Check out the new design

ಪವಿತ್ರ ಕುರ್‌ಆನ್ ಅರ್ಥಾನುವಾದ - ಸ್ವಾಹಿಲಿ ಅನುವಾದ - ಅಬ್ದುಲ್ಲಾ ಮುಹಮ್ಮದ್ ಮತ್ತು ನಾಸಿರ್ ಖಮೀಸ್ * - ಅನುವಾದಗಳ ವಿಷಯಸೂಚಿ


ಅರ್ಥಗಳ ಅನುವಾದ ಅಧ್ಯಾಯ: ಅಲ್ ಅಂಬಿಯಾ   ಶ್ಲೋಕ:

Al-Anbiya

ٱقۡتَرَبَ لِلنَّاسِ حِسَابُهُمۡ وَهُمۡ فِي غَفۡلَةٖ مُّعۡرِضُونَ
Umekaribia wakati wa kuhesabiwa watu juu ya matendo waliyoyatanguliza, pamoja na hivyo, makafiri wanaishi wakiwa kwenye hali ya kupumbaa, wameghafilika na uhakika huu, wakiwa kwenye hali ya kulipa mgongo onyo hili.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
مَا يَأۡتِيهِم مِّن ذِكۡرٖ مِّن رَّبِّهِم مُّحۡدَثٍ إِلَّا ٱسۡتَمَعُوهُ وَهُمۡ يَلۡعَبُونَ
Hakuna kitu chochote katika Qur’ani chenye kuteremka, kinachosomwa kwao na chenye kuwakumbusha upya, isipokuwa huwa wakikisikia wakiwa katika hali ya kucheza na kufanya shere.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
لَاهِيَةٗ قُلُوبُهُمۡۗ وَأَسَرُّواْ ٱلنَّجۡوَى ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ هَلۡ هَٰذَآ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُكُمۡۖ أَفَتَأۡتُونَ ٱلسِّحۡرَ وَأَنتُمۡ تُبۡصِرُونَ
Nyoyo zao zimeghafilika na Qur’ani, zimeshughulika na ubatilifu wa dunia na matamanio yake, hawayafahamu yaliyomo ndani yake. Lakini madhalimu miongoni mwa Makureshi wamejikusanya pamoja juu ya jambo lililofichika, nalo ni kueneza yale ambayo kwayo wanawazuia watu kumuamini Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kwa kuwa yeye ni binadamu mfano wao, hatafautiani na wao katika kitu chochote, na kwamba Qur’ani aliyoileta ni uchawi. (Wanawaambia kwa kusema) «Vipi mutakuja kwake na mumfuate na hali kwamba mnaona kwamba yeye ni binadamu kama nyinyi?»
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
قَالَ رَبِّي يَعۡلَمُ ٱلۡقَوۡلَ فِي ٱلسَّمَآءِ وَٱلۡأَرۡضِۖ وَهُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ
Nabii, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, analirudisha kila jambo kwa Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake na kutukuka ni Kwake, akasema, «Mola wangu Analijua jambo la mbinguni na la ardhini na Anayajua maneno yenu mnayoyasema kwa siri, na Yeye Ndiye Mwenye kuyasikia maneno yenu, Ndiye Mwenye kuzijua hali zenu.» Katika hiya pana tishio kwao na onyo.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
بَلۡ قَالُوٓاْ أَضۡغَٰثُ أَحۡلَٰمِۭ بَلِ ٱفۡتَرَىٰهُ بَلۡ هُوَ شَاعِرٞ فَلۡيَأۡتِنَا بِـَٔايَةٖ كَمَآ أُرۡسِلَ ٱلۡأَوَّلُونَ
Lakini makafiri wameikanusha Qur’ani: kuna wanaosema kwamba ni mchanganyiko wa ndoto zisizo na ukweli, kuna wanaosema kwamba ni uzushi na urongo na si wahyi na kuna wanaosema kwamba Muhammad ni mshairi na kwamba haya ambayo amekuja nayo ni mashairi, na akiwa anataka tumuamini basi na atuletee miujiza yenye kuonekana kama vile ngamia wa Ṣāliḥ na miujiza ya Mūsā na 'Īsā na yale ambayo walikuja nayo Mitume kabla yake.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
مَآ ءَامَنَتۡ قَبۡلَهُم مِّن قَرۡيَةٍ أَهۡلَكۡنَٰهَآۖ أَفَهُمۡ يُؤۡمِنُونَ
Hakuna mji wowote ulioamini kabala ya makafiri wa Makkah ambao watu wake walitaka miujiza kutoka kwa Mtume wao na ikatokea kweli, bali walikanusha na tukawaangamiza. Basi je, makafiri wa Makkah wataamini iwapo itakuwa miujiza waliyoitaka? Sivyo, wao hawataamini.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَمَآ أَرۡسَلۡنَا قَبۡلَكَ إِلَّا رِجَالٗا نُّوحِيٓ إِلَيۡهِمۡۖ فَسۡـَٔلُوٓاْ أَهۡلَ ٱلذِّكۡرِ إِن كُنتُمۡ لَا تَعۡلَمُونَ
Na hatukuwatumiliza kabla yako , ewe Mtume, isipokuwa wanaume wa kibinadamu ambao tunawaletea wahyi, na hatukuwatumiliza Malaika. Basi waulizeni, enyi watu wa Makkah, wenye ujuzi wa vitabu vilivyoteremshwa huko nyuma iwapo hamjui hilo.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَمَا جَعَلۡنَٰهُمۡ جَسَدٗا لَّا يَأۡكُلُونَ ٱلطَّعَامَ وَمَا كَانُواْ خَٰلِدِينَ
Na hatukuwafanya wale Mitume kabla yako wawe nje ya tabia ya binadamu, wasihitaji chakula na kinywaji, na hawakuwa ni wenye kukaa milele wakawa hawafi.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
ثُمَّ صَدَقۡنَٰهُمُ ٱلۡوَعۡدَ فَأَنجَيۡنَٰهُمۡ وَمَن نَّشَآءُ وَأَهۡلَكۡنَا ٱلۡمُسۡرِفِينَ
Kisha tuliwatimizia Manabii na wafuasi wao yale tuliyowaahidi ya ushindi na kuokolewa, na tukawaangamiza wenye kuzionea nafsi zao kwa kumkanusha kwao Mola wao.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
لَقَدۡ أَنزَلۡنَآ إِلَيۡكُمۡ كِتَٰبٗا فِيهِ ذِكۡرُكُمۡۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ
Kwa kweli tumekuteremshia hii Qur’ani; ndani yake kuna enzi yenu na utukufu wenu katika ulimwengu na Akhera iwapo mtajikumbusha nayo. Je, hamuyafahamu yale ambayo kwayo niliwatukuza nyinyi juu ya wasiokuwa nyinyi?
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
 
ಅರ್ಥಗಳ ಅನುವಾದ ಅಧ್ಯಾಯ: ಅಲ್ ಅಂಬಿಯಾ
ಅಧ್ಯಾಯಗಳ ವಿಷಯಸೂಚಿ ಪುಟ ಸಂಖ್ಯೆ
 
ಪವಿತ್ರ ಕುರ್‌ಆನ್ ಅರ್ಥಾನುವಾದ - ಸ್ವಾಹಿಲಿ ಅನುವಾದ - ಅಬ್ದುಲ್ಲಾ ಮುಹಮ್ಮದ್ ಮತ್ತು ನಾಸಿರ್ ಖಮೀಸ್ - ಅನುವಾದಗಳ ವಿಷಯಸೂಚಿ

ಅನುವಾದ - ಡಾ. ಅಬ್ದುಲ್ಲಾ ಮುಹಮ್ಮದ್ ಅಬೂಬಕರ್ ಮತ್ತು ಶೈಖ್ ನಾಸಿರ್ ಖಮೀಸ್

ಮುಚ್ಚಿ