ಪವಿತ್ರ ಕುರ್‌ಆನ್ ಅರ್ಥಾನುವಾದ - ಸ್ವಾಹಿಲಿ ಅನುವಾದ - ಅಬ್ದುಲ್ಲಾ ಮುಹಮ್ಮದ್ ಮತ್ತು ನಾಸಿರ್ ಖಮೀಸ್ * - ಅನುವಾದಗಳ ವಿಷಯಸೂಚಿ


ಅರ್ಥಗಳ ಅನುವಾದ ಅಧ್ಯಾಯ: ಸೂರ ಅಲ್ -ವಾಕಿಅ   ಶ್ಲೋಕ:

Surat Al-Waqi'ah

إِذَا وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ
Kitakaposimama Kiyama.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
لَيۡسَ لِوَقۡعَتِهَا كَاذِبَةٌ
Hakutakuwa na yoyote mwenye kukanusha kusimama kwake.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
خَافِضَةٞ رَّافِعَةٌ
Ni chenye kuwainamisha chini maadui wa Mwenyezi Mungu ndani ya Moto na ni chenye kuwainua juu Peponi wale wenye kumtegemea.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
إِذَا رُجَّتِ ٱلۡأَرۡضُ رَجّٗا
Itakapotikiswa ardhi mtikiso wa nguvu.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَبُسَّتِ ٱلۡجِبَالُ بَسّٗا
Na yakamumunyuliwa majabali mmumunyuo wa kina.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَكَانَتۡ هَبَآءٗ مُّنۢبَثّٗا
Yakawa vumbi lenye kuruka angani lililosukumwa na upepo.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَكُنتُمۡ أَزۡوَٰجٗا ثَلَٰثَةٗ
Na mkawa, enyi viumbe, makundi matatu:
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ
Kundi la watu wa upande wa kulia, wenye daraja kubwa. Ni kikubwa kilioje cheo chao!
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ
Kuna na kundi la watu wa upande wa kushoto, wenye daraja duni. Ni mbaya iliyoje hali yao!
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَٱلسَّٰبِقُونَ ٱلسَّٰبِقُونَ
Na wale waliotangulia mbele kwenye kheri duniani ndio wenye kutangulia mbele kwenye daraja za juu huko Akhera.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
أُوْلَٰٓئِكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ
Wao ndio walioletwa karibu kwa Mwenyezi Mungu,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فِي جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Mola wao Atawatia kwenye mabustani ya Pepo ya starehe.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ
Watayaingia watu wengi watu wa mwanzo wa ummah huu, na ummah wengineo wasiokuwa wao,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَقَلِيلٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ
na wachache miongoni mwa watu mwisho wa ummah huu,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
عَلَىٰ سُرُرٖ مَّوۡضُونَةٖ
wakiwa juu ya vitanda vilivyofumwa kwa dhahabu,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيۡهَا مُتَقَٰبِلِينَ
na wakiwa katika hali ya kuvitegemea na huku wanaelekeana na kukutana.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
يَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ
Wanawazunguka wao kuwatumikia watumishi vijana wasiozeeka wala kufa,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
بِأَكۡوَابٖ وَأَبَارِيقَ وَكَأۡسٖ مِّن مَّعِينٖ
wakiwa na vikombe, mabirika na gilasi kutoka kwenye chemchemi ya pombe yenye kupita ndani ya Pepo,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
لَّا يُصَدَّعُونَ عَنۡهَا وَلَا يُنزِفُونَ
na hawaumwi na vichwa kutokana nayo wala hawarukwi na akili.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَفَٰكِهَةٖ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ
Na watawazunguka wao watumishi vijana na kila kitu wanachokichagua miongoni mwa matunda,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَلَحۡمِ طَيۡرٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ
nyama ya ndege ambayo nafsi zao inavutika nayo.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَحُورٌ عِينٞ
Na watakuwa na wanawake wenye macho makubwa kama kwamba wao,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
كَأَمۡثَٰلِ ٱللُّؤۡلُوِٕ ٱلۡمَكۡنُونِ
kwa usafi wao na uzuri wao, ni lulu iliyohifadhiwa ndani ya mashaza yake,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
hali hayo yakiwa ni malipo yao kwa yale waliokuwa wakiyafanya duniani.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
لَا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا تَأۡثِيمًا
Hawatasikia humo Peponi ubatilifu wala yale ya kuwatia madhambini kuyasikia,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
إِلَّا قِيلٗا سَلَٰمٗا سَلَٰمٗا
isipokuwa maneno yasiyokuwa na kasoro hizi na kusalimiana wao kwa wao.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ
Na watu wa upande wa kulia,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فِي سِدۡرٖ مَّخۡضُودٖ
ni kikubwa kilioje cheo chao na malipo yao!
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَطَلۡحٖ مَّنضُودٖ
Watakuwa kwenye mikunazi isiyo na miba, na ndizi zilizopandana na kupangika,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَظِلّٖ مَّمۡدُودٖ
kila ndizi juu ya nyingine, na vivuli vya daima visivyoondoka,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَمَآءٖ مَّسۡكُوبٖ
na maji yanayotembea yasiyokatika,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ
na matunda mengi
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
لَّا مَقۡطُوعَةٖ وَلَا مَمۡنُوعَةٖ
yasiyomalizika wala kuwaishia wala hakuna kizuizi chochote kinachowazuia wao kuyafikia,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَفُرُشٖ مَّرۡفُوعَةٍ
na matandiko yaliyoinuliwa juu ya vitanda.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
إِنَّآ أَنشَأۡنَٰهُنَّ إِنشَآءٗ
Sisi tumewaumba wanawake wa watu wa Peponi umbile ambalo silo lile umbile lililokuwa duniani, umbile lililokamilika lisilokubali kutoweka,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَجَعَلۡنَٰهُنَّ أَبۡكَارًا
na tumewafanya ni wanawali wenye kujipendekeza kwa waume zao,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
عُرُبًا أَتۡرَابٗا
hali ya kuwa ni marika na wao kimiaka.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
لِّأَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ
Tumewaumbia wanawake hao watu wa upande wa kulia.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ
Nao ni kundi la watu wengi wa mwanzo
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ
na kundi la watu wengi wa mwisho.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَأَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ
Na watu wa upande wa kushoto, ni mbaya iliyoje hali yao na malipo yao!
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ
Watakuwa kwenye upepo ulio moto utokanao na joto la Moto wa Jahanamu utakaozuia pumzi zao, na maji moto yanayochemka,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَظِلّٖ مِّن يَحۡمُومٖ
na kivuli cha moshi mweusi sana,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
لَّا بَارِدٖ وَلَا كَرِيمٍ
usio na mashukio baridi wala mandhari mazuri.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَبۡلَ ذَٰلِكَ مُتۡرَفِينَ
Kwani wao walikuwa duniani wakijistarehesha kwa vitu vya haramu wakijiepusha na yale ambayo Mitume walikuja nayo.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَكَانُواْ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلۡحِنثِ ٱلۡعَظِيمِ
Na walikuwa wamesimama wima katika kumkanusha Mwenyezi Mungu na kumshirikisha na kumuasi, na hawakuwa na nia ya kutubia kwa hayo.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَكَانُواْ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ
Na walikuwa wakisema hali ya kukanusha Ufufuzi, «Je hivi sisi tutafufuliwa tutakapokufa na tukawa mchanga na mifupa iliyochakaa?» Maneno yao hayo yanaonesha kuwa wao walikuwa wakiliona jambo hili la kufufuliwa kuwa liko mbali na ukweli na wakilikanusha.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ
«Je tutafufuliwa sisi na hali baba zetu waliotangulia wamekuwa mchanga uliotapakaa kwenye ardhi?»
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
قُلۡ إِنَّ ٱلۡأَوَّلِينَ وَٱلۡأٓخِرِينَ
Sema uwaambie, «Hakika wa mwanzo na wa mwisho miongoni mwa binadamu
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
لَمَجۡمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ
watakusanywa katika Siku iliyowekewa wakati maalumu, nayo ni Siku ya Kiyama.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
ثُمَّ إِنَّكُمۡ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلۡمُكَذِّبُونَ
«Kisha nyinyi, enyi mliopotea njia ya uongofu mnaokanusha onyo la Mwenyezi Mungu na agizo Lake,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
لَأٓكِلُونَ مِن شَجَرٖ مِّن زَقُّومٖ
ni wenye kula kutokana na mti wa zaqqūm,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ
nao ni katika miti mibaya zaidi, na ni wenye kujaza matumbo yenu kutokana nao kwa sababu ya ukali wa njaa,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَشَٰرِبُونَ عَلَيۡهِ مِنَ ٱلۡحَمِيمِ
na ni wenye kunywa juu yake maji yaliyo moto hadi ya mwisho, yasiyomaliza kiu.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَشَٰرِبُونَ شُرۡبَ ٱلۡهِيمِ
Mtayanywa maji hayo kwa wingi kama vile ngamia wenye kiu wasioshiba maji kwa ugonjwa uliowapata.»
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
هَٰذَا نُزُلُهُمۡ يَوۡمَ ٱلدِّينِ
Adhabu hii watakayoipata ndiyo zawadi Aliyowaandalia Siku ya Kiyama. Katika haya kuna kuwalaumu na kuwacheza shere.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
نَحۡنُ خَلَقۡنَٰكُمۡ فَلَوۡلَا تُصَدِّقُونَ
Sisi tumewaumba, enyi watu, na hamkuwa kitu chochote. Basi si msadiki kuwa kuna kufufuliwa?
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
أَفَرَءَيۡتُم مَّا تُمۡنُونَ
Mnayaonaje maji ya manii mnayoyatupa ndani ya vizazi vya wake zenu,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
ءَأَنتُمۡ تَخۡلُقُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡخَٰلِقُونَ
je nyinyi ndio mnaomuumba mwanadamu kutokana na hayo au ni sisi ndio wenye kuumba?
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
نَحۡنُ قَدَّرۡنَا بَيۡنَكُمُ ٱلۡمَوۡتَ وَمَا نَحۡنُ بِمَسۡبُوقِينَ
Sisi tumekadiria kifo kwenu,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ أَمۡثَٰلَكُمۡ وَنُنشِئَكُمۡ فِي مَا لَا تَعۡلَمُونَ
na sisi si wenye kushindwa kubadilisha umbo lenu Siku ya Kiyama na kuwaumba kwa sifa na namna msizozijua.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَلَقَدۡ عَلِمۡتُمُ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُولَىٰ فَلَوۡلَا تَذَكَّرُونَ
Na hakika mlijua kuwa Mwenyezi Mungu Aliwaumba uumbaji wa kwanza na hamkuwa kitu chochote. Basi si mkumbuke uweza wa Mwenyezi Mungu wa kuwaumba mara nyingine?
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
أَفَرَءَيۡتُم مَّا تَحۡرُثُونَ
Mnazionaje mbegu mnazozipanda?
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
ءَأَنتُمۡ تَزۡرَعُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلزَّٰرِعُونَ
Je ni nyinyi mnaoziotesha kutoka ardhini? Sisi ndio tuaozituliza na kuziotesha ardhini.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
لَوۡ نَشَآءُ لَجَعَلۡنَٰهُ حُطَٰمٗا فَظَلۡتُمۡ تَفَكَّهُونَ
Lau tungalitaka tungaliifanya mimea inayotokana na mbegu hizo kuwa mapepe, haimkiniki kunufaika nayo kwa kula,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
إِنَّا لَمُغۡرَمُونَ
mkawa mnaona ajabu kwa kilichoshukia mimea yenu na mnasema, «Sisi tumepata hasara na ni wenye kuungulika.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ
Bali sisi tumekoseshwa riziki.»
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلۡمَآءَ ٱلَّذِي تَشۡرَبُونَ
Mnayaonaje maji mnayokunywa ili mhuike kwayo?
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
ءَأَنتُمۡ أَنزَلۡتُمُوهُ مِنَ ٱلۡمُزۡنِ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنزِلُونَ
Je ni nyinyi mliyoyateremsha kutoka kwenye mawingu hadi kwenye kituo cha ardhi au ni sisi tuliyoyateremsha ili kuwarehemu nyinyi?
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
لَوۡ نَشَآءُ جَعَلۡنَٰهُ أُجَاجٗا فَلَوۡلَا تَشۡكُرُونَ
Lau tungalitaka tungaliyafanya maji haya yawe na chumvi sana, ikiwa haiwezekani kunufaika nayo kwa kunywa wala kwa mimea. Basi si mumshukuru Mola wenu kwa kuteremsha maji tamu kwa kuwanufaisha nyinyi.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلنَّارَ ٱلَّتِي تُورُونَ
Mnaouonaje moto mnaouwasha?
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
ءَأَنتُمۡ أَنشَأۡتُمۡ شَجَرَتَهَآ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنشِـُٔونَ
Je ni nyinyi mlioufanya mti wake, unaozalisha moto kwa kukwaruzwa, upatikane au ni sisi tulioufanya upatikane?
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
نَحۡنُ جَعَلۡنَٰهَا تَذۡكِرَةٗ وَمَتَٰعٗا لِّلۡمُقۡوِينَ
Sisi tumeufanya moto wenu mnaouwasha ni ukumbusho kwenu wa Moto wa Jahanamu na pia ni manufaa kwa wasafiri.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ
Basi mtakase Mola wako, ewe Nabii, Aliye mtukufu Mwenye ukamilifu wa majina na sifa, Mwingi wa wema na kheri.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
۞ فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَوَٰقِعِ ٱلنُّجُومِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mapomoko ya nyota nyakati za kuzama kwake mbinguni.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٞ لَّوۡ تَعۡلَمُونَ عَظِيمٌ
Nacho ni kiapo kikubwa lau mnajua kadiri yake.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
إِنَّهُۥ لَقُرۡءَانٞ كَرِيمٞ
Hakika hii Qur’ani iliyoteremshiwa Muhammad ni Qur’ani yenye manufaa makubwa, yenye kheri nyingi na yenye elimu tele,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فِي كِتَٰبٖ مَّكۡنُونٖ
iliyo ndani ya Kitabu kilichohifadhiwa, kilichofichwa na macho ya viumbe, nacho ni Kitabu ambacho kiko mikononi mwa Malaika.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُطَهَّرُونَ
Hawaigusi Qur’ani isipokuwa malaika watukufu ambao Mwenyezi Mungu Amewasafisha na aibu na madhambi. Na pia hawaigusi isipokuwa watu waliojitohirisha na ushirikina na janaba na ukosefu wa udhu.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na hii Qur’ani tukufu imeteremshwa kutoka kwa Mola wa viumbe vyote, kwani hiyo ndiyo haki isiyo na shaka ndani yake.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
أَفَبِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ أَنتُم مُّدۡهِنُونَ
je hii Qur’ani, enyi washirikina, mnaikanusha?
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَتَجۡعَلُونَ رِزۡقَكُمۡ أَنَّكُمۡ تُكَذِّبُونَ
Na je mnaifanya shukrani yenu kwa neema za Mola wenu ni kuwa nyinyi mnazikanusha na kukufuru? Hapa pana makaripio kwa anayedharau amri za Qur’ani na kutojali mwito wake.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَلَوۡلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلۡحُلۡقُومَ
Basi je mnaweza pindi roho ya mmoja wenu inapofika kwenye koo katika uchungu wa kifo,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَأَنتُمۡ حِينَئِذٖ تَنظُرُونَ
na hali nyinyi mmehudhuria mnamtazama, kuizuia roho yake ndani ya mwili wake? Hamtaweza hilo!
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنكُمۡ وَلَٰكِن لَّا تُبۡصِرُونَ
Na sisi tuko karibu na yeye zaidi, kupitia Malaika wetu, kuliko nyinyi, lakini nyinyi hamuwaoni.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَلَوۡلَآ إِن كُنتُمۡ غَيۡرَ مَدِينِينَ
Na je mnaweza, iwapo nyinyi si wenye kuhesabiwa wala kulipwa kwa matendo yenu,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
تَرۡجِعُونَهَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
kuirudisha roho kwenye mwili, iwapo nyinyi ni wakweli? Hamtaweza kuirudisha.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ
Basi iwapo yule anayekufa ni kati ya watu wa upande wa kulia, atapata rehema kunjufu na furaha,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَرَوۡحٞ وَرَيۡحَانٞ وَجَنَّتُ نَعِيمٖ
wakati wa kufa kwake, na kila kinachoifurahisha nafsi yake, Na atapata Pepo ya starehe huko Akhera.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ
Na iwapo yule anayekufa ni kati ya watu wa upande wa kulia,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَسَلَٰمٞ لَّكَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ
ataambiwa, «Umesalimika na kuwa kwenye amani, kwa kuwa wewe ni miongoni mwa watu wa upande wa kulia.»
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُكَذِّبِينَ ٱلضَّآلِّينَ
Na iwapo yule anayekufa ni miongoni mwa wenye kukanusha kufufuliwa, waliopotoka na njia ya uongofu,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَنُزُلٞ مِّنۡ حَمِيمٖ
basi atapata makaribisho ya kinywaji cha moto wa Jahanamu kilichochemshwa, kilicho na joto hadi ya mwisho,
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
وَتَصۡلِيَةُ جَحِيمٍ
na atachomwa na Moto na aungulike na adhabu yake kali.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ ٱلۡيَقِينِ
Hakika habari hii tumezokuelezea, ewe Mtume, ni ukweli wa yakini usio na shaka.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ
Basi litakase jina la Mola wako Aliyetukuka na umtakase na yale ambayo madhalimu na wenye kukanusha wanayasema. Mwenyezi Mungu Yuko juu ya yale wanayoyasema ujuu mkubwa sana.
ಅರಬ್ಬಿ ವ್ಯಾಖ್ಯಾನಗಳು:
 
ಅರ್ಥಗಳ ಅನುವಾದ ಅಧ್ಯಾಯ: ಸೂರ ಅಲ್ -ವಾಕಿಅ
ಅಧ್ಯಾಯಗಳ ವಿಷಯಸೂಚಿ ಪುಟ ಸಂಖ್ಯೆ
 
ಪವಿತ್ರ ಕುರ್‌ಆನ್ ಅರ್ಥಾನುವಾದ - ಸ್ವಾಹಿಲಿ ಅನುವಾದ - ಅಬ್ದುಲ್ಲಾ ಮುಹಮ್ಮದ್ ಮತ್ತು ನಾಸಿರ್ ಖಮೀಸ್ - ಅನುವಾದಗಳ ವಿಷಯಸೂಚಿ

ಪವಿತ್ರ ಕುರ್‌ಆನ್ ಸ್ವಾಹಿಲಿ ಅರ್ಥಾನುವಾದ - ಡಾ. ಅಬ್ದುಲ್ಲಾ ಮುಹಮ್ಮದ್ ಅಬೂಬಕರ್ ಮತ್ತು ಶೈಖ್ ನಾಸಿರ್ ಖಮೀಸ್

ಮುಚ್ಚಿ