Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução em Swahili - Áli Muhsin * - Índice de tradução

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Tradução dos significados Surah: Suratu Al-Ala   Versículo:

Surat Al-A'la

سَبِّحِ ٱسۡمَ رَبِّكَ ٱلۡأَعۡلَى
Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa!
Litakase jina la Mola wako Mlezi lilio tukufu na kila kitu kisicho kuwa kinaelekeana nalo.
Os Tafssir em língua árabe:
ٱلَّذِي خَلَقَ فَسَوَّىٰ
Aliye umba, na akaweka sawa!
Aliye umba kila kitu, na akajaalia uumbaji wote sawa sawa katika hukumu na kupangana.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱلَّذِي قَدَّرَ فَهَدَىٰ
Na ambaye amekadiria na akaongoa,.
Na akakadiria kwa kila kitu kwa mujibu wa maslaha yake, na akakiongoza.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱلَّذِيٓ أَخۡرَجَ ٱلۡمَرۡعَىٰ
Na aliye otesha malisho!
Na ambaye akatoa kwenye ardhi mimea namna mbali mbali ya kuwalisha wanyama.
Os Tafssir em língua árabe:
فَجَعَلَهُۥ غُثَآءً أَحۡوَىٰ
Kisha akayafanya makavu, meusi.
Na akaifanya mimea hiyo baada ya kuwa kijani imestawi, ikakauka na imekuwa myeusi!
Os Tafssir em língua árabe:
سَنُقۡرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰٓ
Tutakusomesha wala hutasahau!
Ewe Muhammad! Sisi tutakujaalia uwe ni mwenye kuisoma Qur'ani kwa ufunuo kutoka kwetu, na wala hutosahau utacho kihifadhi.
Os Tafssir em língua árabe:
إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ يَعۡلَمُ ٱلۡجَهۡرَ وَمَا يَخۡفَىٰ
Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
Isipo kuwa anacho taka Mwenyezi Mungu ukisahau, kwani hakika Yeye Mtukufu anayajua wanayo yadhihirisha waja wake na wanayo yaficha, ikiwa maneno au vitendo.
Os Tafssir em língua árabe:
وَنُيَسِّرُكَ لِلۡيُسۡرَىٰ
Na tutakusahilishia yawe mepesi.
Na tutakuwezesha kupita njia ya kufikilia kwa wepesi mambo yako yote.
Os Tafssir em língua árabe:
فَذَكِّرۡ إِن نَّفَعَتِ ٱلذِّكۡرَىٰ
Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.
Basi wakumbushe watu ikiwa kukumbusha kutaleta manufaa, kwani inavyo faa ndio kuwanafiisha.
Os Tafssir em língua árabe:
سَيَذَّكَّرُ مَن يَخۡشَىٰ
Atakumbuka mwenye kuogopa.
Watanafiika kwa ukumbusho wako wanao mwogopa Mwenyezi Mungu.
Os Tafssir em língua árabe:
وَيَتَجَنَّبُهَا ٱلۡأَشۡقَى
Na atajitenga mbali nayo mpotovu,
Na atajitenga na ukumbusho mpotovu anaye shikilia kufanya inda na ukafiri.
Os Tafssir em língua árabe:
ٱلَّذِي يَصۡلَى ٱلنَّارَ ٱلۡكُبۡرَىٰ
Ambaye atauingia Moto mkubwa.
Ambaye ataingia kwenye Moto mkubwa ulio andaliwa kuwa ndio malipo yake.
Os Tafssir em língua árabe:
ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحۡيَىٰ
Tena humo hatakufa wala hawi hai.
Tena hatokufa huko Motoni akapumzika kwa kifo, wala hawi hai kwa uhai wa kustarehe nao.
Os Tafssir em língua árabe:
قَدۡ أَفۡلَحَ مَن تَزَكَّىٰ
Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.
Hakika amefuzu mwenye kujisafisha na ukafiri na maasi.
Os Tafssir em língua árabe:
وَذَكَرَ ٱسۡمَ رَبِّهِۦ فَصَلَّىٰ
Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akaswali.
Na akalikumbuka jina la Muumba wake kwa moyo wake na ulimi wake, na akaswali kwa unyenyekevu kama itakikanavyo.
Os Tafssir em língua árabe:
بَلۡ تُؤۡثِرُونَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا
Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!
Bali nyinyi hamfanyi hayo yanayo pelekea kufanikiwa, lakini katika hima zenu mnatanguliza maisha ya duniani kuliko ya Akhera.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ وَأَبۡقَىٰٓ
Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
Na Akhera ni bora kuliko dunia, kwa usafi wa neema zake, na ni yenye kubaki na kudumu zaidi.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنَّ هَٰذَا لَفِي ٱلصُّحُفِ ٱلۡأُولَىٰ
Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
Hakika haya yote yaliyo tajwa katika Sura hii bila ya shaka yamethibitishwa katika Vitabu vya zamani,
Os Tafssir em língua árabe:
صُحُفِ إِبۡرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ
Vitabu vya Ibrahimu na Musa.
Vitabu vya Ibrahimu na Musa; kwani haya yamewafikiana na mafunzo ya dini zote na yamesajiliwa katika Vitabu vya mbinguni.
Os Tafssir em língua árabe:
 
Tradução dos significados Surah: Suratu Al-Ala
Índice de capítulos Número de página
 
Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução em Swahili - Áli Muhsin - Índice de tradução

Tradução dos significados do Alcorão para o Swahili, pelo Ali Muhsin

Fechar