Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani * - Lexique des traductions

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traduction des sens Sourate: AL-‘ALAQ   Verset:

Surat Al-Alaq

ٱقۡرَأۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلَّذِي خَلَقَ
Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba!
Ewe Muhammad! Soma unayo funuliwa kwa kufunguliwa kwa Jina la Mola wako Mlezi ambaye ni Yeye tu peke yake ndiye Mwenye uweza wa kuumba.
Les exégèses en arabe:
خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِنۡ عَلَقٍ
Amemuumba binaadamu kwa tone la damu!
Amemuumba mtu kwa ukamilifu wa mwili wake na ilimu kutokana na kipande cha damu ambacho hakina chochote cha kupelekea kujiona bora.
Les exégèses en arabe:
ٱقۡرَأۡ وَرَبُّكَ ٱلۡأَكۡرَمُ
Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!
Endelea na kusoma, na Mola wako Mlezi aliye Karimu kushinda wote, atakutukuza wala hatakudharau.
Les exégèses en arabe:
ٱلَّذِي عَلَّمَ بِٱلۡقَلَمِ
Ambaye amefundisha kwa kalamu.
Yeye ndiye ambaye aliye mfunza mtu kuandika kwa kalamu, na wala kwanza hakuwa anajua hayo.
Les exégèses en arabe:
عَلَّمَ ٱلۡإِنسَٰنَ مَا لَمۡ يَعۡلَمۡ
Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.
Amemfunza mtu yasiyo kuwa yanampitia katika mawazo yake.
Les exégèses en arabe:
كَلَّآ إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لَيَطۡغَىٰٓ
Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri.
Ni hakika kweli mtu hupindukia mpaka na hupanda kiburi mbele ya Mola wake Mlezi
Les exégèses en arabe:
أَن رَّءَاهُ ٱسۡتَغۡنَىٰٓ
Akijiona katajirika.
Anapo jiona si mhitaji, katajirika.
Les exégèses en arabe:
إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلرُّجۡعَىٰٓ
Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.
Ewe Muhammad! Hakika ni kwa Mola wako Mlezi peke yake ndiyo yako marejeo ya wote kwa kufufuliwa na kulipwa.
Les exégèses en arabe:
أَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي يَنۡهَىٰ
Umemwona yule anaye mkataza.
Je! Umemwona huyu jeuri
Les exégèses en arabe:
عَبۡدًا إِذَا صَلَّىٰٓ
Mja anapo sali?
Anaye mzuia mja asisali anapo taka kusali?
Les exégèses en arabe:
أَرَءَيۡتَ إِن كَانَ عَلَى ٱلۡهُدَىٰٓ
Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?
Hebu niambie khabari za jeuri huyu kama yeye yumo katika uwongofu katika huku kuzuia kwake,
Les exégèses en arabe:
أَوۡ أَمَرَ بِٱلتَّقۡوَىٰٓ
Au anaamrisha uchamngu?
Au kwamba ndio anaamrisha uchamngu katika hayo anayo amrisha!
Les exégèses en arabe:
أَرَءَيۡتَ إِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰٓ
Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?
Niambie khabari za huyu mwenye kukataza anapo yakadhibisha aliyo kuja nayo Mtume, na akapuuza Imani na vitendo vyema!
Les exégèses en arabe:
أَلَمۡ يَعۡلَم بِأَنَّ ٱللَّهَ يَرَىٰ
Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?
Hivyo hajui kwamba Mwenyezi Mungu anazijua vyema hali zake, naye atamlipa kwazo?
Les exégèses en arabe:
كَلَّا لَئِن لَّمۡ يَنتَهِ لَنَسۡفَعَۢا بِٱلنَّاصِيَةِ
Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!
Kwa kumkemea huyu mwenye kuzuia, anaambiwa kama hakuacha hayo anayo yafanya, basi hapana shaka tutamkokota kwa nguvu tukimshika kwa shungi lake la nywele mpaka Motoni!
Les exégèses en arabe:
نَاصِيَةٖ كَٰذِبَةٍ خَاطِئَةٖ
Shungi la uwongo, lenye makosa!
Hilo shungi lilio juu ya uso wake mwenye kuropokwa uwongo na mwenye athari za ukosefu!
Les exégèses en arabe:
فَلۡيَدۡعُ نَادِيَهُۥ
Basi na awaite wenzake!
Basi yeye awaite wenziwe na watu wa baraza lake wawe ndio wasaidizi duniani au Akhera.
Les exégèses en arabe:
سَنَدۡعُ ٱلزَّبَانِيَةَ
Nasi tutawaita Mazabania!
Sisi tutawaita askari wetu wamsaidie Muhammad na walio pamoja naye, na wapambane na huyo mwenye kukanya na wasaidizi wawasukume kwenye Jahannamu!
Les exégèses en arabe:
كَلَّا لَا تُطِعۡهُ وَٱسۡجُدۡۤ وَٱقۡتَرِب۩
Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee!
Kumnyamazisha huyu mwenye kuzuia, wewe usimkubalie kwa hayo anayo kukataza nayo, na dumu juu ya Swala zako, na endelea na sijida zako, na jijongeze kwa Mola wako Mlezi kwa hivyo.
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Sourate: AL-‘ALAQ
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - Traduction Swahili - Ali Muhsin al-Barwani - Lexique des traductions

Traduction des sens du noble Coran en langue Swahili, par Ali Muhsin al-Barwani.

Fermeture