Check out the new design

ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស * - សន្ទស្សន៍នៃការបកប្រែ


ការបកប្រែអត្ថន័យ ជំពូក​: អាល់កះហ្វុី   អាយ៉ាត់:
وَدَخَلَ جَنَّتَهُۥ وَهُوَ ظَالِمٞ لِّنَفۡسِهِۦ قَالَ مَآ أَظُنُّ أَن تَبِيدَ هَٰذِهِۦٓ أَبَدٗا
Na akaingia shambani kwake , na hali amejidhulumu nafsi yake kwa kukanusha kufufuliwa na kuwa na shaka kwake juu ya kusimama Kiyama, yakampendeza matunda yake na akasema, «Siamini kwamba shamba hili litaangamia muda wa maisha
តាហ្វសៀរជាភាសា​អារ៉ាប់ជាច្រេីន:
وَمَآ أَظُنُّ ٱلسَّاعَةَ قَآئِمَةٗ وَلَئِن رُّدِدتُّ إِلَىٰ رَبِّي لَأَجِدَنَّ خَيۡرٗا مِّنۡهَا مُنقَلَبٗا
na siamini kwamaba Kiyama ni chenye kutukia, na kikitukia kwa kukisia tu, kama unavyodai ewe mwenye kuamini, na nikarudishwa kwa Mola wangu, basi huko Kwake nitapata bora zaidi kuliko shamba hili nirudishiwe na nirejeshewe, kwa ajili ya utukufu wangu na cheo changu Kwake.»
តាហ្វសៀរជាភាសា​អារ៉ាប់ជាច្រេីន:
قَالَ لَهُۥ صَاحِبُهُۥ وَهُوَ يُحَاوِرُهُۥٓ أَكَفَرۡتَ بِٱلَّذِي خَلَقَكَ مِن تُرَابٖ ثُمَّ مِن نُّطۡفَةٖ ثُمَّ سَوَّىٰكَ رَجُلٗا
Mwenzake Muumini akamwambia, huku akimjadili kwa kumuwaidhia, «Vipi wewe utamkanusha Mwenyezi Mungu Aliyekuumba kwa mchanga kisha kwa tone la manii kisha Akakusawazisha kwa kukufanya binadamu mwenye kimo kilicholingana na umbo?» Katika aya hii pana dalili ya kwamba mwenye uweza wa kuanzisha kuumba viumbe ni muweza wa kuwarudisha.
តាហ្វសៀរជាភាសា​អារ៉ាប់ជាច្រេីន:
لَّٰكِنَّا۠ هُوَ ٱللَّهُ رَبِّي وَلَآ أُشۡرِكُ بِرَبِّيٓ أَحَدٗا
«Lakini mimi sisemi maneno hayo yako yanayoonyesha ukafiri wako. Kwa kweli, mimi nasema ‘Mwenye kuneemesha na kufanya hisani ni Mwenyezi Mungu Mola wangu Peke Yake, na mimi simshrikishi yeye katika kumuabudu na yoyote asiyekuwa Yeye.
តាហ្វសៀរជាភាសា​អារ៉ាប់ជាច្រេីន:
وَلَوۡلَآ إِذۡ دَخَلۡتَ جَنَّتَكَ قُلۡتَ مَا شَآءَ ٱللَّهُ لَا قُوَّةَ إِلَّا بِٱللَّهِۚ إِن تَرَنِ أَنَا۠ أَقَلَّ مِنكَ مَالٗا وَوَلَدٗا
«Kwani si ingalikuwa afadhali, ulipoingia kwenye shamba lako na likakupendeza, kama ulimshukuru Mwenyezi Mungu na ukasema, ‘Haya ni yale Aliyenitakia Mwenyezi Mungu, sina nguvu ya kuyapata isipokuwa ni kwa Mwenyezi Mungu.’ Iwapo waniona mimi kuwa ni mchache wa mali na watoto kuliko wewe,
តាហ្វសៀរជាភាសា​អារ៉ាប់ជាច្រេីន:
فَعَسَىٰ رَبِّيٓ أَن يُؤۡتِيَنِ خَيۡرٗا مِّن جَنَّتِكَ وَيُرۡسِلَ عَلَيۡهَا حُسۡبَانٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ فَتُصۡبِحَ صَعِيدٗا زَلَقًا
basi Mwenyezi Mungu huenda Akanipa mimi bora zaidi kuliko shamba lako, na Akakuondolea hiyo neema kwa ukafiri wako, na akailetea shamba yako adhabu kutoka mbinguni ikawa ni ardhi tupu iliyo kavu ambayo nyayo haziwezi kuthibiti juu yake wala hakuna mmea unaoota,
តាហ្វសៀរជាភាសា​អារ៉ាប់ជាច្រេីន:
أَوۡ يُصۡبِحَ مَآؤُهَا غَوۡرٗا فَلَن تَسۡتَطِيعَ لَهُۥ طَلَبٗا
au maji yake ya kuinyosheza yazame ardhini na kukauka usiwezi kuyatoa.»
តាហ្វសៀរជាភាសា​អារ៉ាប់ជាច្រេីន:
وَأُحِيطَ بِثَمَرِهِۦ فَأَصۡبَحَ يُقَلِّبُ كَفَّيۡهِ عَلَىٰ مَآ أَنفَقَ فِيهَا وَهِيَ خَاوِيَةٌ عَلَىٰ عُرُوشِهَا وَيَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي لَمۡ أُشۡرِكۡ بِرَبِّيٓ أَحَدٗا
Yakawa ni kweli yale maneno ya yule Muumini, na shamba likaharibika na vilivyomo ndani vikaangamia, akawa yule kafiri anageuza vitanga vyake vya mikono huku na huku kwa kulilia hasara na majuto kwa gharama aliyoitoa pale, na hali mitiyake imeanguka chini baadhi yake iko juu ya mingine, na akawa yuwasema, «Natamani lau nilizitambua neema za Mwenyezi Mungu na uweza Wake na sikumshirikisha Mwenyezi Mungu na yoyote.» Na haya ni majuto yake wakati ambapo majuto hayamfalii kitu.
តាហ្វសៀរជាភាសា​អារ៉ាប់ជាច្រេីន:
وَلَمۡ تَكُن لَّهُۥ فِئَةٞ يَنصُرُونَهُۥ مِن دُونِ ٱللَّهِ وَمَا كَانَ مُنتَصِرًا
Na hakuwa na kundi la watu, kati ya wale ambao alijifahiri nao, wenye kumtetea na adhabu ya Mwenyezi Mungu yenye kumshukia, wala hakuwa ni mwenye kujitetea kwa nafsi yake na nguvu zake.
តាហ្វសៀរជាភាសា​អារ៉ាប់ជាច្រេីន:
هُنَالِكَ ٱلۡوَلَٰيَةُ لِلَّهِ ٱلۡحَقِّۚ هُوَ خَيۡرٞ ثَوَابٗا وَخَيۡرٌ عُقۡبٗا
Katika shida kama hizi mategemeo na usaidizi huwa uko kwa Mwenyezi Mungu wa haki. Yeye ni bora wa kulipa mema na ni bora wa kuwapa mwisho mwema wale waliyoko hifadhini Mwake.
តាហ្វសៀរជាភាសា​អារ៉ាប់ជាច្រេីន:
وَٱضۡرِبۡ لَهُم مَّثَلَ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا كَمَآءٍ أَنزَلۡنَٰهُ مِنَ ٱلسَّمَآءِ فَٱخۡتَلَطَ بِهِۦ نَبَاتُ ٱلۡأَرۡضِ فَأَصۡبَحَ هَشِيمٗا تَذۡرُوهُ ٱلرِّيَٰحُۗ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ مُّقۡتَدِرًا
Na wapigie watu, ewe Mtume, hasa wale wenye kujiona kati yao, mfano wa hali ya ulimwengu, ambao wameghurika nao, kwa uzuri wake na upesi wa kuondoka kwake, kwamba ni kama maji aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu kutoka juu ambayo kwayo mimea ikatoka kwa idhini Yake na ardhi ikageuka ikawa rangi kijani. Na usipite isipokuwa muda mchache kitahamaka mimea hii ikawa imevunjikavunjika inarushwa na upepo kila upande. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye uweza mkubwa juu ya kila kitu.
តាហ្វសៀរជាភាសា​អារ៉ាប់ជាច្រេីន:
 
ការបកប្រែអត្ថន័យ ជំពូក​: អាល់កះហ្វុី
សន្ទស្សន៍នៃជំពូក លេខ​ទំព័រ
 
ការបកប្រែអត្ថន័យគួរអាន - ការបកប្រែជាភាសាswahili - អាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ និងណាសៀរ ខមុីស - សន្ទស្សន៍នៃការបកប្រែ

ការបកប្រែដោយលោកបណ្ឌិតអាប់ឌុលឡោះ ម៉ូហាំម៉ាត់ អាពូពើកើរ និងលោកណាសៀរ ខមុីស

បិទ