Check out the new design

કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સ્વાહિલી ભાષામાં અનુવાદ - અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અને નાસિર ખમીસ * - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા


શબ્દોનું ભાષાંતર સૂરહ: અન્ નમલ   આયત:
أَمَّن يَبۡدَؤُاْ ٱلۡخَلۡقَ ثُمَّ يُعِيدُهُۥ وَمَن يَرۡزُقُكُم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ وَٱلۡأَرۡضِۗ أَءِلَٰهٞ مَّعَ ٱللَّهِۚ قُلۡ هَاتُواْ بُرۡهَٰنَكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
Na waulize wao: Ni nani anayeanzisha kuumba viumbe, kisha anaviondosha akitaka, kisha anavirudisha? Na ni nani anayewaruzuku nyinyi kutoka mbinguni kwa kuiteremsha mvua? Na ni nani anayehuisha ardhi kwa kuotesha mimea na vinginevyo? Je, kuna muabudiwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu anafanya hayo? Sema, Leteni hoja yenu iwapo nyinyi ni wakweli katika madai yenu kwamba Mwenyezi Mungu Ana mshirika katika mamlaka Yake na ibada Yake.»
અરબી તફસીરો:
قُل لَّا يَعۡلَمُ مَن فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ ٱلۡغَيۡبَ إِلَّا ٱللَّهُۚ وَمَا يَشۡعُرُونَ أَيَّانَ يُبۡعَثُونَ
Sema, ewe Mtume, kuwaambia wao, «Hakuna yoyote ajuwaye, mbinguni wala ardhini, jambo lolote lililofichika ambalo Mwenyezi Mungu Amejihusisha Mwenyewe kulijua. Na wao hawajui ni lini watafufuliwa kutoka makaburini mwao wakati wa Kiyama kusimama.»
અરબી તફસીરો:
بَلِ ٱدَّٰرَكَ عِلۡمُهُمۡ فِي ٱلۡأٓخِرَةِۚ بَلۡ هُمۡ فِي شَكّٖ مِّنۡهَاۖ بَلۡ هُم مِّنۡهَا عَمُونَ
Bali ujuzi wao wa Kiyama utakamilika huko Akhera, huko watakuwa na yakini juu ya Nyumba ya Akhera na vituko vilivyomo watakapoishuhudia. Na wao walipokuwa duniani walikuwa na shaka nayo, bali akili zao zilikuwa zimepofuka hawaiyoni.
અરબી તફસીરો:
وَقَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ أَءِذَا كُنَّا تُرَٰبٗا وَءَابَآؤُنَآ أَئِنَّا لَمُخۡرَجُونَ
Na walisema wale waliokanusha upweke wa Mwenyezi Mungu, «Je, sisi na wazazi wetu tutafufuliwa, tukiwa hai kama tulivyo, baada ya kufa kwetu, baada ya sisi kuwa mchanga?
અરબી તફસીરો:
لَقَدۡ وُعِدۡنَا هَٰذَا نَحۡنُ وَءَابَآؤُنَا مِن قَبۡلُ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّآ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Tuliahidiwa kufufuliwa huku, sisi na wazazi wetu, hapo kabla(tulipokuwa duniani) hatukuuona uhakika wake wala kutokea kwake. Hatukuona ahadi hii isipokuwa ni hadithi za urongo zilizozuliwa na kuandikwa na watu wa kale ndani ya vitabu vyao.
અરબી તફસીરો:
قُلۡ سِيرُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَٱنظُرُواْ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُجۡرِمِينَ
Waambie, ewe Mtume, hawa wakanushaji, «Tembeeni kwenye ardhi mziangalie nyumba za wahalifu waliokuwa kabla yenu muone ulikuwa vipi mwisho wa wenye kuwakanusha Mitume? Mwenyezi Mungu Aliwaangamiza kwa ukanushaji wao, na Mwenyezi Mungu Atawafanya nyinyi kama wao iwapo hamtaamini.»
અરબી તફસીરો:
وَلَا تَحۡزَنۡ عَلَيۡهِمۡ وَلَا تَكُن فِي ضَيۡقٖ مِّمَّا يَمۡكُرُونَ
Usiwe na masikitiko juu ya kukupa mgongo kwao, hao washirikina, na kukukanusha, na usiwe na dhiki moyo wako juu ya vitimbi vyao wanavyokufanyia, kwani Mwenyezi Mungu ni Mwenye kukupa ushindi juu yao.
અરબી તફસીરો:
وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هَٰذَا ٱلۡوَعۡدُ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
Na washirikina wa watu wako, ewe Mtume, wanasema «Itakuwa lini ahadi hii ya adhabu mnayotuahidi kwayo, wewe na wafuasi wako, mkiwa nyinyi ni wakweli katika yale mnayotuahidi?»
અરબી તફસીરો:
قُلۡ عَسَىٰٓ أَن يَكُونَ رَدِفَ لَكُم بَعۡضُ ٱلَّذِي تَسۡتَعۡجِلُونَ
Waambie, ewe Mtume, «Huenda yakawa ni karibu kwenu baadhi ya yale mnayoyafanyia haraka ya adhabu ya Mwenyezi Mungu.»
અરબી તફસીરો:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَذُو فَضۡلٍ عَلَى ٱلنَّاسِ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَشۡكُرُونَ
Na hakika ya Mola wako ni Mwenye nyongeza za wema kwa watu, kwa kuacha kuwaharakishia wao adhabu kwa kumuasi kwao Yeye na kumkanusha. Lakini wengi wao hawamshukuru kwa hilo wakamuamini na wakamtakasia ibada.
અરબી તફસીરો:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَيَعۡلَمُ مَا تُكِنُّ صُدُورُهُمۡ وَمَا يُعۡلِنُونَ
Na kwa hakika, Mola wako ni Yeye Anayekijua kile ambacho vifua vyao vinakificha na kile ambacho vinakifichua wazi.
અરબી તફસીરો:
وَمَا مِنۡ غَآئِبَةٖ فِي ٱلسَّمَآءِ وَٱلۡأَرۡضِ إِلَّا فِي كِتَٰبٖ مُّبِينٍ
Na hakuna kitu chochote kilichofichika na macho ya viumbe, kilichoko mbinguni na ardhini,isipokuwa kiko kwenye Kitabu kilicho waziwazi kilichoko kwa Mwenyezi Mungu. Kitabu hiko kimevizunguka vyote vilivyokuwa na vitakavyokuwa.
અરબી તફસીરો:
إِنَّ هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانَ يَقُصُّ عَلَىٰ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ أَكۡثَرَ ٱلَّذِي هُمۡ فِيهِ يَخۡتَلِفُونَ
Kwa hakika, hii Qur’ani inawapa Wana wa Isrāīl habari ya ukweli katika mambo mengi zaidi ambayo wao wametafautiana juu yake.
અરબી તફસીરો:
 
શબ્દોનું ભાષાંતર સૂરહ: અન્ નમલ
સૂરહ માટે અનુક્રમણિકા પેજ નંબર
 
કુરઆન મજીદના શબ્દોનું ભાષાંતર - સ્વાહિલી ભાષામાં અનુવાદ - અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અને નાસિર ખમીસ - ભાષાંતરોની અનુક્રમણિકા

તેનું અનુવાદ ડૉ. અબ્દુલ્લાહ મુહમ્મદ અબૂબકર અને શૈખ નાસિર ખમીસ દ્વારા કરવામાં આવ્યું છે.

બંધ કરો