Check out the new design

Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili ng Sentro ng Rowad sa Pagsasalin * - Indise ng mga Salin


Salin ng mga Kahulugan Surah: As-Sāffāt   Ayah:

As-Saffat

وَٱلصَّٰٓفَّٰتِ صَفّٗا
Ninaapa kwa wanaojipanga kwa safu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَٱلزَّٰجِرَٰتِ زَجۡرٗا
Na kwa wenye kukataza mabaya.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَٱلتَّٰلِيَٰتِ ذِكۡرًا
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّ إِلَٰهَكُمۡ لَوَٰحِدٞ
Hakika mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
Ang mga Tafsir na Arabe:
رَّبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا وَرَبُّ ٱلۡمَشَٰرِقِ
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّا زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنۡيَا بِزِينَةٍ ٱلۡكَوَاكِبِ
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَحِفۡظٗا مِّن كُلِّ شَيۡطَٰنٖ مَّارِدٖ
Na kulinda na kila shetani muasi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى ٱلۡمَلَإِ ٱلۡأَعۡلَىٰ وَيُقۡذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٖ
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
Ang mga Tafsir na Arabe:
دُحُورٗاۖ وَلَهُمۡ عَذَابٞ وَاصِبٌ
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِلَّا مَنۡ خَطِفَ ٱلۡخَطۡفَةَ فَأَتۡبَعَهُۥ شِهَابٞ ثَاقِبٞ
Isipokuwa anayenyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinachong'ara.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَٱسۡتَفۡتِهِمۡ أَهُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَم مَّنۡ خَلَقۡنَآۚ إِنَّا خَلَقۡنَٰهُم مِّن طِينٖ لَّازِبِۭ
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tuliowaumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unaonata.
Ang mga Tafsir na Arabe:
بَلۡ عَجِبۡتَ وَيَسۡخَرُونَ
Bali unastaajabu, na wao wanafanya masihara.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِذَا ذُكِّرُواْ لَا يَذۡكُرُونَ
Na wanapokumbushwa, hawakumbuki.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِذَا رَأَوۡاْ ءَايَةٗ يَسۡتَسۡخِرُونَ
Na wanapoona Ishara, wanafanya masihara.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَقَالُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ مُّبِينٌ
Na husema: Haya si chochote isipokuwa ni uchawi tu ulio dhahiri.
Ang mga Tafsir na Arabe:
أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ
Ati tukishakufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
Ang mga Tafsir na Arabe:
أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ
Hata baba zetu wa zamani?
Ang mga Tafsir na Arabe:
قُلۡ نَعَمۡ وَأَنتُمۡ دَٰخِرُونَ
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ فَإِذَا هُمۡ يَنظُرُونَ
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndipo wataona!
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَقَالُواْ يَٰوَيۡلَنَا هَٰذَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
Ang mga Tafsir na Arabe:
هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyokuwa mkiikadhibisha.
Ang mga Tafsir na Arabe:
۞ ٱحۡشُرُواْ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ وَأَزۡوَٰجَهُمۡ وَمَا كَانُواْ يَعۡبُدُونَ
Wakusanyeni wale waliodhulumu, na wake zao, na hao ambao wao waliokuwa wakiwaabudu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
مِن دُونِ ٱللَّهِ فَٱهۡدُوهُمۡ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلۡجَحِيمِ
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَقِفُوهُمۡۖ إِنَّهُم مَّسۡـُٔولُونَ
Na wasimamisheni. Hakika hao wataulizwa:
Ang mga Tafsir na Arabe:
مَا لَكُمۡ لَا تَنَاصَرُونَ
Mna nini? Mbona hamsaidiani?
Ang mga Tafsir na Arabe:
بَلۡ هُمُ ٱلۡيَوۡمَ مُسۡتَسۡلِمُونَ
Bali hii leo, watasalimu amri.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ
Wataelekeana wao kwa wao kuulizana.
Ang mga Tafsir na Arabe:
قَالُوٓاْ إِنَّكُمۡ كُنتُمۡ تَأۡتُونَنَا عَنِ ٱلۡيَمِينِ
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
Ang mga Tafsir na Arabe:
قَالُواْ بَل لَّمۡ تَكُونُواْ مُؤۡمِنِينَ
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيۡكُم مِّن سُلۡطَٰنِۭۖ بَلۡ كُنتُمۡ قَوۡمٗا طَٰغِينَ
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَحَقَّ عَلَيۡنَا قَوۡلُ رَبِّنَآۖ إِنَّا لَذَآئِقُونَ
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَأَغۡوَيۡنَٰكُمۡ إِنَّا كُنَّا غَٰوِينَ
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَإِنَّهُمۡ يَوۡمَئِذٖ فِي ٱلۡعَذَابِ مُشۡتَرِكُونَ
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ
Hivyo ndivyo tutakavyowafanyia wahalifu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّهُمۡ كَانُوٓاْ إِذَا قِيلَ لَهُمۡ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ يَسۡتَكۡبِرُونَ
Wao walipokuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu (Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu), wanajivuna.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُوٓاْ ءَالِهَتِنَا لِشَاعِرٖ مَّجۡنُونِۭ
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
Ang mga Tafsir na Arabe:
بَلۡ جَآءَ بِٱلۡحَقِّ وَصَدَّقَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Bali huyu amekuja kwa haki, na amewasadikisha Mitume.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّكُمۡ لَذَآئِقُواْ ٱلۡعَذَابِ ٱلۡأَلِيمِ
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَمَا تُجۡزَوۡنَ إِلَّا مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Wala hamlipwi isipokuwa hayo mliyokuwa mkiyafanya.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliohitariwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
أُوْلَٰٓئِكَ لَهُمۡ رِزۡقٞ مَّعۡلُومٞ
Hao ndio watakaopata riziki maalumu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَوَٰكِهُ وَهُم مُّكۡرَمُونَ
Matunda, nao wataheshimiwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فِي جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Katika Bustani za neema.
Ang mga Tafsir na Arabe:
عَلَىٰ سُرُرٖ مُّتَقَٰبِلِينَ
Wako juu ya viti wameelekeana.
Ang mga Tafsir na Arabe:
يُطَافُ عَلَيۡهِم بِكَأۡسٖ مِّن مَّعِينِۭ
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchemi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
بَيۡضَآءَ لَذَّةٖ لِّلشَّٰرِبِينَ
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
Ang mga Tafsir na Arabe:
لَا فِيهَا غَوۡلٞ وَلَا هُمۡ عَنۡهَا يُنزَفُونَ
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَعِندَهُمۡ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرۡفِ عِينٞ
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha, mazuri.
Ang mga Tafsir na Arabe:
كَأَنَّهُنَّ بَيۡضٞ مَّكۡنُونٞ
Hao wanawake kama mayai yaliyohifadhika.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ
Basi wakaelekeana kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
Ang mga Tafsir na Arabe:
قَالَ قَآئِلٞ مِّنۡهُمۡ إِنِّي كَانَ لِي قَرِينٞ
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nilikuwa na rafiki.
Ang mga Tafsir na Arabe:
يَقُولُ أَءِنَّكَ لَمِنَ ٱلۡمُصَدِّقِينَ
Aliyekuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanaosadiki.
Ang mga Tafsir na Arabe:
أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَدِينُونَ
Ati tukishakufa tukawa udongo na mafupa, ndiyo tutalipwa na kufanyiwa hesabu?
Ang mga Tafsir na Arabe:
قَالَ هَلۡ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ
Atasema: Je, nyie mnawaona?
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَٱطَّلَعَ فَرَءَاهُ فِي سَوَآءِ ٱلۡجَحِيمِ
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
قَالَ تَٱللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرۡدِينِ
Atasema: Wallahi! (Naapa kwa jina la Mwenyezi Mungu) Ulikaribia sana kunipoteza.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَلَوۡلَا نِعۡمَةُ رَبِّي لَكُنتُ مِنَ ٱلۡمُحۡضَرِينَ
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi, bila ya shaka ningelikuwa miongoni mwa waliohudhurishwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
أَفَمَا نَحۡنُ بِمَيِّتِينَ
Je, Sisi hatutakufa?
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِلَّا مَوۡتَتَنَا ٱلۡأُولَىٰ وَمَا نَحۡنُ بِمُعَذَّبِينَ
Isipokuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
لِمِثۡلِ هَٰذَا فَلۡيَعۡمَلِ ٱلۡعَٰمِلُونَ
Kwa mfano wa haya na watende watendao.
Ang mga Tafsir na Arabe:
أَذَٰلِكَ خَيۡرٞ نُّزُلًا أَمۡ شَجَرَةُ ٱلزَّقُّومِ
Je, kukaribishwa hivi si ndiyo bora, au mti wa Zaqqum?
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّا جَعَلۡنَٰهَا فِتۡنَةٗ لِّلظَّٰلِمِينَ
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa waliodhulumu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّهَا شَجَرَةٞ تَخۡرُجُ فِيٓ أَصۡلِ ٱلۡجَحِيمِ
Hakika huo ni mti unaotoka katikati ya Jahannamu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
طَلۡعُهَا كَأَنَّهُۥ رُءُوسُ ٱلشَّيَٰطِينِ
Mashada ya matunda yake kama kwamba ni vichwa vya mashetani.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَإِنَّهُمۡ لَأٓكِلُونَ مِنۡهَا فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo kwayo.
Ang mga Tafsir na Arabe:
ثُمَّ إِنَّ لَهُمۡ عَلَيۡهَا لَشَوۡبٗا مِّنۡ حَمِيمٖ
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji ya moto yaliyochemka.
Ang mga Tafsir na Arabe:
ثُمَّ إِنَّ مَرۡجِعَهُمۡ لَإِلَى ٱلۡجَحِيمِ
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّهُمۡ أَلۡفَوۡاْ ءَابَآءَهُمۡ ضَآلِّينَ
Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَهُمۡ عَلَىٰٓ ءَاثَٰرِهِمۡ يُهۡرَعُونَ
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَلَقَدۡ ضَلَّ قَبۡلَهُمۡ أَكۡثَرُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ
Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَٱنظُرۡ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُنذَرِينَ
Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walioonywa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliohitariwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَلَقَدۡ نَادَىٰنَا نُوحٞ فَلَنِعۡمَ ٱلۡمُجِيبُونَ
Na hakika Nuhu alituita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَنَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥ مِنَ ٱلۡكَرۡبِ ٱلۡعَظِيمِ
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَجَعَلۡنَا ذُرِّيَّتَهُۥ هُمُ ٱلۡبَاقِينَ
Na tuliwajaalia dhuria zake ndio wenye kubakia.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ
Na tukamwachia (sifa njema) kwa waliokuja baadaye.
Ang mga Tafsir na Arabe:
سَلَٰمٌ عَلَىٰ نُوحٖ فِي ٱلۡعَٰلَمِينَ
Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyowalipa wanaofanya mema.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.
Ang mga Tafsir na Arabe:
ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ
Kisha tukawazamisha wale wengine.
Ang mga Tafsir na Arabe:
۞ وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِۦ لَإِبۡرَٰهِيمَ
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِذۡ جَآءَ رَبَّهُۥ بِقَلۡبٖ سَلِيمٍ
Alipomjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِذۡ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦ مَاذَا تَعۡبُدُونَ
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
Ang mga Tafsir na Arabe:
أَئِفۡكًا ءَالِهَةٗ دُونَ ٱللَّهِ تُرِيدُونَ
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَنَظَرَ نَظۡرَةٗ فِي ٱلنُّجُومِ
Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَقَالَ إِنِّي سَقِيمٞ
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَتَوَلَّوۡاْ عَنۡهُ مُدۡبِرِينَ
Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَرَاغَ إِلَىٰٓ ءَالِهَتِهِمۡ فَقَالَ أَلَا تَأۡكُلُونَ
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
Ang mga Tafsir na Arabe:
مَا لَكُمۡ لَا تَنطِقُونَ
Mna nini hata hamsemi?
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَرَاغَ عَلَيۡهِمۡ ضَرۡبَۢا بِٱلۡيَمِينِ
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَأَقۡبَلُوٓاْ إِلَيۡهِ يَزِفُّونَ
Basi wakamjia upesi upesi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
قَالَ أَتَعۡبُدُونَ مَا تَنۡحِتُونَ
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyovichonga wenyewe?
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱللَّهُ خَلَقَكُمۡ وَمَا تَعۡمَلُونَ
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliyekuumbeni nyinyi na hivyo mnavyovifanya!
Ang mga Tafsir na Arabe:
قَالُواْ ٱبۡنُواْ لَهُۥ بُنۡيَٰنٗا فَأَلۡقُوهُ فِي ٱلۡجَحِيمِ
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَأَرَادُواْ بِهِۦ كَيۡدٗا فَجَعَلۡنَٰهُمُ ٱلۡأَسۡفَلِينَ
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini zaidi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَقَالَ إِنِّي ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّي سَيَهۡدِينِ
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
رَبِّ هَبۡ لِي مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَبَشَّرۡنَٰهُ بِغُلَٰمٍ حَلِيمٖ
Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ ٱلسَّعۡيَ قَالَ يَٰبُنَيَّ إِنِّيٓ أَرَىٰ فِي ٱلۡمَنَامِ أَنِّيٓ أَذۡبَحُكَ فَٱنظُرۡ مَاذَا تَرَىٰۚ قَالَ يَٰٓأَبَتِ ٱفۡعَلۡ مَا تُؤۡمَرُۖ سَتَجِدُنِيٓ إِن شَآءَ ٱللَّهُ مِنَ ٱلصَّٰبِرِينَ
Basi alipofika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyoamrishwa, utanikuta mimi, Insha Allah (Mwenyezi Mungu akipenda), katika wanaosubiri.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَلَمَّآ أَسۡلَمَا وَتَلَّهُۥ لِلۡجَبِينِ
Basi wote wawili walipojisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَنَٰدَيۡنَٰهُ أَن يَٰٓإِبۡرَٰهِيمُ
Tulimwita: Ewe Ibrahim!
Ang mga Tafsir na Arabe:
قَدۡ صَدَّقۡتَ ٱلرُّءۡيَآۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyowalipa wanaotenda mema.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلۡبَلَٰٓؤُاْ ٱلۡمُبِينُ
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhahiri.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَفَدَيۡنَٰهُ بِذِبۡحٍ عَظِيمٖ
Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu waliokuja baadaye.
Ang mga Tafsir na Arabe:
سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِبۡرَٰهِيمَ
Iwe salama kwa Ibrahim!
Ang mga Tafsir na Arabe:
كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Hivi ndivyo tunavyowalipa wanaofanya mema.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَبَشَّرۡنَٰهُ بِإِسۡحَٰقَ نَبِيّٗا مِّنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَبَٰرَكۡنَا عَلَيۡهِ وَعَلَىٰٓ إِسۡحَٰقَۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحۡسِنٞ وَظَالِمٞ لِّنَفۡسِهِۦ مُبِينٞ
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuria zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَلَقَدۡ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَنَجَّيۡنَٰهُمَا وَقَوۡمَهُمَا مِنَ ٱلۡكَرۡبِ ٱلۡعَظِيمِ
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَنَصَرۡنَٰهُمۡ فَكَانُواْ هُمُ ٱلۡغَٰلِبِينَ
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَءَاتَيۡنَٰهُمَا ٱلۡكِتَٰبَ ٱلۡمُسۡتَبِينَ
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinachobainisha.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَهَدَيۡنَٰهُمَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلۡمُسۡتَقِيمَ
Na tukawaongoa kwenye njia iliyonyooka.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِمَا فِي ٱلۡأٓخِرِينَ
Na tukawaachia (sifa njema) katika watu waliokuja baadaye.
Ang mga Tafsir na Arabe:
سَلَٰمٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ
Iwe salama kwa Musa na Haruni!
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa walio wema.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّهُمَا مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika wawili hao ni katika waja wetu walioamini.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِنَّ إِلۡيَاسَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِذۡ قَالَ لِقَوۡمِهِۦٓ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia watu wake: Hamumchi Mungu?
Ang mga Tafsir na Arabe:
أَتَدۡعُونَ بَعۡلٗا وَتَذَرُونَ أَحۡسَنَ ٱلۡخَٰلِقِينَ
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji.
Ang mga Tafsir na Arabe:
ٱللَّهَ رَبَّكُمۡ وَرَبَّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمۡ لَمُحۡضَرُونَ
Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ
Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa waliokuja baadaye.
Ang mga Tafsir na Arabe:
سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِلۡ يَاسِينَ
Iwe salama kwa Ilyas.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa walio wema.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِنَّ لُوطٗا لَّمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِذۡ نَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ
Tulipomwokoa yeye na ahali zake wote.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِلَّا عَجُوزٗا فِي ٱلۡغَٰبِرِينَ
Isipokuwa mwanamke mkongwe katika wale waliobakia nyuma.
Ang mga Tafsir na Arabe:
ثُمَّ دَمَّرۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ
Kisha tukawaangamiza wale wengineo.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِنَّكُمۡ لَتَمُرُّونَ عَلَيۡهِم مُّصۡبِحِينَ
Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَبِٱلَّيۡلِۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ
Na usiku. Basi je, hamyatii akilini?
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِذۡ أَبَقَ إِلَى ٱلۡفُلۡكِ ٱلۡمَشۡحُونِ
Alipokimbia akenda katika jahazi lililosheheni.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ ٱلۡمُدۡحَضِينَ
Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walioshindwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَٱلۡتَقَمَهُ ٱلۡحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٞ
Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَلَوۡلَآ أَنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلۡمُسَبِّحِينَ
Na ingelikuwa hakuwa katika wanaomtakasa Mwenyezi Mungu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
لَلَبِثَ فِي بَطۡنِهِۦٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ
Bila ya shaka angelikaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
۞ فَنَبَذۡنَٰهُ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ سَقِيمٞ
Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَأَنۢبَتۡنَا عَلَيۡهِ شَجَرَةٗ مِّن يَقۡطِينٖ
Na tukauotesha juu yake mmea wa aina ya mung'unye.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَأَرۡسَلۡنَٰهُ إِلَىٰ مِاْئَةِ أَلۡفٍ أَوۡ يَزِيدُونَ
Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَـَٔامَنُواْ فَمَتَّعۡنَٰهُمۡ إِلَىٰ حِينٖ
Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَٱسۡتَفۡتِهِمۡ أَلِرَبِّكَ ٱلۡبَنَاتُ وَلَهُمُ ٱلۡبَنُونَ
Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
Ang mga Tafsir na Arabe:
أَمۡ خَلَقۡنَا ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ إِنَٰثٗا وَهُمۡ شَٰهِدُونَ
Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?
Ang mga Tafsir na Arabe:
أَلَآ إِنَّهُم مِّنۡ إِفۡكِهِمۡ لَيَقُولُونَ
Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَلَدَ ٱللَّهُ وَإِنَّهُمۡ لَكَٰذِبُونَ
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
Ang mga Tafsir na Arabe:
أَصۡطَفَى ٱلۡبَنَاتِ عَلَى ٱلۡبَنِينَ
Ati amehiari watoto wa kike kuliko wanaume?
Ang mga Tafsir na Arabe:
مَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ
Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?
Ang mga Tafsir na Arabe:
أَفَلَا تَذَكَّرُونَ
Hamkumbuki?
Ang mga Tafsir na Arabe:
أَمۡ لَكُمۡ سُلۡطَٰنٞ مُّبِينٞ
Au mnayo hoja iliyo wazi?
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَأۡتُواْ بِكِتَٰبِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
Basi leteni Kitabu chenu kama nyinyi ni wakweli.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَجَعَلُواْ بَيۡنَهُۥ وَبَيۡنَ ٱلۡجِنَّةِ نَسَبٗاۚ وَلَقَدۡ عَلِمَتِ ٱلۡجِنَّةُ إِنَّهُمۡ لَمُحۡضَرُونَ
Na wameweka mahusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
سُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ
Ametakasika Mwenyezi Mungu mbali na hayo wanayomsingizia.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَإِنَّكُمۡ وَمَا تَعۡبُدُونَ
Basi hakika nyinyi na mnaowaabudu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
مَآ أَنتُمۡ عَلَيۡهِ بِفَٰتِنِينَ
Hamwezi kuwapoteza.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِلَّا مَنۡ هُوَ صَالِ ٱلۡجَحِيمِ
Isipokuwa yule atakayeingia Motoni.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَمَا مِنَّآ إِلَّا لَهُۥ مَقَامٞ مَّعۡلُومٞ
Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِنَّا لَنَحۡنُ ٱلصَّآفُّونَ
Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِنَّا لَنَحۡنُ ٱلۡمُسَبِّحُونَ
Na hakika sisi ndio wenye kutakasa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِن كَانُواْ لَيَقُولُونَ
Na walikuwapo waliokuwa wakisema.
Ang mga Tafsir na Arabe:
لَوۡ أَنَّ عِندَنَا ذِكۡرٗا مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ
Tungelikuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani.
Ang mga Tafsir na Arabe:
لَكُنَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Bila ya shaka tungelikuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye kumkusudia Yeye tu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَكَفَرُواْ بِهِۦۖ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ
Lakini waliukufuru. Basi watakuja jua.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَلَقَدۡ سَبَقَتۡ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu waliotumwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّهُمۡ لَهُمُ ٱلۡمَنصُورُونَ
Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakaonusuriwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ ٱلۡغَٰلِبُونَ
Na kwamba jeshi letu ndilo litakaloshinda.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَتَوَلَّ عَنۡهُمۡ حَتَّىٰ حِينٖ
Basi waachilie mbali kwa muda.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَأَبۡصِرۡهُمۡ فَسَوۡفَ يُبۡصِرُونَ
Na watazame, nao wataona.
Ang mga Tafsir na Arabe:
أَفَبِعَذَابِنَا يَسۡتَعۡجِلُونَ
Je, wanaiharakishia adhabu yetu?
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمۡ فَسَآءَ صَبَاحُ ٱلۡمُنذَرِينَ
Basi itakaposhuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walioonywa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَتَوَلَّ عَنۡهُمۡ حَتَّىٰ حِينٖ
Na waache kwa muda.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَأَبۡصِرۡ فَسَوۡفَ يُبۡصِرُونَ
Na tazama, na wao wataona.
Ang mga Tafsir na Arabe:
سُبۡحَٰنَ رَبِّكَ رَبِّ ٱلۡعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ
Ametakasika Mola wako Mlezi Mwenye utukufu mbali na yale wanayomzulia.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَسَلَٰمٌ عَلَى ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Na Salamu juu ya Mitume.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Ang mga Tafsir na Arabe:
 
Salin ng mga Kahulugan Surah: As-Sāffāt
Indise ng mga Surah Numero ng Pahina
 
Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili ng Sentro ng Rowad sa Pagsasalin - Indise ng mga Salin

Isinalin ito ng isang pangkat ng Sentro ng Rowad sa Pagsasalin sa pakikipagtulungan ng Samahan ng Da‘wah sa Rabwah at Samahan ng Paglilingkod sa Nilalamang Islāmiko sa mga Wika.

Isara