Traduction des sens du Noble Coran - Traduction en Swahili - 'AbdaLlah Muhammad et Nasser Khamîs * - Lexique des traductions


Traduction des sens Sourate: AL-INFITÂR   Verset:

Surat Al-Infitar

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتۡ
Pindi mbingu zitakapopasuka na ukaharibika mpango wake.
Les exégèses en arabe:
وَإِذَا ٱلۡكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتۡ
Na pindi nyota zitakapoangukiana.
Les exégèses en arabe:
وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ فُجِّرَتۡ
Na pindi Mwenyezi Mungu Atakapozifanya bahari kulipuka na maji yake kutoweka.
Les exégèses en arabe:
وَإِذَا ٱلۡقُبُورُ بُعۡثِرَتۡ
Na pindi makaburi yatakapogeuzwa kwa kufufuliwa waliokuwamo ndani yake.
Les exégèses en arabe:
عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّا قَدَّمَتۡ وَأَخَّرَتۡ
Wakati huo itajua kila nafsi vitendo vyake vyote ilivyovifanya, vilivyotangulia na vilivyoahirika na italipwa kwa vitendo hivyo.
Les exégèses en arabe:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلۡكَرِيمِ
Ewe binadamu unayekanusha kufufuliwa! Ni kipi kilichokufanya uhadaike na ughurike kuhusu Mola wako Mpaji Mwenye kheri nyingi, Anayestahiki kushukuriwa na kutiiwa?
Les exégèses en arabe:
ٱلَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ
Kwani si Yeye Aliyekuumba, Akalisawazisha umbo lako, Akakuweka katika hali ya sawa na Akakurekibisha ili uweze kutekeleza nyadhifa zako,
Les exégèses en arabe:
فِيٓ أَيِّ صُورَةٖ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ
katika sura yoyote ile Aliyoitaka Akakuumba?
Les exégèses en arabe:
كَلَّا بَلۡ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ
Mambo hayako kama vile mnavyosema kwamba nyinyi mna haki ya kumuabudu asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Hesabu na Malipo.
Les exégèses en arabe:
وَإِنَّ عَلَيۡكُمۡ لَحَٰفِظِينَ
Na mjue kuwa wako na nyinyi Malaika wachunguzi,
Les exégèses en arabe:
كِرَامٗا كَٰتِبِينَ
watukufu kwa Mwenyezi Mungu, waandishi wa yale waliyowakilishwa kuyadhibiti. Hakiwapiti, katika vitendo vyenu na siri zenu, chochote.
Les exégèses en arabe:
يَعۡلَمُونَ مَا تَفۡعَلُونَ
Wanayajua mnayoyafanya, ya kheri au ya shari.
Les exégèses en arabe:
إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٖ
Hakika wachamungu wanaotekeleza haki za Mwenyezi Mungu na haki za waja wake watakuwa kwenye neema.
Les exégèses en arabe:
وَإِنَّ ٱلۡفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٖ
Hakika watu waovu waliopuuza haki za Mwenyezi Mungu na haki za waja wake watakuwa katika Moto mkali.
Les exégèses en arabe:
يَصۡلَوۡنَهَا يَوۡمَ ٱلدِّينِ
Ukali wake, Moto huo, utawapata Siku ya Malipo.Na wala wao hawatakuwa ni wenye kughibu,
Les exégèses en arabe:
وَمَا هُمۡ عَنۡهَا بِغَآئِبِينَ
wakawa hawamo ndani ya Moto wa Jahanamu, si kwa kutoka wala kwa kufa.
Les exégèses en arabe:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Ni kipi kinachokujuza ni upi utukufu wa Siku ya Hesabu?
Les exégèses en arabe:
ثُمَّ مَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Kisha ni kipi kinachokujuza ni upi utukufu wa Siku ya Hesabu?
Les exégèses en arabe:
يَوۡمَ لَا تَمۡلِكُ نَفۡسٞ لِّنَفۡسٖ شَيۡـٔٗاۖ وَٱلۡأَمۡرُ يَوۡمَئِذٖ لِّلَّهِ
Siku ya Hesabu, hataweza yoyote kumnufaisha yoyote. Na amri zote Siku Hiyo ni za Mwenyezi Mungu Peke yake Ambaye hakuna mwenye kumshinda, wala hakuna mwenye kumtendesha nguvu, wala hakuna mwenye kushindana na Yeye.
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Sourate: AL-INFITÂR
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - Traduction en Swahili - 'AbdaLlah Muhammad et Nasser Khamîs - Lexique des traductions

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Fermeture