Check out the new design

വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - റുവ്വാദ് തർജമ സെൻ്റർ * - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക


പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: സ്സ്വാഫ്ഫാത്ത്   ആയത്ത്:

As-Saffat

وَٱلصَّٰٓفَّٰتِ صَفّٗا
Ninaapa kwa wanaojipanga kwa safu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَٱلزَّٰجِرَٰتِ زَجۡرٗا
Na kwa wenye kukataza mabaya.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَٱلتَّٰلِيَٰتِ ذِكۡرًا
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّ إِلَٰهَكُمۡ لَوَٰحِدٞ
Hakika mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
رَّبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا وَرَبُّ ٱلۡمَشَٰرِقِ
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّا زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنۡيَا بِزِينَةٍ ٱلۡكَوَاكِبِ
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَحِفۡظٗا مِّن كُلِّ شَيۡطَٰنٖ مَّارِدٖ
Na kulinda na kila shetani muasi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى ٱلۡمَلَإِ ٱلۡأَعۡلَىٰ وَيُقۡذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٖ
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
دُحُورٗاۖ وَلَهُمۡ عَذَابٞ وَاصِبٌ
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِلَّا مَنۡ خَطِفَ ٱلۡخَطۡفَةَ فَأَتۡبَعَهُۥ شِهَابٞ ثَاقِبٞ
Isipokuwa anayenyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinachong'ara.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَٱسۡتَفۡتِهِمۡ أَهُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَم مَّنۡ خَلَقۡنَآۚ إِنَّا خَلَقۡنَٰهُم مِّن طِينٖ لَّازِبِۭ
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tuliowaumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unaonata.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
بَلۡ عَجِبۡتَ وَيَسۡخَرُونَ
Bali unastaajabu, na wao wanafanya masihara.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِذَا ذُكِّرُواْ لَا يَذۡكُرُونَ
Na wanapokumbushwa, hawakumbuki.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِذَا رَأَوۡاْ ءَايَةٗ يَسۡتَسۡخِرُونَ
Na wanapoona Ishara, wanafanya masihara.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَقَالُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ مُّبِينٌ
Na husema: Haya si chochote isipokuwa ni uchawi tu ulio dhahiri.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ
Ati tukishakufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ
Hata baba zetu wa zamani?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قُلۡ نَعَمۡ وَأَنتُمۡ دَٰخِرُونَ
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ فَإِذَا هُمۡ يَنظُرُونَ
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndipo wataona!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَقَالُواْ يَٰوَيۡلَنَا هَٰذَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyokuwa mkiikadhibisha.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
۞ ٱحۡشُرُواْ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ وَأَزۡوَٰجَهُمۡ وَمَا كَانُواْ يَعۡبُدُونَ
Wakusanyeni wale waliodhulumu, na wake zao, na hao ambao wao waliokuwa wakiwaabudu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
مِن دُونِ ٱللَّهِ فَٱهۡدُوهُمۡ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلۡجَحِيمِ
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَقِفُوهُمۡۖ إِنَّهُم مَّسۡـُٔولُونَ
Na wasimamisheni. Hakika hao wataulizwa:
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
مَا لَكُمۡ لَا تَنَاصَرُونَ
Mna nini? Mbona hamsaidiani?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
بَلۡ هُمُ ٱلۡيَوۡمَ مُسۡتَسۡلِمُونَ
Bali hii leo, watasalimu amri.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ
Wataelekeana wao kwa wao kuulizana.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالُوٓاْ إِنَّكُمۡ كُنتُمۡ تَأۡتُونَنَا عَنِ ٱلۡيَمِينِ
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالُواْ بَل لَّمۡ تَكُونُواْ مُؤۡمِنِينَ
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيۡكُم مِّن سُلۡطَٰنِۭۖ بَلۡ كُنتُمۡ قَوۡمٗا طَٰغِينَ
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَحَقَّ عَلَيۡنَا قَوۡلُ رَبِّنَآۖ إِنَّا لَذَآئِقُونَ
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَأَغۡوَيۡنَٰكُمۡ إِنَّا كُنَّا غَٰوِينَ
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَإِنَّهُمۡ يَوۡمَئِذٖ فِي ٱلۡعَذَابِ مُشۡتَرِكُونَ
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ
Hivyo ndivyo tutakavyowafanyia wahalifu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّهُمۡ كَانُوٓاْ إِذَا قِيلَ لَهُمۡ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ يَسۡتَكۡبِرُونَ
Wao walipokuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu (Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu), wanajivuna.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُوٓاْ ءَالِهَتِنَا لِشَاعِرٖ مَّجۡنُونِۭ
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
بَلۡ جَآءَ بِٱلۡحَقِّ وَصَدَّقَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Bali huyu amekuja kwa haki, na amewasadikisha Mitume.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّكُمۡ لَذَآئِقُواْ ٱلۡعَذَابِ ٱلۡأَلِيمِ
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَمَا تُجۡزَوۡنَ إِلَّا مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Wala hamlipwi isipokuwa hayo mliyokuwa mkiyafanya.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliohitariwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أُوْلَٰٓئِكَ لَهُمۡ رِزۡقٞ مَّعۡلُومٞ
Hao ndio watakaopata riziki maalumu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَوَٰكِهُ وَهُم مُّكۡرَمُونَ
Matunda, nao wataheshimiwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فِي جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Katika Bustani za neema.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
عَلَىٰ سُرُرٖ مُّتَقَٰبِلِينَ
Wako juu ya viti wameelekeana.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
يُطَافُ عَلَيۡهِم بِكَأۡسٖ مِّن مَّعِينِۭ
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchemi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
بَيۡضَآءَ لَذَّةٖ لِّلشَّٰرِبِينَ
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
لَا فِيهَا غَوۡلٞ وَلَا هُمۡ عَنۡهَا يُنزَفُونَ
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَعِندَهُمۡ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرۡفِ عِينٞ
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha, mazuri.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
كَأَنَّهُنَّ بَيۡضٞ مَّكۡنُونٞ
Hao wanawake kama mayai yaliyohifadhika.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ
Basi wakaelekeana kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالَ قَآئِلٞ مِّنۡهُمۡ إِنِّي كَانَ لِي قَرِينٞ
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nilikuwa na rafiki.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
يَقُولُ أَءِنَّكَ لَمِنَ ٱلۡمُصَدِّقِينَ
Aliyekuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanaosadiki.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَدِينُونَ
Ati tukishakufa tukawa udongo na mafupa, ndiyo tutalipwa na kufanyiwa hesabu?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالَ هَلۡ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ
Atasema: Je, nyie mnawaona?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَٱطَّلَعَ فَرَءَاهُ فِي سَوَآءِ ٱلۡجَحِيمِ
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالَ تَٱللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرۡدِينِ
Atasema: Wallahi! (Naapa kwa jina la Mwenyezi Mungu) Ulikaribia sana kunipoteza.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَلَوۡلَا نِعۡمَةُ رَبِّي لَكُنتُ مِنَ ٱلۡمُحۡضَرِينَ
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi, bila ya shaka ningelikuwa miongoni mwa waliohudhurishwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَفَمَا نَحۡنُ بِمَيِّتِينَ
Je, Sisi hatutakufa?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِلَّا مَوۡتَتَنَا ٱلۡأُولَىٰ وَمَا نَحۡنُ بِمُعَذَّبِينَ
Isipokuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
لِمِثۡلِ هَٰذَا فَلۡيَعۡمَلِ ٱلۡعَٰمِلُونَ
Kwa mfano wa haya na watende watendao.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَذَٰلِكَ خَيۡرٞ نُّزُلًا أَمۡ شَجَرَةُ ٱلزَّقُّومِ
Je, kukaribishwa hivi si ndiyo bora, au mti wa Zaqqum?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّا جَعَلۡنَٰهَا فِتۡنَةٗ لِّلظَّٰلِمِينَ
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa waliodhulumu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّهَا شَجَرَةٞ تَخۡرُجُ فِيٓ أَصۡلِ ٱلۡجَحِيمِ
Hakika huo ni mti unaotoka katikati ya Jahannamu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
طَلۡعُهَا كَأَنَّهُۥ رُءُوسُ ٱلشَّيَٰطِينِ
Mashada ya matunda yake kama kwamba ni vichwa vya mashetani.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَإِنَّهُمۡ لَأٓكِلُونَ مِنۡهَا فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo kwayo.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
ثُمَّ إِنَّ لَهُمۡ عَلَيۡهَا لَشَوۡبٗا مِّنۡ حَمِيمٖ
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji ya moto yaliyochemka.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
ثُمَّ إِنَّ مَرۡجِعَهُمۡ لَإِلَى ٱلۡجَحِيمِ
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّهُمۡ أَلۡفَوۡاْ ءَابَآءَهُمۡ ضَآلِّينَ
Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَهُمۡ عَلَىٰٓ ءَاثَٰرِهِمۡ يُهۡرَعُونَ
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَلَقَدۡ ضَلَّ قَبۡلَهُمۡ أَكۡثَرُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ
Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَٱنظُرۡ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُنذَرِينَ
Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walioonywa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliohitariwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَلَقَدۡ نَادَىٰنَا نُوحٞ فَلَنِعۡمَ ٱلۡمُجِيبُونَ
Na hakika Nuhu alituita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَنَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥ مِنَ ٱلۡكَرۡبِ ٱلۡعَظِيمِ
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَجَعَلۡنَا ذُرِّيَّتَهُۥ هُمُ ٱلۡبَاقِينَ
Na tuliwajaalia dhuria zake ndio wenye kubakia.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ
Na tukamwachia (sifa njema) kwa waliokuja baadaye.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
سَلَٰمٌ عَلَىٰ نُوحٖ فِي ٱلۡعَٰلَمِينَ
Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyowalipa wanaofanya mema.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ
Kisha tukawazamisha wale wengine.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
۞ وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِۦ لَإِبۡرَٰهِيمَ
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِذۡ جَآءَ رَبَّهُۥ بِقَلۡبٖ سَلِيمٍ
Alipomjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِذۡ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦ مَاذَا تَعۡبُدُونَ
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَئِفۡكًا ءَالِهَةٗ دُونَ ٱللَّهِ تُرِيدُونَ
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَنَظَرَ نَظۡرَةٗ فِي ٱلنُّجُومِ
Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَقَالَ إِنِّي سَقِيمٞ
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَتَوَلَّوۡاْ عَنۡهُ مُدۡبِرِينَ
Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَرَاغَ إِلَىٰٓ ءَالِهَتِهِمۡ فَقَالَ أَلَا تَأۡكُلُونَ
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
مَا لَكُمۡ لَا تَنطِقُونَ
Mna nini hata hamsemi?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَرَاغَ عَلَيۡهِمۡ ضَرۡبَۢا بِٱلۡيَمِينِ
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَأَقۡبَلُوٓاْ إِلَيۡهِ يَزِفُّونَ
Basi wakamjia upesi upesi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالَ أَتَعۡبُدُونَ مَا تَنۡحِتُونَ
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyovichonga wenyewe?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَٱللَّهُ خَلَقَكُمۡ وَمَا تَعۡمَلُونَ
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliyekuumbeni nyinyi na hivyo mnavyovifanya!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَالُواْ ٱبۡنُواْ لَهُۥ بُنۡيَٰنٗا فَأَلۡقُوهُ فِي ٱلۡجَحِيمِ
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَأَرَادُواْ بِهِۦ كَيۡدٗا فَجَعَلۡنَٰهُمُ ٱلۡأَسۡفَلِينَ
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini zaidi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَقَالَ إِنِّي ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّي سَيَهۡدِينِ
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
رَبِّ هَبۡ لِي مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَبَشَّرۡنَٰهُ بِغُلَٰمٍ حَلِيمٖ
Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ ٱلسَّعۡيَ قَالَ يَٰبُنَيَّ إِنِّيٓ أَرَىٰ فِي ٱلۡمَنَامِ أَنِّيٓ أَذۡبَحُكَ فَٱنظُرۡ مَاذَا تَرَىٰۚ قَالَ يَٰٓأَبَتِ ٱفۡعَلۡ مَا تُؤۡمَرُۖ سَتَجِدُنِيٓ إِن شَآءَ ٱللَّهُ مِنَ ٱلصَّٰبِرِينَ
Basi alipofika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyoamrishwa, utanikuta mimi, Insha Allah (Mwenyezi Mungu akipenda), katika wanaosubiri.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَلَمَّآ أَسۡلَمَا وَتَلَّهُۥ لِلۡجَبِينِ
Basi wote wawili walipojisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَنَٰدَيۡنَٰهُ أَن يَٰٓإِبۡرَٰهِيمُ
Tulimwita: Ewe Ibrahim!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَدۡ صَدَّقۡتَ ٱلرُّءۡيَآۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyowalipa wanaotenda mema.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلۡبَلَٰٓؤُاْ ٱلۡمُبِينُ
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhahiri.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَفَدَيۡنَٰهُ بِذِبۡحٍ عَظِيمٖ
Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu waliokuja baadaye.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِبۡرَٰهِيمَ
Iwe salama kwa Ibrahim!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Hivi ndivyo tunavyowalipa wanaofanya mema.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَبَشَّرۡنَٰهُ بِإِسۡحَٰقَ نَبِيّٗا مِّنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَبَٰرَكۡنَا عَلَيۡهِ وَعَلَىٰٓ إِسۡحَٰقَۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحۡسِنٞ وَظَالِمٞ لِّنَفۡسِهِۦ مُبِينٞ
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuria zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَلَقَدۡ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَنَجَّيۡنَٰهُمَا وَقَوۡمَهُمَا مِنَ ٱلۡكَرۡبِ ٱلۡعَظِيمِ
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَنَصَرۡنَٰهُمۡ فَكَانُواْ هُمُ ٱلۡغَٰلِبِينَ
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَءَاتَيۡنَٰهُمَا ٱلۡكِتَٰبَ ٱلۡمُسۡتَبِينَ
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinachobainisha.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَهَدَيۡنَٰهُمَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلۡمُسۡتَقِيمَ
Na tukawaongoa kwenye njia iliyonyooka.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِمَا فِي ٱلۡأٓخِرِينَ
Na tukawaachia (sifa njema) katika watu waliokuja baadaye.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
سَلَٰمٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ
Iwe salama kwa Musa na Haruni!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa walio wema.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّهُمَا مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika wawili hao ni katika waja wetu walioamini.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِنَّ إِلۡيَاسَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِذۡ قَالَ لِقَوۡمِهِۦٓ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia watu wake: Hamumchi Mungu?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَتَدۡعُونَ بَعۡلٗا وَتَذَرُونَ أَحۡسَنَ ٱلۡخَٰلِقِينَ
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
ٱللَّهَ رَبَّكُمۡ وَرَبَّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمۡ لَمُحۡضَرُونَ
Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ
Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa waliokuja baadaye.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِلۡ يَاسِينَ
Iwe salama kwa Ilyas.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa walio wema.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِنَّ لُوطٗا لَّمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِذۡ نَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ
Tulipomwokoa yeye na ahali zake wote.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِلَّا عَجُوزٗا فِي ٱلۡغَٰبِرِينَ
Isipokuwa mwanamke mkongwe katika wale waliobakia nyuma.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
ثُمَّ دَمَّرۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ
Kisha tukawaangamiza wale wengineo.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِنَّكُمۡ لَتَمُرُّونَ عَلَيۡهِم مُّصۡبِحِينَ
Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَبِٱلَّيۡلِۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ
Na usiku. Basi je, hamyatii akilini?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِذۡ أَبَقَ إِلَى ٱلۡفُلۡكِ ٱلۡمَشۡحُونِ
Alipokimbia akenda katika jahazi lililosheheni.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ ٱلۡمُدۡحَضِينَ
Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walioshindwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَٱلۡتَقَمَهُ ٱلۡحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٞ
Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَلَوۡلَآ أَنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلۡمُسَبِّحِينَ
Na ingelikuwa hakuwa katika wanaomtakasa Mwenyezi Mungu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
لَلَبِثَ فِي بَطۡنِهِۦٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ
Bila ya shaka angelikaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
۞ فَنَبَذۡنَٰهُ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ سَقِيمٞ
Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَأَنۢبَتۡنَا عَلَيۡهِ شَجَرَةٗ مِّن يَقۡطِينٖ
Na tukauotesha juu yake mmea wa aina ya mung'unye.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَأَرۡسَلۡنَٰهُ إِلَىٰ مِاْئَةِ أَلۡفٍ أَوۡ يَزِيدُونَ
Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَـَٔامَنُواْ فَمَتَّعۡنَٰهُمۡ إِلَىٰ حِينٖ
Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَٱسۡتَفۡتِهِمۡ أَلِرَبِّكَ ٱلۡبَنَاتُ وَلَهُمُ ٱلۡبَنُونَ
Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ خَلَقۡنَا ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ إِنَٰثٗا وَهُمۡ شَٰهِدُونَ
Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَلَآ إِنَّهُم مِّنۡ إِفۡكِهِمۡ لَيَقُولُونَ
Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَلَدَ ٱللَّهُ وَإِنَّهُمۡ لَكَٰذِبُونَ
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَصۡطَفَى ٱلۡبَنَاتِ عَلَى ٱلۡبَنِينَ
Ati amehiari watoto wa kike kuliko wanaume?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
مَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ
Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَفَلَا تَذَكَّرُونَ
Hamkumbuki?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَمۡ لَكُمۡ سُلۡطَٰنٞ مُّبِينٞ
Au mnayo hoja iliyo wazi?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَأۡتُواْ بِكِتَٰبِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
Basi leteni Kitabu chenu kama nyinyi ni wakweli.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَجَعَلُواْ بَيۡنَهُۥ وَبَيۡنَ ٱلۡجِنَّةِ نَسَبٗاۚ وَلَقَدۡ عَلِمَتِ ٱلۡجِنَّةُ إِنَّهُمۡ لَمُحۡضَرُونَ
Na wameweka mahusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
سُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ
Ametakasika Mwenyezi Mungu mbali na hayo wanayomsingizia.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَإِنَّكُمۡ وَمَا تَعۡبُدُونَ
Basi hakika nyinyi na mnaowaabudu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
مَآ أَنتُمۡ عَلَيۡهِ بِفَٰتِنِينَ
Hamwezi kuwapoteza.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِلَّا مَنۡ هُوَ صَالِ ٱلۡجَحِيمِ
Isipokuwa yule atakayeingia Motoni.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَمَا مِنَّآ إِلَّا لَهُۥ مَقَامٞ مَّعۡلُومٞ
Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِنَّا لَنَحۡنُ ٱلصَّآفُّونَ
Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِنَّا لَنَحۡنُ ٱلۡمُسَبِّحُونَ
Na hakika sisi ndio wenye kutakasa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِن كَانُواْ لَيَقُولُونَ
Na walikuwapo waliokuwa wakisema.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
لَوۡ أَنَّ عِندَنَا ذِكۡرٗا مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ
Tungelikuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
لَكُنَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Bila ya shaka tungelikuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye kumkusudia Yeye tu.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَكَفَرُواْ بِهِۦۖ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ
Lakini waliukufuru. Basi watakuja jua.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَلَقَدۡ سَبَقَتۡ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu waliotumwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّهُمۡ لَهُمُ ٱلۡمَنصُورُونَ
Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakaonusuriwa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ ٱلۡغَٰلِبُونَ
Na kwamba jeshi letu ndilo litakaloshinda.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَتَوَلَّ عَنۡهُمۡ حَتَّىٰ حِينٖ
Basi waachilie mbali kwa muda.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَأَبۡصِرۡهُمۡ فَسَوۡفَ يُبۡصِرُونَ
Na watazame, nao wataona.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
أَفَبِعَذَابِنَا يَسۡتَعۡجِلُونَ
Je, wanaiharakishia adhabu yetu?
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمۡ فَسَآءَ صَبَاحُ ٱلۡمُنذَرِينَ
Basi itakaposhuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walioonywa.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَتَوَلَّ عَنۡهُمۡ حَتَّىٰ حِينٖ
Na waache kwa muda.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَأَبۡصِرۡ فَسَوۡفَ يُبۡصِرُونَ
Na tazama, na wao wataona.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
سُبۡحَٰنَ رَبِّكَ رَبِّ ٱلۡعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ
Ametakasika Mola wako Mlezi Mwenye utukufu mbali na yale wanayomzulia.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَسَلَٰمٌ عَلَى ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Na Salamu juu ya Mitume.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
 
പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: സ്സ്വാഫ്ഫാത്ത്
സൂറത്തുകളുടെ സൂചിക പേജ് നമ്പർ
 
വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - റുവ്വാദ് തർജമ സെൻ്റർ - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക

റബ്‌വ ഇസ്‌ലാമിക് ദഅ്വാ ആൻഡ് ഗൈഡൻസ് സെൻററിൻ്റെയും കോൺടെന്റ് ഇൻ ലാംഗ്വേജസ് സർവീസ് അസോസിയേഷൻ്റെയും സഹകരണത്തോടെ മർകസ് റുവാദ് തർജമ വിഭാഗം വിവർത്തനം ചെയ്തത്.

അടക്കുക