Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Abdullah Muhammad e Nasser Khamis * - Índice de tradução


Tradução dos significados Surah: Suratu Al-Infitar   Versículo:

Surat Al-Infitar

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتۡ
Pindi mbingu zitakapopasuka na ukaharibika mpango wake.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِذَا ٱلۡكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتۡ
Na pindi nyota zitakapoangukiana.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ فُجِّرَتۡ
Na pindi Mwenyezi Mungu Atakapozifanya bahari kulipuka na maji yake kutoweka.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِذَا ٱلۡقُبُورُ بُعۡثِرَتۡ
Na pindi makaburi yatakapogeuzwa kwa kufufuliwa waliokuwamo ndani yake.
Os Tafssir em língua árabe:
عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّا قَدَّمَتۡ وَأَخَّرَتۡ
Wakati huo itajua kila nafsi vitendo vyake vyote ilivyovifanya, vilivyotangulia na vilivyoahirika na italipwa kwa vitendo hivyo.
Os Tafssir em língua árabe:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلۡكَرِيمِ
Ewe binadamu unayekanusha kufufuliwa! Ni kipi kilichokufanya uhadaike na ughurike kuhusu Mola wako Mpaji Mwenye kheri nyingi, Anayestahiki kushukuriwa na kutiiwa?
Os Tafssir em língua árabe:
ٱلَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ
Kwani si Yeye Aliyekuumba, Akalisawazisha umbo lako, Akakuweka katika hali ya sawa na Akakurekibisha ili uweze kutekeleza nyadhifa zako,
Os Tafssir em língua árabe:
فِيٓ أَيِّ صُورَةٖ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ
katika sura yoyote ile Aliyoitaka Akakuumba?
Os Tafssir em língua árabe:
كَلَّا بَلۡ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ
Mambo hayako kama vile mnavyosema kwamba nyinyi mna haki ya kumuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Hesabu na Malipo.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِنَّ عَلَيۡكُمۡ لَحَٰفِظِينَ
Na mjue kuwa wako na nyinyi Malaika wachunguzi,
Os Tafssir em língua árabe:
كِرَامٗا كَٰتِبِينَ
watukufu kwa Mwenyezi Mungu, waandishi wa yale waliyowakilishwa kuyadhibiti. Hakiwapiti, katika vitendo vyenu na siri zenu, chochote.
Os Tafssir em língua árabe:
يَعۡلَمُونَ مَا تَفۡعَلُونَ
Wanayajua mnayoyafanya, ya kheri au ya shari.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٖ
Hakika wachamungu wanaotekeleza haki za Mwenyezi Mungu na haki za waja wake watakuwa kwenye neema.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِنَّ ٱلۡفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٖ
Hakika watu waovu waliopuuza haki za Mwenyezi Mungu na haki za waja wake watakuwa katika Moto mkali.
Os Tafssir em língua árabe:
يَصۡلَوۡنَهَا يَوۡمَ ٱلدِّينِ
Ukali wake, Moto huo, utawapata Siku ya Malipo.Na wala wao hawatakuwa ni wenye kughibu,
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَا هُمۡ عَنۡهَا بِغَآئِبِينَ
wakawa hawamo ndani ya Moto wa Jahanamu, si kwa kutoka wala kwa kufa.
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Ni kipi kinachokujuza ni upi utukufu wa Siku ya Hesabu?
Os Tafssir em língua árabe:
ثُمَّ مَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Kisha ni kipi kinachokujuza ni upi utukufu wa Siku ya Hesabu?
Os Tafssir em língua árabe:
يَوۡمَ لَا تَمۡلِكُ نَفۡسٞ لِّنَفۡسٖ شَيۡـٔٗاۖ وَٱلۡأَمۡرُ يَوۡمَئِذٖ لِّلَّهِ
Siku ya Hesabu, hataweza yoyote kumnufaisha yoyote. Na amri zote Siku Hiyo ni za Mwenyezi Mungu Peke yake Ambaye hakuna mwenye kumshinda, wala hakuna mwenye kumtendesha nguvu, wala hakuna mwenye kushindana na Yeye.
Os Tafssir em língua árabe:
 
Tradução dos significados Surah: Suratu Al-Infitar
Índice de capítulos Número de página
 
Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Abdullah Muhammad e Nasser Khamis - Índice de tradução

Tradução dos significados do Alcorão em suaíli pelo Dr. Abdalla Mohamed Abubakar e Nassor Khamis

Fechar