Check out the new design

Traduction des sens du Noble Coran - La traduction swahili - 'Abd Allah Muhammad et Nâsir Khamîs * - Lexique des traductions


Traduction des sens Sourate: Az Zukhruf   Verset:

Az-Zukhruf

حمٓ
“Hā, Mīm” maelezo yametangulia mwanzoni mwa sura ya Al-Baqarah juu ya herufi zilizokatwa na kutengwa.
Les exégèses en arabe:
وَٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ
Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Ameapa kwa Qur’ani ambayo matamshi yake na maana yake yako waziwazi.
Les exégèses en arabe:
إِنَّا جَعَلۡنَٰهُ قُرۡءَٰنًا عَرَبِيّٗا لَّعَلَّكُمۡ تَعۡقِلُونَ
Hakika sisi tumeiteremsha Qur’ani kwa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kwa lugha ya Kiarabu , huenda nyinyi mkaelewa na mkazingatia maana yake na hoja zake.
Les exégèses en arabe:
وَإِنَّهُۥ فِيٓ أُمِّ ٱلۡكِتَٰبِ لَدَيۡنَا لَعَلِيٌّ حَكِيمٌ
Nayo , kwa hakika, katika Ubao Uliohifadhiwa kwetu sisi ina cheo na heshima za juu, iko thabiti, haina tafauti ndani yake wala kugongana.
Les exégèses en arabe:
أَفَنَضۡرِبُ عَنكُمُ ٱلذِّكۡرَ صَفۡحًا أَن كُنتُمۡ قَوۡمٗا مُّسۡرِفِينَ
Je tuwape nyinyi mgongo na tuache kuwateremshia Qur’ani kwa ajili ya kupuuza kwenu, kutofuata na kupita mipaka kwenu katika kukataa kuiamini?
Les exégèses en arabe:
وَكَمۡ أَرۡسَلۡنَا مِن نَّبِيّٖ فِي ٱلۡأَوَّلِينَ
Tumewatumiliza Manabii wengi katika kame za mwanzo zilizopita kabla ya watu wako, ewe Nabii.
Les exégèses en arabe:
وَمَا يَأۡتِيهِم مِّن نَّبِيٍّ إِلَّا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ
Hawajiwi na Nabii yoyote isipokuwa huwa wakimcheza shere kama vile watu wako walivyokucheza shere, basi tukawaangamiza wale waliowakanusha Mitume wetu, nao walikuwa ni wenye nguvu kali na ushujaa wa kivita kuliko watu wako, ewe Mtume.
Les exégèses en arabe:
فَأَهۡلَكۡنَآ أَشَدَّ مِنۡهُم بَطۡشٗا وَمَضَىٰ مَثَلُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Na yashapita mateso ya wa mwanzo kwa kuangamizwa kwa sababu ya ukanushaji wao, ujeuri wao na kuwacheza shere Mitume wao. Katika haya pana maliwazo kwa Nabii, rehema na amani zimshukie.
Les exégèses en arabe:
وَلَئِن سَأَلۡتَهُم مَّنۡ خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ لَيَقُولُنَّ خَلَقَهُنَّ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡعَلِيمُ
Na unapowauliza, ewe Mtume, hawa washirikina miongoni mwa watu wako, «Ni nani aliyeumba mbingu na ardhi? Wanasema , «Aliyeziumba ni Yule Aliye Mshindi katika mamlaka Yake, Aliye Mjuzi wa hizo na vitu vilivyomo ndani yake, hakuna chochote kinachofichamana Kwake.
Les exégèses en arabe:
ٱلَّذِي جَعَلَ لَكُمُ ٱلۡأَرۡضَ مَهۡدٗا وَجَعَلَ لَكُمۡ فِيهَا سُبُلٗا لَّعَلَّكُمۡ تَهۡتَدُونَ
Aliyewafanyia ardhi kuwa ni (kama) tandiko na mkeka, Akawasahilishia humo njia za maisha yenu na biashara zenu, ili mjiongoze kwa njia hizo kwenye maslahi yenu ya kidini na ya kidunia.
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Sourate: Az Zukhruf
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - La traduction swahili - 'Abd Allah Muhammad et Nâsir Khamîs - Lexique des traductions

Traduit par le Dr. 'Abd Allah Muhammad Abû Bakr et Cheikh Nâsir Khamîs.

Fermeture