クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany * - 対訳の目次

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

対訳 節: (20) 章: イムラ―ン家章
فَإِنۡ حَآجُّوكَ فَقُلۡ أَسۡلَمۡتُ وَجۡهِيَ لِلَّهِ وَمَنِ ٱتَّبَعَنِۗ وَقُل لِّلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡأُمِّيِّـۧنَ ءَأَسۡلَمۡتُمۡۚ فَإِنۡ أَسۡلَمُواْ فَقَدِ ٱهۡتَدَواْۖ وَّإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّمَا عَلَيۡكَ ٱلۡبَلَٰغُۗ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِٱلۡعِبَادِ
Na pindi wakikuhoji, basi sema: Mimi nimeusalimisha uso wangu kumwelekea Mwenyezi Mungu, na kadhaalika walio nifuata. Na waambie walio pewa Kitabu na wasio na kisomo: Je! Mmesilimu? Wakisilimu basi wameongoka. Na wakikengeuka basi juu yako ni kufikisha ujumbe tu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaona waja wake.
Na hawa makafiri wakijadiliana nawe katika Dini hii baada ya wewe kuwapa hoja zote, huna haja kupigizana nao kelele kwa majadiliano. Waambie tu: Mimi na Waumini walio nifuata tumemsafia Mwenyezi Mungu peke yake ibada yetu. Na waambie Mayahudi na Wakristo na washirikina wa Kiarabu: Dalili zimekwisha bainika kwenu, basi silimuni. Wakisilimu inakuwa wameijua njia ya uwongofu na wameifuata. Na wakikataa huna lawama wewe kwa kukataa kwao. Waajibu wako ni kufikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu tu. Na Mwenyezi Mungu anawajua vyema waja wake. Hapana lolote lao, hali yao na vitendo vyao, linalo fichikana kwake.
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 節: (20) 章: イムラ―ン家章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany - 対訳の目次

クルアーン・スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany

閉じる