Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman * - Translations’ Index


Translation of the meanings Surah: Al-Infitār   Ayah:

Surat Al-Infitar

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتۡ
Pindi mbingu zitakapopasuka na ukaharibika mpango wake.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَإِذَا ٱلۡكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتۡ
Na pindi nyota zitakapoangukiana.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ فُجِّرَتۡ
Na pindi Mwenyezi Mungu Atakapozifanya bahari kulipuka na maji yake kutoweka.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَإِذَا ٱلۡقُبُورُ بُعۡثِرَتۡ
Na pindi makaburi yatakapogeuzwa kwa kufufuliwa waliokuwamo ndani yake.
Arabic explanations of the Qur’an:
عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّا قَدَّمَتۡ وَأَخَّرَتۡ
Wakati huo itajua kila nafsi vitendo vyake vyote ilivyovifanya, vilivyotangulia na vilivyoahirika na italipwa kwa vitendo hivyo.
Arabic explanations of the Qur’an:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلۡكَرِيمِ
Ewe binadamu unayekanusha kufufuliwa! Ni kipi kilichokufanya uhadaike na ughurike kuhusu Mola wako Mpaji Mwenye kheri nyingi, Anayestahiki kushukuriwa na kutiiwa?
Arabic explanations of the Qur’an:
ٱلَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ
Kwani si Yeye Aliyekuumba, Akalisawazisha umbo lako, Akakuweka katika hali ya sawa na Akakurekibisha ili uweze kutekeleza nyadhifa zako,
Arabic explanations of the Qur’an:
فِيٓ أَيِّ صُورَةٖ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ
katika sura yoyote ile Aliyoitaka Akakuumba?
Arabic explanations of the Qur’an:
كَلَّا بَلۡ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ
Mambo hayako kama vile mnavyosema kwamba nyinyi mna haki ya kumuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Hesabu na Malipo.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَإِنَّ عَلَيۡكُمۡ لَحَٰفِظِينَ
Na mjue kuwa wako na nyinyi Malaika wachunguzi,
Arabic explanations of the Qur’an:
كِرَامٗا كَٰتِبِينَ
watukufu kwa Mwenyezi Mungu, waandishi wa yale waliyowakilishwa kuyadhibiti. Hakiwapiti, katika vitendo vyenu na siri zenu, chochote.
Arabic explanations of the Qur’an:
يَعۡلَمُونَ مَا تَفۡعَلُونَ
Wanayajua mnayoyafanya, ya kheri au ya shari.
Arabic explanations of the Qur’an:
إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٖ
Hakika wachamungu wanaotekeleza haki za Mwenyezi Mungu na haki za waja wake watakuwa kwenye neema.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَإِنَّ ٱلۡفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٖ
Hakika watu waovu waliopuuza haki za Mwenyezi Mungu na haki za waja wake watakuwa katika Moto mkali.
Arabic explanations of the Qur’an:
يَصۡلَوۡنَهَا يَوۡمَ ٱلدِّينِ
Ukali wake, Moto huo, utawapata Siku ya Malipo.Na wala wao hawatakuwa ni wenye kughibu,
Arabic explanations of the Qur’an:
وَمَا هُمۡ عَنۡهَا بِغَآئِبِينَ
wakawa hawamo ndani ya Moto wa Jahanamu, si kwa kutoka wala kwa kufa.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Ni kipi kinachokujuza ni upi utukufu wa Siku ya Hesabu?
Arabic explanations of the Qur’an:
ثُمَّ مَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Kisha ni kipi kinachokujuza ni upi utukufu wa Siku ya Hesabu?
Arabic explanations of the Qur’an:
يَوۡمَ لَا تَمۡلِكُ نَفۡسٞ لِّنَفۡسٖ شَيۡـٔٗاۖ وَٱلۡأَمۡرُ يَوۡمَئِذٖ لِّلَّهِ
Siku ya Hesabu, hataweza yoyote kumnufaisha yoyote. Na amri zote Siku Hiyo ni za Mwenyezi Mungu Peke yake Ambaye hakuna mwenye kumshinda, wala hakuna mwenye kumtendesha nguvu, wala hakuna mwenye kushindana na Yeye.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Surah: Al-Infitār
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

close