Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução em Swahili - Áli Muhsin * - Índice de tradução

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Tradução dos significados Surah: Suratu Al-Qiyamah   Versículo:

Surat Al-Qiyamah

لَآ أُقۡسِمُ بِيَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
Ninaapa na natilia mkazo kiapo hichi kwa Siku ya Kiyama, na hiyo ni kweli iliyo thibiti;
Os Tafssir em língua árabe:
وَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلنَّفۡسِ ٱللَّوَّامَةِ
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
Na ninaapa na natilia mkazo kiapo hichi kwa nafsi inayo mlaumu mtu kwa dhambi zake na upungufu wake, ya kwamba bila ya shaka yoyote mtafufuliwa baada ya kukusanywa mafupa yenu yaliyo tawanyika.
Os Tafssir em língua árabe:
أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَلَّن نَّجۡمَعَ عِظَامَهُۥ
Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
Hivyo mtu anadhani baada ya kuwa Sisi tulimuumba naye hakuwa kitu chochote, tutakuja shindwa kuyakusanya mafupa yake yaliyooza na yakatapanyika?
Os Tafssir em língua árabe:
بَلَىٰ قَٰدِرِينَ عَلَىٰٓ أَن نُّسَوِّيَ بَنَانَهُۥ
Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
Hasha! Sisi tuna uweza wa kuviweka sawa hata vifupa vya vidole vyake vilivyo vurugika, wachilia mbali mafupa yake makubwa makubwa ya mwili wake.
Os Tafssir em língua árabe:
بَلۡ يُرِيدُ ٱلۡإِنسَٰنُ لِيَفۡجُرَ أَمَامَهُۥ
Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
Hivyo mtu anakanya kufufuliwa? Anataka abakie katika uasi wake katika siku zote zilizo mbakilia katika umri wake ulio salia?
Os Tafssir em língua árabe:
يَسۡـَٔلُ أَيَّانَ يَوۡمُ ٱلۡقِيَٰمَةِ
Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
Anauliza kwa kuona haiwezi kutokea saa ya Kiyama: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
Os Tafssir em língua árabe:
فَإِذَا بَرِقَ ٱلۡبَصَرُ
Basi jicho litapo dawaa!
Jicho litapo tahayari kwa kufazaika na kushtuka,
Os Tafssir em língua árabe:
وَخَسَفَ ٱلۡقَمَرُ
Na mwezi utapo patwa!
Na mwangaza wa mwezi ukapotea,
Os Tafssir em língua árabe:
وَجُمِعَ ٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ
Na likakusanywa jua na mwezi!
Na jua likakusanyika na mwezi kuchomoza magharibi,
Os Tafssir em língua árabe:
يَقُولُ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذٍ أَيۡنَ ٱلۡمَفَرُّ
Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
Mtu hapo atasema: Yako wapi makimbilio kuikimbia hii adhabu?
Os Tafssir em língua árabe:
كَلَّا لَا وَزَرَ
La! Hapana pa kukimbilia!
Huachi, ewe mtu, kutafuta makimbilio? Leo huna pa kukimbilia wewe,
Os Tafssir em língua árabe:
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمُسۡتَقَرُّ
Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
ila kwa Mola wako Mlezi peke yake, ndipo penye matulivu ya waja, Peponi au Motoni.
Os Tafssir em língua árabe:
يُنَبَّؤُاْ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذِۭ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ
Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
Siku hiyo mtu ataambiwa vitendo vyake alivyo vitanguliza na alivyo viakhirisha.
Os Tafssir em língua árabe:
بَلِ ٱلۡإِنسَٰنُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ بَصِيرَةٞ
Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
Bali mtu yeye mwenyewe ni hoja iliyo wazi juu ya nafsi yake inayo mkazania kwa anayo yatenda na anayo yaacha.
Os Tafssir em língua árabe:
وَلَوۡ أَلۡقَىٰ مَعَاذِيرَهُۥ
Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
Na ijapo kuwa atajitolea chungu nzima ya udhuru na akazieneza, hawezi kabisa kuepukana na hoja hizo.
Os Tafssir em língua árabe:
لَا تُحَرِّكۡ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعۡجَلَ بِهِۦٓ
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
Usiuharikishe ulimi wako kwa kuisoma Qur'ani na kujaribu kuihifadhi kwa haraka pale unapo teremshiwa kwa Wahyi.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنَّ عَلَيۡنَا جَمۡعَهُۥ وَقُرۡءَانَهُۥ
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
Hakika ni juu yetu Sisi kuikusanya hiyo katika kifua chako, na kuithibitisha katika ulimi wako.
Os Tafssir em língua árabe:
فَإِذَا قَرَأۡنَٰهُ فَٱتَّبِعۡ قُرۡءَانَهُۥ
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
Akikusomea Mjumbe wetu (Jibril) basi nawe ifuatilize kama unavyo isikia.
Os Tafssir em língua árabe:
ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا بَيَانَهُۥ
Kisha ni juu yetu kuubainisha.
Kisha baada ya hayo ni juu yetu kuibainisha ikiingia tatizo lolote juu yako.
Os Tafssir em língua árabe:
كَلَّا بَلۡ تُحِبُّونَ ٱلۡعَاجِلَةَ
Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
Wacheni kukanya kufufuliwa, na hilo ni jambo la kweli. Lakini nyinyi mnaipenda dunia na starehe zake,
Os Tafssir em língua árabe:
وَتَذَرُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ
Na mnaacha maisha ya Akhera.
Na mnaiacha Akhera na neema zake.
Os Tafssir em língua árabe:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاضِرَةٌ
Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,
Siku hiyo zitakuwapo nyuso nzuri, zenye kumwangalia Mola wao Mlezi bila ya kusema kwa sifa gani, wajihi gani, au masafa gani.
Os Tafssir em língua árabe:
إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٞ
Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
Siku hiyo zitakuwapo nyuso nzuri, zenye kumwangalia Mola wao Mlezi bila ya kusema kwa sifa gani, wajihi gani, au masafa gani.
Os Tafssir em língua árabe:
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذِۭ بَاسِرَةٞ
Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
Na nyuso nyengine zitakuwapo zimenuna, zimekunjana mno, zinangojea zitendewe jambo ambalo kwa kitisho chake linavunja uti wa mgongo.
Os Tafssir em língua árabe:
تَظُنُّ أَن يُفۡعَلَ بِهَا فَاقِرَةٞ
Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
Zinangojea zitendewe jambo ambalo kwa kitisho chake linavunja uti wa mgongo.
Os Tafssir em língua árabe:
كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِيَ
La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
Mna nini na kuipenda dunia ambayo mnaifariki roho inapo fika katika mafupa ya kooni,
Os Tafssir em língua árabe:
وَقِيلَ مَنۡۜ رَاقٖ
Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
Na walio hudhuria wakasema: Yupo wa kumganga huyu kwa haya aliyo nayo?
Os Tafssir em língua árabe:
وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلۡفِرَاقُ
Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
Akayakinisha yule yaliyo mfika mauti kama lililo mshukia ni kuiacha dunia inayo pendwa, na imekwisha mfika shida yake kikomo cha mwisho.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱلۡتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ
Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
Na muundi wa mguu umekwisha ambatana na wa pili wakati wa kutoka roho.
Os Tafssir em língua árabe:
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمَسَاقُ
Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
Kwa Mola wako Mlezi tu siku hiyo ndio machungio ya waja, ama Peponi au Motoni.
Os Tafssir em língua árabe:
فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ
Kwa sababu hakusadiki, wala hakuswali.
Binaadamu amekanya kufufuliwa, na kwa hivyo hakumsadiki Mtume wala Qur'ani. Wala hakumtimizia Mwenyezi Mungu faridha za Swala.
Os Tafssir em língua árabe:
وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Bali alikanusha, na akageuka.
Lakini aliikadhibisha Qur'ani, akaipuuza Imani,
Os Tafssir em língua árabe:
ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ
Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
Na akatoka kwenda kwa watu wake wa nyumbani kwa maringo na kujitapa.
Os Tafssir em língua árabe:
أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰ
Ole wako, ole wako!
Ewe unaye kadhibisha, utaangamia!
Os Tafssir em língua árabe:
ثُمَّ أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰٓ
Kisha Ole wako, ole wako!
Tena utaangamia! Na tena utaangamia, na utaangamia!
Os Tafssir em língua árabe:
أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَن يُتۡرَكَ سُدًى
Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
Hivyo anadhani huyu mtu anaye kanya kufufuliwa kuwa ataachwa hivi hivi akiringa tu katika maisha yake, na akisha kufa iwe basi, wala asifufuliwe akahisabiwa kwa vitendo vyake?
Os Tafssir em língua árabe:
أَلَمۡ يَكُ نُطۡفَةٗ مِّن مَّنِيّٖ يُمۡنَىٰ
Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
Kwani yeye mtu hakuwa ni tone tu ya manii, ilio jaaliwa kuwemo katika tumbo la uzazi?
Os Tafssir em língua árabe:
ثُمَّ كَانَ عَلَقَةٗ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
Kisha hiyo tone ikawa kipande cha damu iliyo ganda, na Mwenyezi Mungu akaiumba, akaisawazisha mpaka ikawa na umbo zuri?
Os Tafssir em língua árabe:
فَجَعَلَ مِنۡهُ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ
Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
Akajaalia namna mbili, mwanamume na mwanamke?
Os Tafssir em língua árabe:
أَلَيۡسَ ذَٰلِكَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحۡـِۧيَ ٱلۡمَوۡتَىٰ
Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?
Je! Huyo Muumba wa mwanzo aliye fanya yote haya, basi si muweza wa kuwahuisha maiti baada ya kuyakusanya mafupa yao?
Os Tafssir em língua árabe:
 
Tradução dos significados Surah: Suratu Al-Qiyamah
Índice de capítulos Número de página
 
Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução em Swahili - Áli Muhsin - Índice de tradução

Tradução dos significados do Alcorão para o Swahili, pelo Ali Muhsin

Fechar