Check out the new design

クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany * - 対訳の目次

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

対訳 章: 送られる者章   節:
أَلَمۡ نَخۡلُقكُّم مِّن مَّآءٖ مَّهِينٖ
Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?
Kwani hatukukuumbeni kutokana na maji yaliyo dhalili, nayo ni manii,
アラビア語 クルアーン注釈:
فَجَعَلۡنَٰهُ فِي قَرَارٖ مَّكِينٍ
Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?
Na tukayaweka maji haya katika pahala patulivu,
アラビア語 クルアーン注釈:
إِلَىٰ قَدَرٖ مَّعۡلُومٖ
Mpaka muda maalumu?
Mpaka kutimilia kuumbwa kwake na kutengenezwa kwake kwa muda anao ujua Mwenyezi Mungu.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَقَدَرۡنَا فَنِعۡمَ ٱلۡقَٰدِرُونَ
Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.
Nasi tukaweka vipimo katika kuumbwa kwake, na kutengenezwa kwake, na kutoka kwake. Basi wabora wa kupima na kukadiria ni Sisi.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
Ole wao hao wanao kadhibisha neema za kuumba na kukadiria.
アラビア語 クルアーン注釈:
أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ كِفَاتًا
Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya
Kwani hatukuifanya ardhi kuwa imekusanya juu ya mgongo wake
アラビア語 クルアーン注釈:
أَحۡيَآءٗ وَأَمۡوَٰتٗا
Walio hai na maiti?
Viumbe vilivyo hai visio hisabika, na vilio kufa visio kadirika,
アラビア語 クルアーン注釈:
وَجَعَلۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ شَٰمِخَٰتٖ وَأَسۡقَيۡنَٰكُم مَّآءٗ فُرَاتٗا
Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?
Na tukaweka milima iliyo thibiti imara mirefu, na tukakunywesheni maji matamu?
アラビア語 クルアーン注釈:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
Wataangamia siku hiyo hao wanao kadhibisha neema hizi!
アラビア語 クルアーン注釈:
ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!
Siku ya kupambanua wataambiwa makafiri: Nendeni huko Motoni mliko kuwa mkikukanusha.
アラビア語 クルアーン注釈:
ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ ظِلّٖ ذِي ثَلَٰثِ شُعَبٖ
Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!
Nendeni kwenye joto la moshi wa Jahannamu ulio gawika kwa ukubwa wake mapande matatu.
アラビア語 クルアーン注釈:
لَّا ظَلِيلٖ وَلَا يُغۡنِي مِنَ ٱللَّهَبِ
Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.
Hapana cha kujikinga na joto la siku hiyo, wala kivuli hicho hakipunguzi joto la mwako hata kidogo.
アラビア語 クルアーン注釈:
إِنَّهَا تَرۡمِي بِشَرَرٖ كَٱلۡقَصۡرِ
Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!
Moto huo hutupa macheche yenye ukubwa kama majumba,
アラビア語 クルアーン注釈:
كَأَنَّهُۥ جِمَٰلَتٞ صُفۡرٞ
Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!
Au utaona hayo macheche kama ngamia weusi wenye kuingia rangi ya manjano.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
Wataangamia siku hiyo wanao kanusha kwamba hizi ndizo sifa za Moto.
アラビア語 クルアーン注釈:
هَٰذَا يَوۡمُ لَا يَنطِقُونَ
Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,
Haya uliyo simuliwa yatatokea katika siku ambayo hawatatamka kitu cha kuwanufaisha,
アラビア語 クルアーン注釈:
وَلَا يُؤۡذَنُ لَهُمۡ فَيَعۡتَذِرُونَ
Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.
Wala hawatakuwa na idhini ya kutamka, wala hawatatoa udhuru, kwani hawana udhuru.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!
Wataangamia siku hiyo wanayo ikadhibisha siku hii.
アラビア語 クルアーン注釈:
هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِۖ جَمَعۡنَٰكُمۡ وَٱلۡأَوَّلِينَ
Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia.
Hii ndiyo siku ya kufafanua baina ya mwenye ukweli, na mwenye uwongo, kwa kuwa kila mmoja atalipwa kwa mujibu wa anavyo stahiki. Enyi mnao mkadhibisha Muhammad! Tumekujaalieni nyinyi na walio kutangulieni walio kadhibisha mfano wenu,
アラビア語 クルアーン注釈:
فَإِن كَانَ لَكُمۡ كَيۡدٞ فَكِيدُونِ
kiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!
Kama mnayo hila ya kujikinga na adhabu basi fanyeni hila hiyo. Basi njooni muepukane na adhabu yangu.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!
Wataangamia siku hiyo wanayo ikadhibisha ahadi ya Mwenyezi Mungu.
アラビア語 クルアーン注釈:
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي ظِلَٰلٖ وَعُيُونٖ
Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem,
Hakika wachamngu wenye kujikinga na adhabu ya Mwenyezi Mungu watakuwa katika kivuli kikubwa, na chemchem zinazo miminika,
アラビア語 クルアーン注釈:
وَفَوَٰكِهَ مِمَّا يَشۡتَهُونَ
Na matunda wanayo yapenda,
Na matunda wanayo yaonea ladha, na wanayo yapenda,
アラビア語 クルアーン注釈:
كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda.
Wataambiwa kwa kuamkiwa na kukirimiwa: Kuleni na mnywe chakula na vinywaji kwa starehe kwa sababu ya vitendo vyema mlivyo kuwa mkivitenda duniani.
アラビア語 クルアーン注釈:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema.
Hakika Sisi huwalipa mfano wa malipo hayo matukufu watu wema.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
Wataangamia siku hiyo wanayo ikadhibisha Pepo.
アラビア語 クルアーン注釈:
كُلُواْ وَتَمَتَّعُواْ قَلِيلًا إِنَّكُم مُّجۡرِمُونَ
Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!
Na makafiri wataambiwa: Kuleni na mjistareheshe kwa starehe isiyo baki muda mrefu, kwani hakika nyinyi ni wakosefu kwa kumshirikisha kwenu Mwenyezi Mungu.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
Wataangamia siku hiyo wanao ikadhibisha neema.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ٱرۡكَعُواْ لَا يَرۡكَعُونَ
Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami.
Na wakiambiwa: Swalini kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, na mnyenyekeeni Yeye, hawanyenyekei wala hawaswali; bali hushikilia kiburi chao!
アラビア語 クルアーン注釈:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
Wataangamia siku wanao kadhibisha amri za Mwenyezi Mungu na makatazo yake.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَبِأَيِّ حَدِيثِۭ بَعۡدَهُۥ يُؤۡمِنُونَ
Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?
Basi maneno gani hawa watayaamini ikiwa hawaiamini Qur'ani, na hali hii ni muujiza ulio toka mbinguni?
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 章: 送られる者章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany - 対訳の目次

Ali Muhsen Alberwanyによる訳。

閉じる