Check out the new design

पवित्र कुरअानको अर्थको अनुवाद - सवाहिली अनुवाद : अब्दुल्लाह मुहम्मद र नासिर खमीस * - अनुवादहरूको सूची


अर्थको अनुवाद सूरः: मअारिज   श्लोक:

Al-Ma'arij

سَأَلَ سَآئِلُۢ بِعَذَابٖ وَاقِعٖ
Ameapiza mwenye kuapiza miongoni mwa washirikina, kujiapiza mwenyewe na kuwaapiza watu wake kuteremkiwa na adhabu,
अरबी व्याख्याहरू:
لِّلۡكَٰفِرِينَ لَيۡسَ لَهُۥ دَافِعٞ
nayo ni yenye kuwashukia bila shaka Siku ya Kiyama.
अरबी व्याख्याहरू:
مِّنَ ٱللَّهِ ذِي ٱلۡمَعَارِجِ
Hakuna mzuiaji yoyote wa kuizuia isipokuwa Mwenyezi Mungu, Mwenye utukufu na haiba.
अरबी व्याख्याहरू:
تَعۡرُجُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ إِلَيۡهِ فِي يَوۡمٖ كَانَ مِقۡدَارُهُۥ خَمۡسِينَ أَلۡفَ سَنَةٖ
Malaika na Jibrili wanapanda kuenda Kwake, Aliyetukuka, kwa siku moja ambayo kadiri yake ni myaka elfu hamsini katika myaka ya duniani, nayo kwa aliyeamini ni kama muda wa Swala moja ya faradhi.
अरबी व्याख्याहरू:
فَٱصۡبِرۡ صَبۡرٗا جَمِيلًا
Basi vumilia, ewe Mtume, kule kufanya kwao shere na kutaka kwao wafikiwe na adhabu kwa haraka, uvumilivu usiokuwa na babaiko wala kumshtakia asiyekuwa Mwenyezi Mungu.
अरबी व्याख्याहरू:
إِنَّهُمۡ يَرَوۡنَهُۥ بَعِيدٗا
Kwa kweli makafiri wanaiona adhabu kuwa iko mbali na wanaona kuwa si yenye kutukia.
अरबी व्याख्याहरू:
وَنَرَىٰهُ قَرِيبٗا
Na sisi tunaiona ni yenye kutukia kwa kipindi cha karibu bila shaka.
अरबी व्याख्याहरू:
يَوۡمَ تَكُونُ ٱلسَّمَآءُ كَٱلۡمُهۡلِ
Siku ambayo mbingu itayayuka iwe ni kama rojo la mafuta,
अरबी व्याख्याहरू:
وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ
na majabali yawe ni kama sufi iliyochanganywa na iliyoshanuliwa na kupeperushwa na upepo.
अरबी व्याख्याहरू:
وَلَا يَسۡـَٔلُ حَمِيمٌ حَمِيمٗا
Wala mtu hatamuuliza jamaa yake wa karibu kuhusu jambo lake, kwani kila mmoja ameshughulishwa na nafsi yake.
अरबी व्याख्याहरू:
 
अर्थको अनुवाद सूरः: मअारिज
अध्यायहरूको (सूरःहरूको) सूची رقم الصفحة
 
पवित्र कुरअानको अर्थको अनुवाद - सवाहिली अनुवाद : अब्दुल्लाह मुहम्मद र नासिर खमीस - अनुवादहरूको सूची

ड. अब्दुल्लाह मुहम्मद अबु बकर र शेख नासिर खमीसले अनुवाद गरेका छन्।

बन्द गर्नुस्