Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman * - Index van vertaling


Vertaling van de betekenissen Surah: Soerat Al-Morsalaat (Zij Die Gezonden Waren)   Vers:

Surat Al-Mursalat

وَٱلۡمُرۡسَلَٰتِ عُرۡفٗا
Anaapa Mwenyezi Mungu kwa upepo unapovuma kwa mfululizo, huu baada ya huu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَٱلۡعَٰصِفَٰتِ عَصۡفٗا
Na kwa upepo wenye kuvuma kwa ukali wenye kuangamiza.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَٱلنَّٰشِرَٰتِ نَشۡرٗا
Na kwa Malaika waliopewa jukumu la mawingu, wakawa wayapeleka pale anapotaka Mwenyezi Mungu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَٱلۡفَٰرِقَٰتِ فَرۡقٗا
Na kwa Malaika wanaoshuka, kutoka kwa Mwenyezi Mungu,
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَٱلۡمُلۡقِيَٰتِ ذِكۡرًا
na amri zinazopambanua baina ya haki na batili na halali na haramu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
عُذۡرًا أَوۡ نُذۡرًا
Na kwa Malaika wanaoupokea wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu na kuuteremsha kwa Manabii Wake, unaowapa viumbe wake udhuru kutoka kwa Mwenyezi Mungu na pia onyo kutoka Kwake, ili watu wasiwe na hoja.
Arabische uitleg van de Qur'an:
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَٰقِعٞ
Hakika jambo la Kiyama mnaloahidiwa pamoja na lile la kuhesabiwa na kulipwa ni lenye kuwa hapana shaka.
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَإِذَا ٱلنُّجُومُ طُمِسَتۡ
Basi nyota zitakapofutwa na mwangaza wake ukaondoka,
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ فُرِجَتۡ
na mbingu zitakapopasuka,
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ نُسِفَتۡ
na majabali yatakapopeperuka na kukueanea huku na kule na yakawa ni mapepe yanayorushwa na upepo,
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَإِذَا ٱلرُّسُلُ أُقِّتَتۡ
Na Mitume watapowekewa wakati na muda wa baina yao na ummah wao na kusemwe,
Arabische uitleg van de Qur'an:
لِأَيِّ يَوۡمٍ أُجِّلَتۡ
«Ni Siku kubwa gani Mitume wameahirishiwa?»
Arabische uitleg van de Qur'an:
لِيَوۡمِ ٱلۡفَصۡلِ
Wameahirishiwa Siku ya hukumu na uamuzi baina ya viumbe.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ
Na nilipi lililokujulisha wewe, ewe binadamu, ni siku gani hiyo ya kutolewa uamuzi na ni zipi shida zake na vituko vyake?
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu makubwa Siku hiyo ni ya wale waliyoikanusha Siku hii iliyoahidiwa.
Arabische uitleg van de Qur'an:
أَلَمۡ نُهۡلِكِ ٱلۡأَوَّلِينَ
Kwani hatukuawaangamiza walitangulia kati ya umma waliopita kwa kuwakanusha kwao Mitume, kama vile watu wa Nūḥ, ‘Ād na Thamūd?
Arabische uitleg van de Qur'an:
ثُمَّ نُتۡبِعُهُمُ ٱلۡأٓخِرِينَ
Kisha tutawakutanisha na wao wale waliokuja nyuma kati ya wale waliokuwa ni kama wao katika ukanushaji na uasi.
Arabische uitleg van de Qur'an:
كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ
Mfano wa uangamizaji huo mkali ndivyo tutakavyowafanya wahalifu kati ya makafiri wa Makkah, kwa kumkanusha kwao Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa kila mwenye kuukanusha upweke wa Mwenyezi Mungu, unabii, kufufuliwa na kuhesabiwa.
Arabische uitleg van de Qur'an:
أَلَمۡ نَخۡلُقكُّم مِّن مَّآءٖ مَّهِينٖ
Je kwani sisi hatukuwaumba nyinyi, enyi mkusanyiko wa makafiri, kutokana na maji dhaifu yaliyo matwevu nayo ni tone la manii,
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَجَعَلۡنَٰهُ فِي قَرَارٖ مَّكِينٍ
tukayaweka maji haya kwenye mahali palipohifadhika, napo ni kizazi cha mwanamke,
Arabische uitleg van de Qur'an:
إِلَىٰ قَدَرٖ مَّعۡلُومٖ
mpaka kipindi maalumu kinachojulikana na Mwenyezi Mungu Aliyetukuka?
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَقَدَرۡنَا فَنِعۡمَ ٱلۡقَٰدِرُونَ
Tukaweza kumuumba, kumtia sura na kumtoa. Basi bora wa wenye kuweza ni s isi.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kukanusha uweza wetu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ كِفَاتًا
Je kwani hatukuifanya hii ardhi mnayoishi juu yake
Arabische uitleg van de Qur'an:
أَحۡيَآءٗ وَأَمۡوَٰتٗا
ikusanye juu ya mgongo wake walio hai wasiohesabika, na ndani ya matumbo yake wafu wasiodhibitika, na
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَجَعَلۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ شَٰمِخَٰتٖ وَأَسۡقَيۡنَٰكُم مَّآءٗ فُرَاتٗا
tukajaalia iwe na majabali yaliyojikita yaliyo marefu ili isitikisike na nyinyi, na tukawanywesha maji tamu yaliyo mazuri?
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa waliozikanusha neema hizi.
Arabische uitleg van de Qur'an:
ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Wataambiwa makafiri Siku ya Kiyama, «Endeni kwenye adhabu ya moto wa Jahanamu mliokuwa mkiukanusha duniani.
Arabische uitleg van de Qur'an:
ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ ظِلّٖ ذِي ثَلَٰثِ شُعَبٖ
Endeni mjifinike kwenye kivuli cha moshi wa moto wa Jahanamu ambacho hapo panachembuka vipande vitatu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
لَّا ظَلِيلٖ وَلَا يُغۡنِي مِنَ ٱللَّهَبِ
Kivuli hiko hakimfanyi mtu ahifadhike na joto la Siku hiyo wala hakizuii muwako wa Moto chochote.
Arabische uitleg van de Qur'an:
إِنَّهَا تَرۡمِي بِشَرَرٖ كَٱلۡقَصۡرِ
Hakika moto wa Jahanamu unarusha macheche makubwa ya moto, kila cheche moja katika hayo ni kama jengo lililoimarishwa katika ukubwa na urefu wa kuenda juu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
كَأَنَّهُۥ جِمَٰلَتٞ صُفۡرٞ
Kama kwamba hizo cheche za moto wa Jahanamu zinazopaa juu ni ngamia weusi ambao rangi yao imeingia kwenye umanjano.»
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali kwa wenye kukanusha mateso yaliyoahidiwa na Mwenyezi Mungu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
هَٰذَا يَوۡمُ لَا يَنطِقُونَ
Hii ndiyo Siku ya Kiyama ambayo wakanushaji hawatatamka maneno ya kuwanufaisha
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَلَا يُؤۡذَنُ لَهُمۡ فَيَعۡتَذِرُونَ
wala hawatapewa idhini ya kusema wakatoa nyudhuru, kwa kuwa hawatakuwa na udhuru wowote.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali kwa wenye kuikanusha siku hii na yaliyomo ndani yake.
Arabische uitleg van de Qur'an:
هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِۖ جَمَعۡنَٰكُمۡ وَٱلۡأَوَّلِينَ
Hii ni Siku ambayo Mwenyezi Mungu Atatoa uamuzi baina ya viumbe, na ukweli na ubatilifu utapambanuka. Tutawakusanya nyinyi Siku hiyo, enyi makafiri wa ummah huu, pamoja na makafiri wa mwanzo miongoni mwa ummah waliopita.
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَإِن كَانَ لَكُمۡ كَيۡدٞ فَكِيدُونِ
Basi mkiwa na hila za kujitoa na adhabu, tumieni hila zenu na mziokoe nafsi zenu na msukosuko wa Mwenyezi Mungu na mateso Yake.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuikanusha Siku ya Kiyama.
Arabische uitleg van de Qur'an:
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي ظِلَٰلٖ وَعُيُونٖ
Hakika ya wale waliomuogopa Mola wao duniani na wakaiogopa adhabu Yake kwa kufuata amri Zake na kujiepusha na makatazo Yake. Wao Siku ya Kiyama watakuwa kwenye vivuli vya miti vilivyonyoka, na chemchemi za maji zinazotembea,
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَفَوَٰكِهَ مِمَّا يَشۡتَهُونَ
na matunda mengi yanayopendwa na nafsi zao ambayo wao wanastarehe nayo. Hapo waambiwe,
Arabische uitleg van de Qur'an:
كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
«Kuleni chakula chenye ladha na mnyweni kinywaji chenye kufurahisha kwa sababu ya matendo mema mliyoyatanguliza duniani.»
Arabische uitleg van de Qur'an:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Sisi, kwa mfano wa malipo hayo makubwa, tutawalipa watu wema katika matendo yao na utiifu wao kwetu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuikanusha Siku ya Malipo na Hesabu, na kuzikanusha sterehe na mateso yaliyomo Siku hiyo.
Arabische uitleg van de Qur'an:
كُلُواْ وَتَمَتَّعُواْ قَلِيلًا إِنَّكُم مُّجۡرِمُونَ
Kisha Mwenyezi Mungu Akawaonya makafiri kwa kusema, «Kuleni aina ya vyakula vya ladha duniani na stareheni kwa matamanio yake yenye kumalizika kwa muda mchache, hakika nyinyi ni wahalifu kwa kumshirikisha kwenu Mwenyezi Mungu.»
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuikanusha Siku ya kuhesabiwa na kulipwa.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ٱرۡكَعُواْ لَا يَرۡكَعُونَ
Na wanapoambiwa hawa washirikina, «Mswalieni Mwenyezi Mungu na mnyenyekeeni,» hawanyenyekei wala hawaswali, bali wanaendelea kuonyesha kiburi chao.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuzikanusha aya za Mwenyezi Mungu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَبِأَيِّ حَدِيثِۭ بَعۡدَهُۥ يُؤۡمِنُونَ
Iwapo wao hawataiamini hii Qur’ani, basi wataamini kitabu gani na maneno gani baada yake? Na Qur’ani yenyewe ni Kitabu kilichobainisha kila kitu, kilicho wazi katika hekima zake, hukumu zake na habari zake, chenye kushinda katika matamko yake na maana yake.
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Surah: Soerat Al-Morsalaat (Zij Die Gezonden Waren)
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Swahili vertaling,Abdallah Mohammed Abubaker en Nassor Khamis Abdarahman - Index van vertaling

De vertaling van de betekenissen van de Heilige Koran naar het Swahili, vertaald door Dr. Abdullah Mohammed Abu Bakr en Sheikh Naser Khamis.

Sluit