Check out the new design

《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 拉瓦德翻译中心。 * - 译解目录


含义的翻译 章: 隋法提   段:

As-Saffat

وَٱلصَّٰٓفَّٰتِ صَفّٗا
Ninaapa kwa wanaojipanga kwa safu.
阿拉伯语经注:
فَٱلزَّٰجِرَٰتِ زَجۡرٗا
Na kwa wenye kukataza mabaya.
阿拉伯语经注:
فَٱلتَّٰلِيَٰتِ ذِكۡرًا
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
阿拉伯语经注:
إِنَّ إِلَٰهَكُمۡ لَوَٰحِدٞ
Hakika mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
阿拉伯语经注:
رَّبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا وَرَبُّ ٱلۡمَشَٰرِقِ
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
阿拉伯语经注:
إِنَّا زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنۡيَا بِزِينَةٍ ٱلۡكَوَاكِبِ
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
阿拉伯语经注:
وَحِفۡظٗا مِّن كُلِّ شَيۡطَٰنٖ مَّارِدٖ
Na kulinda na kila shetani muasi.
阿拉伯语经注:
لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى ٱلۡمَلَإِ ٱلۡأَعۡلَىٰ وَيُقۡذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٖ
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
阿拉伯语经注:
دُحُورٗاۖ وَلَهُمۡ عَذَابٞ وَاصِبٌ
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
阿拉伯语经注:
إِلَّا مَنۡ خَطِفَ ٱلۡخَطۡفَةَ فَأَتۡبَعَهُۥ شِهَابٞ ثَاقِبٞ
Isipokuwa anayenyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinachong'ara.
阿拉伯语经注:
فَٱسۡتَفۡتِهِمۡ أَهُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَم مَّنۡ خَلَقۡنَآۚ إِنَّا خَلَقۡنَٰهُم مِّن طِينٖ لَّازِبِۭ
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tuliowaumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unaonata.
阿拉伯语经注:
بَلۡ عَجِبۡتَ وَيَسۡخَرُونَ
Bali unastaajabu, na wao wanafanya masihara.
阿拉伯语经注:
وَإِذَا ذُكِّرُواْ لَا يَذۡكُرُونَ
Na wanapokumbushwa, hawakumbuki.
阿拉伯语经注:
وَإِذَا رَأَوۡاْ ءَايَةٗ يَسۡتَسۡخِرُونَ
Na wanapoona Ishara, wanafanya masihara.
阿拉伯语经注:
وَقَالُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ مُّبِينٌ
Na husema: Haya si chochote isipokuwa ni uchawi tu ulio dhahiri.
阿拉伯语经注:
أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ
Ati tukishakufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
阿拉伯语经注:
أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ
Hata baba zetu wa zamani?
阿拉伯语经注:
قُلۡ نَعَمۡ وَأَنتُمۡ دَٰخِرُونَ
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
阿拉伯语经注:
فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ فَإِذَا هُمۡ يَنظُرُونَ
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndipo wataona!
阿拉伯语经注:
وَقَالُواْ يَٰوَيۡلَنَا هَٰذَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
阿拉伯语经注:
هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyokuwa mkiikadhibisha.
阿拉伯语经注:
۞ ٱحۡشُرُواْ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ وَأَزۡوَٰجَهُمۡ وَمَا كَانُواْ يَعۡبُدُونَ
Wakusanyeni wale waliodhulumu, na wake zao, na hao ambao wao waliokuwa wakiwaabudu.
阿拉伯语经注:
مِن دُونِ ٱللَّهِ فَٱهۡدُوهُمۡ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلۡجَحِيمِ
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
阿拉伯语经注:
وَقِفُوهُمۡۖ إِنَّهُم مَّسۡـُٔولُونَ
Na wasimamisheni. Hakika hao wataulizwa:
阿拉伯语经注:
مَا لَكُمۡ لَا تَنَاصَرُونَ
Mna nini? Mbona hamsaidiani?
阿拉伯语经注:
بَلۡ هُمُ ٱلۡيَوۡمَ مُسۡتَسۡلِمُونَ
Bali hii leo, watasalimu amri.
阿拉伯语经注:
وَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ
Wataelekeana wao kwa wao kuulizana.
阿拉伯语经注:
قَالُوٓاْ إِنَّكُمۡ كُنتُمۡ تَأۡتُونَنَا عَنِ ٱلۡيَمِينِ
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
阿拉伯语经注:
قَالُواْ بَل لَّمۡ تَكُونُواْ مُؤۡمِنِينَ
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
阿拉伯语经注:
وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيۡكُم مِّن سُلۡطَٰنِۭۖ بَلۡ كُنتُمۡ قَوۡمٗا طَٰغِينَ
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
阿拉伯语经注:
فَحَقَّ عَلَيۡنَا قَوۡلُ رَبِّنَآۖ إِنَّا لَذَآئِقُونَ
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
阿拉伯语经注:
فَأَغۡوَيۡنَٰكُمۡ إِنَّا كُنَّا غَٰوِينَ
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
阿拉伯语经注:
فَإِنَّهُمۡ يَوۡمَئِذٖ فِي ٱلۡعَذَابِ مُشۡتَرِكُونَ
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
阿拉伯语经注:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ
Hivyo ndivyo tutakavyowafanyia wahalifu.
阿拉伯语经注:
إِنَّهُمۡ كَانُوٓاْ إِذَا قِيلَ لَهُمۡ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ يَسۡتَكۡبِرُونَ
Wao walipokuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu (Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu), wanajivuna.
阿拉伯语经注:
وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُوٓاْ ءَالِهَتِنَا لِشَاعِرٖ مَّجۡنُونِۭ
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
阿拉伯语经注:
بَلۡ جَآءَ بِٱلۡحَقِّ وَصَدَّقَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Bali huyu amekuja kwa haki, na amewasadikisha Mitume.
阿拉伯语经注:
إِنَّكُمۡ لَذَآئِقُواْ ٱلۡعَذَابِ ٱلۡأَلِيمِ
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
阿拉伯语经注:
وَمَا تُجۡزَوۡنَ إِلَّا مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Wala hamlipwi isipokuwa hayo mliyokuwa mkiyafanya.
阿拉伯语经注:
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliohitariwa.
阿拉伯语经注:
أُوْلَٰٓئِكَ لَهُمۡ رِزۡقٞ مَّعۡلُومٞ
Hao ndio watakaopata riziki maalumu.
阿拉伯语经注:
فَوَٰكِهُ وَهُم مُّكۡرَمُونَ
Matunda, nao wataheshimiwa.
阿拉伯语经注:
فِي جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Katika Bustani za neema.
阿拉伯语经注:
عَلَىٰ سُرُرٖ مُّتَقَٰبِلِينَ
Wako juu ya viti wameelekeana.
阿拉伯语经注:
يُطَافُ عَلَيۡهِم بِكَأۡسٖ مِّن مَّعِينِۭ
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchemi.
阿拉伯语经注:
بَيۡضَآءَ لَذَّةٖ لِّلشَّٰرِبِينَ
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
阿拉伯语经注:
لَا فِيهَا غَوۡلٞ وَلَا هُمۡ عَنۡهَا يُنزَفُونَ
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
阿拉伯语经注:
وَعِندَهُمۡ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرۡفِ عِينٞ
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha, mazuri.
阿拉伯语经注:
كَأَنَّهُنَّ بَيۡضٞ مَّكۡنُونٞ
Hao wanawake kama mayai yaliyohifadhika.
阿拉伯语经注:
فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ
Basi wakaelekeana kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
阿拉伯语经注:
قَالَ قَآئِلٞ مِّنۡهُمۡ إِنِّي كَانَ لِي قَرِينٞ
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nilikuwa na rafiki.
阿拉伯语经注:
يَقُولُ أَءِنَّكَ لَمِنَ ٱلۡمُصَدِّقِينَ
Aliyekuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanaosadiki.
阿拉伯语经注:
أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَدِينُونَ
Ati tukishakufa tukawa udongo na mafupa, ndiyo tutalipwa na kufanyiwa hesabu?
阿拉伯语经注:
قَالَ هَلۡ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ
Atasema: Je, nyie mnawaona?
阿拉伯语经注:
فَٱطَّلَعَ فَرَءَاهُ فِي سَوَآءِ ٱلۡجَحِيمِ
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
阿拉伯语经注:
قَالَ تَٱللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرۡدِينِ
Atasema: Wallahi! (Naapa kwa jina la Mwenyezi Mungu) Ulikaribia sana kunipoteza.
阿拉伯语经注:
وَلَوۡلَا نِعۡمَةُ رَبِّي لَكُنتُ مِنَ ٱلۡمُحۡضَرِينَ
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi, bila ya shaka ningelikuwa miongoni mwa waliohudhurishwa.
阿拉伯语经注:
أَفَمَا نَحۡنُ بِمَيِّتِينَ
Je, Sisi hatutakufa?
阿拉伯语经注:
إِلَّا مَوۡتَتَنَا ٱلۡأُولَىٰ وَمَا نَحۡنُ بِمُعَذَّبِينَ
Isipokuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
阿拉伯语经注:
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
阿拉伯语经注:
لِمِثۡلِ هَٰذَا فَلۡيَعۡمَلِ ٱلۡعَٰمِلُونَ
Kwa mfano wa haya na watende watendao.
阿拉伯语经注:
أَذَٰلِكَ خَيۡرٞ نُّزُلًا أَمۡ شَجَرَةُ ٱلزَّقُّومِ
Je, kukaribishwa hivi si ndiyo bora, au mti wa Zaqqum?
阿拉伯语经注:
إِنَّا جَعَلۡنَٰهَا فِتۡنَةٗ لِّلظَّٰلِمِينَ
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa waliodhulumu.
阿拉伯语经注:
إِنَّهَا شَجَرَةٞ تَخۡرُجُ فِيٓ أَصۡلِ ٱلۡجَحِيمِ
Hakika huo ni mti unaotoka katikati ya Jahannamu.
阿拉伯语经注:
طَلۡعُهَا كَأَنَّهُۥ رُءُوسُ ٱلشَّيَٰطِينِ
Mashada ya matunda yake kama kwamba ni vichwa vya mashetani.
阿拉伯语经注:
فَإِنَّهُمۡ لَأٓكِلُونَ مِنۡهَا فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo kwayo.
阿拉伯语经注:
ثُمَّ إِنَّ لَهُمۡ عَلَيۡهَا لَشَوۡبٗا مِّنۡ حَمِيمٖ
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji ya moto yaliyochemka.
阿拉伯语经注:
ثُمَّ إِنَّ مَرۡجِعَهُمۡ لَإِلَى ٱلۡجَحِيمِ
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
阿拉伯语经注:
إِنَّهُمۡ أَلۡفَوۡاْ ءَابَآءَهُمۡ ضَآلِّينَ
Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
阿拉伯语经注:
فَهُمۡ عَلَىٰٓ ءَاثَٰرِهِمۡ يُهۡرَعُونَ
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
阿拉伯语经注:
وَلَقَدۡ ضَلَّ قَبۡلَهُمۡ أَكۡثَرُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
阿拉伯语经注:
وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ
Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
阿拉伯语经注:
فَٱنظُرۡ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُنذَرِينَ
Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walioonywa.
阿拉伯语经注:
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliohitariwa.
阿拉伯语经注:
وَلَقَدۡ نَادَىٰنَا نُوحٞ فَلَنِعۡمَ ٱلۡمُجِيبُونَ
Na hakika Nuhu alituita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
阿拉伯语经注:
وَنَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥ مِنَ ٱلۡكَرۡبِ ٱلۡعَظِيمِ
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
阿拉伯语经注:
وَجَعَلۡنَا ذُرِّيَّتَهُۥ هُمُ ٱلۡبَاقِينَ
Na tuliwajaalia dhuria zake ndio wenye kubakia.
阿拉伯语经注:
وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ
Na tukamwachia (sifa njema) kwa waliokuja baadaye.
阿拉伯语经注:
سَلَٰمٌ عَلَىٰ نُوحٖ فِي ٱلۡعَٰلَمِينَ
Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
阿拉伯语经注:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyowalipa wanaofanya mema.
阿拉伯语经注:
إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.
阿拉伯语经注:
ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ
Kisha tukawazamisha wale wengine.
阿拉伯语经注:
۞ وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِۦ لَإِبۡرَٰهِيمَ
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake.
阿拉伯语经注:
إِذۡ جَآءَ رَبَّهُۥ بِقَلۡبٖ سَلِيمٍ
Alipomjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
阿拉伯语经注:
إِذۡ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦ مَاذَا تَعۡبُدُونَ
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
阿拉伯语经注:
أَئِفۡكًا ءَالِهَةٗ دُونَ ٱللَّهِ تُرِيدُونَ
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
阿拉伯语经注:
فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
阿拉伯语经注:
فَنَظَرَ نَظۡرَةٗ فِي ٱلنُّجُومِ
Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
阿拉伯语经注:
فَقَالَ إِنِّي سَقِيمٞ
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
阿拉伯语经注:
فَتَوَلَّوۡاْ عَنۡهُ مُدۡبِرِينَ
Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
阿拉伯语经注:
فَرَاغَ إِلَىٰٓ ءَالِهَتِهِمۡ فَقَالَ أَلَا تَأۡكُلُونَ
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
阿拉伯语经注:
مَا لَكُمۡ لَا تَنطِقُونَ
Mna nini hata hamsemi?
阿拉伯语经注:
فَرَاغَ عَلَيۡهِمۡ ضَرۡبَۢا بِٱلۡيَمِينِ
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
阿拉伯语经注:
فَأَقۡبَلُوٓاْ إِلَيۡهِ يَزِفُّونَ
Basi wakamjia upesi upesi.
阿拉伯语经注:
قَالَ أَتَعۡبُدُونَ مَا تَنۡحِتُونَ
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyovichonga wenyewe?
阿拉伯语经注:
وَٱللَّهُ خَلَقَكُمۡ وَمَا تَعۡمَلُونَ
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliyekuumbeni nyinyi na hivyo mnavyovifanya!
阿拉伯语经注:
قَالُواْ ٱبۡنُواْ لَهُۥ بُنۡيَٰنٗا فَأَلۡقُوهُ فِي ٱلۡجَحِيمِ
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
阿拉伯语经注:
فَأَرَادُواْ بِهِۦ كَيۡدٗا فَجَعَلۡنَٰهُمُ ٱلۡأَسۡفَلِينَ
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini zaidi.
阿拉伯语经注:
وَقَالَ إِنِّي ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّي سَيَهۡدِينِ
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
阿拉伯语经注:
رَبِّ هَبۡ لِي مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
阿拉伯语经注:
فَبَشَّرۡنَٰهُ بِغُلَٰمٍ حَلِيمٖ
Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
阿拉伯语经注:
فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ ٱلسَّعۡيَ قَالَ يَٰبُنَيَّ إِنِّيٓ أَرَىٰ فِي ٱلۡمَنَامِ أَنِّيٓ أَذۡبَحُكَ فَٱنظُرۡ مَاذَا تَرَىٰۚ قَالَ يَٰٓأَبَتِ ٱفۡعَلۡ مَا تُؤۡمَرُۖ سَتَجِدُنِيٓ إِن شَآءَ ٱللَّهُ مِنَ ٱلصَّٰبِرِينَ
Basi alipofika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyoamrishwa, utanikuta mimi, Insha Allah (Mwenyezi Mungu akipenda), katika wanaosubiri.
阿拉伯语经注:
فَلَمَّآ أَسۡلَمَا وَتَلَّهُۥ لِلۡجَبِينِ
Basi wote wawili walipojisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
阿拉伯语经注:
وَنَٰدَيۡنَٰهُ أَن يَٰٓإِبۡرَٰهِيمُ
Tulimwita: Ewe Ibrahim!
阿拉伯语经注:
قَدۡ صَدَّقۡتَ ٱلرُّءۡيَآۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyowalipa wanaotenda mema.
阿拉伯语经注:
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلۡبَلَٰٓؤُاْ ٱلۡمُبِينُ
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhahiri.
阿拉伯语经注:
وَفَدَيۡنَٰهُ بِذِبۡحٍ عَظِيمٖ
Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
阿拉伯语经注:
وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu waliokuja baadaye.
阿拉伯语经注:
سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِبۡرَٰهِيمَ
Iwe salama kwa Ibrahim!
阿拉伯语经注:
كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Hivi ndivyo tunavyowalipa wanaofanya mema.
阿拉伯语经注:
إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.
阿拉伯语经注:
وَبَشَّرۡنَٰهُ بِإِسۡحَٰقَ نَبِيّٗا مِّنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
阿拉伯语经注:
وَبَٰرَكۡنَا عَلَيۡهِ وَعَلَىٰٓ إِسۡحَٰقَۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحۡسِنٞ وَظَالِمٞ لِّنَفۡسِهِۦ مُبِينٞ
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuria zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
阿拉伯语经注:
وَلَقَدۡ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
阿拉伯语经注:
وَنَجَّيۡنَٰهُمَا وَقَوۡمَهُمَا مِنَ ٱلۡكَرۡبِ ٱلۡعَظِيمِ
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
阿拉伯语经注:
وَنَصَرۡنَٰهُمۡ فَكَانُواْ هُمُ ٱلۡغَٰلِبِينَ
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
阿拉伯语经注:
وَءَاتَيۡنَٰهُمَا ٱلۡكِتَٰبَ ٱلۡمُسۡتَبِينَ
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinachobainisha.
阿拉伯语经注:
وَهَدَيۡنَٰهُمَا ٱلصِّرَٰطَ ٱلۡمُسۡتَقِيمَ
Na tukawaongoa kwenye njia iliyonyooka.
阿拉伯语经注:
وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِمَا فِي ٱلۡأٓخِرِينَ
Na tukawaachia (sifa njema) katika watu waliokuja baadaye.
阿拉伯语经注:
سَلَٰمٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ
Iwe salama kwa Musa na Haruni!
阿拉伯语经注:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa walio wema.
阿拉伯语经注:
إِنَّهُمَا مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika wawili hao ni katika waja wetu walioamini.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّ إِلۡيَاسَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
阿拉伯语经注:
إِذۡ قَالَ لِقَوۡمِهِۦٓ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia watu wake: Hamumchi Mungu?
阿拉伯语经注:
أَتَدۡعُونَ بَعۡلٗا وَتَذَرُونَ أَحۡسَنَ ٱلۡخَٰلِقِينَ
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji.
阿拉伯语经注:
ٱللَّهَ رَبَّكُمۡ وَرَبَّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
阿拉伯语经注:
فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمۡ لَمُحۡضَرُونَ
Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa.
阿拉伯语经注:
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa.
阿拉伯语经注:
وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ
Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa waliokuja baadaye.
阿拉伯语经注:
سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِلۡ يَاسِينَ
Iwe salama kwa Ilyas.
阿拉伯语经注:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa walio wema.
阿拉伯语经注:
إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika yeye ni katika waja wetu walioamini.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّ لُوطٗا لَّمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
阿拉伯语经注:
إِذۡ نَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ
Tulipomwokoa yeye na ahali zake wote.
阿拉伯语经注:
إِلَّا عَجُوزٗا فِي ٱلۡغَٰبِرِينَ
Isipokuwa mwanamke mkongwe katika wale waliobakia nyuma.
阿拉伯语经注:
ثُمَّ دَمَّرۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ
Kisha tukawaangamiza wale wengineo.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّكُمۡ لَتَمُرُّونَ عَلَيۡهِم مُّصۡبِحِينَ
Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi.
阿拉伯语经注:
وَبِٱلَّيۡلِۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ
Na usiku. Basi je, hamyatii akilini?
阿拉伯语经注:
وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
阿拉伯语经注:
إِذۡ أَبَقَ إِلَى ٱلۡفُلۡكِ ٱلۡمَشۡحُونِ
Alipokimbia akenda katika jahazi lililosheheni.
阿拉伯语经注:
فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ ٱلۡمُدۡحَضِينَ
Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walioshindwa.
阿拉伯语经注:
فَٱلۡتَقَمَهُ ٱلۡحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٞ
Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
阿拉伯语经注:
فَلَوۡلَآ أَنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلۡمُسَبِّحِينَ
Na ingelikuwa hakuwa katika wanaomtakasa Mwenyezi Mungu.
阿拉伯语经注:
لَلَبِثَ فِي بَطۡنِهِۦٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ
Bila ya shaka angelikaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
阿拉伯语经注:
۞ فَنَبَذۡنَٰهُ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ سَقِيمٞ
Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
阿拉伯语经注:
وَأَنۢبَتۡنَا عَلَيۡهِ شَجَرَةٗ مِّن يَقۡطِينٖ
Na tukauotesha juu yake mmea wa aina ya mung'unye.
阿拉伯语经注:
وَأَرۡسَلۡنَٰهُ إِلَىٰ مِاْئَةِ أَلۡفٍ أَوۡ يَزِيدُونَ
Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
阿拉伯语经注:
فَـَٔامَنُواْ فَمَتَّعۡنَٰهُمۡ إِلَىٰ حِينٖ
Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
阿拉伯语经注:
فَٱسۡتَفۡتِهِمۡ أَلِرَبِّكَ ٱلۡبَنَاتُ وَلَهُمُ ٱلۡبَنُونَ
Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
阿拉伯语经注:
أَمۡ خَلَقۡنَا ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ إِنَٰثٗا وَهُمۡ شَٰهِدُونَ
Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?
阿拉伯语经注:
أَلَآ إِنَّهُم مِّنۡ إِفۡكِهِمۡ لَيَقُولُونَ
Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema.
阿拉伯语经注:
وَلَدَ ٱللَّهُ وَإِنَّهُمۡ لَكَٰذِبُونَ
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
阿拉伯语经注:
أَصۡطَفَى ٱلۡبَنَاتِ عَلَى ٱلۡبَنِينَ
Ati amehiari watoto wa kike kuliko wanaume?
阿拉伯语经注:
مَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ
Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?
阿拉伯语经注:
أَفَلَا تَذَكَّرُونَ
Hamkumbuki?
阿拉伯语经注:
أَمۡ لَكُمۡ سُلۡطَٰنٞ مُّبِينٞ
Au mnayo hoja iliyo wazi?
阿拉伯语经注:
فَأۡتُواْ بِكِتَٰبِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
Basi leteni Kitabu chenu kama nyinyi ni wakweli.
阿拉伯语经注:
وَجَعَلُواْ بَيۡنَهُۥ وَبَيۡنَ ٱلۡجِنَّةِ نَسَبٗاۚ وَلَقَدۡ عَلِمَتِ ٱلۡجِنَّةُ إِنَّهُمۡ لَمُحۡضَرُونَ
Na wameweka mahusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.
阿拉伯语经注:
سُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ
Ametakasika Mwenyezi Mungu mbali na hayo wanayomsingizia.
阿拉伯语经注:
إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa.
阿拉伯语经注:
فَإِنَّكُمۡ وَمَا تَعۡبُدُونَ
Basi hakika nyinyi na mnaowaabudu.
阿拉伯语经注:
مَآ أَنتُمۡ عَلَيۡهِ بِفَٰتِنِينَ
Hamwezi kuwapoteza.
阿拉伯语经注:
إِلَّا مَنۡ هُوَ صَالِ ٱلۡجَحِيمِ
Isipokuwa yule atakayeingia Motoni.
阿拉伯语经注:
وَمَا مِنَّآ إِلَّا لَهُۥ مَقَامٞ مَّعۡلُومٞ
Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّا لَنَحۡنُ ٱلصَّآفُّونَ
Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّا لَنَحۡنُ ٱلۡمُسَبِّحُونَ
Na hakika sisi ndio wenye kutakasa.
阿拉伯语经注:
وَإِن كَانُواْ لَيَقُولُونَ
Na walikuwapo waliokuwa wakisema.
阿拉伯语经注:
لَوۡ أَنَّ عِندَنَا ذِكۡرٗا مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ
Tungelikuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani.
阿拉伯语经注:
لَكُنَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Bila ya shaka tungelikuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye kumkusudia Yeye tu.
阿拉伯语经注:
فَكَفَرُواْ بِهِۦۖ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ
Lakini waliukufuru. Basi watakuja jua.
阿拉伯语经注:
وَلَقَدۡ سَبَقَتۡ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu waliotumwa.
阿拉伯语经注:
إِنَّهُمۡ لَهُمُ ٱلۡمَنصُورُونَ
Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakaonusuriwa.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ ٱلۡغَٰلِبُونَ
Na kwamba jeshi letu ndilo litakaloshinda.
阿拉伯语经注:
فَتَوَلَّ عَنۡهُمۡ حَتَّىٰ حِينٖ
Basi waachilie mbali kwa muda.
阿拉伯语经注:
وَأَبۡصِرۡهُمۡ فَسَوۡفَ يُبۡصِرُونَ
Na watazame, nao wataona.
阿拉伯语经注:
أَفَبِعَذَابِنَا يَسۡتَعۡجِلُونَ
Je, wanaiharakishia adhabu yetu?
阿拉伯语经注:
فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمۡ فَسَآءَ صَبَاحُ ٱلۡمُنذَرِينَ
Basi itakaposhuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walioonywa.
阿拉伯语经注:
وَتَوَلَّ عَنۡهُمۡ حَتَّىٰ حِينٖ
Na waache kwa muda.
阿拉伯语经注:
وَأَبۡصِرۡ فَسَوۡفَ يُبۡصِرُونَ
Na tazama, na wao wataona.
阿拉伯语经注:
سُبۡحَٰنَ رَبِّكَ رَبِّ ٱلۡعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ
Ametakasika Mola wako Mlezi Mwenye utukufu mbali na yale wanayomzulia.
阿拉伯语经注:
وَسَلَٰمٌ عَلَى ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Na Salamu juu ya Mitume.
阿拉伯语经注:
وَٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 章: 隋法提
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 拉瓦德翻译中心。 - 译解目录

由拉瓦德翻译中心团队与拉布瓦 الدعوة协会和伊斯兰内容服务协会合作翻译。

关闭