Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Abdullah Muchammed ir Naser Khamis * - Vertimų turinys


Reikšmių vertimas Sūra: Sūra Al-Vaaki`ah   Aja (Korano eilutė):

Surat Al-Waqi'ah

إِذَا وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ
Kitakaposimama Kiyama.
Tafsyrai arabų kalba:
لَيۡسَ لِوَقۡعَتِهَا كَاذِبَةٌ
Hakutakuwa na yoyote mwenye kukanusha kusimama kwake.
Tafsyrai arabų kalba:
خَافِضَةٞ رَّافِعَةٌ
Ni chenye kuwainamisha chini maadui wa Mwenyezi Mungu ndani ya Moto na ni chenye kuwainua juu Peponi wale wenye kumtegemea.
Tafsyrai arabų kalba:
إِذَا رُجَّتِ ٱلۡأَرۡضُ رَجّٗا
Itakapotikiswa ardhi mtikiso wa nguvu.
Tafsyrai arabų kalba:
وَبُسَّتِ ٱلۡجِبَالُ بَسّٗا
Na yakamumunyuliwa majabali mmumunyuo wa kina.
Tafsyrai arabų kalba:
فَكَانَتۡ هَبَآءٗ مُّنۢبَثّٗا
Yakawa vumbi lenye kuruka angani lililosukumwa na upepo.
Tafsyrai arabų kalba:
وَكُنتُمۡ أَزۡوَٰجٗا ثَلَٰثَةٗ
Na mkawa, enyi viumbe, makundi matatu:
Tafsyrai arabų kalba:
فَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ
Kundi la watu wa upande wa kulia, wenye daraja kubwa. Ni kikubwa kilioje cheo chao!
Tafsyrai arabų kalba:
وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ
Kuna na kundi la watu wa upande wa kushoto, wenye daraja duni. Ni mbaya iliyoje hali yao!
Tafsyrai arabų kalba:
وَٱلسَّٰبِقُونَ ٱلسَّٰبِقُونَ
Na wale waliotangulia mbele kwenye kheri duniani ndio wenye kutangulia mbele kwenye daraja za juu huko Akhera.
Tafsyrai arabų kalba:
أُوْلَٰٓئِكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ
Wao ndio walioletwa karibu kwa Mwenyezi Mungu,
Tafsyrai arabų kalba:
فِي جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Mola wao Atawatia kwenye mabustani ya Pepo ya starehe.
Tafsyrai arabų kalba:
ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ
Watayaingia watu wengi watu wa mwanzo wa ummah huu, na ummah wengineo wasiokuwa wao,
Tafsyrai arabų kalba:
وَقَلِيلٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ
na wachache miongoni mwa watu mwisho wa ummah huu,
Tafsyrai arabų kalba:
عَلَىٰ سُرُرٖ مَّوۡضُونَةٖ
wakiwa juu ya vitanda vilivyofumwa kwa dhahabu,
Tafsyrai arabų kalba:
مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيۡهَا مُتَقَٰبِلِينَ
na wakiwa katika hali ya kuvitegemea na huku wanaelekeana na kukutana.
Tafsyrai arabų kalba:
يَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ
Wanawazunguka wao kuwatumikia watumishi vijana wasiozeeka wala kufa,
Tafsyrai arabų kalba:
بِأَكۡوَابٖ وَأَبَارِيقَ وَكَأۡسٖ مِّن مَّعِينٖ
wakiwa na vikombe, mabirika na gilasi kutoka kwenye chemchemi ya pombe yenye kupita ndani ya Pepo,
Tafsyrai arabų kalba:
لَّا يُصَدَّعُونَ عَنۡهَا وَلَا يُنزِفُونَ
na hawaumwi na vichwa kutokana nayo wala hawarukwi na akili.
Tafsyrai arabų kalba:
وَفَٰكِهَةٖ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ
Na watawazunguka wao watumishi vijana na kila kitu wanachokichagua miongoni mwa matunda,
Tafsyrai arabų kalba:
وَلَحۡمِ طَيۡرٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ
nyama ya ndege ambayo nafsi zao inavutika nayo.
Tafsyrai arabų kalba:
وَحُورٌ عِينٞ
Na watakuwa na wanawake wenye macho makubwa kama kwamba wao,
Tafsyrai arabų kalba:
كَأَمۡثَٰلِ ٱللُّؤۡلُوِٕ ٱلۡمَكۡنُونِ
kwa usafi wao na uzuri wao, ni lulu iliyohifadhiwa ndani ya mashaza yake,
Tafsyrai arabų kalba:
جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
hali hayo yakiwa ni malipo yao kwa yale waliokuwa wakiyafanya duniani.
Tafsyrai arabų kalba:
لَا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا تَأۡثِيمًا
Hawatasikia humo Peponi ubatilifu wala yale ya kuwatia madhambini kuyasikia,
Tafsyrai arabų kalba:
إِلَّا قِيلٗا سَلَٰمٗا سَلَٰمٗا
isipokuwa maneno yasiyokuwa na kasoro hizi na kusalimiana wao kwa wao.
Tafsyrai arabų kalba:
وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ
Na watu wa upande wa kulia,
Tafsyrai arabų kalba:
فِي سِدۡرٖ مَّخۡضُودٖ
ni kikubwa kilioje cheo chao na malipo yao!
Tafsyrai arabų kalba:
وَطَلۡحٖ مَّنضُودٖ
Watakuwa kwenye mikunazi isiyo na miba, na ndizi zilizopandana na kupangika,
Tafsyrai arabų kalba:
وَظِلّٖ مَّمۡدُودٖ
kila ndizi juu ya nyingine, na vivuli vya daima visivyoondoka,
Tafsyrai arabų kalba:
وَمَآءٖ مَّسۡكُوبٖ
na maji yanayotembea yasiyokatika,
Tafsyrai arabų kalba:
وَفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ
na matunda mengi
Tafsyrai arabų kalba:
لَّا مَقۡطُوعَةٖ وَلَا مَمۡنُوعَةٖ
yasiyomalizika wala kuwaishia wala hakuna kizuizi chochote kinachowazuia wao kuyafikia,
Tafsyrai arabų kalba:
وَفُرُشٖ مَّرۡفُوعَةٍ
na matandiko yaliyoinuliwa juu ya vitanda.
Tafsyrai arabų kalba:
إِنَّآ أَنشَأۡنَٰهُنَّ إِنشَآءٗ
Sisi tumewaumba wanawake wa watu wa Peponi umbile ambalo silo lile umbile lililokuwa duniani, umbile lililokamilika lisilokubali kutoweka,
Tafsyrai arabų kalba:
فَجَعَلۡنَٰهُنَّ أَبۡكَارًا
na tumewafanya ni wanawali wenye kujipendekeza kwa waume zao,
Tafsyrai arabų kalba:
عُرُبًا أَتۡرَابٗا
hali ya kuwa ni marika na wao kimiaka.
Tafsyrai arabų kalba:
لِّأَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ
Tumewaumbia wanawake hao watu wa upande wa kulia.
Tafsyrai arabų kalba:
ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ
Nao ni kundi la watu wengi wa mwanzo
Tafsyrai arabų kalba:
وَثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ
na kundi la watu wengi wa mwisho.
Tafsyrai arabų kalba:
وَأَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ
Na watu wa upande wa kushoto, ni mbaya iliyoje hali yao na malipo yao!
Tafsyrai arabų kalba:
فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ
Watakuwa kwenye upepo ulio moto utokanao na joto la Moto wa Jahanamu utakaozuia pumzi zao, na maji moto yanayochemka,
Tafsyrai arabų kalba:
وَظِلّٖ مِّن يَحۡمُومٖ
na kivuli cha moshi mweusi sana,
Tafsyrai arabų kalba:
لَّا بَارِدٖ وَلَا كَرِيمٍ
usio na mashukio baridi wala mandhari mazuri.
Tafsyrai arabų kalba:
إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَبۡلَ ذَٰلِكَ مُتۡرَفِينَ
Kwani wao walikuwa duniani wakijistarehesha kwa vitu vya haramu wakijiepusha na yale ambayo Mitume walikuja nayo.
Tafsyrai arabų kalba:
وَكَانُواْ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلۡحِنثِ ٱلۡعَظِيمِ
Na walikuwa wamesimama wima katika kumkanusha Mwenyezi Mungu na kumshirikisha na kumuasi, na hawakuwa na nia ya kutubia kwa hayo.
Tafsyrai arabų kalba:
وَكَانُواْ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ
Na walikuwa wakisema hali ya kukanusha Ufufuzi, «Je hivi sisi tutafufuliwa tutakapokufa na tukawa mchanga na mifupa iliyochakaa?» Maneno yao hayo yanaonesha kuwa wao walikuwa wakiliona jambo hili la kufufuliwa kuwa liko mbali na ukweli na wakilikanusha.
Tafsyrai arabų kalba:
أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ
«Je tutafufuliwa sisi na hali baba zetu waliotangulia wamekuwa mchanga uliotapakaa kwenye ardhi?»
Tafsyrai arabų kalba:
قُلۡ إِنَّ ٱلۡأَوَّلِينَ وَٱلۡأٓخِرِينَ
Sema uwaambie, «Hakika wa mwanzo na wa mwisho miongoni mwa binadamu
Tafsyrai arabų kalba:
لَمَجۡمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ
watakusanywa katika Siku iliyowekewa wakati maalumu, nayo ni Siku ya Kiyama.
Tafsyrai arabų kalba:
ثُمَّ إِنَّكُمۡ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلۡمُكَذِّبُونَ
«Kisha nyinyi, enyi mliopotea njia ya uongofu mnaokanusha onyo la Mwenyezi Mungu na agizo Lake,
Tafsyrai arabų kalba:
لَأٓكِلُونَ مِن شَجَرٖ مِّن زَقُّومٖ
ni wenye kula kutokana na mti wa zaqqūm,
Tafsyrai arabų kalba:
فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ
nao ni katika miti mibaya zaidi, na ni wenye kujaza matumbo yenu kutokana nao kwa sababu ya ukali wa njaa,
Tafsyrai arabų kalba:
فَشَٰرِبُونَ عَلَيۡهِ مِنَ ٱلۡحَمِيمِ
na ni wenye kunywa juu yake maji yaliyo moto hadi ya mwisho, yasiyomaliza kiu.
Tafsyrai arabų kalba:
فَشَٰرِبُونَ شُرۡبَ ٱلۡهِيمِ
Mtayanywa maji hayo kwa wingi kama vile ngamia wenye kiu wasioshiba maji kwa ugonjwa uliowapata.»
Tafsyrai arabų kalba:
هَٰذَا نُزُلُهُمۡ يَوۡمَ ٱلدِّينِ
Adhabu hii watakayoipata ndiyo zawadi Aliyowaandalia Siku ya Kiyama. Katika haya kuna kuwalaumu na kuwacheza shere.
Tafsyrai arabų kalba:
نَحۡنُ خَلَقۡنَٰكُمۡ فَلَوۡلَا تُصَدِّقُونَ
Sisi tumewaumba, enyi watu, na hamkuwa kitu chochote. Basi si msadiki kuwa kuna kufufuliwa?
Tafsyrai arabų kalba:
أَفَرَءَيۡتُم مَّا تُمۡنُونَ
Mnayaonaje maji ya manii mnayoyatupa ndani ya vizazi vya wake zenu,
Tafsyrai arabų kalba:
ءَأَنتُمۡ تَخۡلُقُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡخَٰلِقُونَ
je nyinyi ndio mnaomuumba mwanadamu kutokana na hayo au ni sisi ndio wenye kuumba?
Tafsyrai arabų kalba:
نَحۡنُ قَدَّرۡنَا بَيۡنَكُمُ ٱلۡمَوۡتَ وَمَا نَحۡنُ بِمَسۡبُوقِينَ
Sisi tumekadiria kifo kwenu,
Tafsyrai arabų kalba:
عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ أَمۡثَٰلَكُمۡ وَنُنشِئَكُمۡ فِي مَا لَا تَعۡلَمُونَ
na sisi si wenye kushindwa kubadilisha umbo lenu Siku ya Kiyama na kuwaumba kwa sifa na namna msizozijua.
Tafsyrai arabų kalba:
وَلَقَدۡ عَلِمۡتُمُ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُولَىٰ فَلَوۡلَا تَذَكَّرُونَ
Na hakika mlijua kuwa Mwenyezi Mungu Aliwaumba uumbaji wa kwanza na hamkuwa kitu chochote. Basi si mkumbuke uweza wa Mwenyezi Mungu wa kuwaumba mara nyingine?
Tafsyrai arabų kalba:
أَفَرَءَيۡتُم مَّا تَحۡرُثُونَ
Mnazionaje mbegu mnazozipanda?
Tafsyrai arabų kalba:
ءَأَنتُمۡ تَزۡرَعُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلزَّٰرِعُونَ
Je ni nyinyi mnaoziotesha kutoka ardhini? Sisi ndio tuaozituliza na kuziotesha ardhini.
Tafsyrai arabų kalba:
لَوۡ نَشَآءُ لَجَعَلۡنَٰهُ حُطَٰمٗا فَظَلۡتُمۡ تَفَكَّهُونَ
Lau tungalitaka tungaliifanya mimea inayotokana na mbegu hizo kuwa mapepe, haimkiniki kunufaika nayo kwa kula,
Tafsyrai arabų kalba:
إِنَّا لَمُغۡرَمُونَ
mkawa mnaona ajabu kwa kilichoshukia mimea yenu na mnasema, «Sisi tumepata hasara na ni wenye kuungulika.
Tafsyrai arabų kalba:
بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ
Bali sisi tumekoseshwa riziki.»
Tafsyrai arabų kalba:
أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلۡمَآءَ ٱلَّذِي تَشۡرَبُونَ
Mnayaonaje maji mnayokunywa ili mhuike kwayo?
Tafsyrai arabų kalba:
ءَأَنتُمۡ أَنزَلۡتُمُوهُ مِنَ ٱلۡمُزۡنِ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنزِلُونَ
Je ni nyinyi mliyoyateremsha kutoka kwenye mawingu hadi kwenye kituo cha ardhi au ni sisi tuliyoyateremsha ili kuwarehemu nyinyi?
Tafsyrai arabų kalba:
لَوۡ نَشَآءُ جَعَلۡنَٰهُ أُجَاجٗا فَلَوۡلَا تَشۡكُرُونَ
Lau tungalitaka tungaliyafanya maji haya yawe na chumvi sana, ikiwa haiwezekani kunufaika nayo kwa kunywa wala kwa mimea. Basi si mumshukuru Mola wenu kwa kuteremsha maji tamu kwa kuwanufaisha nyinyi.
Tafsyrai arabų kalba:
أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلنَّارَ ٱلَّتِي تُورُونَ
Mnaouonaje moto mnaouwasha?
Tafsyrai arabų kalba:
ءَأَنتُمۡ أَنشَأۡتُمۡ شَجَرَتَهَآ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنشِـُٔونَ
Je ni nyinyi mlioufanya mti wake, unaozalisha moto kwa kukwaruzwa, upatikane au ni sisi tulioufanya upatikane?
Tafsyrai arabų kalba:
نَحۡنُ جَعَلۡنَٰهَا تَذۡكِرَةٗ وَمَتَٰعٗا لِّلۡمُقۡوِينَ
Sisi tumeufanya moto wenu mnaouwasha ni ukumbusho kwenu wa Moto wa Jahanamu na pia ni manufaa kwa wasafiri.
Tafsyrai arabų kalba:
فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ
Basi mtakase Mola wako, ewe Nabii, Aliye mtukufu Mwenye ukamilifu wa majina na sifa, Mwingi wa wema na kheri.
Tafsyrai arabų kalba:
۞ فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَوَٰقِعِ ٱلنُّجُومِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mapomoko ya nyota nyakati za kuzama kwake mbinguni.
Tafsyrai arabų kalba:
وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٞ لَّوۡ تَعۡلَمُونَ عَظِيمٌ
Nacho ni kiapo kikubwa lau mnajua kadiri yake.
Tafsyrai arabų kalba:
إِنَّهُۥ لَقُرۡءَانٞ كَرِيمٞ
Hakika hii Qur’ani iliyoteremshiwa Muhammad ni Qur’ani yenye manufaa makubwa, yenye kheri nyingi na yenye elimu tele,
Tafsyrai arabų kalba:
فِي كِتَٰبٖ مَّكۡنُونٖ
iliyo ndani ya Kitabu kilichohifadhiwa, kilichofichwa na macho ya viumbe, nacho ni Kitabu ambacho kiko mikononi mwa Malaika.
Tafsyrai arabų kalba:
لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُطَهَّرُونَ
Hawaigusi Qur’ani isipokuwa malaika watukufu ambao Mwenyezi Mungu Amewasafisha na aibu na madhambi. Na pia hawaigusi isipokuwa watu waliojitohirisha na ushirikina na janaba na ukosefu wa udhu.
Tafsyrai arabų kalba:
تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na hii Qur’ani tukufu imeteremshwa kutoka kwa Mola wa viumbe vyote, kwani hiyo ndiyo haki isiyo na shaka ndani yake.
Tafsyrai arabų kalba:
أَفَبِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ أَنتُم مُّدۡهِنُونَ
je hii Qur’ani, enyi washirikina, mnaikanusha?
Tafsyrai arabų kalba:
وَتَجۡعَلُونَ رِزۡقَكُمۡ أَنَّكُمۡ تُكَذِّبُونَ
Na je mnaifanya shukrani yenu kwa neema za Mola wenu ni kuwa nyinyi mnazikanusha na kukufuru? Hapa pana makaripio kwa anayedharau amri za Qur’ani na kutojali mwito wake.
Tafsyrai arabų kalba:
فَلَوۡلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلۡحُلۡقُومَ
Basi je mnaweza pindi roho ya mmoja wenu inapofika kwenye koo katika uchungu wa kifo,
Tafsyrai arabų kalba:
وَأَنتُمۡ حِينَئِذٖ تَنظُرُونَ
na hali nyinyi mmehudhuria mnamtazama, kuizuia roho yake ndani ya mwili wake? Hamtaweza hilo!
Tafsyrai arabų kalba:
وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنكُمۡ وَلَٰكِن لَّا تُبۡصِرُونَ
Na sisi tuko karibu na yeye zaidi, kupitia Malaika wetu, kuliko nyinyi, lakini nyinyi hamuwaoni.
Tafsyrai arabų kalba:
فَلَوۡلَآ إِن كُنتُمۡ غَيۡرَ مَدِينِينَ
Na je mnaweza, iwapo nyinyi si wenye kuhesabiwa wala kulipwa kwa matendo yenu,
Tafsyrai arabų kalba:
تَرۡجِعُونَهَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
kuirudisha roho kwenye mwili, iwapo nyinyi ni wakweli? Hamtaweza kuirudisha.
Tafsyrai arabų kalba:
فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ
Basi iwapo yule anayekufa ni kati ya watu wa upande wa kulia, atapata rehema kunjufu na furaha,
Tafsyrai arabų kalba:
فَرَوۡحٞ وَرَيۡحَانٞ وَجَنَّتُ نَعِيمٖ
wakati wa kufa kwake, na kila kinachoifurahisha nafsi yake, Na atapata Pepo ya starehe huko Akhera.
Tafsyrai arabų kalba:
وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ
Na iwapo yule anayekufa ni kati ya watu wa upande wa kulia,
Tafsyrai arabų kalba:
فَسَلَٰمٞ لَّكَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ
ataambiwa, «Umesalimika na kuwa kwenye amani, kwa kuwa wewe ni miongoni mwa watu wa upande wa kulia.»
Tafsyrai arabų kalba:
وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُكَذِّبِينَ ٱلضَّآلِّينَ
Na iwapo yule anayekufa ni miongoni mwa wenye kukanusha kufufuliwa, waliopotoka na njia ya uongofu,
Tafsyrai arabų kalba:
فَنُزُلٞ مِّنۡ حَمِيمٖ
basi atapata makaribisho ya kinywaji cha moto wa Jahanamu kilichochemshwa, kilicho na joto hadi ya mwisho,
Tafsyrai arabų kalba:
وَتَصۡلِيَةُ جَحِيمٍ
na atachomwa na Moto na aungulike na adhabu yake kali.
Tafsyrai arabų kalba:
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ ٱلۡيَقِينِ
Hakika habari hii tumezokuelezea, ewe Mtume, ni ukweli wa yakini usio na shaka.
Tafsyrai arabų kalba:
فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ
Basi litakase jina la Mola wako Aliyetukuka na umtakase na yale ambayo madhalimu na wenye kukanusha wanayasema. Mwenyezi Mungu Yuko juu ya yale wanayoyasema ujuu mkubwa sana.
Tafsyrai arabų kalba:
 
Reikšmių vertimas Sūra: Sūra Al-Vaaki`ah
Sūrų turinys Puslapio numeris
 
Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Abdullah Muchammed ir Naser Khamis - Vertimų turinys

Kilniojo Korano reikšmių vertimas į suahilių k., išvertė Dr. Abdullah Muchammed Abu Bakr ir šeichas Naser Khamis.

Uždaryti