Check out the new design

पवित्र कुरअानको अर्थको अनुवाद - सवाहिली अनुवाद : अब्दुल्लाह मुहम्मद र नासिर खमीस * - अनुवादहरूको सूची


अर्थको अनुवाद सूरः: कमर   श्लोक:
وَمَآ أَمۡرُنَآ إِلَّا وَٰحِدَةٞ كَلَمۡحِۭ بِٱلۡبَصَرِ
Na haikuwa amri yetu ya kuamuru jambo tukitaka liwe isipokuwa ni kuliambia neno moja nalo ni «kuwa» nalo likawa palepale kama vile kupeleka jicho kuangalia kitu, haichelewi hata kiasi cha jicho kupepesa.
अरबी व्याख्याहरू:
وَلَقَدۡ أَهۡلَكۡنَآ أَشۡيَاعَكُمۡ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ
Na kwa hakika tuliwaangamiza wale waliofanana na nyinyi katika ukafiri miongoni mwa ummah waliopita. Basi je, kuna mwenye kuwaidhika kwa mateso na adhabu?
अरबी व्याख्याहरू:
وَكُلُّ شَيۡءٖ فَعَلُوهُ فِي ٱلزُّبُرِ
Na kila kitu walichokifanya wale wanaofanana na nyinyi waliopita, cha kheri au cha shari, kimeandikwa kwenye Vitabu ambavyo Malaika watunzi wenye kudhibiti waliviandika.
अरबी व्याख्याहरू:
وَكُلُّ صَغِيرٖ وَكَبِيرٖ مُّسۡتَطَرٌ
Na kila dogo au kubwa katika matendo yao limesajiliwa ndani ya madaftari yao, na watalipwa kwayo.
अरबी व्याख्याहरू:
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّٰتٖ وَنَهَرٖ
Hakika wachamungu watakuwa kwenye mabustani ya Pepo makubwa na mito mipana Siku ya Kiyama.
अरबी व्याख्याहरू:
فِي مَقۡعَدِ صِدۡقٍ عِندَ مَلِيكٖ مُّقۡتَدِرِۭ
Kwenye kikao cha haki, kisochokuwa na maneno ya upuuzi wala ya kuwatia madhambini, mbele ya Mwenyezi Mungu, Aliye Mfalme Mkubwa, Muumba vitu vyote, Mwenye uweza wa kila kitu, Aliyetukuka na kuwa juu.
अरबी व्याख्याहरू:
 
अर्थको अनुवाद सूरः: कमर
अध्यायहरूको (सूरःहरूको) सूची رقم الصفحة
 
पवित्र कुरअानको अर्थको अनुवाद - सवाहिली अनुवाद : अब्दुल्लाह मुहम्मद र नासिर खमीस - अनुवादहरूको सूची

ड. अब्दुल्लाह मुहम्मद अबु बकर र शेख नासिर खमीसले अनुवाद गरेका छन्।

बन्द गर्नुस्