पवित्र कुरअानको अर्थको अनुवाद - सवाहिली अनुवाद : अब्दुल्लाह मुहम्मद र नासिर खमीस * - अनुवादहरूको सूची


अर्थको अनुवाद सूरः: सूरतुत्तीन   श्लोक:

Surat At-Tin

وَٱلتِّينِ وَٱلزَّيۡتُونِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa tini na zaituni, nayo ni miongoni mwa matunda yanayojulikana.
अरबी व्याख्याहरू:
وَطُورِ سِينِينَ
Na Anaapa kwa jabali la Ṭūr Sīnā’ ambalo Mwenyezi Mungu Alisema na Mūsā juu yake.
अरबी व्याख्याहरू:
وَهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ ٱلۡأَمِينِ
Na Anaapa kwa Mji huu wa amani, usiokuwa na mambo ya kutisha. Nao ni mji wa Makkah, chimbuko la Uislamu.
अरबी व्याख्याहरू:
لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِيٓ أَحۡسَنِ تَقۡوِيمٖ
Hakika Tumemuumba binadamu katika sura nzuri.
अरबी व्याख्याहरू:
ثُمَّ رَدَدۡنَٰهُ أَسۡفَلَ سَٰفِلِينَ
Kisha Tutampeleka Motoni akiwa hakumtii Mweyezi Mungu na hakuwafuata Mitume.
अरबी व्याख्याहरू:
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ فَلَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونٖ
Isipokuwa wale walioamini na wakafanya amali njema; wao watakuwa na malipo makubwa yasiyokatika wala kupungua.
अरबी व्याख्याहरू:
فَمَا يُكَذِّبُكَ بَعۡدُ بِٱلدِّينِ
Ni lipi linalokupelekea wewe, ewe binadamu, kukanusha kufufuliwa na kulipwa, hali ya kuwa kuna dalili wazi kwamba Mwenyezi Mungu Ana uweza wa kufanya hayo?
अरबी व्याख्याहरू:
أَلَيۡسَ ٱللَّهُ بِأَحۡكَمِ ٱلۡحَٰكِمِينَ
Je, Hakuwa Mwenyezi Mungu , Ambaye Ameiweka Siku hii kutoa uamuzi baina ya watu, ni muadilifu zaidi ya wanaosifika kuwa ni waadilifu katika kila Alichokiumba? Kwani? Alikuwa. Basi wataachwa viumbe rebe: hawaamrishwi wala hawakatazwi wala hawalipwi kwa mema wala hawateswi kwa mabaya? Hilo si sahihi wala haliwi.
अरबी व्याख्याहरू:
 
अर्थको अनुवाद सूरः: सूरतुत्तीन
अध्यायहरूको (सूरःहरूको) सूची رقم الصفحة
 
पवित्र कुरअानको अर्थको अनुवाद - सवाहिली अनुवाद : अब्दुल्लाह मुहम्मद र नासिर खमीस - अनुवादहरूको सूची

पवित्र कुर्आनको अर्थको स्वाहिली भाषामा अनुवाद, अनुवादक : डा. अब्दुल्लाह मुहम्मद अबू बक्र र शैख नासिर खमीस ।

बन्द गर्नुस्