Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani * - Lexique des traductions

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduction des sens Verset: (31) Sourate: YOUNOUS
قُلۡ مَن يَرۡزُقُكُم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ وَٱلۡأَرۡضِ أَمَّن يَمۡلِكُ ٱلسَّمۡعَ وَٱلۡأَبۡصَٰرَ وَمَن يُخۡرِجُ ٱلۡحَيَّ مِنَ ٱلۡمَيِّتِ وَيُخۡرِجُ ٱلۡمَيِّتَ مِنَ ٱلۡحَيِّ وَمَن يُدَبِّرُ ٱلۡأَمۡرَۚ فَسَيَقُولُونَ ٱللَّهُۚ فَقُلۡ أَفَلَا تَتَّقُونَ
Sema: Ni nani anaye kuruzukuni kutoka mbinguni na kwenye ardhi? Au ni nani anaye miliki kusikia na kuona? Na nani amtoaye hai kutoka maiti, na akamtoa maiti kutoka aliye hai? Na nani anaye yadabiri mambo yote? Watasema:Allah, Mwenyezi Mungu. Basi sema: Je! Hamchi?
Ewe Mtume! Lingania kwenye Tawhidi safi, na useme: Nani anaye kuleteeni riziki kutoka mbinguni inapo teremka mvua, na katika ardhi inapo mea mimea na kuzaa? Na nani aliye kupeni kusikia na kuona? Na nani anaye toa vilio hai kutokana na vilio maiti, kama mimea, nayo ni hai kutokana na ardhi maiti? Nani anaye mtoa maiti kutokana na hai, kama mtu anavyo kufa? Na nani anaye panga na kuendesha mambo yote ya ulimwengu kwa kudra yake na hikima yake? Wataungama: Hapana pa kukimbilia! Kwa hakika ni Mwenyezi Mungu peke yake ndiye mtenda yote. Ewe Mtume! Waambie watapo ungama: Si waajibu mkubwa kuit'ii Haki, na kumkhofu Mwenyezi Mungu, Mmiliki Ufalme wote?
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Verset: (31) Sourate: YOUNOUS
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani - Lexique des traductions

Traduction des sens du noble Coran en langue Swahili, par Ali Muhsin al-Barwani.

Fermeture