Check out the new design

पवित्र कुरअानको अर्थको अनुवाद - सवाहिली अनुवाद : अब्दुल्लाह मुहम्मद र नासिर खमीस * - अनुवादहरूको सूची


अर्थको अनुवाद सूरः: हश्र   श्लोक:
ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ شَآقُّواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥۖ وَمَن يُشَآقِّ ٱللَّهَ فَإِنَّ ٱللَّهَ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ
Hilo- lililowapata Mayahudi duniani na linalowangojea huko Akhera- ni kuwa wao walienda kinyume sana na amri ya Mwenyezi Mungu na amri ya Mtume Wake, wakawapiga vita na wakafanya harakati za kuwaasi. Basi yoyote mwenye kuenda kinyume na Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, hakika Mwenmyezi Mungu Atamtesa vikali.
अरबी व्याख्याहरू:
مَا قَطَعۡتُم مِّن لِّينَةٍ أَوۡ تَرَكۡتُمُوهَا قَآئِمَةً عَلَىٰٓ أُصُولِهَا فَبِإِذۡنِ ٱللَّهِ وَلِيُخۡزِيَ ٱلۡفَٰسِقِينَ
Mitende mnayoikata au mnayoiacha imesimama juu ya mashina yake bila ya kuigusa , ni kwa idhini ya Mwenyezi Mungu na amri Yake, na ili Awadhalilishe kwa hilo wale waliotoka nje ya utiifu Kwake wenye kuenda kinyume na amri Yake na makatazo Yake, kwa kuwapa nguvu nyinyi kuikata mitende yao na kuichoma.
अरबी व्याख्याहरू:
وَمَآ أَفَآءَ ٱللَّهُ عَلَىٰ رَسُولِهِۦ مِنۡهُمۡ فَمَآ أَوۡجَفۡتُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ خَيۡلٖ وَلَا رِكَابٖ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ يُسَلِّطُ رُسُلَهُۥ عَلَىٰ مَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ
Na yale mali ya Mayahudi wa Banū al- Nadīr ambayo Mwenyezi Mungu Amewaletea, hamkupanda farasi wala ngamia ili myapate, lakini Mwenyezi Mungu Anawapa nguvu wajumbe Wake juu ya anayemtaka miongoni mwa maadui Wake, wakajisalimsha bila ya vita. (Mali hayo yanaitwa fay’), na fay’ ni mali yaliyochukuliwa kwa makafiri kwa haki bila ya vita. Na Mwenyezi Mungu kwa kila jambo ni Muweza, hakuna kitu chochote kinachomshinda.
अरबी व्याख्याहरू:
مَّآ أَفَآءَ ٱللَّهُ عَلَىٰ رَسُولِهِۦ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡقُرَىٰ فَلِلَّهِ وَلِلرَّسُولِ وَلِذِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَٱلۡيَتَٰمَىٰ وَٱلۡمَسَٰكِينِ وَٱبۡنِ ٱلسَّبِيلِ كَيۡ لَا يَكُونَ دُولَةَۢ بَيۡنَ ٱلۡأَغۡنِيَآءِ مِنكُمۡۚ وَمَآ ءَاتَىٰكُمُ ٱلرَّسُولُ فَخُذُوهُ وَمَا نَهَىٰكُمۡ عَنۡهُ فَٱنتَهُواْۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَۖ إِنَّ ٱللَّهَ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ
Hayo mali ya washirikina wa watu wa miji ambayo Mwenyezi Mungu Amewaletea bila kupanda farasi wala ngamia, basi hayo ni ya Mwenyezi Mungu na ya Mtume Wake, yatatumiwa kwa maslahi ya Waislamu kwa jumla, jamaa wa karibu wa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na mayatima: nao ni watoto maskini waliofiliwa na baba zao, maskini: nao ni wenye uhitaji na ufukara, na ibn al-sabīl: naye ni mgeni msafiri ambaye matumizi yake yameisha na mali yake yamemalizika. Hiyo ni kwa sababu mali yasiwe ni milki inayozunguka kwa matajiri peke yao, na mafukara na maskini wakanyimwa nayo. Na mali yoyote ambayo Mtume Amewapatia au sheria yoyote aliyowawekea, basi chukueni, na chochote kile alichowakataza basi komekeni nacho. Na muogopeni Mwenyezi Mungu kwa kufuata amri Zake na kuepuka makatazo Yake. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye mateso makali kwa anayemuasi na kuenda kinyume na amri Yake na makatazo Yake. Na aya hii ni msingi wa ulazima wa kufuata Sunnah iwe ni ya maneno, ya vitendo au ya kukubali jambo lifanyike kwa kutolikataza.
अरबी व्याख्याहरू:
لِلۡفُقَرَآءِ ٱلۡمُهَٰجِرِينَ ٱلَّذِينَ أُخۡرِجُواْ مِن دِيَٰرِهِمۡ وَأَمۡوَٰلِهِمۡ يَبۡتَغُونَ فَضۡلٗا مِّنَ ٱللَّهِ وَرِضۡوَٰنٗا وَيَنصُرُونَ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥٓۚ أُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلصَّٰدِقُونَ
Pia wanapewa mali hayo, ambayo Mwenyezi Mungu Amemletea Mtume Wake, mafukara waliohama, wale waliolazimishwa na makafiri wa Makkah watoke kwenye majumba yao na waache mali yao na huku wanaomba kwa mwenyezi Mungu Awafanyie hisani ya kuwapa riziki duniani na radhi kesho Akhera, na wanaitetea Dini ya Mwenyezi Mungu na Mtume Wake kwa kupigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu. Hao ndio wakweli ambao walikuwa wakweli wa maneno yao na vitendo vyao.
अरबी व्याख्याहरू:
وَٱلَّذِينَ تَبَوَّءُو ٱلدَّارَ وَٱلۡإِيمَٰنَ مِن قَبۡلِهِمۡ يُحِبُّونَ مَنۡ هَاجَرَ إِلَيۡهِمۡ وَلَا يَجِدُونَ فِي صُدُورِهِمۡ حَاجَةٗ مِّمَّآ أُوتُواْ وَيُؤۡثِرُونَ عَلَىٰٓ أَنفُسِهِمۡ وَلَوۡ كَانَ بِهِمۡ خَصَاصَةٞۚ وَمَن يُوقَ شُحَّ نَفۡسِهِۦ فَأُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ
Na wale wakazi wa Madina na walioamini kabla ya Waumini wa Makkah hawajahamia Madina, nao ni Anṣār (Waumini wenyeji wa Madina) wanawapenda Muhājirūn (Waumini waliohamia Madina) na wanawaliwaza kwa mali yao wala hawaoni wivu juu yao kwa mali ya fay’ waliyopewa, na wanawatanguliza waliohama na wenye uhitaji na ufukara juu ya nafsi zao, japokuwa wao wana uhitaji na ufukara. Na yoyote aliyesalimika na ubahili na uzuiaji mali yaliyomzidi, basi hao ndio wenye kufuzu waliofaulu kupata matakwa yao.
अरबी व्याख्याहरू:
 
अर्थको अनुवाद सूरः: हश्र
अध्यायहरूको (सूरःहरूको) सूची رقم الصفحة
 
पवित्र कुरअानको अर्थको अनुवाद - सवाहिली अनुवाद : अब्दुल्लाह मुहम्मद र नासिर खमीस - अनुवादहरूको सूची

ड. अब्दुल्लाह मुहम्मद अबु बकर र शेख नासिर खमीसले अनुवाद गरेका छन्।

बन्द गर्नुस्