Hao ndio Mwenyezi Mungu amewalaani. Na ambaye Mwenyezi Mungu amemlaani basi hutamwona kuwa na mwenye kumnusuru. [52]
[52] Hao ndio alio watupa Mwenyezi Mungu na akawafukuzilia mbali kutoka kwenye rehema yake. Na mwenye kutupwa na Mwenyezi Mungu na akatolewa kwenye rehema yake basi kabisa huyo hana wa kumnusuru na kumlinda na ghadhabu ya Mola wake Mlezi.
Au wanawahusudu watu kwa yale aliyo wapa Mwenyezi Mungu kwa fadhila yake? Basi tuliwapa ukoo wa Ibrahim Kitabu na hikima na tukawapa utawala mkubwa. [54]
[54] Na vipi watu hawa wanavyo waonea maya Waarabu? Na wakaona ni jambo kuu kuwa Mwenyezi Mungu alivyo wapa fadhila yake kwa kuwatolea Nabii kutokana nao, na ilhali Mwenyezi Mungu alimpa Ibrahim na ukoo wake - naye ni baba yenu (Mayahudi na Wakristo), na baba yao (Waislamu pia) - Kitabu kilicho teremshwa kwa ufunuo, na Unabii na Utawala ulio mkubwa!
Basi wapo miongoni mwao waliyo yaamini, na wapo walio yakataa. Na Jahannamu yatosha kuwa ni moto wa kuwateketeza. [55]
[55] Miongoni mwa walio pelekewa Nabii Ibrahim na ukoo wake wapo wenye kukiamini Kitabu kilicho teremshiwa kwao, na wapo walio kipa nyongo wakajitenga nacho. Na jaza ya hawa wenye kujitenga na wito wa Haki ni Jahannamu yenye moto wa kuteketeza.
Hakika wale walio zikataa Ishara zetu tutawaingiza Motoni. Kila zitapo wiva ngozi zao tutawabadilishia ngozi nyengine ili waionje hiyo adhabu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye hikima. [56]
[56] Hakika wanao pinga hoja zetu zenye kubainisha wazi wazi, na wakawakanusha Manabii, tutakuja watia kwenye Moto utakao babua ngozi zao. Na kila zikisita kuhisi adhabu Mwenyezi Mungu atawabadilishia ngozi nyengine mpya ili machungu ya adhabu yabaki yakiendelea. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye ushindi katika mambo yake, na Mwenye hikima katika vitendo vyake. Humuadhibu mwenye kumpinga na akabaki na upinzani mpaka kufa kwake. Qur'an Tukufu imeitangulia sayansi ya kisasa, ikathibitisha kuwa katika ngozi mishipa ya kuhisi, Navo, imetanda kama wavu, na hiyo hupokea mishipa yote ya kuhisi machungu, joto na baridi na mengineyo. Na hayo hayakujuulikana ila hivi karibuni.
Na wale walio amini na wakatenda mema tutawaingiza katika Pepo zipitazo mito kati yake kwa kudumu humo milele. Huko watakuwa na wake walio takasika, na tutawaingiza katika vivuli vizuri kweli. [57]
[57] Na ambao walio yasadiki yaliyo wajia kutoka kwa Mola wao Mlezi, na wakatenda vitendo vyema, tutawalipa kwa Imani yao na vitendo vyao na tutawaingiza katika Mabustani ya Peponi yapitayo mito chini ya miti yake. Uhai wao hauna kikomo kabisa. Nao humo watakuwa na wake walio t'ahirika na kila la aibu na uchafu. Tutawapa uhai wa starehe chini ya vivuli vizuri vya kudumu, waishi maisha mema yenye neema isiyo kwisha.
Hakika Mwenyezi Mungu anakuamrisheni mzirudishe amana kwa wenyewe. Na mnapo hukumu baina ya watu mhukumu kwa uadilifu. Hakika haya anayo kuwaidhini Mwenyezi Mungu ni mazuri sana. Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kusikia, Mwenye kuona. [58]
[58] Hakika Mwenyezi Mungu anakuamrisheni nyinyi Waumini mrejeshe vyote mlio pewa amana, kutokana na Mwenyezi Mungu au kutokana na watu, kwa wenyewe kwa uadilifu. Basi msifanye jeuri katika kuhukumu. Haya ni mawaidha yanayo toka kwa Mola wenu Mlezi. Basi yafanyieni pupa kuyafuata. Bora ya mawaidha ni yanayo tokana naye Yeye. Hakika Mwenyezi Mungu daima ni Mwenye kusikia yasemwayo, ni Mwenye kuyaona yatendwayo. Basi anamjua anaye rejesha amana, na anaye fanya khiana, na anaye hukumu kwa uadilifu, na anaye fanya jeuri. Na kila mmoja atamlipa kwa atendalo.
Enyi mlio amini! Mt'iini Mwenyezi Mungu, na mt'iini Mtume na wenye madaraka katika nyinyi. Na mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume, ikiwa mnamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Hayo ndiyo bora zaidi na ndiyo yenye mwisho mwema. [59]
[59] Enyi mlio sadiki aliyo kuja nayo Muhammad! Mt'iini Mwenyezi Mungu, na mt'iini Mtume, na wale wanao tawala mambo yenu miongoni mwa Waislamu wanao simama juu ya haki na uadilifu, na wanatekeleza Sharia ya Mwenyezi Mungu. Na mkizozana katika jambo baina yenu basi rejeeni kwenye Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunna ya Mtume wake ili mpate kujua hukumu yake. Kwani Yeye Mwenyezi Mungu amekuteremshieni Kitabu chake na Mtume wake amebainisha hicho Kitabu. Na katika hayo ipo hukumu ya hayo mnayo khitalifiana kwayo. Haya ni kwa mujibu wa Imani yenu kumuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Na haya ndio bora kwenu ili mpate kuongoka kwendea uadilifu katika mnayo khitalifiana kwayo, na mwisho wake ndio mzuri zaidi. Kwani hivyo ndio kuzuia zisitokee khilafu zinazo pelekea ugomvi na upotovu.
Contents of the translations can be downloaded and re-published, with the following terms and conditions:
1. No modification, addition, or deletion of the content.
2. Clearly referring to the publisher and the source (QuranEnc.com).
3. Mentioning the version number when re-publishing the translation.
4. Keeping the transcript information inside the document.
5. Notifying the source (QuranEnc.com) of any note on the translation.
6. Updating the translation according to the latest version issued from the source (QuranEnc.com).
7. Inappropriate advertisements must not be included when displaying translations of the meanings of the Noble Quran.
លទ្ធផលស្វែងរក:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".