Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani * - Lexique des traductions

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduction des sens Verset: (20) Sourate: AL ‘IMRÂN
فَإِنۡ حَآجُّوكَ فَقُلۡ أَسۡلَمۡتُ وَجۡهِيَ لِلَّهِ وَمَنِ ٱتَّبَعَنِۗ وَقُل لِّلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡأُمِّيِّـۧنَ ءَأَسۡلَمۡتُمۡۚ فَإِنۡ أَسۡلَمُواْ فَقَدِ ٱهۡتَدَواْۖ وَّإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّمَا عَلَيۡكَ ٱلۡبَلَٰغُۗ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِٱلۡعِبَادِ
Na pindi wakikuhoji, basi sema: Mimi nimeusalimisha uso wangu kumwelekea Mwenyezi Mungu, na kadhaalika walio nifuata. Na waambie walio pewa Kitabu na wasio na kisomo: Je! Mmesilimu? Wakisilimu basi wameongoka. Na wakikengeuka basi juu yako ni kufikisha ujumbe tu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaona waja wake.
Na hawa makafiri wakijadiliana nawe katika Dini hii baada ya wewe kuwapa hoja zote, huna haja kupigizana nao kelele kwa majadiliano. Waambie tu: Mimi na Waumini walio nifuata tumemsafia Mwenyezi Mungu peke yake ibada yetu. Na waambie Mayahudi na Wakristo na washirikina wa Kiarabu: Dalili zimekwisha bainika kwenu, basi silimuni. Wakisilimu inakuwa wameijua njia ya uwongofu na wameifuata. Na wakikataa huna lawama wewe kwa kukataa kwao. Waajibu wako ni kufikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu tu. Na Mwenyezi Mungu anawajua vyema waja wake. Hapana lolote lao, hali yao na vitendo vyao, linalo fichikana kwake.
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Verset: (20) Sourate: AL ‘IMRÂN
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani - Lexique des traductions

Traduction des sens du noble Coran en langue Swahili, par Ali Muhsin al-Barwani.

Fermeture