Check out the new design

വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്. * - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക


പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: ത്വാഹാ   ആയത്ത്:
وَأَنَا ٱخۡتَرۡتُكَ فَٱسۡتَمِعۡ لِمَا يُوحَىٰٓ
Na mimi nimekuteua , ewe Mūsā, kwa ujumbe wangu, basi sikiliza yale unayoletewa ya wahyi kutoka kwangu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّنِيٓ أَنَا ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّآ أَنَا۠ فَٱعۡبُدۡنِي وَأَقِمِ ٱلصَّلَوٰةَ لِذِكۡرِيٓ
Mimi Ndiye Mwenyezi Mungu, hakuna mwenye kuabudiwa kwa haki isipokuwa mimi, sina mshirika, basi niabudu mimi na usimamishe Swala ili unikumbuke ndani yake.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّ ٱلسَّاعَةَ ءَاتِيَةٌ أَكَادُ أُخۡفِيهَا لِتُجۡزَىٰ كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا تَسۡعَىٰ
Hakika Kiyama ambacho watu hapo watafufuliwa hapana budi ni chenye kutukia. Nakaribia kukificha kwangu mimi mwenyewe, basi ni vipi atakijua mtu yoyote miongoni mwa viumbe. Hivyo ni apate kulipwa kila mtu kwa alilolitenda ulimwenguni, liwe zuri au baya.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَلَا يَصُدَّنَّكَ عَنۡهَا مَن لَّا يُؤۡمِنُ بِهَا وَٱتَّبَعَ هَوَىٰهُ فَتَرۡدَىٰ
Basi asikuepushe, ewe Mūsā, na kukiamini na kujitayarisha nacho, asiyekikubali kuwa kitatukia na asiyetenda ya kumfaa huko na akayafuata matamanio ya nafsi yake na akakikanusha, kwani ukifanya hivyo utaangamia.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَمَا تِلۡكَ بِيَمِينِكَ يَٰمُوسَىٰ
Na ni nini hii iliyo kwenye mkono wako wa kulia, ewe Mūsā?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالَ هِيَ عَصَايَ أَتَوَكَّؤُاْ عَلَيۡهَا وَأَهُشُّ بِهَا عَلَىٰ غَنَمِي وَلِيَ فِيهَا مَـَٔارِبُ أُخۡرَىٰ
Akasema Mūsā, «Hii ni ni fimbo yangu, naitegemea katika kwenda na ninapigia miti ili mbuzi wangu walishe majani yake yanayoanguka na pia nina maslahi nayo mengine.»
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالَ أَلۡقِهَا يَٰمُوسَىٰ
Mwenyezi Mungu Akamwambia Mūsā, «Itupe fimbo yako!»
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَأَلۡقَىٰهَا فَإِذَا هِيَ حَيَّةٞ تَسۡعَىٰ
Mūsā akaitupa chini, ikageuka kwa amri ya Mwenyezi Mungu ikawa nyoka anayetembea, na Mūsā akaona jambo kubwa na akazunguka kukimbia.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالَ خُذۡهَا وَلَا تَخَفۡۖ سَنُعِيدُهَا سِيرَتَهَا ٱلۡأُولَىٰ
Mwenyezi Mungu Akasema kumwambia Mūsā, «Mshike huyo nyoka na usimuogope, tutamrudisha kuwa fimbo vile alivyokuwa mwanzo.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَٱضۡمُمۡ يَدَكَ إِلَىٰ جَنَاحِكَ تَخۡرُجۡ بَيۡضَآءَ مِنۡ غَيۡرِ سُوٓءٍ ءَايَةً أُخۡرَىٰ
Na ukumbatie mkono wako kwenye ubavu wako chini ya shina la mkono utatoka hali ni mweupe kama barafu bila ya kuwa na mbalanga, ili iwe ni alama nyingine.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
لِنُرِيَكَ مِنۡ ءَايَٰتِنَا ٱلۡكُبۡرَى
Tumefanya hivyo ili kukuonesha , ewe Mūsā, dalili zetu kubwa zenye kutolea ushahidi uweza wetu, ukubwa wa ufalme wetu na usahihi wa utume wako.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ
Enda, ewe Mūsā, kwa Fir'awn, kwa kuwa yeye amepitisha kipimo chake na ametoka kwenye utiifu wa Mola wake, umuite kwenye kumpwekesha Mwenyezi Mungu na kumuabudu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالَ رَبِّ ٱشۡرَحۡ لِي صَدۡرِي
Mūsā akasema, «Ewe Mola wangu! Nikunjulie kifua changu,
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَيَسِّرۡ لِيٓ أَمۡرِي
nirahisishie mambo yangu
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَٱحۡلُلۡ عُقۡدَةٗ مِّن لِّسَانِي
na nifungulie ulimi wangu uwe na ufasaha wa matamshi,
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
يَفۡقَهُواْ قَوۡلِي
ili waelewe maneno yangu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَٱجۡعَل لِّي وَزِيرٗا مِّنۡ أَهۡلِي
Na unipatie msaidizi miongoni mwa watu wangu,
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
هَٰرُونَ أَخِي
naye ni Hārūn ndugu yangu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
ٱشۡدُدۡ بِهِۦٓ أَزۡرِي
Nitilie nguvu kwa yeye na uuthibitishe mgongo wangu kwa ajili yake.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَأَشۡرِكۡهُ فِيٓ أَمۡرِي
Na umshirikishe na mimi katika unabii na ufikishaji ujumbe.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
كَيۡ نُسَبِّحَكَ كَثِيرٗا
Tupate kukuepusha na kila sifa ya upungufu na tukutakase kwa wingi,
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَنَذۡكُرَكَ كَثِيرًا
na tukutaje kwa wingi na tukushukuru.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّكَ كُنتَ بِنَا بَصِيرٗا
Kwa hakika, wewe ni mwenye kutuona, hakuna chochote kinachofichika kwako miongoni mwa vitendo vyetu.»
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالَ قَدۡ أُوتِيتَ سُؤۡلَكَ يَٰمُوسَىٰ
Mwenyezi Mungu Akasema, «Nishakupa kila ulichokiomba, ewe Mūsā.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَلَقَدۡ مَنَنَّا عَلَيۡكَ مَرَّةً أُخۡرَىٰٓ
«Na tulikupa , ewe Mūsā, kabla ya neema hii, neema nyingine ulipokuwa ni mtoto wa kunyonya tukakuokoa na unyanyasaji wa Fir'awn.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
 
പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: ത്വാഹാ
സൂറത്തുകളുടെ സൂചിക പേജ് നമ്പർ
 
വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്. - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക

വിവർത്തനം: ഡോ. അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് അബൂബക്കർ & ശൈഖ് നാസ്വിർ ഖമീസ്

അടക്കുക