Hakika Waumini wa kweli ni walio muamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake; na wanapo kuwa pamoja naye kwa jambo la kuwakhusu wote hawaondoki mpaka wamtake ruhusa. Kwa hakika wale wanao kuomba ruhusa, hao ndio wanao muamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Na wakikuomba ruhusa kwa baadhi ya kazi zao, mruhusu umtakaye miongoni mwao, uwaombee msamaha kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemmu. [62]
[62] Hakika Waumini wenye kusadiki ni wale ambao wamemuamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na wala hawamwachi Mtume peke yake katika jambo muhimu linalo hitajia wajumuike pamoja kwa ajili yake, kama mfano wa Jihadi. Ila baada ya kumtaka ruhusa ya kuondoka na wakakubaliwa, hakika wanao kukadiri wewe, ewe Nabii, kama unavyo stahiki, na wanatambua umuhimu wa huo mkusanyiko hawaondoki ila baada ya wewe kukubali. Hao ndio wenye kusadiki katika Imani yao kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Basi wakikutaka ruhusa hawa kwenda kufanya baadhi ya maslaha yao mpe ruhusa umtakaye katika wao, pindi ukimwona kuwa ana haja kweli ya kuondoka, na si dharura kwa mkutano kuwapo yeye. Juu ya hivyo waombee maghfira kwa Mwenyezi Mungu kwa kuondoka kwao, ambako kwa hakika hakuelekei kabisa. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mkunjufu wa maghfira na rehema.
Msifanye wito wa Mtume baina yenu kama wito wa nyinyi kwa nyinyi. Hakika Mwenyezi Mungu anawajua miongoni mwenu wanao ondoka kwa uficho. Basi nawatahadhari wanao khalifu amri yake, usije ukawapata msiba au ikawapata adhabu chungu. [63]
[63] Fanyeni hima kuhishimu wito wa Mtume kukuiteni kukusanyika kwa mambo muhimu. Na muitikieni huo wito wake, wala msifanye wito huo kama mnavyo itana nyinyi kwa nyinyi, kuwa inafaa kupuuza na kuondoka mpendavyo. Wala msiondoke ila baada ya kutaka ruhusa na mkakubaliwa, na tena iwe katika mipaka ya ufinyo kabisa, na dharura za shida. Na Mwenyezi Mungu Subhanahu anawajua wanao ondoka bila ya idhini wakijificha ficha kati ya watu ili ati Mtume asiwaone. Na watahadhari wanao kwenda kinyume na amri ya Mwenyezi Mungu asije Subhanahu akawapatiliza kwa uasi wao wakapata mateso makali duniani kama ukame na mitetemeko, au akawapa adhabu yenye wingi wa uchungu aliyo waandalia Akhera, nayo ni ya Motoni.
Jueni kuwa hakika ni vya Mwenyezi Mungu vilivyomo mbinguni na ardhini. Hakika Yeye anajua mlio nayo. Na siku mtapo rudishwa kwake atawaeleza waliyo yafanya. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu. [64]
[64] Zindukaneni enyi watu! Mjue kuwa Mwenyezi Mungu peke yake ndiye Mwenye kumiliki mbingu na ardhi, na viliomo ndani yao. Anayajua mlio nayo, ukafiri wenu na Uislamu wenu, na uasi wenu, na ut'iifu wenu. Basi msiende kinyume na amri yake. Na Yeye atawapa khabari watu, watapo rejea kwake Siku ya Kiyama, kwa yote waliyo yatenda duniani, na atawalipa kwayo. Kwani Yeye amekizunguka kila kitu kwa ujuzi wake.
Contents of the translations can be downloaded and re-published, with the following terms and conditions:
1. No modification, addition, or deletion of the content.
2. Clearly referring to the publisher and the source (QuranEnc.com).
3. Mentioning the version number when re-publishing the translation.
4. Keeping the transcript information inside the document.
5. Notifying the source (QuranEnc.com) of any note on the translation.
6. Updating the translation according to the latest version issued from the source (QuranEnc.com).
7. Inappropriate advertisements must not be included when displaying translations of the meanings of the Noble Quran.
លទ្ធផលស្វែងរក:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".