichwa! [16]
[16] Utakubabua mikono yako, na miguu yako, na viungo vyako vyote,
আরবি তাফসীরসমূহ:
تَدۡعُواْ مَنۡ أَدۡبَرَ وَتَوَلَّىٰ
Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka. [17]
[17] Utanadi kwa jina la huyo aliye iacha Haki, na akaacha ut'iifu,
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَجَمَعَ فَأَوۡعَىٰٓ
Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi. [18]
[18] Na akakusanya mali akayaweka katika mabweta yake, wala hakutoa haki ya Mwenyezi Mungu iliomo katika hayo mali!
আরবি তাফসীরসমূহ:
۞ إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ خُلِقَ هَلُوعًا
Hakika mtu ameumbwa na papara. [19]
[19] Hakika tabia ya binaadamu ni papara, mwingi wa kupapatika,
আরবি তাফসীরসমূহ:
إِذَا مَسَّهُ ٱلشَّرُّ جَزُوعٗا
Inapo mgusa shari hupapatika. [20]
[20] Na kutoridhika akifikiwa na lolote la karaha na uzito,
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَإِذَا مَسَّهُ ٱلۡخَيۡرُ مَنُوعًا
Na inapo mgusa kheri huizuilia. [21]
[21] Na ni mwingi wa kuzuia na kunyima akipata kheri na neema.
আরবি তাফসীরসমূহ:
إِلَّا ٱلۡمُصَلِّينَ
Isipo kuwa wanao swali, [22]
[22] Isipo kuwa wanao swali,
আরবি তাফসীরসমূহ:
ٱلَّذِينَ هُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ دَآئِمُونَ
Ambao wanadumisha Sala zao, [23]
[23] Ambao wanadumisha Swala zao, hawakikosi hata kipindi kimoja.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَٱلَّذِينَ فِيٓ أَمۡوَٰلِهِمۡ حَقّٞ مَّعۡلُومٞ
Na ambao katika mali yao iko haki maalumu [24]
[24] Na wale ambao katika mali yao ipo haki iliyo ainiwa
আরবি তাফসীরসমূহ:
لِّلسَّآئِلِ وَٱلۡمَحۡرُومِ
Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba; [25]
[25] iliyo wekwa kwa ajili ya masikini mwenye kuomba kutaka msaada, na anaye jizuilia kuomba pia. (Katika wanao zuilika kuomba wanaingia si wenye kustahi na kuona vibaya tu, bali pia wasio weza kuomba kama watoto wachanga, wagonjwa, na wanyama pia.)
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَٱلَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ
Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo, [26]
[26] Na wale wanao isadiki Siku ya Malipo, basi wanajitayarisha kwa ajili yake;
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَٱلَّذِينَ هُم مِّنۡ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشۡفِقُونَ
Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi. [27]
[27] Na wale wanao iogopa adhabu ya Mola wao Mlezi basi wanajikinga nayo wala hawajitii katika jambo la kuwaletea adhabu hiyo.
আরবি তাফসীরসমূহ:
إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمۡ غَيۡرُ مَأۡمُونٖ
Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo. [28]
[28] Kwani hakika adhabu ya Mola wao Mlezi hapana hata mmoja anaye weza kuaminika nayo isimpate.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِفُرُوجِهِمۡ حَٰفِظُونَ
Na ambao wanahifadhi tupu zao. [29]
[29] Na ambao wanazihifadhi tupu zao hata hawaemewi na matamanio yao.
আরবি তাফসীরসমূহ:
إِلَّا عَلَىٰٓ أَزۡوَٰجِهِمۡ أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُهُمۡ فَإِنَّهُمۡ غَيۡرُ مَلُومِينَ
Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi [30]
[30] Lakini kwa wake zao na masuria wao hawazihifadhi; kwa sababu hapo hawalaumiwi kuifuata tabia ya maumbile.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَمَنِ ٱبۡتَغَىٰ وَرَآءَ ذَٰلِكَ فَأُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡعَادُونَ
Lakini wanao taka kinyume ya haya, basi hao ndio wanao ruka mipaka. [31]
[31] Basi mwenye kutafuta starehe ya maingiliano kwa wasio kuwa wake na masuria, basi hao tena ni wenye kuikiuka halali na kuingia katika haramu.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِأَمَٰنَٰتِهِمۡ وَعَهۡدِهِمۡ رَٰعُونَ
Na ambao wanazichunga amana zao na ahadi zao, [32]
[32] Na hao wenye kuzihifadhi amana za sharia na amana za waja wa Mwenyezi Mungu, na walio lazimika nayo kwa Mwenyezi Mungu na kwa watu bila ya kukhuni wala kupunja,
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَٱلَّذِينَ هُم بِشَهَٰدَٰتِهِمۡ قَآئِمُونَ
Na ambao wanasimama imara katika ushahidi wao, [33]
[33] Na ambao kwa shahada zao wamesimama sawa sawa kwa haki bila ya kuficha wanalo lijua,
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَٱلَّذِينَ هُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ يُحَافِظُونَ
Na ambao wanazihifadhi Sala zao. [34]
[34] Na wanao hifadhi Swala zao wakizisali sawasawa kwa ukamilifu -
আরবি তাফসীরসমূহ:
أُوْلَٰٓئِكَ فِي جَنَّٰتٖ مُّكۡرَمُونَ
Hao ndio watakao hishimiwa Peponi. [35]
[35] Watu wenye sifa kama hizo nzuri watakuwa ni wenye kuhishimiwa mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu huko Peponi.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَمَالِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ قِبَلَكَ مُهۡطِعِينَ
Wana nini wale walio kufuru wanakutumbulia macho tu? [36]
[36] Kitu gani kinawapelekea hao walio kufuru kukujia mbio mbio ?
আরবি তাফসীরসমূহ:
عَنِ ٱلۡيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ عِزِينَ
Makundi kwa makundi upande wa kulia na upande wa kushoto! [37]
[37] Kutoka kuliani na kushotoni kwa makundi?
আরবি তাফসীরসমূহ:
أَيَطۡمَعُ كُلُّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ أَن يُدۡخَلَ جَنَّةَ نَعِيمٖ
Kwani kila mmoja wao anatumai kuingizwa katika Pepo ya neema? [38]
[38] Je, kwani kila mmoja wao ana tamaa ya kuingia kwenye Pepo yenye neema, baada ya kusikia kuwa Mwenyezi Mungu amemuahidi Mtume wake na Waumini kuwatia Peponi?
আরবি তাফসীরসমূহ:
كَلَّآۖ إِنَّا خَلَقۡنَٰهُم مِّمَّا يَعۡلَمُونَ
La, hasha! Hakika Sisi tumewaumba kutokana na wanacho kijua. [39]
[39] Basi nawaache hiyo tamaa yao ya kuingia Peponi. Hakika Sisi tumewaumba wao kutokana na maji ya kudharauliwa.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَلَآ أُقۡسِمُ بِرَبِّ ٱلۡمَشَٰرِقِ وَٱلۡمَغَٰرِبِ إِنَّا لَقَٰدِرُونَ
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote na magharibi zote kwamba Sisi tunaweza [40]
[40] Naapa kwa Mola Mlezi wa mashariki zote, na magharibi zote za siku, na sayari na hidaya, kwamba hakika bila ya shaka Sisi tuna uweza wa kuwaangamiza,
আরবি তাফসীরসমূহ:
 
অর্থসমূহের অনুবাদ সূরা: আল-মাআরিজ
সূরাসমূহের সূচী পৃষ্ঠার নাম্বার
 
কুরআনুল কারীমের অর্থসমূহের অনুবাদ - সোয়াহিলি ভাষায় অনুবাদ- আলী মুহসিন আল-বারওয়ানী - অনুবাদসমূহের সূচী

‘আলী মুহসিন আল-বারওয়ানী অনূদিত।

বন্ধ