Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Kiswahili vertaling - Ali Mohsin Al-Barwani * - Index van vertaling

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Vertaling van de betekenissen Surah: Soerat Az-Zalzalah (Het Geschudene)   Vers:

Surat Az-Zalzalah

إِذَا زُلۡزِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ زِلۡزَالَهَا
Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!
Ikitisika ardhi kwa mtikiso mkubwa, na ikasukika kwa ukomo wa kutisika na kusukika kunako mkinika na ikaweza kuchukua!
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَأَخۡرَجَتِ ٱلۡأَرۡضُ أَثۡقَالَهَا
Na itakapo toa ardhi mizigo yake!
Na ardhi ikatoa yote yaliomo katika ndani ya tumbo lake, ikiwa khazina au maiti walio kwisha zikwa!
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَقَالَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا لَهَا
Na mtu akasema: Ina nini?
Na binaadamu akasema kwa kushtuka na khofu: Ardhi hii ina nini hata inatikisika hivi, na inatoa vilivyomo tumboni mwake, ndio Saa imefika?
Arabische uitleg van de Qur'an:
يَوۡمَئِذٖ تُحَدِّثُ أَخۡبَارَهَا
Siku hiyo itahadithia khabari zake.
Siku hiyo ardhi itamsimulia mtu khabari zake zilio mshitua,
Arabische uitleg van de Qur'an:
بِأَنَّ رَبَّكَ أَوۡحَىٰ لَهَا
Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!
Kwani Mlezi wake na Muumba wake atakuwa kaifunulia, kaipa Wahyi, na kaiamuru itetemeke na ijisuke suke, ndio ikafanya upesi kutekeleza amri.
Arabische uitleg van de Qur'an:
يَوۡمَئِذٖ يَصۡدُرُ ٱلنَّاسُ أَشۡتَاتٗا لِّيُرَوۡاْ أَعۡمَٰلَهُمۡ
Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!
Siku hiyo watu watatoka makaburini mbio, nao wamo katika mtafaruku, wapate kuziona hisabu zao na malipo yao aliyo waahidi Mwenyezi Mungu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٍ خَيۡرٗا يَرَهُۥ
Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!
Basi mwenye kufanya hata kitu chenye uzito wa punje ya mchanga cha kheri ataiona katika daftari lake, na atapata malipo yake.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٖ شَرّٗا يَرَهُۥ
Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!
Na mwenye kufanya shari ya uzito wa chembe ya mchanga ataiona kadhaalika, na atapata malipo yake. Wala Mola wako Mlezi hatamdhulumu yeyote.
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Surah: Soerat Az-Zalzalah (Het Geschudene)
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Kiswahili vertaling - Ali Mohsin Al-Barwani - Index van vertaling

Vertaling van de betekenissen van de Heilige Koran naar het Swahili, vertaald door Ali Mohsin Al-Barwani.

Sluit