Check out the new design

पवित्र कुरअानको अर्थको अनुवाद - सवाहिली अनुवाद : अब्दुल्लाह मुहम्मद र नासिर खमीस * - अनुवादहरूको सूची


अर्थको अनुवाद सूरः: बकरः   श्लोक:
وَإِذۡ نَجَّيۡنَٰكُم مِّنۡ ءَالِ فِرۡعَوۡنَ يَسُومُونَكُمۡ سُوٓءَ ٱلۡعَذَابِ يُذَبِّحُونَ أَبۡنَآءَكُمۡ وَيَسۡتَحۡيُونَ نِسَآءَكُمۡۚ وَفِي ذَٰلِكُم بَلَآءٞ مِّن رَّبِّكُمۡ عَظِيمٞ
Kumbukeni neema Yetu juu yenu, tulipowaokoa nyinyi na mateso ya Fir'awn na wafuasi wake, waliokuwa wakiwaonjesha nyinyi adhabu kali sana, wakiwaua watoto wenu wa kiume kwa wingi na kuwaacha wanawake wenu kwa kutumika na kudhalilishwa. Katika hilo, ni mtihani kwenu kutoka kwa Mola wenu. Na katika kuokolewa kwenu na yeye, ni neema kubwa ambayo inapasa kwenu mumshukuru Mwenyezi Mungu Aliyetukuka katika kila zama zenu na vizazi vyenu.
अरबी व्याख्याहरू:
وَإِذۡ فَرَقۡنَا بِكُمُ ٱلۡبَحۡرَ فَأَنجَيۡنَٰكُمۡ وَأَغۡرَقۡنَآ ءَالَ فِرۡعَوۡنَ وَأَنتُمۡ تَنظُرُونَ
Kumbukeni neema Yetu juu yenu, tulipoipambanua bahari kwa ajili yenu na tukafanya ndani yake njia kavu, mkavuka na tukawaokoa na Fir'awn na askari wake na msizame majini. Fir'awn na askari wake walipoingia kwenye njia mlizopitia, tuliwazamisha majini mbele ya macho yenu.
अरबी व्याख्याहरू:
وَإِذۡ وَٰعَدۡنَا مُوسَىٰٓ أَرۡبَعِينَ لَيۡلَةٗ ثُمَّ ٱتَّخَذۡتُمُ ٱلۡعِجۡلَ مِنۢ بَعۡدِهِۦ وَأَنتُمۡ ظَٰلِمُونَ
Kumbukeni neema Yetu juu yenu, tulipompa Musa agizo la masiku arubaini la kuiteremshiwa Taurati, iwe ni uongofu na nuru kwenu, na punde tu alipoondoka mlichukua fursa ya kuwa yeye hayupo kwa muda mchache, mkamfanya ndama, mliyomtengeneza kwa mikono yenu, kuwa ni mungu wenu wa kuabudiwa badala ya Mwenyezi Mungu. Huu ni ukanushaji Mwenyezi Mungu mbaya kabisa. Na nyinyi mlikuwa madhalimu kwa kumfanya ndama ni Mungu.
अरबी व्याख्याहरू:
ثُمَّ عَفَوۡنَا عَنكُم مِّنۢ بَعۡدِ ذَٰلِكَ لَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ
Kisha tukawasamehe kitendo hiki kibaya, tukakubali toba yenu baada ya kurudi Musa kwa kutarajia kuwa mtamshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema Zake na fadhila Zake juu yenu, na hamtaendelea kwenye ukafiri na uasi.
अरबी व्याख्याहरू:
وَإِذۡ ءَاتَيۡنَا مُوسَى ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡفُرۡقَانَ لَعَلَّكُمۡ تَهۡتَدُونَ
Na Kumbukeni neema Yetu juu yenu, tulipompa Mūsā Kitabu chenye kupambanua baina ya haki na batili- nacho ni Taurati- ili muongoke na mtoke kwenye upotevu.
अरबी व्याख्याहरू:
وَإِذۡ قَالَ مُوسَىٰ لِقَوۡمِهِۦ يَٰقَوۡمِ إِنَّكُمۡ ظَلَمۡتُمۡ أَنفُسَكُم بِٱتِّخَاذِكُمُ ٱلۡعِجۡلَ فَتُوبُوٓاْ إِلَىٰ بَارِئِكُمۡ فَٱقۡتُلُوٓاْ أَنفُسَكُمۡ ذَٰلِكُمۡ خَيۡرٞ لَّكُمۡ عِندَ بَارِئِكُمۡ فَتَابَ عَلَيۡكُمۡۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلتَّوَّابُ ٱلرَّحِيمُ
Na Kumbukeni neema Zetu kwenu, aliposema Mūsā kuwaambia watu wake, “Hakika nyinyi mlijidhulumu nafsi zenu kwa kumfanya ndama ni mungu, basi tubieni kwa Muumba wenu kwa kuuana nyinyi kwa nyinyi. Kufanya hivyo ni bora kwenu mbele ya Muumba wenu kuliko kukaa milele Motoni.” Na nyinyi mlifuata amri hiyo, ndipo Mwenyezi Mungu Akawafanyia wema kwa kuikubali toba yenu. Hakika Yeye, Aliyetukuka, ni Ndiye Mwingi wa kukubali toba za wenye kutubia miongoni mwa waja wake na ni Ndiye Mwenye kuwarehemu.
अरबी व्याख्याहरू:
وَإِذۡ قُلۡتُمۡ يَٰمُوسَىٰ لَن نُّؤۡمِنَ لَكَ حَتَّىٰ نَرَى ٱللَّهَ جَهۡرَةٗ فَأَخَذَتۡكُمُ ٱلصَّٰعِقَةُ وَأَنتُمۡ تَنظُرُونَ
Na Kumbukeni pindi mliposema, “Ewe Mūsā! Hatutakuamini kuwa maneno tunayoyasikia kutoka kwako ni maneno ya Mwenyezi Mungu mpaka tumuone Mwenyezi Mungu waziwazi,” ukashuka moto kutoka mbinguni, na nyinyi mnauona kwa macho yenu, ukawaua kwa sababu ya madhambi yenu na ujasiri wenu kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka.
अरबी व्याख्याहरू:
ثُمَّ بَعَثۡنَٰكُم مِّنۢ بَعۡدِ مَوۡتِكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ
Kisha tukawahuisha baada ya kufa kwenu kwa kimondo cha moto, ili muishukuru neema ya Mwenyezi Mungu kwenu. Kifo hiki kilikuwa ni adhabu kwao, kisha aliwafufua wakaendelea kuishi mpaka muda wao kumalizika.
अरबी व्याख्याहरू:
وَظَلَّلۡنَا عَلَيۡكُمُ ٱلۡغَمَامَ وَأَنزَلۡنَا عَلَيۡكُمُ ٱلۡمَنَّ وَٱلسَّلۡوَىٰۖ كُلُواْ مِن طَيِّبَٰتِ مَا رَزَقۡنَٰكُمۡۚ وَمَا ظَلَمُونَا وَلَٰكِن كَانُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ يَظۡلِمُونَ
Na Kumbukeni neema Zetu mlipokuwa mnahangaika kwenye ardhi, tukawaletea kiwingu cha kuwafinika ili kiwakinge na joto la jua, tukawateremshia mann, nacho ni ktu kifananacho na gundi chenye ladha ya asali; na tukawateremshia salwa, nayo ni aina ya ndege wafananao na tomboro; na tukawaambia, “Kuleni vitu vizuri tulivyowaruzuku na msiende kinyume na dini ya Mwenyezi Mungu,” lakini hamkufuata amri. Na wao hawakutudhulumu sisi kwa kuzikanusha neema hizi, lakini walikuwa wakijidhulumu nafsi zao, Kwani mwisho mbaya wa dhuluma utawarudia wao.
अरबी व्याख्याहरू:
 
अर्थको अनुवाद सूरः: बकरः
अध्यायहरूको (सूरःहरूको) सूची رقم الصفحة
 
पवित्र कुरअानको अर्थको अनुवाद - सवाहिली अनुवाद : अब्दुल्लाह मुहम्मद र नासिर खमीस - अनुवादहरूको सूची

ड. अब्दुल्लाह मुहम्मद अबु बकर र शेख नासिर खमीसले अनुवाद गरेका छन्।

बन्द गर्नुस्