Check out the new design

Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - De Swahili vertaling - Ali Mohsen Al-Barwani * - Index van vertaling

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Vertaling van de betekenissen Surah: Al-Lail   Vers:

Al-Lail

وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰ
Naapa kwa usiku unapo funika! [1]
[1] Naapa kwa usiku kinapo enea kiza chake!
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ
Na mchana unapo dhihiri! [2]
[2] Na naapa kwa mchana unapo zagaa mwangaza wake!
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ
Na kwa Aliye umba dume na jike! [3]
[3] Na naapa kwa Mjuzi aliye umba viwili viwili, dume na jike, katika kila vinavyo zaliwa!
Arabische uitleg van de Qur'an:
إِنَّ سَعۡيَكُمۡ لَشَتَّىٰ
Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali. [4]
[4] Hakika juhudi zenu bila ya shaka zimekhitalifiana; kwani wapo wenye kubahatika katika juhudi zao, na wako wasio bahatika.
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَأَمَّا مَنۡ أَعۡطَىٰ وَٱتَّقَىٰ
Ama mwenye kutoa na akamchamngu! [5]
[5] Ama mwenye kutoa katika Njia ya Mwenyezi Mungu, na akamkhofu Mola wake Mlezi, na kwa hivyo akaepuka anayo yakataza,
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَصَدَّقَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ
Na akaliwafiki lilio jema! [6]
[6] Na akayakinika kufuata fadhila njema, nayo ni Imani kumuamini Mwenyezi Mungu kwa kumjua,
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡيُسۡرَىٰ
Tutamsahilishia yawe mepesi. [7]
[7] Basi Sisi tutamtengenezea awe katika khulka ya wepesi na raha kwa kumwongoza kwenye njia ya kheri.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَأَمَّا مَنۢ بَخِلَ وَٱسۡتَغۡنَىٰ
Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake! [8]
[8] Ama mwenye kufanya ubakhili kwa mali yake asitoe haki ya Mwenyezi Mungu iliomo humo, na akawa hana haja na yatokayo kwa Mwenyezi Mungu,
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَكَذَّبَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ
Na akakanusha lilio jema! [9]
[9] Na akakadhibisha khulka nzuri,
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡعُسۡرَىٰ
Tutamsahilishia yawe mazito! [10]
[10] Basi huyo tutamtengenezea khulka ambayo inapelekea uzito na mashaka ya milele.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَمَا يُغۡنِي عَنۡهُ مَالُهُۥٓ إِذَا تَرَدَّىٰٓ
Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia? [11]
[11] Na kitu gani katika adhabu ambacho hayo mali yake yataweza kumkinga nacho, atapo teketea yeye mwenyewe mzima?
Arabische uitleg van de Qur'an:
إِنَّ عَلَيۡنَا لَلۡهُدَىٰ
Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu. [12]
[12] Hakika ni juu yetu, Sisi, kwa kufuatana na hikima yetu, ndio tuwabainishie viumbe njia ya uwongofu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَإِنَّ لَنَا لَلۡأٓخِرَةَ وَٱلۡأُولَىٰ
Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia. [13]
[13] Na juu yetu Sisi peke yetu, bila ya shaka, hili jambo la kuendesha yaliomo duniani na Akhera.
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَأَنذَرۡتُكُمۡ نَارٗا تَلَظَّىٰ
Basi nakuonyeni na Moto unao waka! [14]
[14] Ndio maana tukakutieni khofu ya Moto unao waka na kuripuka!
Arabische uitleg van de Qur'an:
لَا يَصۡلَىٰهَآ إِلَّا ٱلۡأَشۡقَى
Hatauingia ila mwovu kabisa! [15]
[15] Hawauingii kwa kudumu ila kafiri
Arabische uitleg van de Qur'an:
ٱلَّذِي كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Anaye kadhibisha na kupa mgongo. [16]
[16] Aliye ikadhibisha Haki na akazipuuza Ishara za Mola wake Mlezi.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلۡأَتۡقَى
Na mchamngu ataepushwa nao, [17]
[17] Na atakuwa mbali na huo Moto aliye mwingi wa kujikinga na ukafiri na maasi,
Arabische uitleg van de Qur'an:
ٱلَّذِي يُؤۡتِي مَالَهُۥ يَتَزَكَّىٰ
Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa. [18]
[18] Amabye hutoa mali yake wakati wa nafasi ili kujisafisha na uchafu wa ubakhili, na najsi ya uchoyo.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُۥ مِن نِّعۡمَةٖ تُجۡزَىٰٓ
Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa. [19]
[19] Na mtoaji huyu si kama anaye mtu yeyote ambaye ndio anamlipa kwa neema aliyo mfanyia zamani,
Arabische uitleg van de Qur'an:
إِلَّا ٱبۡتِغَآءَ وَجۡهِ رَبِّهِ ٱلۡأَعۡلَىٰ
Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa. [20]
[20] Bali anatoa hicho kwa kutafuta radhi ya Mola wake Mlezi Mtukufu tu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَلَسَوۡفَ يَرۡضَىٰ
Naye atakuja ridhika! [21]
[21] Na bila ya shaka atakuja pata kutoka kwa Mola wake Mlezi anacho kitaka kwa njia za ukamilifu kabisa, hata itimie radhi kwake.
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Surah: Al-Lail
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - De Swahili vertaling - Ali Mohsen Al-Barwani - Index van vertaling

Vertaald door Ali Mohsen Al-Barwani.

Sluit