Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Sadržaj prijevodā


Prijevod značenja Sura: Sura el-En'am   Ajet:

Surat Al-An'am

ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَجَعَلَ ٱلظُّلُمَٰتِ وَٱلنُّورَۖ ثُمَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِرَبِّهِمۡ يَعۡدِلُونَ
Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mwenye sifa ambazo zote ni sifa za ukamilifu, Mwenye neema za nje na za ndani, za kidini na za kidunia, Ambaye Aliumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, Aliumba giza na mwangaza kwa kupishana usiku na mchana. Katika hili pana ishara ya utukufu wa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na kuwa Yeye Peke Yake Anastahiki kuabudiwa. Haifai kwa yoyote kumshirikisha mwengine na Yeye. Na pamoja na uwazi huu, makafiri wanamsawazisha mwingine na Mwenyezi Mungu na wanamshirikisha na Yeye.
Tefsiri na arapskom jeziku:
هُوَ ٱلَّذِي خَلَقَكُم مِّن طِينٖ ثُمَّ قَضَىٰٓ أَجَلٗاۖ وَأَجَلٞ مُّسَمًّى عِندَهُۥۖ ثُمَّ أَنتُمۡ تَمۡتَرُونَ
Yeye Ndiye Ambaye Alimuumba baba yenu Ādam kutokana na udongo na nyinyi mnatokana na kizazi chake, kisha Akaandika muda wa kusalia kwenu katika uhai huu wa kilimwengu, na Akaandika muda mwingine maalumu hakuna aujuwao isipokuwa Yeye, Aliyetukuka na kuwa juu, nayo ni Siku ya Kiyama. Kisha nyinyi baada ya haya mnashuku juu ya uwezo wa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, wa kufufua baada ya kufa.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَهُوَ ٱللَّهُ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَفِي ٱلۡأَرۡضِ يَعۡلَمُ سِرَّكُمۡ وَجَهۡرَكُمۡ وَيَعۡلَمُ مَا تَكۡسِبُونَ
Na Mwenyezi Mungu, Aliyetakata na kila sifa ya upungufu, Ndiye Mola Mwenye kuabudiwa kwa haki mbinguni na ardhini. Na miongoni mwa dalili za uungu wake ni kwamba Yeye Anayajua yote mnayoyaficha, enyi watu, na mnayoyadhihirisha na Anayajua matendo yenu yote, mazuri na mabaya. Na kwa ajili hii, Yeye Peke Yake, Aliyetukuka na kuwa juu, Ndiye Mola Anayestahiki kuabudiwa.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَا تَأۡتِيهِم مِّنۡ ءَايَةٖ مِّنۡ ءَايَٰتِ رَبِّهِمۡ إِلَّا كَانُواْ عَنۡهَا مُعۡرِضِينَ
Makafiri hawa Ambao wanamshirikisha mwingine na Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, wamejiwa na hoja zilizo wazi na dalili dhahiri juu upweke wa Mwenyezi Mungu, Aiyetukuka na kuwa juu, na ukweli wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, juu ya utume wake na yale aliyokuja nayo. Lakini punde tu yalipowajia waliyaepuka na kukataa kuyakubali na wasiyaamini.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَقَدۡ كَذَّبُواْ بِٱلۡحَقِّ لَمَّا جَآءَهُمۡ فَسَوۡفَ يَأۡتِيهِمۡ أَنۢبَٰٓؤُاْ مَا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ
Makafiri hawa waliikataa haki ambayo alikuja nayo Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na wakawafanyia shere walinganizi wake kwa sababu ya ujinga walionao kuhusu Mwenyezi Mungu na kughurika kwao na muhula Aliowapa. Basi watakuja kuyaona yale waliyoyafanyia shere kuwa ni haki na ni kweli. Na Mwenyezi Mungu Atawabainishia wakanushaji urongo wao na uzushi wao na awalipe kwa hayo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَلَمۡ يَرَوۡاْ كَمۡ أَهۡلَكۡنَا مِن قَبۡلِهِم مِّن قَرۡنٖ مَّكَّنَّٰهُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ مَا لَمۡ نُمَكِّن لَّكُمۡ وَأَرۡسَلۡنَا ٱلسَّمَآءَ عَلَيۡهِم مِّدۡرَارٗا وَجَعَلۡنَا ٱلۡأَنۡهَٰرَ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهِمۡ فَأَهۡلَكۡنَٰهُم بِذُنُوبِهِمۡ وَأَنشَأۡنَا مِنۢ بَعۡدِهِمۡ قَرۡنًا ءَاخَرِينَ
Kwani hawayajui, hawa wanaoukanusha upweke wa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na kustahiki Kwake, Peke Yake, kuabudiwa na wanaomkanusha Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,, yale yaliyowashukia watu waliokanusha kabla yao ya maangamivu na uharibifu? Hao tuliwapa utulivu kwenye ardhi kwa namna ambayo hatukuwapa nyinyi, enyi makafiri, utulivu kama huo na tuliwaneemesha kwa kuwateremshia mivua na kupita mito chini ya makao yao kwa njia ya kuwanyoshea na kuwapa muhula, wakazikanusha neema za Mwenyezi Mungu na wakawakanusha Mitume. Hapo tuliwaangamiza kwa sababu ya madhambi yao na tukawaumba baada yao watu wengine walioshika nafasi zao katika kuiamirisha ardhi.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَوۡ نَزَّلۡنَا عَلَيۡكَ كِتَٰبٗا فِي قِرۡطَاسٖ فَلَمَسُوهُ بِأَيۡدِيهِمۡ لَقَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ مُّبِينٞ
Na lau tulikuteremshia kitabu kutoka mbinguni, katika kurasa, wakazigusa washirikina hawa kwa mikono yao, wanagalisema, «Uliokuja nao ni uchawi ulio wazi uliobainika».
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَقَالُواْ لَوۡلَآ أُنزِلَ عَلَيۡهِ مَلَكٞۖ وَلَوۡ أَنزَلۡنَا مَلَكٗا لَّقُضِيَ ٱلۡأَمۡرُ ثُمَّ لَا يُنظَرُونَ
Na walisema washirikina hawa, «Si Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Amteremshie Muhammad Malaika kutoka mbinguni ili amsadiki kwa yale aliyokuja nayo Ya utume.» Na lau tulimteremsha Malaika kutoka mbinguni kwa kujibu ombi lao, uamuzi wa kuwaangamiza ungalipitishwa, na wasingepewa muhula wa kutubia, kwani imetangulia kwenye ujuzi wa Mwenyezi Mungu kuwa wao hawataamini.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَوۡ جَعَلۡنَٰهُ مَلَكٗا لَّجَعَلۡنَٰهُ رَجُلٗا وَلَلَبَسۡنَا عَلَيۡهِم مَّا يَلۡبِسُونَ
Na lau kama tulimfanya mtume aliyeteremshwa kwao ni Malaika, kwani hawakukinai na Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, tungalimfanya Malaika huyo kwenye sura za mwanadamu, ili waweze kumsikia na kusema naye. Kwani haimkiniki kwao kumuona Malaika katika sura zake za kimalaika. Na lau Malaika aliwajia kwa sura za mtu, jambo hilo lingaliwafanya wachanganyikiwe kama lilivyowafanya wachanganyikiwe jambo la Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَقَدِ ٱسۡتُهۡزِئَ بِرُسُلٖ مِّن قَبۡلِكَ فَحَاقَ بِٱلَّذِينَ سَخِرُواْ مِنۡهُم مَّا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ
Na kwa kuwa kutaka kwao kuteremshwa Malaika kulikuwa ni kwa njia ya kumfanyia shere Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, Mwenyeyezi Mungu, Aliyetukuka, Aliwaelezea kwamba kuwafanyia shere Mitume, amani iwashukie, si jambo jipya; kwani jambo hilo lilitukia kwa makafiri waliopita kuwafanyia Mitume wao, wakazungukwa na adhabu ambayo walikuwa wakiifanyia shere na wakipinga kuja kwake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ سِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ ثُمَّ ٱنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُكَذِّبِينَ
Sema kuwaambia, ewe Mtume, «Endeni katika ardhi kisha muangalie: namna gani Mwenyezi Mungu aliwaletea maangamivu na hizaya mwishoni? Basi tahadharini yasiwafikie mfano wa maanguko yao, na ogopeni yasije yakawashukia nyinyi kama yale yaliyowashukia wao.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُل لِّمَن مَّا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ قُل لِّلَّهِۚ كَتَبَ عَلَىٰ نَفۡسِهِ ٱلرَّحۡمَةَۚ لَيَجۡمَعَنَّكُمۡ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ لَا رَيۡبَ فِيهِۚ ٱلَّذِينَ خَسِرُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ فَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Ni ya nani mamlaka ya mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake?» Sema, «Ni ya Mwenyezi Mungu. Na kama mnavyolikubali hilo na kulijua, basi muabuduni Yeye Peke Yake. Mwenyezi Mungu Amechukua ahadi juu ya nafsi Yake kurehemu, Hatawaangusiliza waja Wake kwa kuwatesa. Kwa hakika Atawakusanya nyinyi kwenye Siku ya Kiyama ambayo haina shaka ili mhesabiwe na mlipwe. Wale waliomshirikisha Mwenyezi Mungu wamejiangamiza nafsi zao; wao hawampwekeshi Mwenyezi Mungu wala hawaiamini ahadi Yake ya Pepo na Moto na hawaukubali unabii wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,.
Tefsiri na arapskom jeziku:
۞ وَلَهُۥ مَا سَكَنَ فِي ٱلَّيۡلِ وَٱلنَّهَارِۚ وَهُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ
Ni wa Mwenyezi Mungu umiliki wa kila kitu, kilicho mbinguni na ardhini, kilichotulia na kinachotembea, kilichofichika na kilicho wazi. Vyote ni watumwa Wake na viumbe Vyake na viko chini ya utendeshaji nguvu Wake, uendeshaji Wake na upangaji Wake. Yeye Ndiye Msikizi wa maneno ya waja Wake, Ndiye Mjuzi wa siri zao na matendo yao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ أَغَيۡرَ ٱللَّهِ أَتَّخِذُ وَلِيّٗا فَاطِرِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَهُوَ يُطۡعِمُ وَلَا يُطۡعَمُۗ قُلۡ إِنِّيٓ أُمِرۡتُ أَنۡ أَكُونَ أَوَّلَ مَنۡ أَسۡلَمَۖ وَلَا تَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa wanaomshirikisha Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na asiyekuwa Yeye, «Je, nimchukue asiyekuwa Mwenyezi Mungu kuwa ni msaidizi na ni mwokozi, na hali Yeye ni Muumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, na Yeye Ndiye Mwenye kuwaruzuku viumbe Wake na hakuna mwenye kumruzuku Yeye?» Sema,ewe Mtume, «Mimi nimeamrishwa niwe ni wa mwanzo aliyemnyenyekea Yeye na kumwandama katiika umma huu. Na nimekatazwa kuwa ni miongoni mwa wanaomshirikisha Yeye na asiyekuwa Yeye.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ إِنِّيٓ أَخَافُ إِنۡ عَصَيۡتُ رَبِّي عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa wenye kumshirikisha Mwenyezi Mungu na asiyekuwa Yeye, «Mimi naogopa nikimuasi Mola wangu, nikaenda kinyume na maamrisho Yake, na nikamshirikisha Yeye na asiyekuwa Yeye, kuteremkiwa na adhabu kubwa Siku ya Kiyama.
Tefsiri na arapskom jeziku:
مَّن يُصۡرَفۡ عَنۡهُ يَوۡمَئِذٖ فَقَدۡ رَحِمَهُۥۚ وَذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡمُبِينُ
Yule ambaye Mwenyezi Mungu Amemuepushia adhabu kali hiyo, basi Amemrehemu. Kuepushwa huko ndiko kufaulu kuliko wazi kwa kuokolewa na adhabu kubwa.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِن يَمۡسَسۡكَ ٱللَّهُ بِضُرّٖ فَلَا كَاشِفَ لَهُۥٓ إِلَّا هُوَۖ وَإِن يَمۡسَسۡكَ بِخَيۡرٖ فَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ
Na Akikupatia Mwenyezi Mungu jambo la kukudhuru, kama ufukara na ugonjwa, hakuna mwenye kuliondoa hilo isipokuwa Yeye; na Akikupatia zuri, kama utajiri na afya, hakuna mwenye kuondoa wema wake na hakuna mwenye kuzuia mapitisho Yake, kwani Yeye, Aliyetukuka na kuwa juu, ni muweza wa kila kitu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَهُوَ ٱلۡقَاهِرُ فَوۡقَ عِبَادِهِۦۚ وَهُوَ ٱلۡحَكِيمُ ٱلۡخَبِيرُ
Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kila sifa ya upungufu, Ndiye Mwenye kutendesha nguvu, Aliye juu ya waja Wake. Shingo zimemdhalilikia na majabari wamenyongeka Kwake. Yeye Ndiye Mwenye hekima Anayeweka vitu mahali pake kulingana na hekima Yake. Ndiye Mtambuzi Ambaye hakuna kitu chenye kufichika Kwake. Na mwenye kusifika na sifa hizi inapasa asishirikishwe. Katika aya hii pana kuthibitisha sifa ya ujuu kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, kuwa Yuko juu ya ya viumbe vyake vyote; ujuu wa aina zote unaonasibiana na utukufu Wake, kutakasika na kila sifa ya upungufu ni Kwake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ أَيُّ شَيۡءٍ أَكۡبَرُ شَهَٰدَةٗۖ قُلِ ٱللَّهُۖ شَهِيدُۢ بَيۡنِي وَبَيۡنَكُمۡۚ وَأُوحِيَ إِلَيَّ هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانُ لِأُنذِرَكُم بِهِۦ وَمَنۢ بَلَغَۚ أَئِنَّكُمۡ لَتَشۡهَدُونَ أَنَّ مَعَ ٱللَّهِ ءَالِهَةً أُخۡرَىٰۚ قُل لَّآ أَشۡهَدُۚ قُلۡ إِنَّمَا هُوَ إِلَٰهٞ وَٰحِدٞ وَإِنَّنِي بَرِيٓءٞ مِّمَّا تُشۡرِكُونَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Ni kitu gani chenye ushahidi zaidi katika kuthibitisha ukweli wangu katika haya ninayowaambia kwamba mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu?» Sema, «Mwenyezi Mungu ni shahidi baina yangu mimi na nyinyi.» Yaani: yeye Ndiye Mjuzi wa niliyokuja nayo kwenu na yale mtakayonambia. «Na Mwenyezi Mungu Ameniletea mimi Qur’ani hii kwa njia ya wahyi ili ni waonye nayo adhabu ya Mwenyezi Mungu isiwashukie, na niwaonye nayo ummah wengine ambao itawafikia.» Nyinyi mnakubali kwamba, pamoja na Mwenyezi Mungu, pana waabudiwa wengine mnaowashirikisha Naye. Waambie, ewe Mtume, «Mimi sitoi ushahidi juu ya lile mlilolikubali. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mola mmoja Asiye na mshirika. Na mimi nimejiepusha na kila mshirika mnayemuabudu pamoja na Yeye.
Tefsiri na arapskom jeziku:
ٱلَّذِينَ ءَاتَيۡنَٰهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ يَعۡرِفُونَهُۥ كَمَا يَعۡرِفُونَ أَبۡنَآءَهُمُۘ ٱلَّذِينَ خَسِرُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ فَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ
Wale tuliowapa Taurati na Injili wanamjua Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kwa sifa Zake zilizoandikwa kwao kama wanavyowajua watoto wao. Na kama ilivyo wao hawachanganyikiwi kuwajua watoto wao walio mbele yao kuwapambanua na wengine, vilevile Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, hachanganyiki na mwingine, kwa sababu ya uwazi wa sifa zake zilizo ndani ya vitabu vyao. Lakini wao walifuata matamanio yao, walipomkanusha Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na yale aliyokuja nayo, ndipo wakapata hasara nafsi zao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبًا أَوۡ كَذَّبَ بِـَٔايَٰتِهِۦٓۚ إِنَّهُۥ لَا يُفۡلِحُ ٱلظَّٰلِمُونَ
Hakuna yoyote mwenye udhalimu mbaya zaidi kuliko yule aliyemzulia Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, urongo na akadai kwamba Yeye Ana washirika katika ibada, au akadai kwamba Yeye Ana mtoto au mke, au akazikanusha hoja Zake na dalili ambazo kwazo Aliwapa nguvu Mitume Wake, amani iwashukie. Hakika ya mambo ni kwamba madhalimu waliomzulia Mwenyezi Mungu urongo hawafaulu na hawapati matakwa yao ulimwenguni wala Akhera.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَيَوۡمَ نَحۡشُرُهُمۡ جَمِيعٗا ثُمَّ نَقُولُ لِلَّذِينَ أَشۡرَكُوٓاْ أَيۡنَ شُرَكَآؤُكُمُ ٱلَّذِينَ كُنتُمۡ تَزۡعُمُونَ
Na wajihadhari washirikina hawa wenye kuzikanusha aya za Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na Siku ambayo tutawafufua kisha tutasema kuwaambia, «Wako wapi waungu wenu ambao mlikuwa mkidai kuwa wao ni washirika na Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, ili wawaombee nyinyi?»
Tefsiri na arapskom jeziku:
ثُمَّ لَمۡ تَكُن فِتۡنَتُهُمۡ إِلَّآ أَن قَالُواْ وَٱللَّهِ رَبِّنَا مَا كُنَّا مُشۡرِكِينَ
Kisha hayakuwa majibu yao, walipojaribiwa na kupewa mtihani kwa kuulizwa kuhusu washirika wao, isipokuwa walijitoa na wao na wakaapa kwamba wao hawakuwa ni wenye kumshirikisha yoyote na Mwenyezi Mungu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
ٱنظُرۡ كَيۡفَ كَذَبُواْ عَلَىٰٓ أَنفُسِهِمۡۚ وَضَلَّ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ
Fikiri, ewe Mtume, vipi washirikina hawa wanasema urongo juu ya nafsi zao, na wao kesho Akhera watajiepusha na ushirikina! Yatawaondokea wao na kuwapotea yale waliokuwa wakiyadhania ya kuwa waungu wao watawaombea.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمِنۡهُم مَّن يَسۡتَمِعُ إِلَيۡكَۖ وَجَعَلۡنَا عَلَىٰ قُلُوبِهِمۡ أَكِنَّةً أَن يَفۡقَهُوهُ وَفِيٓ ءَاذَانِهِمۡ وَقۡرٗاۚ وَإِن يَرَوۡاْ كُلَّ ءَايَةٖ لَّا يُؤۡمِنُواْ بِهَاۖ حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءُوكَ يُجَٰدِلُونَكَ يَقُولُ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّآ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Kati ya washirikina hawa kuna wanaokusikiliza usomapo Qur’ani, ewe Mtume, na isifike kwenye nyoyo zao. Kwa kuwa wao, kwa sababu ya kufuata matamanio yao, tumeweka vifuniko juu ya nyoyo zao wasipate kuifahamu Qur’ani. Na tumejaalia kwenye masikio yao uzito na uziwi, hayasikii wala hayafahamu chochote. Na wanapoziona dalili nyingi zenye kuonyesha ukweli wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, hawaziamini. Na hata wakikujia , ewe Mtume, baada ya kuzishuhudia dalili zenye kuonesha ukweli wako, huwa wakisema wenye kuzikanusha aya za Mwenyezi Mungu, «Haya tunayoyasikia si chochote isipokuwa ni ngano zinazohadithiwa na watu wa kale zisizo na ukweli.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَهُمۡ يَنۡهَوۡنَ عَنۡهُ وَيَنۡـَٔوۡنَ عَنۡهُۖ وَإِن يُهۡلِكُونَ إِلَّآ أَنفُسَهُمۡ وَمَا يَشۡعُرُونَ
Na washirikina hawa wanawakataza watu kumfuata Mtume Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na kumsikiliza, na wao wenyewe wanajiepusha naye. Na wao hawamuangamizi yoyote, kwa kuzuia kwao njia ya Mwenyezi Mungu isifuatwe, isipokuwa nafsi zao wenyewe, na wao hawatambui kuwa wajishughulisha na mambo ya kuzitia kwenye maangamivu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَوۡ تَرَىٰٓ إِذۡ وُقِفُواْ عَلَى ٱلنَّارِ فَقَالُواْ يَٰلَيۡتَنَا نُرَدُّ وَلَا نُكَذِّبَ بِـَٔايَٰتِ رَبِّنَا وَنَكُونَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Na lau utawaona, ewe Mtume, washirikina hawa Siku ya Kiyama, utaona jambo kubwa, nalo ni wakati wao watakapofungwa juu ya Moto, na watakaposhuhudia yaliyomo humo miongoni mwa minyororo na pingu, na kujionea kwa macho yao mambo makubwa hayo na vituko hivyo. Hapo watasema, «Twatamani turudishwe kwenye maisha ya kilimwengu, tupate kuziamini aya za Mwenyezi Mungu na tuzitumie na tuwe ni miongoni mwa Waumini.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
بَلۡ بَدَا لَهُم مَّا كَانُواْ يُخۡفُونَ مِن قَبۡلُۖ وَلَوۡ رُدُّواْ لَعَادُواْ لِمَا نُهُواْ عَنۡهُ وَإِنَّهُمۡ لَكَٰذِبُونَ
Mambo si kama hivyo! Bali Siku ya Kiyama yatawadhihirikia wao yale waliokuwa wakiyafanya kwa nafsi zao, ya kuamini ukweli wa yale ambayo Mitume walikuja nayo ulimwenguni, ingawa walikuwa wakiwadhihirishia wafuasi wao kinyume chake. Na lau ilikadiriwa warudishwe ulimwenguni na waongezewe muda, wangalirudi kwenye upinzani kwa kukufuru na kukanusha. Na kwa kweli wao ni warongo katika neno lao, «Lau tutarudishwa ulimwenguni hatungalizikanusha aya za Mola wetu na tungalikuwa Waumini.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَقَالُوٓاْ إِنۡ هِيَ إِلَّا حَيَاتُنَا ٱلدُّنۡيَا وَمَا نَحۡنُ بِمَبۡعُوثِينَ
Na hawa washirikina wanaokanusha kufufuliwa wanasema, «Hakuna maisha isipokuwa maisha haya tuliyonayo, na sisi si wenye kufufuliwa baada yakufa kwetu.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَوۡ تَرَىٰٓ إِذۡ وُقِفُواْ عَلَىٰ رَبِّهِمۡۚ قَالَ أَلَيۡسَ هَٰذَا بِٱلۡحَقِّۚ قَالُواْ بَلَىٰ وَرَبِّنَاۚ قَالَ فَذُوقُواْ ٱلۡعَذَابَ بِمَا كُنتُمۡ تَكۡفُرُونَ
Na lau utawaona, ewe Mtume, wenye kukanusha kufufuliwa watakapofungwa mbele ya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, ili uamuzi wa Mwenyezi Mungu upite kuhusu wao Siku ya Kiyama, ungaliona hali mbaya sana, pindi Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, Atakaposema, «Je, ufufuzi huu, mliokuwa mkiukanusha ulimwenguni, si kweli?» Watasema, «Kwani? Tunaapa kwa Mola wetu kuwa huu ni kweli.» Hapo Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Atasema, «Basi onjeni adhabu kwa mlivyokuwa mkikufuru,» yaani, adhabu ambayo mlikuwa mkiikanusha ulimwenguni kwa sababu ya kumkataa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na Mtume Wake Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قَدۡ خَسِرَ ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِلِقَآءِ ٱللَّهِۖ حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءَتۡهُمُ ٱلسَّاعَةُ بَغۡتَةٗ قَالُواْ يَٰحَسۡرَتَنَا عَلَىٰ مَا فَرَّطۡنَا فِيهَا وَهُمۡ يَحۡمِلُونَ أَوۡزَارَهُمۡ عَلَىٰ ظُهُورِهِمۡۚ أَلَا سَآءَ مَا يَزِرُونَ
Hakika wamepata hasara wale waliokanusha kufufuliwa baada ya kufa. Mpaka Kiyama kitakaposimama na wakashutushwa kwa mwisho mbaya, watazipigia nafsi zao kelele za majuto juu ya kile walichokipoteza katika maisha yao ya ulimwenguni, hali ya kwamba wanabeba madhambi yao juu ya migongo yao. Ni mibaya iliyoje mizigo hiyo mizito iliyo miovu ambayo wataibeba!
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَا ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَآ إِلَّا لَعِبٞ وَلَهۡوٞۖ وَلَلدَّارُ ٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لِّلَّذِينَ يَتَّقُونَۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ
Maisha ya kilimwengu hayakuwa, katika wingi wa hali zake, isipokuwa ni udanganyifu na ubatilifu. Na matendo mema, kwa kutengeneza nyumba ya Akhera, ndiyo bora kwa wenye kumcha Mwenyezi Mungu, wakajikinga na adhabu Yake kwa kumtii na kujiepusha na mambo ya kumuasi. Kwani hamuelewi, enyi washirikina mlioghurika na pambo la uhai wa kilimwengu, mukayatanguliza yanayosalia mbele ya yanayomalizika?
Tefsiri na arapskom jeziku:
قَدۡ نَعۡلَمُ إِنَّهُۥ لَيَحۡزُنُكَ ٱلَّذِي يَقُولُونَۖ فَإِنَّهُمۡ لَا يُكَذِّبُونَكَ وَلَٰكِنَّ ٱلظَّٰلِمِينَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ يَجۡحَدُونَ
Hakika sisi tunajua kwamba msimamo wa kaumu zako wa kukukanusha waziwazi unakutia huzuni moyoni mwako. Basi subiri na ujitulize. Kwani wao hawakukanushi wewe kutoka ndani ya roho zao; wao waamini ukweli wako, lakini wao kwa udhalimu na uadui walionao, wanazikataa hoja zilizo wazi zinazoonyesha ukweli wako, ndipo wakakufanya mrongo kwa yale uliyokuja nayo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَقَدۡ كُذِّبَتۡ رُسُلٞ مِّن قَبۡلِكَ فَصَبَرُواْ عَلَىٰ مَا كُذِّبُواْ وَأُوذُواْ حَتَّىٰٓ أَتَىٰهُمۡ نَصۡرُنَاۚ وَلَا مُبَدِّلَ لِكَلِمَٰتِ ٱللَّهِۚ وَلَقَدۡ جَآءَكَ مِن نَّبَإِيْ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Hakika makafiri waliwakanusha Mitume kabla yako Aliyowatuma Mwenyezi Mungu, Aliyotukuka, kwa umma wao. Wao waliudhiwa katika kufuata njia Yake na wakasubiri juu ya hilo na wakaendelea katika ulinganizi wao na bidii yao mpaka ikawajia nusura ya Mwenyezi Mungu. Na hakuna mwenye kuyageuza maneno ya Mwenyezi Mungu, nayo ni yale Aliyoyateremsha kwa Nabii Wake Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, yenye ahadi Yake kwamba Atampa ushindi juu ya wanaomfanyia uadui. Na hakika imekujia wewe, ewe Mtume, habari ya Mitume waliokuwa kabla yako na nusura ya Mwenyezi Mungu iliyohakikishika kwao na mateso ya Mwenyezi Mungu na ghadhabu Zake zilizowafikia wenye kuwakanausha. Basi wewe una kiolezo chema na mfano wa kuiga kutoka kwa Mitume waliotangulia. Katika hili pana kumliwaza Mtume , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِن كَانَ كَبُرَ عَلَيۡكَ إِعۡرَاضُهُمۡ فَإِنِ ٱسۡتَطَعۡتَ أَن تَبۡتَغِيَ نَفَقٗا فِي ٱلۡأَرۡضِ أَوۡ سُلَّمٗا فِي ٱلسَّمَآءِ فَتَأۡتِيَهُم بِـَٔايَةٖۚ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ لَجَمَعَهُمۡ عَلَى ٱلۡهُدَىٰۚ فَلَا تَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡجَٰهِلِينَ
Na iwapo umekuwa ni mzito kwako, ewe Muhammad, upinzani wa hawa washirikina na kujiepusha kwao kukubali ulinganizi wako, basi ukiweza kujifanyia mapito ndani ya ardhi, au ngazi ya kupandia mbinguni ili uwaletee alama na dalili ya usahihi wa maneno yako, zisizokuwa hizi tulizokuletea, fanya hivyo. Na lau Mwenyezi Mungu Alitaka kuwakusanya kwenye uongofu ambao nyinyi munao na kuwaongoza kwenye Imani, Angalifanya hivyo. Lakini Hakulitaka hilo, kwa hekima Anayoijua Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake. Basi, usiwe kabisa ni miongoni mwa wale wajinga ambao huzuni zao zilizidi na wakawa na majonzi mpaka hayo yakawapelekea kwenye babaiko kubwa.
Tefsiri na arapskom jeziku:
۞ إِنَّمَا يَسۡتَجِيبُ ٱلَّذِينَ يَسۡمَعُونَۘ وَٱلۡمَوۡتَىٰ يَبۡعَثُهُمُ ٱللَّهُ ثُمَّ إِلَيۡهِ يُرۡجَعُونَ
Hakika wale wanaokukubali wewe, ewe Mtume, kwa yale unayoyalingania ya uongofu ni wale ambao wanayasikia maneno kwa kuyakubali. Ama makafiri, wao wamo kwenye hesabu ya wafu. Kwani uhai wa kikweli unakuwa kwa Uislamu. Na wafu, Mwenyezi Mungu Atawatoa kutoka kwenye makaburi yao wakiwa hai. Kisha watarudi Kwake Siku ya Kiyama ili watimiziwe hesabu yao na malipo yao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَقَالُواْ لَوۡلَا نُزِّلَ عَلَيۡهِ ءَايَةٞ مِّن رَّبِّهِۦۚ قُلۡ إِنَّ ٱللَّهَ قَادِرٌ عَلَىٰٓ أَن يُنَزِّلَ ءَايَةٗ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ
Na washirikina walisema, kwa ujeuri na kiburi, «Kwa nini Mwenyezi Mungu Hateremshi alama iyoneshayo ukweli wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, miongoni mwa alama za kimiujiza.» Waambie, ewe Mtume, «Mwenyezi Mungu ni muweza wa kuwateremshia miujiza, lakini wengi wao hawajui kwamba kuteremsha miujiza kunakuwa kulingana na hekima Yake, Aliyetukuka.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَا مِن دَآبَّةٖ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَا طَٰٓئِرٖ يَطِيرُ بِجَنَاحَيۡهِ إِلَّآ أُمَمٌ أَمۡثَالُكُمۚ مَّا فَرَّطۡنَا فِي ٱلۡكِتَٰبِ مِن شَيۡءٖۚ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّهِمۡ يُحۡشَرُونَ
Hakuna katika ardhi mnyama yoyote anayetembea chini au ndege anayepaa juu kwa mbawa zake isipokuwa ni aina ya makundi yaliyoumbwa kama nyinyi. Hatukuacha katika Allawh, Almaḥfūd (Ubao Uliohifadhiwa) chochote isiopokuwa tumekithibitisha. Kisha wao, Siku ya Kiyama, watafufuliwa wapelekwe kwa Mola wao, na hapo Mwenyezi Mungu Atamhesabu kila mtu kwa alilolitenda.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا صُمّٞ وَبُكۡمٞ فِي ٱلظُّلُمَٰتِۗ مَن يَشَإِ ٱللَّهُ يُضۡلِلۡهُ وَمَن يَشَأۡ يَجۡعَلۡهُ عَلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ
Na wale waliozikanusha hoja za Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, ni viziwi hawasikii yanayowafaa, ni mabubu hawaitamki haki. Wao wametunduwaa kwenye giza, hawakufuata njia iliyolingana sawa. Yule ambaye Mwenyezi Mungu Anataka kumpoteza Anampoteza na yule Anayetaka kumuongoza Anamfanya awe kwenye njia iliyolingana sawa.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ أَرَءَيۡتَكُمۡ إِنۡ أَتَىٰكُمۡ عَذَابُ ٱللَّهِ أَوۡ أَتَتۡكُمُ ٱلسَّاعَةُ أَغَيۡرَ ٱللَّهِ تَدۡعُونَ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia washirikina, «Nipeni habari, ikiwajia adhabu ya Mwenyezi Mungu ulimwenguni, au ikawajia saa ya nyinyi kufufuliwa, je, mutamuomba hapo asiyekuwa Mwenyezi Mungu awaondolee shida iliyowakumba, iwapo nyinyi ni wakweli kwamba waungu wenu mnaowaabudu badala ya Mwenyezi Mungu wanawanufaisha au kuwadhuru?»
Tefsiri na arapskom jeziku:
بَلۡ إِيَّاهُ تَدۡعُونَ فَيَكۡشِفُ مَا تَدۡعُونَ إِلَيۡهِ إِن شَآءَ وَتَنسَوۡنَ مَا تُشۡرِكُونَ
Bali hapo mtamuomba Mola wenu Aliyewaumba, si mwingine, na mtamtaka Awaokoe na Awaondolee shida kubwa zilizowashukia Akitaka, kwani Yeye Ndiye Muweza wa kila kitu; na wakati huo mtaacha masanamu wenu na wategemewa wenu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَآ إِلَىٰٓ أُمَمٖ مِّن قَبۡلِكَ فَأَخَذۡنَٰهُم بِٱلۡبَأۡسَآءِ وَٱلضَّرَّآءِ لَعَلَّهُمۡ يَتَضَرَّعُونَ
Hakika tuliwatuma, ewe Mtume, Wajumbe kuwaendea makundi ya watu kabla yako kuwalingania kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, wakawakanusha na tukawapa mtihani katika mali yao, kwa ufukara mwingi na dhiki za maisha, na tukawapa mitihani katika miili yao, kwa magonjwa na kuumwa, ili wajidhalilishe kwa Mola wao na wanyenyekee Kwake Peke Yake kwa ibada.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَلَوۡلَآ إِذۡ جَآءَهُم بَأۡسُنَا تَضَرَّعُواْ وَلَٰكِن قَسَتۡ قُلُوبُهُمۡ وَزَيَّنَ لَهُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ مَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Basi si ilipowajia, umma hawa wenye kukanusha, mitihani yetu wajidhalilishe kwetu. Lakini wao nyoyo zao zilisusuwaa na Shetani aliwapambia yale ambayo waliokuwa wakiyafanya ya maasia na wakiyaleta ya ushirikina.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَلَمَّا نَسُواْ مَا ذُكِّرُواْ بِهِۦ فَتَحۡنَا عَلَيۡهِمۡ أَبۡوَٰبَ كُلِّ شَيۡءٍ حَتَّىٰٓ إِذَا فَرِحُواْ بِمَآ أُوتُوٓاْ أَخَذۡنَٰهُم بَغۡتَةٗ فَإِذَا هُم مُّبۡلِسُونَ
Basi walipoacha kufuata amri za Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, kwa kuzipa mgongo, tuliwafungulia milango ya kila kitu miongoni mwa riziki, ndipo tukawabadilishia shida kwa kuwapa raha ya maisha, na tukawabadilishia magonjwa kwa kuwapa uzima wa miili, kwa kuwavuta kidogo kidogo. Hata watakapofanya kiburi na wakajiona kwa mema na neema tulizowapa, tutawashushia adhabu ya ghafla, wakitahamaki watajikuta wamekata tamaa wamekatika na kila zuri.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَقُطِعَ دَابِرُ ٱلۡقَوۡمِ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْۚ وَٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Watu hawa walimalizwa na kuangamizwa walipomkanusha Mwenyezi Mungu na kumkanusha Mtume Wake; hakuna yoyote aliyesalia kati yao. Shukrani na sifa njema ni za Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Muumba na Mwenye kumiliki kila kitu, kwa kuwapa ushindi mawalii Wake na kuwaangamiza maadui Zake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ أَرَءَيۡتُمۡ إِنۡ أَخَذَ ٱللَّهُ سَمۡعَكُمۡ وَأَبۡصَٰرَكُمۡ وَخَتَمَ عَلَىٰ قُلُوبِكُم مَّنۡ إِلَٰهٌ غَيۡرُ ٱللَّهِ يَأۡتِيكُم بِهِۗ ٱنظُرۡ كَيۡفَ نُصَرِّفُ ٱلۡأٓيَٰتِ ثُمَّ هُمۡ يَصۡدِفُونَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia washirikina hawa, «Nambieni ikiwa Mwenyezi Mungu Ameyaondoa masikizi yenu Akawafanya viziwi, Akayaondoa macho yenu Akawafanya vipofu na Akapiga mhuri juu ya nyoyo zenu mkawa hamufahamu neno, basi ni mola gani asiyekuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, awezaye kuwarudishia nyinyi vitu hivyo?» Angalia, ewe Mtume, ni namna gani sisi tunawatolea hoja aina mbalimbali, kisha wao baada yake wanakataa kukumbuka na kuzingatia?
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ أَرَءَيۡتَكُمۡ إِنۡ أَتَىٰكُمۡ عَذَابُ ٱللَّهِ بَغۡتَةً أَوۡ جَهۡرَةً هَلۡ يُهۡلَكُ إِلَّا ٱلۡقَوۡمُ ٱلظَّٰلِمُونَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia washirikina hawa, «Nambieni iwapo mateso ya Mwenyezi Mungu yamewashukia ghafla na hali kwamba nyinyi hamuna hisia nayo, au yakawa waziwazi yanaonekana na nyinyi mnayaangalia: Je, kwani kuna wanaoteswa isipokuwa wale watu madhalimu ambao wamekiuka mpaka kwa kuipeleka ibada kwa asiyekuwa Mwenyezi mungu, Aliyetukuka, na kwa kukanusha kwao Mitume Yake?»
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَا نُرۡسِلُ ٱلۡمُرۡسَلِينَ إِلَّا مُبَشِّرِينَ وَمُنذِرِينَۖ فَمَنۡ ءَامَنَ وَأَصۡلَحَ فَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ
Na hatuwatumi wajumbe wetu isipokuwa wenye kuwapa bishara njema wenye kututii kuwa watakuwa na starehe ya daima, na kuwapa onyo wenye kuasi kuwa watakuwa na adhabu kali. Basi mwenye kuamini, akawasadiki mitume na akafanya mema, hao hawataogopa wakati wa kukutana na Mola wao wala hawatakuwa na masikitiko juu ya chochote walichokikosa miongoni mwa hadhi za kilimwengu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا يَمَسُّهُمُ ٱلۡعَذَابُ بِمَا كَانُواْ يَفۡسُقُونَ
Na wale waliozikanusha aya zetu za Qur’ani na miujiza, hao itawapata adhabu Siku ya Kiyama kwa sababu ya ukafiri wao na kutoka kwao kwenye twaa ya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُل لَّآ أَقُولُ لَكُمۡ عِندِي خَزَآئِنُ ٱللَّهِ وَلَآ أَعۡلَمُ ٱلۡغَيۡبَ وَلَآ أَقُولُ لَكُمۡ إِنِّي مَلَكٌۖ إِنۡ أَتَّبِعُ إِلَّا مَا يُوحَىٰٓ إِلَيَّۚ قُلۡ هَلۡ يَسۡتَوِي ٱلۡأَعۡمَىٰ وَٱلۡبَصِيرُۚ أَفَلَا تَتَفَكَّرُونَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia washirikina hawa, «Mimi sidai kuwa ninamiliki hazina za mbingu na ardhi nikawa ninazitumia nitakavyo; na sidai kuwa mimi najua al-ghayb (yasiyoonekana); na sidai kuwa mimi ni Malaika. Mimi ni Mtume kutoka kwa Mwenyezi Mungu, nafuata yale nliyoteremshiwa kwa njia ya wahyi na nawafikishia watu wahyi Wake.» Waambie, ewe Mtume, washirikina hawa. «Je, kafiri aliye kipofu wa kutoziona aya za Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, asiziamini yuko sawa na Muumini anayeziona aya za Mwenyezi Mungu na akaziamini? Kwani nyinyi hamuzifikirii aya za Mwanye ili muione haki na muiamini?»
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَأَنذِرۡ بِهِ ٱلَّذِينَ يَخَافُونَ أَن يُحۡشَرُوٓاْ إِلَىٰ رَبِّهِمۡ لَيۡسَ لَهُم مِّن دُونِهِۦ وَلِيّٞ وَلَا شَفِيعٞ لَّعَلَّهُمۡ يَتَّقُونَ
Na watishe, ewe Mtume, kwa hii Qur’ani wale ambao wanajua kuwa wao watafufuliwa wapelekwe kwa Mola wao. Wao wanaiyamini ahadi ya Mwenyezi Mungu ya kuwalipa mema wenye kufanya wema na kuwalipa maovu wenye kufanya uovu. Wao hawana, isipokuwa Mwenyezi Mungu, mtegemewa mwenye kuwanusuru wala muombezi mwenye kuwaombea mbele Yake Aliyetukuka Akawaokoa na adhabu Yake. Kwani huenda wao wakamcha Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, kwa kuyafanya maamrisho na kuyaepuka makatazo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَا تَطۡرُدِ ٱلَّذِينَ يَدۡعُونَ رَبَّهُم بِٱلۡغَدَوٰةِ وَٱلۡعَشِيِّ يُرِيدُونَ وَجۡهَهُۥۖ مَا عَلَيۡكَ مِنۡ حِسَابِهِم مِّن شَيۡءٖ وَمَا مِنۡ حِسَابِكَ عَلَيۡهِم مِّن شَيۡءٖ فَتَطۡرُدَهُمۡ فَتَكُونَ مِنَ ٱلظَّٰلِمِينَ
Na usiwatenge, ewe Nabii, kukaa na wewe Waislamu wanyonge wanaomuabudu Mola wao mwanzo wa mchana na mwisho wake, hali wakitaka, kwa matendo yao mema, radhi za Mwenyezi Mungu. Kitu chochote kuhusu hesabu ya maskini hawa hakiko juu yako; hesabu yao iko juu ya Mwenyezi Mungu. Na si juu yao chochote kuhusu hesabu yako. Basi ukiwatenga , utakuwa ni miongoni mwa wenye kuivuka mipaka ya Mwenyezi Mungu, wenye kuweka vitu mahali pasipokuwa pake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَكَذَٰلِكَ فَتَنَّا بَعۡضَهُم بِبَعۡضٖ لِّيَقُولُوٓاْ أَهَٰٓؤُلَآءِ مَنَّ ٱللَّهُ عَلَيۡهِم مِّنۢ بَيۡنِنَآۗ أَلَيۡسَ ٱللَّهُ بِأَعۡلَمَ بِٱلشَّٰكِرِينَ
Na hivyo basi Mwenyezi Mungu Amewapa mtihani waja Wake kwa kutafautiana mafungu yao ya riziki na umbo, Akawafanya baadhi yao matajiri na wengine maskini, baadhi yao wenye nguvu na wengine madhaifu Na Akawafanya baadhi yao ni wahitaji wa wengine ili kuwajaribu kwa hilo, wapate makafiri matajiri kusema, «Ni madhaifu hawa, miongoni mwetu, Mwenyezi Mungu Amewapa neema ya Uislamu?» Kwani Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, si Mjuzi zaidi wa wanaoshukuru neema Yake Akawaafikia kwenye uongofu wa dini Yake?
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِذَا جَآءَكَ ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِـَٔايَٰتِنَا فَقُلۡ سَلَٰمٌ عَلَيۡكُمۡۖ كَتَبَ رَبُّكُمۡ عَلَىٰ نَفۡسِهِ ٱلرَّحۡمَةَ أَنَّهُۥ مَنۡ عَمِلَ مِنكُمۡ سُوٓءَۢا بِجَهَٰلَةٖ ثُمَّ تَابَ مِنۢ بَعۡدِهِۦ وَأَصۡلَحَ فَأَنَّهُۥ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Na wakikujia, ewe Nabii, wale wanaoamini aya za Mwenyezi Mungu zenye kushuhudia ukweli wako juu ya Qur’ani na mengineyo, kutaka fatuwa kuhusu toba ya madhambi yao yaliyotangulia, basi wakirimu kwa kuwarudishia salamu na uwape bishara ya rehema ya Mwenyezi Mungu iliyo kunjufu. Kwani Yeye, Aliyetukuka na kuwa juu, Ametoa ahadi Yake Mwenyewe kuwarehemu waja Wake kwa kuwafanyia wema kwamba mwenye kufanya dhambi kwa kutojua mwisho wake mbaya na kuwa linapelekea kukasirikiwa na Mwenyezi Mungu-Basi kila mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu kwa kukosea au kwa kusudi huwa ni mjinga kwa mtizamo huu, ingawa ajua kuwa ni haramu- kisha baada yake akatubia na akaendelea kufanya matendo mema, basi Mwenyezi Mungu Atamsamehe dhambi lake, kwani Yeye ni Mwingi wa kusamehe kwa waja Wake wenye kutubia, ni Mwingi wa rehema kwao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَكَذَٰلِكَ نُفَصِّلُ ٱلۡأٓيَٰتِ وَلِتَسۡتَبِينَ سَبِيلُ ٱلۡمُجۡرِمِينَ
Na mfano wa ufafanuzi huu tuliokufafanulia, tunakufafanulia, ewe Mtume, hoja zilizo wazi kwa kila mtu, ili ifunuke njia ya watu wa haki wanayoikanusha watu wa batili, na ifunuke njia ya watu wa batili wenye kuwaendea kinyume Mitume.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ إِنِّي نُهِيتُ أَنۡ أَعۡبُدَ ٱلَّذِينَ تَدۡعُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِۚ قُل لَّآ أَتَّبِعُ أَهۡوَآءَكُمۡ قَدۡ ضَلَلۡتُ إِذٗا وَمَآ أَنَا۠ مِنَ ٱلۡمُهۡتَدِينَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Hakika Mwenyezi Mungu, Aliyeshinda na kutukuka, Amenikataza niabudu masanamu ambao mnaowaabudu badala Yake.» Na uwaambie, «Sitafuata matamanio yenu. Nitakuwa nimepotea njia ya sawa nikifuata matamanio yenu na sitakuwa ni miongoni mwa walioongoka.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ إِنِّي عَلَىٰ بَيِّنَةٖ مِّن رَّبِّي وَكَذَّبۡتُم بِهِۦۚ مَا عِندِي مَا تَسۡتَعۡجِلُونَ بِهِۦٓۚ إِنِ ٱلۡحُكۡمُ إِلَّا لِلَّهِۖ يَقُصُّ ٱلۡحَقَّۖ وَهُوَ خَيۡرُ ٱلۡفَٰصِلِينَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Mimi niko kwenye hoja iliyo wazi ya sheria ya Mwenyezi Mungu Aliyoniletea kwa njia ya wahyi. Nayo ni kumpwekesha Mwenyezi Mungu Peke Yake kwa ibada. Na hili mlilikanusha. Na haliko kwenye uwezo wangu jambo la kuwateremshia adhabu mnayoitaka kwa haraka. Na uamuzi wa kuchelewesha hilo uko tu kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka. Yeye Anahadithia ukweli na Yeye Ndiye bora wa kupambanua baina ya haki na batili kwa uamuzi Wake na hukumu Yake.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُل لَّوۡ أَنَّ عِندِي مَا تَسۡتَعۡجِلُونَ بِهِۦ لَقُضِيَ ٱلۡأَمۡرُ بَيۡنِي وَبَيۡنَكُمۡۗ وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِٱلظَّٰلِمِينَ
Sema, ewe Mtume, «Lau mimi nina mamlaka ya kuwateremshia adhabu ambayo mnaitaka kwa haraka, ningaliiteremsha kwenu, na uamuzi, baina yangu mimi na nyinyi, ungalitoka. Lakini hilo liko kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka. Na Yeye Anawajua zaidi madhalimu ambao wamepita mipaka yao wakawashirikisha wengine pamoja na Yeye.
Tefsiri na arapskom jeziku:
۞ وَعِندَهُۥ مَفَاتِحُ ٱلۡغَيۡبِ لَا يَعۡلَمُهَآ إِلَّا هُوَۚ وَيَعۡلَمُ مَا فِي ٱلۡبَرِّ وَٱلۡبَحۡرِۚ وَمَا تَسۡقُطُ مِن وَرَقَةٍ إِلَّا يَعۡلَمُهَا وَلَا حَبَّةٖ فِي ظُلُمَٰتِ ٱلۡأَرۡضِ وَلَا رَطۡبٖ وَلَا يَابِسٍ إِلَّا فِي كِتَٰبٖ مُّبِينٖ
Na kwa Mwenyezi Mungu , Aliyetukuka na kuwa juu, kuna mafātih( al-ghayb, yaani: hazina za mambo ya ghaibu yaliyofichika, hakuna azijuwazo ila Yeye. Miongoni mwazo ni ujuzi wa Kiyama, kuteremka mvua, viliyomo ndani ya zao, matendo ya siku zinazokuja na mahala mtu atakapokufa. Na Anajua kila kilichoko barani na baharini. Na hakuna jani, linaloanguka kutoka kwenye mmea wowote, isipokuwa Yuwalijua. Na kila chembe iliyofichika ardhini na kila kibichi na kikavu, kimethibitishwa kwenye kitabu kilicho wazi kisicho na utatizi nacho ni Al-Lawh(Al-Maḥfūẓ ( Ubao Uliohifadhiwa)
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَهُوَ ٱلَّذِي يَتَوَفَّىٰكُم بِٱلَّيۡلِ وَيَعۡلَمُ مَا جَرَحۡتُم بِٱلنَّهَارِ ثُمَّ يَبۡعَثُكُمۡ فِيهِ لِيُقۡضَىٰٓ أَجَلٞ مُّسَمّٗىۖ ثُمَّ إِلَيۡهِ مَرۡجِعُكُمۡ ثُمَّ يُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Na Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, Ndiye Anayezichukua roho zenu usiku kwa namna inayofanana na vile roho hizo zinachukuliwa kipindi cha kifo, na Anayajua matendo mnayoyafanya mchana, kisha Anazirudisha roho zenu kwenye miili yenu kwa kuamka kutoka usingizini kipindi cha mchana kwa namna inayofanana na kuhuisha baada kufa, ili umalizike muda maalumu uliowekwa wa maisha yenu ulimwenguni. Kisha marejeo yenu ni kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, baada ya kufufuliwa kwenu kutoka kwenye makaburi yenu mkiwa hai. Kisha Atawaelezea yale mliokuwa mkiyafanya kipindi cha maisha yenu ya ulimengu. Kisha Atawalipa kwa hayo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَهُوَ ٱلۡقَاهِرُ فَوۡقَ عِبَادِهِۦۖ وَيُرۡسِلُ عَلَيۡكُمۡ حَفَظَةً حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءَ أَحَدَكُمُ ٱلۡمَوۡتُ تَوَفَّتۡهُ رُسُلُنَا وَهُمۡ لَا يُفَرِّطُونَ
Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Ndiye Al-Qāhir (Mtendesha nguvu), Aliye juu ya waja Wake, ujuu wa kila namana usio na mipaka unaonasibiana na utkufu Wake, kutakata na kila sifa mbaya ni Kwake na kutukuka ni Kwake. Kila kitu kinaunyenyekea utukufu Wake na ukubwa Wake. Yeye Anawatuma kwa waja Wake Malaika kuyadhibiti matendo yao na kuyahesabu. Mpaka kifo kinapomshukia mmoja wao, Malaika wa mauti na wasaidizi wake wanaichukua roho yake, na wao hawaachi kutekeleza walichoamrishwa kukifanya.
Tefsiri na arapskom jeziku:
ثُمَّ رُدُّوٓاْ إِلَى ٱللَّهِ مَوۡلَىٰهُمُ ٱلۡحَقِّۚ أَلَا لَهُ ٱلۡحُكۡمُ وَهُوَ أَسۡرَعُ ٱلۡحَٰسِبِينَ
Kisha hawa waliokufa watarudishwa kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Mola wao wa kweli. Jua utanabahi kwamba hukumu na uamuzi baina ya waja Wake, Siku ya Kiyama, ni Vyake Yeye tu. Na Yeye Ndiye Mwpesi wa wenye kuhesabu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ مَن يُنَجِّيكُم مِّن ظُلُمَٰتِ ٱلۡبَرِّ وَٱلۡبَحۡرِ تَدۡعُونَهُۥ تَضَرُّعٗا وَخُفۡيَةٗ لَّئِنۡ أَنجَىٰنَا مِنۡ هَٰذِهِۦ لَنَكُونَنَّ مِنَ ٱلشَّٰكِرِينَ
Waambie, ewe Mtume, hawa washirikina, «Ni nani mwenye kuwaokoa na vitisho vya magiza ya bara na bahari? Kwani si Mwenyezi Mungu mnayemuomba kwenye matatizo mkionesha unyonge wenu kwa dhahiri na kwa siri? Huwa mkisema, ‘Hakika Mola wetu Akituokoa na vitisho hivi, tutakuwa ni wenye kushukuru kwa kumuabudu, Aliyeshinda na kutukuka, Peke Yake, Asiye na mshirika.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلِ ٱللَّهُ يُنَجِّيكُم مِّنۡهَا وَمِن كُلِّ كَرۡبٖ ثُمَّ أَنتُمۡ تُشۡرِكُونَ
Waambie, ewe Mtume, «Mwenyezi Mungu, Peke Yake, Ndiye Mwenye kuwaokoa na vitisho hivyi na kila tatizo, kisha nyinyi baada ya hapo mnawashirikisha wengine pamoja Naye katika ibada.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ هُوَ ٱلۡقَادِرُ عَلَىٰٓ أَن يَبۡعَثَ عَلَيۡكُمۡ عَذَابٗا مِّن فَوۡقِكُمۡ أَوۡ مِن تَحۡتِ أَرۡجُلِكُمۡ أَوۡ يَلۡبِسَكُمۡ شِيَعٗا وَيُذِيقَ بَعۡضَكُم بَأۡسَ بَعۡضٍۗ ٱنظُرۡ كَيۡفَ نُصَرِّفُ ٱلۡأٓيَٰتِ لَعَلَّهُمۡ يَفۡقَهُونَ
Sema, ewe Mtume, «Mwenyezi Mungu, Aliyeshinda na kutukuka, Ndiye Muweza, Peke Yake, kuwatumia adhabu kutoka juu yenu, kama kupigwa majiwe au mvua ya mafuriko na mfano wake, au kutoka chini ya miguu yenu, kama mitetemeko ya ardhi na kuzama ndani ardhi, au Awavurugie mambo yenu muwe makundi yanayozozana, mnauana nyinyi kwa nyinyi,» Angalia, ewe Mtume, vipi tunazifanya aina mbalimbali hoja zetu zilizo wazi kwa hawa washirikina ili waelewe na wazingatie!
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَكَذَّبَ بِهِۦ قَوۡمُكَ وَهُوَ ٱلۡحَقُّۚ قُل لَّسۡتُ عَلَيۡكُم بِوَكِيلٖ
Na waliikanusha hii Qur’ani makafiri kati ya watu wako, ewe Mtume; nayo ni kitabu chenye ukweli katika kila kilichokuja nacho, Waambie, «Mimi si mlinzi wala mtunzi juuu yenu. Mimi ni mjumbe wa Mwenyezi Mungu, nawafikishia nyinyi yale niliotumwa nayo kwenu,.
Tefsiri na arapskom jeziku:
لِّكُلِّ نَبَإٖ مُّسۡتَقَرّٞۚ وَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَ
Kila habari ina kituo cha kutulia na kikomo cha kukomea, hapo haki na batili zitafunuka. Na mtajua, enyi makafiri, mwisho wa jambo lenu, itakaposhuka adhabu ya Mwenyezi Mungu kwenu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِذَا رَأَيۡتَ ٱلَّذِينَ يَخُوضُونَ فِيٓ ءَايَٰتِنَا فَأَعۡرِضۡ عَنۡهُمۡ حَتَّىٰ يَخُوضُواْ فِي حَدِيثٍ غَيۡرِهِۦۚ وَإِمَّا يُنسِيَنَّكَ ٱلشَّيۡطَٰنُ فَلَا تَقۡعُدۡ بَعۡدَ ٱلذِّكۡرَىٰ مَعَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلظَّٰلِمِينَ
Na uwaonapo, ewe Mtume, washirikina wanaoleta maneno juu ya aya za Qur’ani, kwa urongo na kwa kufanya shere, jiepushe na wao mpaka waingie kwenye maneno mengine. Na iwapo Shetani amekusahaulisha jambo hili, basi baada ya kukumbuka usikae pamoja na watu wenye uadui walioleta maneno ya urongo juu ya aya za Mwenyezi Mungu,
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَا عَلَى ٱلَّذِينَ يَتَّقُونَ مِنۡ حِسَابِهِم مِّن شَيۡءٖ وَلَٰكِن ذِكۡرَىٰ لَعَلَّهُمۡ يَتَّقُونَ
Na wale Waumini wanaomuogopa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, wakatii amri Zake na wakaepuka makatazo Yake, hawana jaukumu lolote juu ya hesabu ya Mwenyezi Mungu kwa wale wenye kuvama kwenye maneno yasiyofaa, wenye kuzifanyia shere aya za Mwenyezi Mungu. Lakini ni juu yao wawaidhie waache kulete maneno hayo ya batili, kwani huenda wao wakamcha Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَذَرِ ٱلَّذِينَ ٱتَّخَذُواْ دِينَهُمۡ لَعِبٗا وَلَهۡوٗا وَغَرَّتۡهُمُ ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَاۚ وَذَكِّرۡ بِهِۦٓ أَن تُبۡسَلَ نَفۡسُۢ بِمَا كَسَبَتۡ لَيۡسَ لَهَا مِن دُونِ ٱللَّهِ وَلِيّٞ وَلَا شَفِيعٞ وَإِن تَعۡدِلۡ كُلَّ عَدۡلٖ لَّا يُؤۡخَذۡ مِنۡهَآۗ أُوْلَٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ أُبۡسِلُواْ بِمَا كَسَبُواْۖ لَهُمۡ شَرَابٞ مِّنۡ حَمِيمٖ وَعَذَابٌ أَلِيمُۢ بِمَا كَانُواْ يَكۡفُرُونَ
Na waache, ewe Mtume, hawa washirikina ambao wameifanya dini ya Uislamu ni mchezo na pumbao, wazifanyia shere aya za Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na yamewaghuri wao maisha ya kilimwengu pamoja na pambo lake. Na wakumbushe, kwa Qur’ani, hawa washirikina na wengineo, ili nafsi isifungike kwa madhambi yake na kumkanusha kwake Mola wake. Haina, isipokuwa Mwenyezi Mungu, mlinzi mwenye kuinusuru akaiokoa na adhabu Yake, wala muombezi mwenye kuiyombea mbele Yake. Na ikitoa ili kujikomboa kiwango kiwacho cha fidia haitakubaliwa kwake. Hao ndio ambao wamefungika na dhambi zao. Watakuwa na kinywaji moto sana na adhabu yenye kuumiza Motoni, kwa sababu ya kumkanusha kwao Mwnyezi Mungu, Aliyetukuka, Mtume Wake, Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na dini ya Uislamu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ أَنَدۡعُواْ مِن دُونِ ٱللَّهِ مَا لَا يَنفَعُنَا وَلَا يَضُرُّنَا وَنُرَدُّ عَلَىٰٓ أَعۡقَابِنَا بَعۡدَ إِذۡ هَدَىٰنَا ٱللَّهُ كَٱلَّذِي ٱسۡتَهۡوَتۡهُ ٱلشَّيَٰطِينُ فِي ٱلۡأَرۡضِ حَيۡرَانَ لَهُۥٓ أَصۡحَٰبٞ يَدۡعُونَهُۥٓ إِلَى ٱلۡهُدَى ٱئۡتِنَاۗ قُلۡ إِنَّ هُدَى ٱللَّهِ هُوَ ٱلۡهُدَىٰۖ وَأُمِرۡنَا لِنُسۡلِمَ لِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Je, tuabudu, asiyekuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, masanamu yasionufaisha wala kudhuru? Je, turudi ukafirini baada ya Mwenyezi Mungu kutuongoza kwenye Uislamu, tukafanana, katika kurudi kwetu ukafirini, na aliyeharibika akili yake kwa kusawazwa na mashetani akapotea njia ardhini na hali yeye ana marafiki wenye akili, wenye Imani, wamwita kwenye njia ya sawa ambayo wao wako akawa anakataa?» Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Uongofu wa Mwenyezi Mungu Aliyenituma mimi ndio uongofu wa haki. Na sote tumeamrishwa tujisalimishe kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Bwana wa vuimbe vyote, kwa kumuabudu, Peke Yake, Asiye na mshirika, kwani Yeye Ndiye Mola na Mmiliki wa kila kitu.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَأَنۡ أَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَٱتَّقُوهُۚ وَهُوَ ٱلَّذِيٓ إِلَيۡهِ تُحۡشَرُونَ
Na hivyohivyo tumeamrishwa tusimamishe Swala kikamilifu, tumuogope Yeye kwa kufanya maamrisho Yake na kuepuka makatazo Yake. Na Yeye, Aliyetukuka na kuwa juu, Ndiye Ambaye Kwake Yeye watakusanywa viumbe wote Siku ya Kiyama.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَهُوَ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ بِٱلۡحَقِّۖ وَيَوۡمَ يَقُولُ كُن فَيَكُونُۚ قَوۡلُهُ ٱلۡحَقُّۚ وَلَهُ ٱلۡمُلۡكُ يَوۡمَ يُنفَخُ فِي ٱلصُّورِۚ عَٰلِمُ ٱلۡغَيۡبِ وَٱلشَّهَٰدَةِۚ وَهُوَ ٱلۡحَكِيمُ ٱلۡخَبِيرُ
Na Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa pungufu ni Kwake, Ndiye Aliyeumba mbingu na ardhi kwa haki. Na taja,ewe Mtume, Atakaposema Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama, «Kuwa» na ikawa kulingana na amri Yake, kama kupepesa macho au muda mfupi zaidi. Neno lake Ndio haki iliokamilika. Na ni Wake ufalme, Peke Yake, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, Siku Malaika atakapovuvia Parapanda, mvuvio wa pili ambao, kwa huo, roho zitarudi kwenye miili. Na Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni kwake, Ndiye Anayeyajua yaliyofichika na hisi zenu, enyi watu, mnayoyaona kwa macho yenu. Yeye Ndiye Mwenye hekima, Anayeweka mambo mahali pake, Mtambuzi wa mambo ya viumbe Vyake. Na Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Ndiye Anayehusika na mambo haya na mengineyo, mwanzo na mwisho, kuanzisha kuumba na ukomo wake. Na Yeye, Peke Yake, Ndiye Ambaye inapasa kwa waja kufuata sheria Yake, kujisalimisha kwa hukumu Yake na kuwa nahamu ya kupata radhi Zake na msamaha Wake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
۞ وَإِذۡ قَالَ إِبۡرَٰهِيمُ لِأَبِيهِ ءَازَرَ أَتَتَّخِذُ أَصۡنَامًا ءَالِهَةً إِنِّيٓ أَرَىٰكَ وَقَوۡمَكَ فِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٖ
Na kumbuka, ewe Mtume, mahujiano ya Ibrāhīm, amani imshukiye, na baba yake Āzar. Ibrāhīm alipomwambia, «Je, unawafanya masanamu ni waungu, unawaabudu badala ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka? Mimi nakuona wewe na watu wako muko kwenye upotevu uliyo wazi, muko kando na njia ya haki.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَكَذَٰلِكَ نُرِيٓ إِبۡرَٰهِيمَ مَلَكُوتَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَلِيَكُونَ مِنَ ٱلۡمُوقِنِينَ
Na kama tulivyomuongoza Ibrāhīm, amani imshukiye, kwenye haki katika jambo la ibada, tunamuonesha ufalme mkubwa unaokusanya mbingu na ardhi na uwezo wenye kushinda, ili awe miongoni mwa wenye kuvama katika Imani.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَلَمَّا جَنَّ عَلَيۡهِ ٱلَّيۡلُ رَءَا كَوۡكَبٗاۖ قَالَ هَٰذَا رَبِّيۖ فَلَمَّآ أَفَلَ قَالَ لَآ أُحِبُّ ٱلۡأٓفِلِينَ
Giza la usiku lilipomuingilia Ibrāhīm, amani imshukiye, na kumfinika, alijadiliana na watu wake ili kuwathibitishia kuwa dini yao ni ya urongo. Na wao walikuwa wakiabudu nyota. Ibrāhīm, amani imshukiye, aliona nyota, akasema, akiwavuta watu wake, ili awathibitishie tawhīd (upweke wa Mwenyezi Mungu) kihoja, «Hii ni mola wangu.» Nyota ilipozama alisema, «Mimi siwapendi waungu wanaozama.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَلَمَّا رَءَا ٱلۡقَمَرَ بَازِغٗا قَالَ هَٰذَا رَبِّيۖ فَلَمَّآ أَفَلَ قَالَ لَئِن لَّمۡ يَهۡدِنِي رَبِّي لَأَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلضَّآلِّينَ
Ibrāhīm alipouona mwezi umechomoza alisema kuwaambia watu wake kwa njia ya kumvuta mtesi, «Huu ni mola wangu.» Ulipozama, alisema, akiwa ahitajia uongofu wa Mola wake, «Asiponiongoza Mola wangu kwenye usawa juu ya kumpwekesha Yeye nitakuwa ni miongoni mwa watu waliopotea njia ya sawa kwa kumuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَلَمَّا رَءَا ٱلشَّمۡسَ بَازِغَةٗ قَالَ هَٰذَا رَبِّي هَٰذَآ أَكۡبَرُۖ فَلَمَّآ أَفَلَتۡ قَالَ يَٰقَوۡمِ إِنِّي بَرِيٓءٞ مِّمَّا تُشۡرِكُونَ
Alipoliona jua limechomoza, alisema kuwaambia watu wake, «Hili ni mola wangu, hili ni kubwa kuliko nyota na mwezi.» Lilipozama, alisema kuwaambia watu wake, «Mimi nimejiepusha na ushirikina mulionao wa kuabudu mizimu, nyota na masanamu mnayoabudu badala ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka.
Tefsiri na arapskom jeziku:
إِنِّي وَجَّهۡتُ وَجۡهِيَ لِلَّذِي فَطَرَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ حَنِيفٗاۖ وَمَآ أَنَا۠ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ
«Mimi nimeelekea kwa uso wangu, katika ibada, kwa Mwenyezi Mungu, Aliyeshinda na kutukuka, Peke Yake, kwani Yeye Ndiye Aliyeumba mbingu na ardhi, nikiwa kando na ushirikina na nikielekea kwenye kumpwekesha Mwenyezi Mungu. Na mimi sikuwa ni miongoni mwa wenye kuwashirikisha wengine pamoja na Mwenyezi Mungu.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَحَآجَّهُۥ قَوۡمُهُۥۚ قَالَ أَتُحَٰٓجُّوٓنِّي فِي ٱللَّهِ وَقَدۡ هَدَىٰنِۚ وَلَآ أَخَافُ مَا تُشۡرِكُونَ بِهِۦٓ إِلَّآ أَن يَشَآءَ رَبِّي شَيۡـٔٗاۚ وَسِعَ رَبِّي كُلَّ شَيۡءٍ عِلۡمًاۚ أَفَلَا تَتَذَكَّرُونَ
Watu wake walimjadili kuhusu kumpwekesha Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, akasema «Mwanijadili juu ya kumpwekesha kwangu Mwenyezi Mungu kwa ibada, na hali Yeye Ameniongoza nikaujua upweke Wake? Na iwapo nyinyi mnanitisha na waungu wenu wasije wakanidhuru, basi mimi siwaogopi na hawatanidhuru isipokuwa Mola wangu Atake jambo. Mola wangu Ameenea kila kitu kwa ujuzi. Basi hamkumbuki mkajua kuwa Yeye, Peke Yake, Ndiye Mstahiki wa kuabudiwa?
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَكَيۡفَ أَخَافُ مَآ أَشۡرَكۡتُمۡ وَلَا تَخَافُونَ أَنَّكُمۡ أَشۡرَكۡتُم بِٱللَّهِ مَا لَمۡ يُنَزِّلۡ بِهِۦ عَلَيۡكُمۡ سُلۡطَٰنٗاۚ فَأَيُّ ٱلۡفَرِيقَيۡنِ أَحَقُّ بِٱلۡأَمۡنِۖ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ
«Na ni vipi nitaogopa masanamu yenu na hali nyinyi hamumuogopi Mola wangu Aliyewaumba na Akayaumba masanamu yenu ambayo mnamshirikisha nayo Mwenyezi Mungu katika ibada, bila ya kuwa na hoja yoyote juu ya hilo? Basi ni lipi kati ya makundi mawili, kundi la washirikina na kundi la wenye kumpwekesha Mwenyezi Mungu, lenye haki zaidi ya utulivu na usalama na kuaminika na adhabu ya Mwenyezi Mungu? Iwapo mnajua ukweli wa ninayoyasema, niambieni.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَلَمۡ يَلۡبِسُوٓاْ إِيمَٰنَهُم بِظُلۡمٍ أُوْلَٰٓئِكَ لَهُمُ ٱلۡأَمۡنُ وَهُم مُّهۡتَدُونَ
Wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakafuata sheria Yake kivitendo, na wasichanganye imani yao na ushirikina, wao ndio wenye utulivu na usalama na wao ndio walioongozwa kwenye njia ya haki.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَتِلۡكَ حُجَّتُنَآ ءَاتَيۡنَٰهَآ إِبۡرَٰهِيمَ عَلَىٰ قَوۡمِهِۦۚ نَرۡفَعُ دَرَجَٰتٖ مَّن نَّشَآءُۗ إِنَّ رَبَّكَ حَكِيمٌ عَلِيمٞ
Hoja hiyo ambayo Ibrāhīm, amani imshukiye, aliwahoji nayo watu wake ndiyo hoja yetu tuliyomuongoza nayo mpaka hoja yao ikakatika. Tunamtukuza daraja tunayemtaka, miongoni mwa waja wetu, ulimwenguni na Akhera, Hakika Mola wako ni Mwenye hekima katika kuendesha mambo ya waja Wake, ni Mjuzi kuhusu wao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَوَهَبۡنَا لَهُۥٓ إِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَۚ كُلًّا هَدَيۡنَاۚ وَنُوحًا هَدَيۡنَا مِن قَبۡلُۖ وَمِن ذُرِّيَّتِهِۦ دَاوُۥدَ وَسُلَيۡمَٰنَ وَأَيُّوبَ وَيُوسُفَ وَمُوسَىٰ وَهَٰرُونَۚ وَكَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Na tulimneemesha Ibrāhīm, amani imshukiye, kwa kumruzuku Is’ḥāq kuwa mtoto wake na Ya‘qūb kuwa mjukuu. Na wote wawili tuliwaongoza kwenye njia ya uongofu. Pia tulimuongoza Nūḥ kwenye haki, kabla ya Ibrāhīm na Isḥāq na Ya’qūb. Na pia tuliwaongoza kwenye haki, kati ya kizazi cha Nūḥ, Dāwūd, Sulaimān, Ayyūb, Yūsuf, Mūsā na Hārūn, amani iwashukie. Na kama tulivyowajazi Manabii hawa kwa wema wao, ndivyo tunavyomjazi kila mwema.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَزَكَرِيَّا وَيَحۡيَىٰ وَعِيسَىٰ وَإِلۡيَاسَۖ كُلّٞ مِّنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Na vilivile tulimuongoza Zakariyyā, Yaḥyā, ‘Īsā na Ilyās. Na Manabii wote hawa, amani iwashukie, ni miongoni mwa watu wema.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِسۡمَٰعِيلَ وَٱلۡيَسَعَ وَيُونُسَ وَلُوطٗاۚ وَكُلّٗا فَضَّلۡنَا عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na tulimuongoza, vilevile, Ismā‘īl, Ilyasa‘ na Lūṭ,. Na Mitume wote hawa tuliwatukuza juu ya watu wa zama zao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمِنۡ ءَابَآئِهِمۡ وَذُرِّيَّٰتِهِمۡ وَإِخۡوَٰنِهِمۡۖ وَٱجۡتَبَيۡنَٰهُمۡ وَهَدَيۡنَٰهُمۡ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ
Na pia tuliwaongoza kwenye haki tuliowataka kuwaongoza kati ya wazazi wa hawa, watoto wao na ndugu zao. Na tuliwateua wao wafuate Dini yetu na wafikishe ujumbe wetu kwa wale tuliowatuma kwao. Na tuliwaonesha njia sahihi, isiyopotoka, nayo ni ile ya kumpwekesha Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na kumwepusha na mambo ya kumshirkisha..
Tefsiri na arapskom jeziku:
ذَٰلِكَ هُدَى ٱللَّهِ يَهۡدِي بِهِۦ مَن يَشَآءُ مِنۡ عِبَادِهِۦۚ وَلَوۡ أَشۡرَكُواْ لَحَبِطَ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Uongofu huo ni taufiki ya Mwenyezi Mungu ambayo kwayo Anamuongoza Anayemtaka miongoni mwa waja Wake. Na lau hawa Manabii walimshirikisha Mwenyezi Mungu, kwa kuchukulia na kukadiria, amali zao zingalipomoka. Kwani Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Hakubali amali yoyote pamoja na ushirikina.
Tefsiri na arapskom jeziku:
أُوْلَٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ ءَاتَيۡنَٰهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡحُكۡمَ وَٱلنُّبُوَّةَۚ فَإِن يَكۡفُرۡ بِهَا هَٰٓؤُلَآءِ فَقَدۡ وَكَّلۡنَا بِهَا قَوۡمٗا لَّيۡسُواْ بِهَا بِكَٰفِرِينَ
Manabii hao tuliowaneemesha kwa uongofu na unabii, ndio wale tuliowapa Kitabu, kama vile kurasa za Ibrāhīm, Taurati ya Muūsā, Zaburi ya Dāwūd na Injili ya Īsā. Na tuliwapa ufahamu wa Vitabu hivi na tukawateua kufikisha wahyi wetu. Na iwapo makafiri wa watu wako, ewe Mtume, watazikanusha aya za hii Qur’ani, basi tumewategemezea watu wengine jambo hilo, - yaani: Muhājirūn (masahaba waliohamia Madina pamoja na Mtume) na Ans,ār (masahaba wenyeji wa Madina) na wafuasi wao mpaka Siku ya Kiyama- ambao hawatakuwa ni wenye kuzikanusha. Bali watakuwa ni wenye kuziamini, ni wenye kuzitumia.
Tefsiri na arapskom jeziku:
أُوْلَٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ هَدَى ٱللَّهُۖ فَبِهُدَىٰهُمُ ٱقۡتَدِهۡۗ قُل لَّآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ أَجۡرًاۖ إِنۡ هُوَ إِلَّا ذِكۡرَىٰ لِلۡعَٰلَمِينَ
Manabii hao waliotajwa ndio ambao Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Amewaongoza kwenye dini Yake ya haki. Basi fuata uongofu wao, ewe Muhammad, na andama njia yao. Waambie washirikina, «Mimi sitaki kutoka kwenu, kwa kufikisha Uislamu, badala ya ulimwengu. Malipo yangu yako kwa Mwenyezi Mungu. Na Uislamu ni kuita watu wote kwenye njia iliyolingana sawa na ni ukumbusho kwenu na kwa kila aliyekuwa kama nyinyi, kati ya wale wanaoendelea kwenye batili; huenda nyinyi mkawaidhika nao mkanufaika.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَا قَدَرُواْ ٱللَّهَ حَقَّ قَدۡرِهِۦٓ إِذۡ قَالُواْ مَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ عَلَىٰ بَشَرٖ مِّن شَيۡءٖۗ قُلۡ مَنۡ أَنزَلَ ٱلۡكِتَٰبَ ٱلَّذِي جَآءَ بِهِۦ مُوسَىٰ نُورٗا وَهُدٗى لِّلنَّاسِۖ تَجۡعَلُونَهُۥ قَرَاطِيسَ تُبۡدُونَهَا وَتُخۡفُونَ كَثِيرٗاۖ وَعُلِّمۡتُم مَّا لَمۡ تَعۡلَمُوٓاْ أَنتُمۡ وَلَآ ءَابَآؤُكُمۡۖ قُلِ ٱللَّهُۖ ثُمَّ ذَرۡهُمۡ فِي خَوۡضِهِمۡ يَلۡعَبُونَ
Na hawa washirikina hawakumtukuza Mwenyezi Mungu ipasavyo kumtukuza, kwani walikanusha kwamba Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Amemteremshia yoyote miongoni mwa binadamu, chochote katika wahyi wake. Waambie, ewe Mtume, «Iwapo mambo ni kama mnavyodai, ni nani aliyeteremsha kitabu alichokuja nacho Mūsā kwa watu wake, kikiwa ni mwangaza kwa watu na mwongozo kwao?» Kisha maneno yakaelekea kwa Mayahudi kwa kuwakemea kwa kusema «Mnakigawanya kitabu hiki kwenye kurasa mbalimbali, nyingine mnazionesha na nyingi katika hizo mnazificha.- Kati ya hizo walizozificha ni maelezo ya sifa za Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na unabii wake.- Pia Mwenyezi Mungu Aliwafundisha, nyinyi Waarabu, Qur’ani ambayo Aliiteremsha kwenu, ndani yake mna habari ya walio kabla yenu na walio baada yenu na yatakayokuwa baada ya kufa kwenu, habari ambazo hamkuwa mkizijuwa, nyinyi wala wazazi wenu.» Sema, «Mwenyezi Mungu Ndiye Aliyeiteremsha.» Kisha waache hawa wavame na kucheza katika mazungumzo yao ya ubatili.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَهَٰذَا كِتَٰبٌ أَنزَلۡنَٰهُ مُبَارَكٞ مُّصَدِّقُ ٱلَّذِي بَيۡنَ يَدَيۡهِ وَلِتُنذِرَ أُمَّ ٱلۡقُرَىٰ وَمَنۡ حَوۡلَهَاۚ وَٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ يُؤۡمِنُونَ بِهِۦۖ وَهُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ يُحَافِظُونَ
Na hii Qur’ani ni Kitabu tulichokuteremshia, chenye manufaa makubwa, kinatoa ushahidi juu ya ukweli wa vitabu vilivyoteremshwa vilivyokuja kabla yake na juu ya kwamba vinatoka kwa Mwenyezi Mungu. Tumekiteremsha ili uwatishie nayo, watu wa Makkah na walioko pambizoni mwake kwenye majimbo yote ya ardhi, adhabu ya Mwenyezi Mungu na mateso Yake. Na wenye kuamini uhai wa Akhera, wanaamini kwamba Qur’ani ni maneno ya Mwenyezi Mungu na wanajilazimisha kusimamisha Swala kwa nyakati zake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبًا أَوۡ قَالَ أُوحِيَ إِلَيَّ وَلَمۡ يُوحَ إِلَيۡهِ شَيۡءٞ وَمَن قَالَ سَأُنزِلُ مِثۡلَ مَآ أَنزَلَ ٱللَّهُۗ وَلَوۡ تَرَىٰٓ إِذِ ٱلظَّٰلِمُونَ فِي غَمَرَٰتِ ٱلۡمَوۡتِ وَٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ بَاسِطُوٓاْ أَيۡدِيهِمۡ أَخۡرِجُوٓاْ أَنفُسَكُمُۖ ٱلۡيَوۡمَ تُجۡزَوۡنَ عَذَابَ ٱلۡهُونِ بِمَا كُنتُمۡ تَقُولُونَ عَلَى ٱللَّهِ غَيۡرَ ٱلۡحَقِّ وَكُنتُمۡ عَنۡ ءَايَٰتِهِۦ تَسۡتَكۡبِرُونَ
Ni nani mbaya zaidi wa udhalimu kuliko yule aliyemzulia Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, neno la urongo, akadai kwamba Yeye Hakumtuma mjumbe yoyote miongoni mwa wanadamu, au akafanya madai ya urongo kwamba Mwenyezi Mungu Amemletea wahyi na hali hakumletea wahyi wowote, au akadai kwamba yeye ni muweza wa kuteremsha mfano wa Qur’ani Aliyoiteremsha Mwenyezi Mungu? Na lau wawaona hawa wenye kupita mpaka, nao wako kwenye vitisho vya kufa, ungaliona jambo la kufazaisha, huku Malaika wakizitwaa roho zao, wameikunjua mikono yao kwa adhabu, wanawaambia, «Zitoeni nafsi zenu. Leo mtadhalilishwa upeo wa kudhalilishwa, kama mlivyokuwa mkisema urongo juu ya Mwenyezi Mungu na mkiona kiburi kufuata aya Zake na kuandama Mitume Wake.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَقَدۡ جِئۡتُمُونَا فُرَٰدَىٰ كَمَا خَلَقۡنَٰكُمۡ أَوَّلَ مَرَّةٖ وَتَرَكۡتُم مَّا خَوَّلۡنَٰكُمۡ وَرَآءَ ظُهُورِكُمۡۖ وَمَا نَرَىٰ مَعَكُمۡ شُفَعَآءَكُمُ ٱلَّذِينَ زَعَمۡتُمۡ أَنَّهُمۡ فِيكُمۡ شُرَكَٰٓؤُاْۚ لَقَد تَّقَطَّعَ بَيۡنَكُمۡ وَضَلَّ عَنكُم مَّا كُنتُمۡ تَزۡعُمُونَ
Hakika mumetujia ili muhesabiwe na mulipwe mkiwa peke yenu, kama tulivyowafanya mpatikane ulimwenguni mara ya kwanza mkiwa miguu mitupu, hamuna nguo, mumeviacha nyuma yenu vitu ambavyo tuliwamakinisha navyo miongoni mwa mali ya ulimwenguni mliokuwa mkijigamba nayo. Na hatuwaoni masanamu wako na nyinyi Akhera ambao mlikuwa mkiitakidi kuwa watawaombea na mkidai kuwa ni washirika pamoja na Mwenyezi Mungu katika ibada. Mashikamano yaliyokuwa kati yenu ulimenguni yameondoka, na yamewaondokea yale mliokuwa mkiyadai kwamba waungu wenu ni washirika wa Mwenyezi Mungu katika ibada, na imefunuka wazi kwamba nyinyi ndio mliopata hasara ya nafsi zenu, watu wenu na mali yenu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
۞ إِنَّ ٱللَّهَ فَالِقُ ٱلۡحَبِّ وَٱلنَّوَىٰۖ يُخۡرِجُ ٱلۡحَيَّ مِنَ ٱلۡمَيِّتِ وَمُخۡرِجُ ٱلۡمَيِّتِ مِنَ ٱلۡحَيِّۚ ذَٰلِكُمُ ٱللَّهُۖ فَأَنَّىٰ تُؤۡفَكُونَ
Hakika Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Anapasua mbegu ukatoka mmea, na Anapasua koko ukatoka mti. Anatoa chenye uhai kutokana na kilichokufa, kama vile binadamu na mnyama kutokana na tone la manii ya binadamu na mnyama. Na Anatoa kilichokufa kutokana na chenye uhai, kama tone la manii linalotokana na binadamu na mnyama. Huyo Ndiye Mwenyezi Mungu. Yaani Mwenye kufanya hili ni Mwenyezi Mungu, Peke Yake, Asiye na mshirika, Anayestahiki kuabudiwa. Basi vipi nyinyi mtaepushwa na haki mpelekwe kwenye batili mkamuabudu pamoja na Yeye mwingine asiyekuwa Yeye?
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَالِقُ ٱلۡإِصۡبَاحِ وَجَعَلَ ٱلَّيۡلَ سَكَنٗا وَٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَ حُسۡبَانٗاۚ ذَٰلِكَ تَقۡدِيرُ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡعَلِيمِ
Na Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake na kutukuka ni Kwake, Ndiye Ambaye Alipasua mwangaza wa asubuhi kutoka kwenye giza la usiku, na Akaufanya usiku ni wakati wa utulivu, anatulia humo anayechoka mchana na kupata fungu lake la mapumziko, na Akalifanya jua na mwezi zinatembea katika njia zake kwa hesabu ya sawsawa iliyokadiriwa, haibadiliki wala haigongani. Hayo ndiyo makadirio ya Al- ’Azīz, Mwenye kushinda, ambaye ufalme Wake umeshinda, Al- ’Alīm, Aliye Mjuzi wa maslahi ya viumbe Wake na kuendesha mambo yao. Al- ’Azīz na Al- ’Alīm ni miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu mazuri yanayoonesha ukamilifu wa ushindi na ujuzi.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَهُوَ ٱلَّذِي جَعَلَ لَكُمُ ٱلنُّجُومَ لِتَهۡتَدُواْ بِهَا فِي ظُلُمَٰتِ ٱلۡبَرِّ وَٱلۡبَحۡرِۗ قَدۡ فَصَّلۡنَا ٱلۡأٓيَٰتِ لِقَوۡمٖ يَعۡلَمُونَ
Na Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, Ndiye Aliyewawekea, enyi watu, nyota ni alama ya nyinyi kujua njia kipindi cha usiku mnapopotea kwa sababu ya giza lingi, barani na baharini. Tumezifafanua hoja zilizo wazi, ili wazizingatie miongoni mwenu wenye elimu ya kumjua Mwenyezi Mungu na sheria Yake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَهُوَ ٱلَّذِيٓ أَنشَأَكُم مِّن نَّفۡسٖ وَٰحِدَةٖ فَمُسۡتَقَرّٞ وَمُسۡتَوۡدَعٞۗ قَدۡ فَصَّلۡنَا ٱلۡأٓيَٰتِ لِقَوۡمٖ يَفۡقَهُونَ
Na Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, Ndiye Aliyeanza kuwaumba, enyi watu, kutokana na Ādam, amani imshukiye, Alipomuumba kwa udongo, kisha mkawa nyinyi ni kizazi chenye kuendelea kutokana na yeye, Akawafanyia kituo cha nyinyi kutulia, nacho ni zao za wanawake; na Akawafanyia hazina ya nyinyi kuhifadhiwa , nayo ni migongo ya wanaume. Tumeshawabainishia hoja na kuwapambanulia dalili na kuzithibitisha kwa watu wenye kufahamu vituo vya hoja na sehemu za mazingatio.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَهُوَ ٱلَّذِيٓ أَنزَلَ مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ فَأَخۡرَجۡنَا بِهِۦ نَبَاتَ كُلِّ شَيۡءٖ فَأَخۡرَجۡنَا مِنۡهُ خَضِرٗا نُّخۡرِجُ مِنۡهُ حَبّٗا مُّتَرَاكِبٗا وَمِنَ ٱلنَّخۡلِ مِن طَلۡعِهَا قِنۡوَانٞ دَانِيَةٞ وَجَنَّٰتٖ مِّنۡ أَعۡنَابٖ وَٱلزَّيۡتُونَ وَٱلرُّمَّانَ مُشۡتَبِهٗا وَغَيۡرَ مُتَشَٰبِهٍۗ ٱنظُرُوٓاْ إِلَىٰ ثَمَرِهِۦٓ إِذَآ أَثۡمَرَ وَيَنۡعِهِۦٓۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكُمۡ لَأٓيَٰتٖ لِّقَوۡمٖ يُؤۡمِنُونَ
Na Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa za pungufu ni Kwake, Nadiye Aliyetaramsha mvua kutoka kwenye mawingu, Akatoa kwayo mimea ya kila kitu, Akatoa, kutokana na mimea, nafaka na miti mibichi, kisha akatoa kwenye mimea ya nafaka mbegu zilizoshikana, kama masuke ya mahindi, ngano na mpunga. Na Akatoa kutoka kwenye kizao cha mtende, nacho ni kile ambacho karara la tende linachomoza hapo, mitungo ambayo kuitunda ni karibu. Na Akatoa, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, mashamba ya mizabibu. Na Akatoa mizaituni na mikomamanga ambayo majani yake yanafanana na matunda yake yanatafautiana kimaumbile, uatamu na kitabia. Angalieni, enyi watu, matunda ya mimea hii inapotoa mazao na kuiva kwake na kustawi kwake yanapostawi. Hakika katika hayo, enyi watu, kuna dalili ya ukamilifu wa uwezo wa muumba vitu hivi, hekima Yake na rehema Yake kwa watu wenye kumuamini Yeye, Aliyetukuka, na kuzifuata sheria Yake kivitendo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَجَعَلُواْ لِلَّهِ شُرَكَآءَ ٱلۡجِنَّ وَخَلَقَهُمۡۖ وَخَرَقُواْ لَهُۥ بَنِينَ وَبَنَٰتِۭ بِغَيۡرِ عِلۡمٖۚ سُبۡحَٰنَهُۥ وَتَعَٰلَىٰ عَمَّا يَصِفُونَ
Na hawa washirikina wamefanya majini ni washirika wa Mwenyezi Mungu katika ibada, kwa kuitakidi kwao kuwa wao wanalete manufaa au madhara, na hali Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Amewaumba wao na wanavyoviabudu kutoka kwenye ‘adam ( hali ya kutokuwako). Basi ni Yeye Aliyepwkeka kwa kuumba, Peke Yake, na inapasa Apwekeke kwa kuabudiwa Peke Yake, Asiye na mshirika. Na, kwa kweli, hawa washirikina walisema urongo kumzulia Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, walipomnasibishia Yeye watoto wa kiume na wakike, kwa kutojua kwao sifa Zake za ukamilifu zinazompasa. Ameepuka na kuwa juu ya yale, ambayo walimnasibisha nayo washirikina, ya urongo na uzushi.
Tefsiri na arapskom jeziku:
بَدِيعُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ أَنَّىٰ يَكُونُ لَهُۥ وَلَدٞ وَلَمۡ تَكُن لَّهُۥ صَٰحِبَةٞۖ وَخَلَقَ كُلَّ شَيۡءٖۖ وَهُوَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٞ
Na Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Ndiye Aliyezipatisha mbingu na ardhi na vilivyomo humo, kwa namna isiyokuwa na mfano uliotangulia. Vipi Awe na mtoto, na hakuwa na mke? Ametukuka Mwenyezi Mungu kutukuka kukubwa na yale wanayoyasema washirikina, Na Yeye Ndiye Aliyeumba kila kitu kutokana na hali ya kutokuwako na hakuna chochote chenye kufichika Kwake katika mambo ya viumbe.
Tefsiri na arapskom jeziku:
ذَٰلِكُمُ ٱللَّهُ رَبُّكُمۡۖ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۖ خَٰلِقُ كُلِّ شَيۡءٖ فَٱعۡبُدُوهُۚ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ وَكِيلٞ
Huyo, enyi washirikina, Ndiye Mola wenu, Aliyeshinda na kutukuka; hapana Mwenye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Yeye; Mwenye kuumba kila kitu. Basi mwandameni na mumnyenyekee kwa kumtii na kumuabudu. Na Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, ni Mtegemewa na ni Mtunzi, Anayaendesha mambo ya viumbe vyake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
لَّا تُدۡرِكُهُ ٱلۡأَبۡصَٰرُ وَهُوَ يُدۡرِكُ ٱلۡأَبۡصَٰرَۖ وَهُوَ ٱللَّطِيفُ ٱلۡخَبِيرُ
Macho hayamuoni Mwenyezi Mungu ulimwenguni. Ama kwenye nyumba ya Akhera, Waumini watamuona Mola wao bila kumuenea. Na Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, anayafikia macho na kuyazunguka, na kuyajua vile yalivyo. Na Yeye ni Al-Latīf (Mpole) kwa mawalii Wake, Anayejua mambo yenye upeo wa udogo, Al-Khabīr (Mtambuzi) Anayejua mambo ya ndani.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قَدۡ جَآءَكُم بَصَآئِرُ مِن رَّبِّكُمۡۖ فَمَنۡ أَبۡصَرَ فَلِنَفۡسِهِۦۖ وَمَنۡ عَمِيَ فَعَلَيۡهَاۚ وَمَآ أَنَا۠ عَلَيۡكُم بِحَفِيظٖ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Mumejiwa na hoja zilizo wazi kutoka kwa Mola wenu, mnaonea nazo uongofu na upotevu, miongoni mwa zile zilizokusanywa na Qur’ani na akaja nazo Mtume, rehema na amani zimshukiye. Basi mwenye kufunukiwa na hoja hizi na akayaamini yale yanayolekezwa nazo, faida yake itamfikia mwenyewe. Na yule ambaye hakuuona uongofu baada ya hoja kumfunukia , basi amejikosea mwenyewe. Na mimi si mtunzi wa kudhibiti matendo yenu. Mimi ni mfikishaji tu. Na Mwenyezi Mungu Anamuongoza Anayemtaka na Anampoteza Anayemtaka kulingana na ujuzi Wake na hekima Yake.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَكَذَٰلِكَ نُصَرِّفُ ٱلۡأٓيَٰتِ وَلِيَقُولُواْ دَرَسۡتَ وَلِنُبَيِّنَهُۥ لِقَوۡمٖ يَعۡلَمُونَ
Na kama tulivyowafafanulia washirikina, katika hii Qur’ani, hoja zilizo wazi juu ya jambo la kumpwekesha Mwenyezi Mungu, utume na marejeo ya Kiyama, tunawafafanulia hoja katika kila wasichokijua. Na hapo wanasema urongo, «Umejifunza kutoka kwa watu wa Kitabu!» Na ili tufafanue haki, kwa kuzileta aya, kwa watu wanaoijua na kuikubali na kuifuata, nao ni waliomuamini Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na kile alichoteremshiwa.
Tefsiri na arapskom jeziku:
ٱتَّبِعۡ مَآ أُوحِيَ إِلَيۡكَ مِن رَّبِّكَۖ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۖ وَأَعۡرِضۡ عَنِ ٱلۡمُشۡرِكِينَ
Fuata, ewe Mtume, wahyi tuliokuteremshia, wenye maamrisho na makatazo ambayo, kubwa lake ni kumpwekesha Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, na kuita watu huko. Na usijali ushindani wa washirikina na madai yao ya urongo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ مَآ أَشۡرَكُواْۗ وَمَا جَعَلۡنَٰكَ عَلَيۡهِمۡ حَفِيظٗاۖ وَمَآ أَنتَ عَلَيۡهِم بِوَكِيلٖ
Na lau Mwenyezi Mungu Alitaka wasishirikishe hawa washirikina hawangalishirikisha, lakini Yeye, Aliyetukuka, ni Mjuzi wa yatakayokuwa ya ubaya wa uchaguzi wao na kufuata kwao matamanio yaliyopotoka. Na hatukukufanya wewe ni mchunguzi wa kuwatunzia matendo yao wala hukuwa ni msimamizi wao wa kuwapangia maslahi yao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَا تَسُبُّواْ ٱلَّذِينَ يَدۡعُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ فَيَسُبُّواْ ٱللَّهَ عَدۡوَۢا بِغَيۡرِ عِلۡمٖۗ كَذَٰلِكَ زَيَّنَّا لِكُلِّ أُمَّةٍ عَمَلَهُمۡ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّهِم مَّرۡجِعُهُمۡ فَيُنَبِّئُهُم بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Na msiyatukane, enyi Waislamu, masanamu ambyo washirikina wanayaabudu, kwa ajili ya kuziba kipengele, ili hilo lisije likawafanya wao wamtukane Mwenyezi Mungu kwa ujinga na kwa uadui, bila ya kuwa na ujuzi. Na kama tulivyowapambia hawa matendo yao mabaya, yakiwa ni mateso kwao kwa uchaguzi wao mbaya, ndivyo tulivyowapambia kila umma matendo yao. Kisha marejeo yao wote ni kwa Mola wao; hapo Mwenyezi Mungu Awaambie matendo yao waliokuwa wakiyatenda ulimwenguni kisha Awalipe kwayo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَأَقۡسَمُواْ بِٱللَّهِ جَهۡدَ أَيۡمَٰنِهِمۡ لَئِن جَآءَتۡهُمۡ ءَايَةٞ لَّيُؤۡمِنُنَّ بِهَاۚ قُلۡ إِنَّمَا ٱلۡأٓيَٰتُ عِندَ ٱللَّهِۖ وَمَا يُشۡعِرُكُمۡ أَنَّهَآ إِذَا جَآءَتۡ لَا يُؤۡمِنُونَ
Na waliapa washirikina hawa viyapo vya mkazo, «Lau Atatujia Muhammad kwa alama yenye miujiza, tutayaamini yale aliyoyaleta.» Sema, ewe Mtume, «Kuja kwa miujiza yenye kushinda kunatokana na Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka. Yeye Ndiye Mwenye uwezo wa kuileta Akitaka.» Na nilipi liwajulishalo nyinyi, enyi Waumini: huenda miujiza hii ikija hawataiamini hawa washirikina?.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَنُقَلِّبُ أَفۡـِٔدَتَهُمۡ وَأَبۡصَٰرَهُمۡ كَمَا لَمۡ يُؤۡمِنُواْ بِهِۦٓ أَوَّلَ مَرَّةٖ وَنَذَرُهُمۡ فِي طُغۡيَٰنِهِمۡ يَعۡمَهُونَ
Na tutazigeuza nyoyo zao na macho yao, tuweke kizuizi baina yake na kunufaika na alama za Mwenyezi mungu, wasiziamini kama walivyokuwa hawakuziamini aya za Qur’ani zilipoteremka kwa mara ya kwanza, na tutawaacha wao wameduwaa katika kumuasi kwao Mwenyezi Mungu, hawaongoki kwenye haki na usawa.
Tefsiri na arapskom jeziku:
۞ وَلَوۡ أَنَّنَا نَزَّلۡنَآ إِلَيۡهِمُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ وَكَلَّمَهُمُ ٱلۡمَوۡتَىٰ وَحَشَرۡنَا عَلَيۡهِمۡ كُلَّ شَيۡءٖ قُبُلٗا مَّا كَانُواْ لِيُؤۡمِنُوٓاْ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ يَجۡهَلُونَ
Na lau kama sisi tungaliyaitikia maombi ya washirikina hawa na kuwateremshia Malaika kutoka mbinguni na tukawafufulia wafu wakazungumza nao na tukawakusanyia kila kitu walichokitaka wakakiona ana kwa ana, hawangaliyakubali yale uliyowaitia, ewe Mtume, na hawangaliyatumia, isipokuwa yule ambaye Mwenyezi Mungu Alimtakia uongofu. Lakini wengi wa hawa makafiri hawaijui haki ambayo umekuja nayo kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَكَذَٰلِكَ جَعَلۡنَا لِكُلِّ نَبِيٍّ عَدُوّٗا شَيَٰطِينَ ٱلۡإِنسِ وَٱلۡجِنِّ يُوحِي بَعۡضُهُمۡ إِلَىٰ بَعۡضٖ زُخۡرُفَ ٱلۡقَوۡلِ غُرُورٗاۚ وَلَوۡ شَآءَ رَبُّكَ مَا فَعَلُوهُۖ فَذَرۡهُمۡ وَمَا يَفۡتَرُونَ
Na kama tulivyokujaribu wewe, ewe Mtume, kwa maadui zako miongoni mwa washirikina, tuliwajaribu Manabii wote, amani iwashukie, kwa maadui miongoni mwa waasi wa watu wao na maadui miongoni mwa waasi wa majini, wanapelekeana wenyewe kwa wenyewe maneno waliyoyapamba kwa uharibifu, ili adanganyike mwenye kuyasikia na apate kupotea njia ya Mwenyezi Mungu. Na lau Mola wako, Aliyetukuka na kuwa juu, Alitaka, angaliweka kizuizi kati yao na ule uadui, lakini huo ni mtihani kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Basi waache na kile wanachokibuni cha urongo na uzushi.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلِتَصۡغَىٰٓ إِلَيۡهِ أَفۡـِٔدَةُ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ وَلِيَرۡضَوۡهُ وَلِيَقۡتَرِفُواْ مَا هُم مُّقۡتَرِفُونَ
Na ili zielekee huko nyoyo za makafiri ambao hawaamini maisha ya Akhera wala hawayafanyii matendo ya kuwafaa, na ili nafsi zao zipate kuyapenda, na ili wapate kuyafanya maovu ambayo wao ni wenye kuyafanya. Katika haya, pana onyo kubwa kwao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَفَغَيۡرَ ٱللَّهِ أَبۡتَغِي حَكَمٗا وَهُوَ ٱلَّذِيٓ أَنزَلَ إِلَيۡكُمُ ٱلۡكِتَٰبَ مُفَصَّلٗاۚ وَٱلَّذِينَ ءَاتَيۡنَٰهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ يَعۡلَمُونَ أَنَّهُۥ مُنَزَّلٞ مِّن رَّبِّكَ بِٱلۡحَقِّۖ فَلَا تَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمُمۡتَرِينَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Kwani kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, Aliye Mola wangu na Mola wenu, natafuta uamuzi kati yangu na nyinyi, na hali Yeye, kutakasika na sifa pungufu ni Kwake, Amewateremshia Qur’ani ambayo ndani yake pana ufafanuzi wa uamuzi wa yale ambayo mlikuwa mkiteta juu yake kuhusu mambo yangu na mambo yenu?» Na Wana wa Isrāīl waliopewa na Mwenyezi Mungu Taurati na Injili wana ujuzi wa yakini kwamba hii Qur’ani imeteremshwa kwako, ewe Mtume, kutoka kwa Mola wako kwa haki. Basi usiwe, tena usiwe, ni miongoni mwa wenye shaka juu ya chochote ambacho tumekuletea wahyi.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَتَمَّتۡ كَلِمَتُ رَبِّكَ صِدۡقٗا وَعَدۡلٗاۚ لَّا مُبَدِّلَ لِكَلِمَٰتِهِۦۚ وَهُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ
Na limekamilika neno la Mola wako, nalo ni Qur’ani, likiwa lina ukweli wa habari na maneno, lenye uadilifu wa hukumu. Hakuna anayeweza kuyabadilisha maneno yake yaliyokamilika. Na Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, Ndiye Mwenye kuyasikia wanayoyasema waja Wake, Ndiye mwenye kuyajua mambo yao yaliyo waziwazi na yaliyojificha
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِن تُطِعۡ أَكۡثَرَ مَن فِي ٱلۡأَرۡضِ يُضِلُّوكَ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَإِنۡ هُمۡ إِلَّا يَخۡرُصُونَ
Na lau itakadiriwa, ewe Mtume, kwamba wewe uliwasikiliza wengi kati ya watu wanaokaa ardhini, kwa kweli wanagalikupoteza ukawa kando na dini ya Mwenyezi Mungu. Kwani wao hawaendi isipokuwa kwenye yale wanayoyaona kuwa ni haki kwa kuwaiga wakale wao. Na hawakuwa wao isipokuwa tu wanadhania na wanasema urongo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ مَن يَضِلُّ عَن سَبِيلِهِۦۖ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ
Na kwa hakika, Mola wako Ndiye Anayewajua zaidi wenye kupotea njia ya uongofu; na Yeye Anawajuwa zaidi, kuliko nyinyi, wale walio kwenye njia ya uongofu na usawa; hafichiki Kwake yoyote katika wao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَكُلُواْ مِمَّا ذُكِرَ ٱسۡمُ ٱللَّهِ عَلَيۡهِ إِن كُنتُم بِـَٔايَٰتِهِۦ مُؤۡمِنِينَ
Basi kuleni, kati ya wanyama waliochinjwa, wale ambao jina la Mwenyezi Mungu lilitajwa wakati wa kuchinjwa, iwapo nyinyi mnaziamini hoja za Mwenyezi Mungu, aliyetukuka, zilizo wazi.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَا لَكُمۡ أَلَّا تَأۡكُلُواْ مِمَّا ذُكِرَ ٱسۡمُ ٱللَّهِ عَلَيۡهِ وَقَدۡ فَصَّلَ لَكُم مَّا حَرَّمَ عَلَيۡكُمۡ إِلَّا مَا ٱضۡطُرِرۡتُمۡ إِلَيۡهِۗ وَإِنَّ كَثِيرٗا لَّيُضِلُّونَ بِأَهۡوَآئِهِم بِغَيۡرِ عِلۡمٍۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُعۡتَدِينَ
Na kitu gani kinachowazuia, enyi Waislamu, kumla mnyama ambaye jina la Mwenyezi Mungu lilitajwa wakati wa kuchinjwa, ambapo Mwenyezi Mungu, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, Amewaelezea nyinyi yote aliyoyaharamisha kwenu? Lakini yale ya haramu ambayo dharura imepelekea yatumiwe, kwa sababu ya njaa, kama mfu, basi mumehalalishiwa. Na wengi, kati ya wapotofu, wanawapoteza wafuasi wao na kuwaepusha na njia ya Mwenyezi Mungu katika kuhalalisha haramu na kuharamisha halali kwa matakwa yao kwa ujinga walionao. Kwa hakika, Mola wako, ewe Mtume, Ndiye Amjuwaye zaidi yule aliyekiuka mipaka Yake katika hayo; na Yeye Ndiye Atakayesimamia hesabu yake na malipo yake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَذَرُواْ ظَٰهِرَ ٱلۡإِثۡمِ وَبَاطِنَهُۥٓۚ إِنَّ ٱلَّذِينَ يَكۡسِبُونَ ٱلۡإِثۡمَ سَيُجۡزَوۡنَ بِمَا كَانُواْ يَقۡتَرِفُونَ
Na acheni, enyi watu, maasia yote, yaliyo waziwazi na yaliyo ya siri. Hakika wale wanaofanya maasia, Mola wao Atawatesa kwa sababu ya yale maovu ambyo walikuwa wakiyafanya.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَا تَأۡكُلُواْ مِمَّا لَمۡ يُذۡكَرِ ٱسۡمُ ٱللَّهِ عَلَيۡهِ وَإِنَّهُۥ لَفِسۡقٞۗ وَإِنَّ ٱلشَّيَٰطِينَ لَيُوحُونَ إِلَىٰٓ أَوۡلِيَآئِهِمۡ لِيُجَٰدِلُوكُمۡۖ وَإِنۡ أَطَعۡتُمُوهُمۡ إِنَّكُمۡ لَمُشۡرِكُونَ
Na wala msile, enyi Waislamu, katika vichinjwa, yule ambaye halikutajwa jina la Mwenyezi Mungu wakati wa kuchinjwa, kama mfu na aliochinjiwa masanamu na majini na wasiokuwa hao. Na kwa hakika kuwala wanyama hao ni kutoka kwenye twaa ya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka. Na majini waasi wanawatia marafiki zao, miongoni mwa mashetani wa kibinadamu, ushawiwishi wa kuwatatiza kuhusu uharamu wa kula mfu; wanawaamrisha wawaambie Waislamu wanapobishana nao, «Hakika nyinyi, kwa kutokula kwenu mfu, huwa hamli anachokiua Mwenyezi Mungu, ambapo mnakula mnachokichinja.» Na iwapo mtawasikiliza, enyi Waislamu, katika kuhalalisha mfu, basi nyinyi mtakuwa sawa na wao katika ushirikina.
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَوَمَن كَانَ مَيۡتٗا فَأَحۡيَيۡنَٰهُ وَجَعَلۡنَا لَهُۥ نُورٗا يَمۡشِي بِهِۦ فِي ٱلنَّاسِ كَمَن مَّثَلُهُۥ فِي ٱلظُّلُمَٰتِ لَيۡسَ بِخَارِجٖ مِّنۡهَاۚ كَذَٰلِكَ زُيِّنَ لِلۡكَٰفِرِينَ مَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Je, yule ambaye amekufa katika upotofu, ameangamia na ameshangaa, tukaufufua moyo wake kwa Imani, tukamuongoza kwenye Imani na tukamuafikia kuwafuata Mitume Wake, akawa anaishi kwenye miangaza ya uongofu, atakuwa ni kama mfano wa yule aliye ndani ya ujinga, matamanio ya moyo na namna mbalimbali za upotevu, asiyeongokewa kwenye sehemu yoyote ya kupenya na hana wa kumuokoa na yale ambayo yumo ndani yake? Hao wawili hawalingani. Na kama nilivyomuachilia kafiri huyu anayebishana na nyinyi, enyi Waumini, nikampambia vitendo vyake viovu akaviona ni vyema, vilevile nimewapambia wenye kukanusha vitendo vyao viovu ili wapaswe, kwa hilo, kupata adhabu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَكَذَٰلِكَ جَعَلۡنَا فِي كُلِّ قَرۡيَةٍ أَكَٰبِرَ مُجۡرِمِيهَا لِيَمۡكُرُواْ فِيهَاۖ وَمَا يَمۡكُرُونَ إِلَّا بِأَنفُسِهِمۡ وَمَا يَشۡعُرُونَ
Na mfano huu uliopatikana kwa viongozi wa makafiri huko Maka wa kuzuia dini ya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, tumeweka katika kila mji watu waovu wanaongozwa na wakubwa wao, ili wapate kufanya vitimbi humo kwa kuzuia dini ya Mwenyezi Mungu; na wao hawazifanyii vitimbi isipokuwa nafsi zao, na wala hawalihisi hilo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِذَا جَآءَتۡهُمۡ ءَايَةٞ قَالُواْ لَن نُّؤۡمِنَ حَتَّىٰ نُؤۡتَىٰ مِثۡلَ مَآ أُوتِيَ رُسُلُ ٱللَّهِۘ ٱللَّهُ أَعۡلَمُ حَيۡثُ يَجۡعَلُ رِسَالَتَهُۥۗ سَيُصِيبُ ٱلَّذِينَ أَجۡرَمُواْ صَغَارٌ عِندَ ٱللَّهِ وَعَذَابٞ شَدِيدُۢ بِمَا كَانُواْ يَمۡكُرُونَ
Na pindi inapowajia washirikina hawa, miongoni mwa watu wa Maka, hoja iliyo waziwazi juu ya unabii wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, wanasema baadhi ya wakubwa wao, «Kamwe hatutaukubali unabii wake mpaka Mwenyezi Mungu Atupe unabii na miujiza mfano wa Aliyowapa wajumbe wake waliotangulia» Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Aliwajibu kwa neno lake,: “Mwenyezi Mungu Anajua zaidi wapi Auweke ujumbe Wake.» Kwa maana kuwa Anawajua wale wanaofaa kubeba ujumbe Wake na kuufikisha kwa Watu. Utawapata unyonge wakiukaji mipaka hawa, na watakuwa na adhabu iumizayo ndani ya Moto wa Jahanamu kwa sababu ya vitimbi vyao kwa Uislamu na watu wake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَمَن يُرِدِ ٱللَّهُ أَن يَهۡدِيَهُۥ يَشۡرَحۡ صَدۡرَهُۥ لِلۡإِسۡلَٰمِۖ وَمَن يُرِدۡ أَن يُضِلَّهُۥ يَجۡعَلۡ صَدۡرَهُۥ ضَيِّقًا حَرَجٗا كَأَنَّمَا يَصَّعَّدُ فِي ٱلسَّمَآءِۚ كَذَٰلِكَ يَجۡعَلُ ٱللَّهُ ٱلرِّجۡسَ عَلَى ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ
Basi yule ambaye Mwenyezi Mungu Anataka kumuafukia aikubali haki, Anakikunjua kifua chake kukubali Imani na upweke wa Mwenyezi Mungu; na yule ambaye Anataka kumpoteza , Anakifanya kifua chake kiwe katika hali ya dhiki kubwa na kukunjika katika kuukubali uongofu, kama hali ya anayepaa kwenye tabaka za anga za juu, hapo akapatwa na uzito mkubwa wa kuvuta pumzi. Na kama anavyovifanya Mwenyezi Mungu vifua vya makafiri vibanike sana na kukunjika, hivyo basi ndivyo Atakavyowapatia adhabu wale wasiomuamini.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَهَٰذَا صِرَٰطُ رَبِّكَ مُسۡتَقِيمٗاۗ قَدۡ فَصَّلۡنَا ٱلۡأٓيَٰتِ لِقَوۡمٖ يَذَّكَّرُونَ
Na haya tuliliyokubainishia, ewe Mtume, ndio njia inayofikisha kwenye radhi za Mola Wako na Pepo Yake. Tumezifunua wazi hoja kwa yule anayekumbuka miongoni mwa wenye akili zilizokomaa.
Tefsiri na arapskom jeziku:
۞ لَهُمۡ دَارُ ٱلسَّلَٰمِ عِندَ رَبِّهِمۡۖ وَهُوَ وَلِيُّهُم بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Wale wanaokumbuka watapata mbele ya Mola wao, Aliyetukuka na kuwa juu, Siku ya Kiyama Nyumba ya Salama na Amani, isiyo na makero, nayo ni Pepo. Na yeye, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, ni Mwenye kuwanusuru na kuwalinda; hayo yakiwa ni malipo kwao kwa matendo yao mema.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَيَوۡمَ يَحۡشُرُهُمۡ جَمِيعٗا يَٰمَعۡشَرَ ٱلۡجِنِّ قَدِ ٱسۡتَكۡثَرۡتُم مِّنَ ٱلۡإِنسِۖ وَقَالَ أَوۡلِيَآؤُهُم مِّنَ ٱلۡإِنسِ رَبَّنَا ٱسۡتَمۡتَعَ بَعۡضُنَا بِبَعۡضٖ وَبَلَغۡنَآ أَجَلَنَا ٱلَّذِيٓ أَجَّلۡتَ لَنَاۚ قَالَ ٱلنَّارُ مَثۡوَىٰكُمۡ خَٰلِدِينَ فِيهَآ إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُۚ إِنَّ رَبَّكَ حَكِيمٌ عَلِيمٞ
Na kumbuka, ewe Mtume, ile Siku Atakayowakusanya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, makafiri na wategemewa wao, miongoni mwa mashetani wa kijini, na kuwaambia, «Enyi mkusanyiko wa majini, hakika mumewapoteza binadamu wengi.» Na watasema wategemewa wao miongoni mwa makafiri wa kibinadamu, «EweMola wetu, kila mmoja katika sisi amenufaika na mwengine, na tumefikia kikomo ambacho umekiweka kwetu kwa kumalizika uhai wetu wa duniani.» Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Atasema Awaambie, «Moto ndio mashukio yenu, mtakaa milele, isipokuwa yule ambaye Mwenyezi Mungu Ametaka asikaye milele,» miongoni mwa walioasi wenye kumpwekesha Mwenyezi Mungu. Hakika Mola wako ni Mwingi wa hekima katika uendeshaji Wake na utengenezaji Wake, ni Mjuzi mno wa mambo yote ya waja Wake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَكَذَٰلِكَ نُوَلِّي بَعۡضَ ٱلظَّٰلِمِينَ بَعۡضَۢا بِمَا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ
Na kama tulivyowapa uwezo mashetani wa kijini juu ya makafiri wa kibinadamu wakawa ni wategemewa wao, hivyohivyo tunawapa uwezo madhalimu wa kibinadamu juu ya wenyewe kwa wenyewe duniani kwa sababu ya maasia wayafanyayo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
يَٰمَعۡشَرَ ٱلۡجِنِّ وَٱلۡإِنسِ أَلَمۡ يَأۡتِكُمۡ رُسُلٞ مِّنكُمۡ يَقُصُّونَ عَلَيۡكُمۡ ءَايَٰتِي وَيُنذِرُونَكُمۡ لِقَآءَ يَوۡمِكُمۡ هَٰذَاۚ قَالُواْ شَهِدۡنَا عَلَىٰٓ أَنفُسِنَاۖ وَغَرَّتۡهُمُ ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَا وَشَهِدُواْ عَلَىٰٓ أَنفُسِهِمۡ أَنَّهُمۡ كَانُواْ كَٰفِرِينَ
Enyi majini na binadamu mlio washirikina, kwani hawakuwajia Mitume miongoni mwenu- Maandiko yanaonesha kuwa Mitume wanatoka kwa wanadamu tu.[4]- wanaowapa habari za alama zangu zilizo wazi, zinazokusanya maamrisho na makatazo, zinazofafanua kheri na shari na wanaowaonya kukumbana na adhabu yangu Siku ya Kiyama? Watasema washirikina hawa, maijini na binadamu, «Tumeshuhudia juu ya nafsi zetu kwamba Mitume wako wametufikishia aya zako na wametuonya makutano ya Siku yetu hii, na sisi tukawakanusha.» Na hawa washirikina, liliwadanganya wao pambo la maisha ya dunia. Na walizishuhudilia nafsi zao kwamba wao walikuwa wakiukataa upweke wa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na wakiwafanya warongo Mitume Wake, amani iwashukie.
[4]Hii ndio kauli yenye nguvu ya maimamu wa nyuma na waliokuja baada yao. Na hii 1 aya si dalili wazi ya kuwa kuna Mitume wa kijini. Angalia Tafsiri ya lbn Kathīr katika kusherehi aya hii.
Tefsiri na arapskom jeziku:
ذَٰلِكَ أَن لَّمۡ يَكُن رَّبُّكَ مُهۡلِكَ ٱلۡقُرَىٰ بِظُلۡمٖ وَأَهۡلُهَا غَٰفِلُونَ
Ili asiadhibiwe yoyote kwa kujidhulumu nafsi yake kwa kufanya maovu na hali ulinganizi wa Uislamu haujamfikia, sisi tulituma Mitume na tukateremsha Vitabu kwa kuwaondolea majini na binadamu hoja watakayoichukua kama kisingizio. Hivyo ndivyo tulivyowaondolea hoja umma waliyopita, hatukumuadhibu yoyote isipokuwa baada ya kuwapelekea Mitume.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلِكُلّٖ دَرَجَٰتٞ مِّمَّا عَمِلُواْۚ وَمَا رَبُّكَ بِغَٰفِلٍ عَمَّا يَعۡمَلُونَ
Na kila mwenye kufanya vitendo vya kumtii Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, vya kumuasi ana daraja kutokana na vitendo vyake, Mwenyezi Mungu Atamfikishia viwango hivyo na Atamlipa kwavyo. Na Mola wako, ewe Mtume, Hakuwa ni Mwenye kughafilika na wanayoyafanya waja Wake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَرَبُّكَ ٱلۡغَنِيُّ ذُو ٱلرَّحۡمَةِۚ إِن يَشَأۡ يُذۡهِبۡكُمۡ وَيَسۡتَخۡلِفۡ مِنۢ بَعۡدِكُم مَّا يَشَآءُ كَمَآ أَنشَأَكُم مِّن ذُرِّيَّةِ قَوۡمٍ ءَاخَرِينَ
Na Mola wako, ewe Mtume, Aliyewaamrisha watu kumuabudu, Ndiye Mkwasi Peke Yake, na viumbe wote wanamhitajia Yeye. Na Yeye, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, Ndiye Mwenye rehema kunjufu. Na lau Alitaka Angaliwaangamiza na Akawaleta watu wengine wasiokuwa nyinyi watakaokuwa badala yenu baada ya kumalizika kwenu na watende matendo ya kumtii Yeye, Aliyetukuka, kama Alivyowaleta nyinyi kutokamana na kizazi cha watu wengine waliokuwako kabla yenu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
إِنَّ مَا تُوعَدُونَ لَأٓتٖۖ وَمَآ أَنتُم بِمُعۡجِزِينَ
Hakika yale mateso ambayo Anawaahidi nayo Mola wenu, enyi washirikina, kwa ukafiri wenu, ni yenye kuwapata. Na hamutamlemea Mola wenu kwa kumkimbia. Kwani Yeye ana uwezo wa kuwarudisha, hata kama mtakuwa mumegeuka mumekuwa mchanga na mifupa.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ يَٰقَوۡمِ ٱعۡمَلُواْ عَلَىٰ مَكَانَتِكُمۡ إِنِّي عَامِلٞۖ فَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَ مَن تَكُونُ لَهُۥ عَٰقِبَةُ ٱلدَّارِۚ إِنَّهُۥ لَا يُفۡلِحُ ٱلظَّٰلِمُونَ
Sema, ewe Mtume, «Enyi watu wangu, fanyeni kwa njia yenu, na mimi nitafanya kwa njia yangu ambayo Mola wangu, Aliyetukuka na kuwa juu, Aliniwekea. Mtakuja kujua, pindi mateso yatakapowashukia, ni nani atakayekuwa na mwisho mwema?» Hakika hatafaulu kupata radhi za Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na Pepo yule aliyekiuka mpaka Wake na akadhulumu, na akamshirikisha pamoja na Mwenyezi Mungu asiyekuwa Yeye.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَجَعَلُواْ لِلَّهِ مِمَّا ذَرَأَ مِنَ ٱلۡحَرۡثِ وَٱلۡأَنۡعَٰمِ نَصِيبٗا فَقَالُواْ هَٰذَا لِلَّهِ بِزَعۡمِهِمۡ وَهَٰذَا لِشُرَكَآئِنَاۖ فَمَا كَانَ لِشُرَكَآئِهِمۡ فَلَا يَصِلُ إِلَى ٱللَّهِۖ وَمَا كَانَ لِلَّهِ فَهُوَ يَصِلُ إِلَىٰ شُرَكَآئِهِمۡۗ سَآءَ مَا يَحۡكُمُونَ
Na wale wenye kumshirikisha Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, waliziweka kando sehemu ya vitu Alivyoviumba miongoni mwa mazao, matunda na wanyama howa wakawapatia wageni na maskini; na wakaziweka kando sehemu nyingine za vitu hivi kwa washirika wao, miongoni mwa masanamu na mizimu. Basi zile zilizotengewa washirika wao zafikishwa kwao peke yao, na hazifiki kwa Mwenyezi Mungu; na zile zilizotengewa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, zinafika kwa washirika wao. Ni mbaya ulioje uaumuzi wa hao watu na kigawanyo chao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَكَذَٰلِكَ زَيَّنَ لِكَثِيرٖ مِّنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ قَتۡلَ أَوۡلَٰدِهِمۡ شُرَكَآؤُهُمۡ لِيُرۡدُوهُمۡ وَلِيَلۡبِسُواْ عَلَيۡهِمۡ دِينَهُمۡۖ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ مَا فَعَلُوهُۖ فَذَرۡهُمۡ وَمَا يَفۡتَرُونَ
Na kama ambavyo mashetani waliwapambia washirikina wamtengee Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, katika mazao na wanyama howa, fungu maalumu na fungu kwa washirika wao, vilevile mashetani wamewapambia wengi kati ya washirikina kuwaua watoto wao kwa kuchelea ufukara, ili wawaingize wazazi hawa kwenye maangamivu kwa kuziua nafsi ambazo Mwenyezi Mungu Ameharamisha kuuliwa isipokuwa kwa haki, na ili wawavurugie dini yao iwachanganyikie wapate kupotea na waangamie. Na lau Angalitaka Mwenyezi Mungu wasiifanye hilo hawangalilifanya, lakini Yeye Amelikadiria liwe kwa kujua Kwake uovu wa hali yao na marejeo yao. Basi waache, ewe Mtume, na mambo yao, katika yale ya urongo wanayoyazua , na Mwenyezi Mungu Atahukumu baina yako na wao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَقَالُواْ هَٰذِهِۦٓ أَنۡعَٰمٞ وَحَرۡثٌ حِجۡرٞ لَّا يَطۡعَمُهَآ إِلَّا مَن نَّشَآءُ بِزَعۡمِهِمۡ وَأَنۡعَٰمٌ حُرِّمَتۡ ظُهُورُهَا وَأَنۡعَٰمٞ لَّا يَذۡكُرُونَ ٱسۡمَ ٱللَّهِ عَلَيۡهَا ٱفۡتِرَآءً عَلَيۡهِۚ سَيَجۡزِيهِم بِمَا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ
Na walisema washirikina kwamba ngamia hawa na makulima haya ni vitu haramu; haifai kuvila kwa mtu yoyote isipokuwa yule wanayemruhusu, kulingana na madai yao, miongoni mwa wasimamizi wa mizimu na wengineo. Na hawa ni ngamia ambao ilipewa heshima migongo yao, haifai kupandwa wala kubebeshwa vitu juu yake kwa namana yoyote. Na hawa ni ngamia ambao hawawatajii jina la Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, katika jambo lolote linalowahusu wao.Waliyafanya hayo kwa urongo utokao kwao, kumzulia Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu Atawalipa kwa urongo waliokuwa wakimzulia Yeye, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَقَالُواْ مَا فِي بُطُونِ هَٰذِهِ ٱلۡأَنۡعَٰمِ خَالِصَةٞ لِّذُكُورِنَا وَمُحَرَّمٌ عَلَىٰٓ أَزۡوَٰجِنَاۖ وَإِن يَكُن مَّيۡتَةٗ فَهُمۡ فِيهِ شُرَكَآءُۚ سَيَجۡزِيهِمۡ وَصۡفَهُمۡۚ إِنَّهُۥ حَكِيمٌ عَلِيمٞ
Na walisema washirikina, «Watoto waliyomo ndani ya wanyama howa, wakizaliwa wakiwa hai, ni halali tu kwa wanaume kati yetu na ni haramu kwa wanawake miongoni mwetu.» Na wakizaliwa nao wamekufa wanashirikiana katika kuwatumia. Mwenyezi Mungu Atawatesa kwa kujiwekea sheria za kuhalalisha na kuharamisha ambazo Mwenyezi Mungu hakuziruhusu. Hakika Yeye Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, ni Mwingi wa hekima katika uendeshaji Wake mambo ya viumbe Wake, Mjuzi sana kuhusu wao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قَدۡ خَسِرَ ٱلَّذِينَ قَتَلُوٓاْ أَوۡلَٰدَهُمۡ سَفَهَۢا بِغَيۡرِ عِلۡمٖ وَحَرَّمُواْ مَا رَزَقَهُمُ ٱللَّهُ ٱفۡتِرَآءً عَلَى ٱللَّهِۚ قَدۡ ضَلُّواْ وَمَا كَانُواْ مُهۡتَدِينَ
Hakika wamepata hasara na wameangamia wale ambao, kwa udhaifu wa akili zao na kwa ujinga wao, waliwaua watoto wao na wakaziharamisha, kwa kumzulia Mwenyezi Mungu urongo, zile Alizowaruzuku. Wako mabali na haki na hawakuwa ni miongoni mwa watu wa uongofu na muelekeo wa sawa. Kuhalalisha na kuharamisha ni miongoni mwa mambo mahususi ya uungu katika uwekaji sheria. Halali ni Aliyoihalalisha Mwenyezi Mungu, na haramu ni Aliyoiharamisha Mwenyezi Mungu. Na haipasii kwa yoyote kati ya viumbe wake, awe mmoja au kundi, kuwaekea sheria waja Wake ambayo Mwenyezi Mungu Hakuidhinisha.
Tefsiri na arapskom jeziku:
۞ وَهُوَ ٱلَّذِيٓ أَنشَأَ جَنَّٰتٖ مَّعۡرُوشَٰتٖ وَغَيۡرَ مَعۡرُوشَٰتٖ وَٱلنَّخۡلَ وَٱلزَّرۡعَ مُخۡتَلِفًا أُكُلُهُۥ وَٱلزَّيۡتُونَ وَٱلرُّمَّانَ مُتَشَٰبِهٗا وَغَيۡرَ مُتَشَٰبِهٖۚ كُلُواْ مِن ثَمَرِهِۦٓ إِذَآ أَثۡمَرَ وَءَاتُواْ حَقَّهُۥ يَوۡمَ حَصَادِهِۦۖ وَلَا تُسۡرِفُوٓاْۚ إِنَّهُۥ لَا يُحِبُّ ٱلۡمُسۡرِفِينَ
Na Mwenyezi Mungu, kutkata na sifa za upungufu ni Kwake na kutukuka ni Kwake, Ndiye Aliyewaanzishia mashamba: miongoni mwa mimea yake kuna ile iliyoinuliwa juu ya ardhi na kuegemezewa vitu vyingine, kama mizabibu, na miongoni mwayo kuna isiyoinuliwa, bali inasimama yenyewe kwenye vigogo vyake, kama mitende na miti mingine ya mazao. Mimea yote hiyo ikiwa ina tamu tafauti. Mizabibu na mikomamanga, maumbile yake yanafanana na matunda yake yanatafautiana tamu yake. Kuleni, enyi watu, matunda yake na mtoe Zaka zake zilizolazimishwa kwenu siku mnapoyavuna na kuyatungua, na msiikiuke mipaka ya usawa katika kutoa mali na kula chakula na mengineyo. Hakika Yeye, Mwenyezi Mungu, Hawapendi wenye kukiuka mipaka Yake kwa kutumia mali katika njia zisokuwa zake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمِنَ ٱلۡأَنۡعَٰمِ حَمُولَةٗ وَفَرۡشٗاۚ كُلُواْ مِمَّا رَزَقَكُمُ ٱللَّهُ وَلَا تَتَّبِعُواْ خُطُوَٰتِ ٱلشَّيۡطَٰنِۚ إِنَّهُۥ لَكُمۡ عَدُوّٞ مُّبِينٞ
Na Ameleta katika wanyama wale ambao wametayarishwa kwa kubebeshwa kwa kuwa ni wakubwa na ni warefu, kama ngamia. Na miongoni mwao kuna waliotayarishwa si kwa kubebeshwa kwa kuwa ni wadogo na wafupi, kama ng’ombe, mbuzi na kondoo. Kuleni wale Aliyowahalalishia nyinyi Mwenyezi Mungu miongoni mwa hawa wanyama, wala msiwaharamishe wale Aliyowahalalisha miongoni mwao kwa kufuata njia za Shetani kama walivyofanya washirikina. Hakika Shetani, kwenu nyinyi, ni adui mwenye uadui wa wazi.
Tefsiri na arapskom jeziku:
ثَمَٰنِيَةَ أَزۡوَٰجٖۖ مِّنَ ٱلضَّأۡنِ ٱثۡنَيۡنِ وَمِنَ ٱلۡمَعۡزِ ٱثۡنَيۡنِۗ قُلۡ ءَآلذَّكَرَيۡنِ حَرَّمَ أَمِ ٱلۡأُنثَيَيۡنِ أَمَّا ٱشۡتَمَلَتۡ عَلَيۡهِ أَرۡحَامُ ٱلۡأُنثَيَيۡنِۖ نَبِّـُٔونِي بِعِلۡمٍ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
Wanyama hawa ambao Mwenyezi Mungu Amewaruzuku waja Wake, miongoni mwa ngamia, ng’ombe, mbuzi na kondoo, ni aina nane: nne kati ya hizo ni mbuzi na kondoo, nao ni kondoo: waume na wake, na mbuzi: wume na wake. Sema, ewe Mtume, uwaambie hao washirikina, «Kwani Mwenyezi Mungu Amewaharamisha madume wawili wa mbuzi na kondoo?» Wakisema, «Ndio», watakuwa wamesema urongo kuhusu hilo. Sababu wao hawalifanyi kila dume la kondoo na mbuzi kuwa ni haramu. Na waambie, «Kwani Mwenyezi Mungu Amewaharamisha majike wawili wa mbuzi na kondoo?» wakisema, «Ndio», watakuwa pia wamesema urongo. Sababu wao hawamuharamishi kila mwanambuzi na mwanakondoo mke. Na sema uwaambie, «Kwani Mwenyezi Mungu Amewaharamisha watoto walio matumboni mwa majike wawili wa mbuzi na kondoo walio na mimba?» Wakisema, «Ndio.» Watakuwa wamesema urongo pia. Kwani hawaiharamishi kila mimba ya namna hiyo. Nambieni kwa misingi ya elimu inayoonesha usahihi wa msimamo wenu, mkiwa ni wakweli katika hayo mnayoyanasibisha kwa Mola wenu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمِنَ ٱلۡإِبِلِ ٱثۡنَيۡنِ وَمِنَ ٱلۡبَقَرِ ٱثۡنَيۡنِۗ قُلۡ ءَآلذَّكَرَيۡنِ حَرَّمَ أَمِ ٱلۡأُنثَيَيۡنِ أَمَّا ٱشۡتَمَلَتۡ عَلَيۡهِ أَرۡحَامُ ٱلۡأُنثَيَيۡنِۖ أَمۡ كُنتُمۡ شُهَدَآءَ إِذۡ وَصَّىٰكُمُ ٱللَّهُ بِهَٰذَاۚ فَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبٗا لِّيُضِلَّ ٱلنَّاسَ بِغَيۡرِ عِلۡمٍۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّٰلِمِينَ
Na aina nne nyingine ni aina mbili za ngamia, waume na wake, na aina mbili za ng’ombe, waume na wake. Sema, ewe Mtume, kuwaambia washirikina hao, «Kwani Mwenyezi Mungu Amewaharamisha madume wawili au majike wawili? Au Ameharamisha vilivyomo ndani ya matumbo ya majike wawili, wawe madume au majike? Au mlikuwa, enyi washirikina, mupo pindi Mwanyezi Mungu Alipowapa wasia wa uharamu huu wa wanyama howa? Hakuna dhalimu mbaya zaidi kuliko yule aliyemzulia Mwenyezi Mungu urongo, ili awapotoshe watu, kwa ujinga wake, na njia ya uongofu. Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Hamuelekezi kwenye muelekeo wa sawa yule aliyekiuka mpaka wake, akamzulia urongo Mola wake na akawapoteza watu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُل لَّآ أَجِدُ فِي مَآ أُوحِيَ إِلَيَّ مُحَرَّمًا عَلَىٰ طَاعِمٖ يَطۡعَمُهُۥٓ إِلَّآ أَن يَكُونَ مَيۡتَةً أَوۡ دَمٗا مَّسۡفُوحًا أَوۡ لَحۡمَ خِنزِيرٖ فَإِنَّهُۥ رِجۡسٌ أَوۡ فِسۡقًا أُهِلَّ لِغَيۡرِ ٱللَّهِ بِهِۦۚ فَمَنِ ٱضۡطُرَّ غَيۡرَ بَاغٖ وَلَا عَادٖ فَإِنَّ رَبَّكَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Sema, ewe Mtume, mimi sipati, kati ya yale aliyoniletea wahyi Mwenyezi Mungu, kitu kilicho haramu kwa mwenye kukila, kati ya vile mnavyovitaja kwamba vimeharamishwa miongoni mwa wanyama howa, isipokuwa awe amekufa bila kuchinjwa, au ni damu itiririkayo, au iwe ni nyama ya nguruwe, kwani hiyo ni najisi, au akawa ni mnyama ambaye kuchinjwa kwake kumetoka nje ya utiifu wa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, kama akiwa mnyama aliyechinjwa ametajiwa jina la asiyekuwa Mwenyezi Mungu, wakati wa kuchinjwa. Basi mwenye kulazimika kula chochote kati ya hizo zilizoharamishwa kwa dharura ya njaa kali, pasi na kutaka kujifurahisha wala kukiuka mpaka wa dharura, hakika Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, ni mwenye kumsamehe, ni mwenye huruma naye. Na hakika imethibiti, baadaye, kwa mafundisho ya Mtume kuwa ni haramu kula kila mnyama mwitu anayewinda kwa kutumia meno, kila ndege anayewinda kwa kutumia kucha, punda na mbwa.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَعَلَى ٱلَّذِينَ هَادُواْ حَرَّمۡنَا كُلَّ ذِي ظُفُرٖۖ وَمِنَ ٱلۡبَقَرِ وَٱلۡغَنَمِ حَرَّمۡنَا عَلَيۡهِمۡ شُحُومَهُمَآ إِلَّا مَا حَمَلَتۡ ظُهُورُهُمَآ أَوِ ٱلۡحَوَايَآ أَوۡ مَا ٱخۡتَلَطَ بِعَظۡمٖۚ ذَٰلِكَ جَزَيۡنَٰهُم بِبَغۡيِهِمۡۖ وَإِنَّا لَصَٰدِقُونَ
Na watajie washirikina hawa, ewe Mtume, wanyama na ndege tuliowaharamishia Mayahudi: nao ni kila ambaye hana pasuko vidoleni mwake, kama ngamia na mbuni, na mafuta ya ng’ombe, mbuzi na kondoo isipokuwa yale mafuta yaliyoshikana na migongo ya wanyama hao na tumbo zao, au yaliyoshikana na mfupa wa mkia na mbavu na mfano wake. Uharamishaji huu uliotajwa juu ya Mayahudi ni adhabu kutoka kwetu kwa sababu ya matendo yao maovu. Na sisi ni wakweli kwa yale tuliyoyaeleza kuhusu wao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَإِن كَذَّبُوكَ فَقُل رَّبُّكُمۡ ذُو رَحۡمَةٖ وَٰسِعَةٖ وَلَا يُرَدُّ بَأۡسُهُۥ عَنِ ٱلۡقَوۡمِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ
Na wakikufanya mrongo, ewe Mtume, wanaokwenda kinyume na wewe miongoni mwa washirikina, Mayahudi na wengineo, waambie, «Mola wenu, Aliyetukuka na kuwa juu, ni Mwenye rehema kunjufu. Na wala haiyepushwi adhabu Yake kwa watu walitenda maovu wakapata madhambi na wakajitokeza wazi na ubaya. Katika haya pana onyo kwao, kwa kwenda kwao kinyume na Mtume , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Tefsiri na arapskom jeziku:
سَيَقُولُ ٱلَّذِينَ أَشۡرَكُواْ لَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ مَآ أَشۡرَكۡنَا وَلَآ ءَابَآؤُنَا وَلَا حَرَّمۡنَا مِن شَيۡءٖۚ كَذَٰلِكَ كَذَّبَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ حَتَّىٰ ذَاقُواْ بَأۡسَنَاۗ قُلۡ هَلۡ عِندَكُم مِّنۡ عِلۡمٖ فَتُخۡرِجُوهُ لَنَآۖ إِن تَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَإِنۡ أَنتُمۡ إِلَّا تَخۡرُصُونَ
Watasema wale walioshirikisha, «Lau Mwenyezi Mungu Alitaka tusishirikishe, sisi na baba zetu, na tusihararamishe kitu chochote kinyume na matakwa Yake, hatungalifanya hilo.» Hapo Mwenyezi Mungu Aliwarudi kwa kuwaeleza kwamba utata huu ulivumishwa na makafiri kabla yao, wakautumia kuukanusha ulinganizi wa Mitume wao na wakaendelea kufanya hivyo mpaka ikawateremkia adhabu ya Mwenyezi Mungu. Waambie, ewe Mtume, «Je, mnayo elimu sahihi mtuoneshe, juu ya wanyama howa na makulima mliyoharamisha na juu ya madai yenu kwamba Mwenyezi Mungu Aliwatakia ukafiri, Akauridhia kwenu na Akaupendelea kwenu? Hamuna mnachofuata, katika mambo ya dini, isipokuwa dhana tu; na hamukuwa nyinyi isipokuwa mnasema urongo.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ فَلِلَّهِ ٱلۡحُجَّةُ ٱلۡبَٰلِغَةُۖ فَلَوۡ شَآءَ لَهَدَىٰكُمۡ أَجۡمَعِينَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia wao, «Mwenyezi Mungu, Alietukuka na kuwa juu, Ndiye Mwenye hoja ya mkato, yenye kuzikata dhana zenu. Na lau Alitaka Angaliwaongoza nyote kwenye muelekeo wa sawa.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ هَلُمَّ شُهَدَآءَكُمُ ٱلَّذِينَ يَشۡهَدُونَ أَنَّ ٱللَّهَ حَرَّمَ هَٰذَاۖ فَإِن شَهِدُواْ فَلَا تَشۡهَدۡ مَعَهُمۡۚ وَلَا تَتَّبِعۡ أَهۡوَآءَ ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا وَٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ وَهُم بِرَبِّهِمۡ يَعۡدِلُونَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Waleteni mashahidi wenu ambao watatoa ushahidi kwamba Mwenyezi Mungu Ndiye Aliyeharamisha vile mlivyoviharamisha vya makulima na wanyama howa.» Wakitoa ushahidi huo, kwa urongo na uzushi, usiwaamini wala usikubaliane na wale waliojitolea uamuzi wenyewe kulingana na mapendeleo ya nafsi zao, wakazikanusha aya za Mwenyezi Mungu katika yale waliyoyashikilia ya kukiharamisha Alichokihalalisha Mwenyezi Mungu na kukihalalisha Alichokiharamisha Mwenyezi Mungu. Wala usiwafuate wale ambao hawayaamini maisha ya Akhera wala wasiotenda vitendo vya kuwafaa huko na wale ambao Mola wao wanamshirikisha wakawa wanamuabudu mwingine pamoja na Yeye.
Tefsiri na arapskom jeziku:
۞ قُلۡ تَعَالَوۡاْ أَتۡلُ مَا حَرَّمَ رَبُّكُمۡ عَلَيۡكُمۡۖ أَلَّا تُشۡرِكُواْ بِهِۦ شَيۡـٔٗاۖ وَبِٱلۡوَٰلِدَيۡنِ إِحۡسَٰنٗاۖ وَلَا تَقۡتُلُوٓاْ أَوۡلَٰدَكُم مِّنۡ إِمۡلَٰقٖ نَّحۡنُ نَرۡزُقُكُمۡ وَإِيَّاهُمۡۖ وَلَا تَقۡرَبُواْ ٱلۡفَوَٰحِشَ مَا ظَهَرَ مِنۡهَا وَمَا بَطَنَۖ وَلَا تَقۡتُلُواْ ٱلنَّفۡسَ ٱلَّتِي حَرَّمَ ٱللَّهُ إِلَّا بِٱلۡحَقِّۚ ذَٰلِكُمۡ وَصَّىٰكُم بِهِۦ لَعَلَّكُمۡ تَعۡقِلُونَ
Waambie, ewe Mtume, «Njooni niwasomee Yale Aliyoyaharamishia Mwenyezi Mungu: Msishirikishe pamoja na Mwenyezi Mungu kitu chochote, miongoni mwa viumbe Vyake katika kumuabudu Yeye; bali zielekezeni aina zote za ibada Kwake Yeye Peke Yake, kama kucha, kutaraji, kuomba na megineyo. Muwafanyie wema wazazi wawili kwa kuwasaidia, kuwaombea Mungu na mengineyo ya wema kama hayo Msiwaue watoto wenu kwa sababu ya ufukara uliowshukia, kwani Mwenyezi Mungu Anawaruzuku nyinyi na wao. Wala msiyasongelee madhambi makubwa yaliyo wazi na yaliyofichika. Na msiiue nafsi ambayo Mwenyezi Mungu Ameharamisha kuuawa, isipokuwa kwa njia ya haki, nayo ni kuchukuliwa kisasi kwa aliyeua, au kwa uzinifu baada ya kuoa au kuolewa, au kuacha Uislamu. Hayo yaliyotajwa ni miongoni mwa yale ambayo Mwenyezi Mungu Amewkataza nayo na Akawapa maagizo muyaepuke na ni miongoni mwa yale Aliyowaamrisha nyinyi kwayo. Amweausia nayo Mola wenu ili mupate kuyaitia akilini maamrisho Yake na Makatazo Yake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَلَا تَقۡرَبُواْ مَالَ ٱلۡيَتِيمِ إِلَّا بِٱلَّتِي هِيَ أَحۡسَنُ حَتَّىٰ يَبۡلُغَ أَشُدَّهُۥۚ وَأَوۡفُواْ ٱلۡكَيۡلَ وَٱلۡمِيزَانَ بِٱلۡقِسۡطِۖ لَا نُكَلِّفُ نَفۡسًا إِلَّا وُسۡعَهَاۖ وَإِذَا قُلۡتُمۡ فَٱعۡدِلُواْ وَلَوۡ كَانَ ذَا قُرۡبَىٰۖ وَبِعَهۡدِ ٱللَّهِ أَوۡفُواْۚ ذَٰلِكُمۡ وَصَّىٰكُم بِهِۦ لَعَلَّكُمۡ تَذَكَّرُونَ
«Wala msiyasogelee, enyi wasimamizi, mali ya yatima isipokuwa kwa namana ya kuyatengeneza na kuyafanya yenye faida, mpaka atakapofikia myaka ya kubaleghe na awe mwangalifu. Na pindi afikiapo umri huo, mpeni mali yake. Na tekelezeni vipimo na mizani kwa usawa kwa namna ambayo utekelezaji utakuwa umefanyika kwa ukamilifu. Na mtakapojibidiisha uwezo wenu, hapana ubaya kwenu katika yale ambayo huenda yakawa na upungufu upande wenu. Kwani hatumlazimishi mtu isipokuwa uwezo wake. Na msemapo, basi jitahidini katika maneno yenu kuchunga usawa pasi na kupotoka kwenye haki kwenye utoaji habari au ushahidi au hukumu au kwenye uombezi, hata kama yule ambaye neno hilo linamuhusu yeye ana ujamaa na nyinyi, msilemee upande wake bila ya haki. Na tekelezeni yale aliyowaagiza mufanye ya kujilazimisha na sheria Yake. Hukumu hizo mlizosomewa, Mola wenu Amewausia mzifuate kwa matarajio kwmba mkumbuke mwisho wa mambo yenu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَأَنَّ هَٰذَا صِرَٰطِي مُسۡتَقِيمٗا فَٱتَّبِعُوهُۖ وَلَا تَتَّبِعُواْ ٱلسُّبُلَ فَتَفَرَّقَ بِكُمۡ عَن سَبِيلِهِۦۚ ذَٰلِكُمۡ وَصَّىٰكُم بِهِۦ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ
«Na miongoni mwa mambo aliyowausia Mwenyezi Mungu ni kwamba huu Uislamu ndio njia ya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, iliyolingana sawa. Basi ifuateni wala msifuate njia za upotevu zikawatawanya na kuwaepusha na njia ya Mwenyezi Mungu iliyolingana sawa. Muelekeo huo upande wa njia nyofu, ndio Aliowausia nao Mwenyzi Mungu ili mjikinge na adhabu Yake kwa kuyatekeleza maamrisho Yake na kijitenga na makatazo Yake.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
ثُمَّ ءَاتَيۡنَا مُوسَى ٱلۡكِتَٰبَ تَمَامًا عَلَى ٱلَّذِيٓ أَحۡسَنَ وَتَفۡصِيلٗا لِّكُلِّ شَيۡءٖ وَهُدٗى وَرَحۡمَةٗ لَّعَلَّهُم بِلِقَآءِ رَبِّهِمۡ يُؤۡمِنُونَ
Kisha sema, ewe Mtume, uwaambie hawa washirikina, «Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Ndiye Aliyempa Mūsā Taurati, kwa kuzitimiza neema Zake kwa watu wa mila yake wanaofanya wema, na kwa kufafanua kila kitu katika mambo ya dini yao, na kuwapa uongofu na muelekeo wa njia iliyolingana sawa, na kuwarehemu, kwa matumaini kuwa watakubali kwamba kuna kufufuliwa baada ya kufa na kuna hesabu na malipo, na hilo liwafanya watende mema.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَهَٰذَا كِتَٰبٌ أَنزَلۡنَٰهُ مُبَارَكٞ فَٱتَّبِعُوهُ وَٱتَّقُواْ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ
Na hii Qur’ani ni kitabu tulichokiteremsha kwa Nabii wetu Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie. Kheri yeke ni nyingi. Basi kifuateni kwa yale anayowaamrisha na kuwakataza. Na muogopeni Mwenyezi Mungu msije mkaenda kinyume na amri Yake yoyote, kwa matumaini kuwa mtarehemewa na mtaokolewa na adhabu Yake na mpate malipo Yake mema.
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَن تَقُولُوٓاْ إِنَّمَآ أُنزِلَ ٱلۡكِتَٰبُ عَلَىٰ طَآئِفَتَيۡنِ مِن قَبۡلِنَا وَإِن كُنَّا عَن دِرَاسَتِهِمۡ لَغَٰفِلِينَ
Na tumeiteremsha hii Qur’ani, ili msije mkasema, enyi makafiri wa Kiaarabu, «Hakika Kitabu kutoka mbinguni waliteremshiwa Mayahudi na Wanaswara; na sisi tuna mambo ya kutushughulisha kutowahi kuvisoma vitabu vyao; na sisi hatuna ujuzi navyo wala maarifa.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
أَوۡ تَقُولُواْ لَوۡ أَنَّآ أُنزِلَ عَلَيۡنَا ٱلۡكِتَٰبُ لَكُنَّآ أَهۡدَىٰ مِنۡهُمۡۚ فَقَدۡ جَآءَكُم بَيِّنَةٞ مِّن رَّبِّكُمۡ وَهُدٗى وَرَحۡمَةٞۚ فَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّن كَذَّبَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَصَدَفَ عَنۡهَاۗ سَنَجۡزِي ٱلَّذِينَ يَصۡدِفُونَ عَنۡ ءَايَٰتِنَا سُوٓءَ ٱلۡعَذَابِ بِمَا كَانُواْ يَصۡدِفُونَ
Na ili msije mkasema, enyi washirikina, «Lau kama sisi tuliteremshiwa kitabu kutoka mbinguni, kama walivyoteremshiwa Mayahudi na Wanaswara, tungalikuwa na muelekeo madhubuti sana kwenye njia ya haki kuliko wao.» Hakika kimewajia Kitabu kwa lugha ya Kiarabu chenye ufafanuzi. Na hiyo ni hoja iliyo wazi kutoka kwa Mola wenu, ni muongozo wa njia ya haki na ni rehema kwa umma huu. Na hapana yoyote mbaya wa dhuluma na uadui kuliko yule aliyezikanusha hoja za Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na akazipa mgongo. Basi hawa wenye kupa mgongo tutawatesa mateso makubwa kwenye Moto wa Jahanamu, kwa sababu ya kuzipa mgongo kwao aya zetu na kuzuia kwao njia zetu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
هَلۡ يَنظُرُونَ إِلَّآ أَن تَأۡتِيَهُمُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ أَوۡ يَأۡتِيَ رَبُّكَ أَوۡ يَأۡتِيَ بَعۡضُ ءَايَٰتِ رَبِّكَۗ يَوۡمَ يَأۡتِي بَعۡضُ ءَايَٰتِ رَبِّكَ لَا يَنفَعُ نَفۡسًا إِيمَٰنُهَا لَمۡ تَكُنۡ ءَامَنَتۡ مِن قَبۡلُ أَوۡ كَسَبَتۡ فِيٓ إِيمَٰنِهَا خَيۡرٗاۗ قُلِ ٱنتَظِرُوٓاْ إِنَّا مُنتَظِرُونَ
Kwani wanangojea, hawa wenye kukataa na wakazuia watu wasiifuate njia ya Mwenyezi Mungu, isipokuwa awajie wao Malaika wa mauti na wasaidizi wake kuzichukua roho zao au aje Mola wako, ewe Mtume, kutoa uamuzi kati ya waja wake Siku ya Kiyama, au zije baadhi ya alama za Kiyama na vitambulisho vyake vinavyoashiria kuja kwake, navyo ni kuchomoza jua kutoka upande wake wa Magharibi? Basi litakapokuwa hilo hakuna nafsi yoyote itakayofaidika na Imani yake, iwapo haikuwa imeamini kabla ya hapo, wala hayatakubaliwa matendo mema mapya ya hiyo nafsi, ikiwa ilikuwa imeamini, iwapo haikuwa imeyatenda kabla ya hapo. Waambie, ewe Mtume, «Ngojeeni kuja kwake, ili mpate kumjua aliye kwenye usawa na aliye kwenye makosa, na mtenda maovu na mtenda mema. Sisi tunalingojea hilo.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
إِنَّ ٱلَّذِينَ فَرَّقُواْ دِينَهُمۡ وَكَانُواْ شِيَعٗا لَّسۡتَ مِنۡهُمۡ فِي شَيۡءٍۚ إِنَّمَآ أَمۡرُهُمۡ إِلَى ٱللَّهِ ثُمَّ يُنَبِّئُهُم بِمَا كَانُواْ يَفۡعَلُونَ
Hakika wale walioigawanya dini yao, baada ya kuwa mkusanyiko mmoja juu ya kumpwekesha Mwenyezi Mungu na kufuata sheria Yake kivitendo, wakawa ni makundi na mapote, wewe, ewe Mtume, uko mbali na wao. Hukumu yao iko kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, kisha Yeye Atawapa habari za matendo yao, Amlipe aliyetubia miongoni mwao na akafanya wema, kwa wema wake na Amtese mtenda maovu kwa uovu wake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
مَن جَآءَ بِٱلۡحَسَنَةِ فَلَهُۥ عَشۡرُ أَمۡثَالِهَاۖ وَمَن جَآءَ بِٱلسَّيِّئَةِ فَلَا يُجۡزَىٰٓ إِلَّا مِثۡلَهَا وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ
Mwenye kukutana na Mola wake, Siku ya Kiyama, akiwa na jema moja miongoni mwa matendo mazuri, atapata mema mfano wake mara kumi. Na mwenye kukutana na Mola wake akiwa ana ovu moja, hatateswa isipokuwa kadiri ya mfano wa ovu hilo, na wao hawatadhulumiwa hata kiasi cha uzito wa chungu mdogo.
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ إِنَّنِي هَدَىٰنِي رَبِّيٓ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ دِينٗا قِيَمٗا مِّلَّةَ إِبۡرَٰهِيمَ حَنِيفٗاۚ وَمَا كَانَ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Mimi Ameniongoza Mola wangu kwenye njia iliyolingana sawa yenye kufikisha kwenye Pepo Yake, nayo ni Dini ya Uislamu yenye kusimamia mambo ya dunia na ya Akhera; nayo ni Dini ya kumpwekesha Mwenyezi Mungu, Dini ya Ibrāhīm, amani imshukiye. Na Ibrāhīm, amani imshukiye, hakuwa ni miongoni mwa wenye kumshirikisha pamoja na Mwenyezi Mungu asiyekuwa Yeye.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ إِنَّ صَلَاتِي وَنُسُكِي وَمَحۡيَايَ وَمَمَاتِي لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia hawa washirikina, «Hakika Swala yangu na nusuk yangu, yaani kuchinja kwangu ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, Peke Yake; si kwa ajili ya masanamu wala wafu wala majini wala wasiokuwa hao kati ya wale, wasiokuwa Mwenyezi Mungu, mnaowachinja na kutaja majina yasiyokua jina Lake, kama mnavyofanya.. Pia uhai wangu na kufa kwangu ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, Mola wa viumbe wote.
Tefsiri na arapskom jeziku:
لَا شَرِيكَ لَهُۥۖ وَبِذَٰلِكَ أُمِرۡتُ وَأَنَا۠ أَوَّلُ ٱلۡمُسۡلِمِينَ
«Asiye na mshirika katika uungu Wake wala katika uola Wake wala katika majina Yake na sifa Zake. Kumpwekesha huko Mwenyezi Mungu kulikosafishika ndiko Alikoniamrisha mimi Mola wangu, Aliyetukuka na kuwa juu. Na mimi ni wa kwanza kumfuata Mwenyezi Mungu kikamilifu katika umma huu.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
قُلۡ أَغَيۡرَ ٱللَّهِ أَبۡغِي رَبّٗا وَهُوَ رَبُّ كُلِّ شَيۡءٖۚ وَلَا تَكۡسِبُ كُلُّ نَفۡسٍ إِلَّا عَلَيۡهَاۚ وَلَا تَزِرُ وَازِرَةٞ وِزۡرَ أُخۡرَىٰۚ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّكُم مَّرۡجِعُكُمۡ فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ فِيهِ تَخۡتَلِفُونَ
Sema, ewe Mtume, «Kwani natafuta mola mwingine asiyekuwa Mwenyezi Mungu, na hali Yeye ni Muumba wa kila kitu, ni Mwenye kukimiliki na kukiendesha?» Na hafanyi Mwanadamu yoyote tendo baya isipokuwa dhambi zake zitamshukia mwenyewe, wala haitabeba, nafsi yenye dhambi, dhambi za nafsi nynigine. Kisha marejeo yenu ni kwa Mola wenu Siku ya Kiyama, awape habari ya yale mliokuwa mkitafautiana juu yake katika mambo ya dini.»
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَهُوَ ٱلَّذِي جَعَلَكُمۡ خَلَٰٓئِفَ ٱلۡأَرۡضِ وَرَفَعَ بَعۡضَكُمۡ فَوۡقَ بَعۡضٖ دَرَجَٰتٖ لِّيَبۡلُوَكُمۡ فِي مَآ ءَاتَىٰكُمۡۗ إِنَّ رَبَّكَ سَرِيعُ ٱلۡعِقَابِ وَإِنَّهُۥ لَغَفُورٞ رَّحِيمُۢ
Na Mwenyezi Mungu, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, Ndiye Aliyewafanya nyinyi mushike nafasi za waliowatangulia katika ardhi baada ya Mwenyezi Mungu kuwaondoa na kuwaweka nyinyi badala yao, mupate kuiamirisha baada yao kwa kumtii Mola wenu. Na amewainua daraja baadhi yenu, katika mapato na nguvu, juu ya wengine ili kuwapa mtihani katika alichowapa miongoni mwa neema Zake, apate kuwa wazi kwa watu mwenye kushukuru na asiyeshukuru. Hakika Mola wako ni Mwepesi wa adhabu kwa aliyemkanusha na kumuasi. Na Yeye ni Mwingi wa msamaha kwa aliyemuamini na akafaya matendo mema na akatubia na dhambi yenye kuangamiza, ni Mwenye huruma Kwake. Al-Ghafūr (Mwingi wa kusamehe)na Al-Raḥīm (Mwenye kurehemu) ni majina mawili matukufu katika majina ya Mwenyezi Mungu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
 
Prijevod značenja Sura: Sura el-En'am
Indeks sura Broj stranice
 
Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Sadržaj prijevodā

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Zatvaranje