Check out the new design

ශුද්ධවූ අල් කුර්ආන් අර්ථ කථනය - ස්වහීලී පරිවර්තනය - අබ්දුල්ලා මුහම්මද් සහ නාසර් ඛමීස් * - පරිවර්තන පටුන


අර්ථ කථනය පරිච්ඡේදය: අන් නජ්ම්   වාක්‍යය:

An-Najm

وَٱلنَّجۡمِ إِذَا هَوَىٰ
Anaapa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kwa nyota zinapozama zikawa hazionekani
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
مَا ضَلَّ صَاحِبُكُمۡ وَمَا غَوَىٰ
kwamba Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, hakupotoka kwenye njia ya uongofu na haki, na hakutoka nje ya njia ya usawa. Bali yeye yuko kwenye upeo wa unyofu, usawa na uthabiti.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
وَمَا يَنطِقُ عَنِ ٱلۡهَوَىٰٓ
Kutamka kwake hakutokani na matamanio ya nafsi yake. Haikuwa
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
إِنۡ هُوَ إِلَّا وَحۡيٞ يُوحَىٰ
Qur’ani na haikuwa Sunnah isipokuwa ni wahyi unaotoka kwa Mwenyezi Mungu kwa Nabii Wake Muahammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
عَلَّمَهُۥ شَدِيدُ ٱلۡقُوَىٰ
Alimfundisha Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, Malaika mwenye nguvu nyingi,
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
ذُو مِرَّةٖ فَٱسۡتَوَىٰ
mwenye mandhari mazuri, naye ni Jibrili, amani imshukie, aliyejitokeza kwa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
وَهُوَ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡأَعۡلَىٰ
na akalingana kwa umbo lake la kihakika, kwenye pembe za sehemu za juu, nao ni pembe za jua linapochomoza.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
ثُمَّ دَنَا فَتَدَلَّىٰ
Kisha Jibrili akakaribia kwa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
فَكَانَ قَابَ قَوۡسَيۡنِ أَوۡ أَدۡنَىٰ
na akazidi kukaribia mpaka ikawa kukaribia kwake ni kiasi cha nyuta mbili au karibu zaidi.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
فَأَوۡحَىٰٓ إِلَىٰ عَبۡدِهِۦ مَآ أَوۡحَىٰ
Hapo Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, alimpelekea wahyi mja Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kile alichokituma kwa wahyi kupitia Jibrili, amani imshukie.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
مَا كَذَبَ ٱلۡفُؤَادُ مَا رَأَىٰٓ
Haukukanusha moyo wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kile alichokiona kwa macho yake.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
أَفَتُمَٰرُونَهُۥ عَلَىٰ مَا يَرَىٰ
Je mnamkanusha Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amni zimshukie, mkajadiliana naye juu ya kile alichokiona na kukishuhudia miongoni mwa alama za Mola wake?
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
وَلَقَدۡ رَءَاهُ نَزۡلَةً أُخۡرَىٰ
Na Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, alimuona Jibrili, kwa sura zake za uhakika Alizomuumba nazo Mwenyezi Mungu,
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
عِندَ سِدۡرَةِ ٱلۡمُنتَهَىٰ
mara nyingine hapo penye Sidrah al-Muntahā- mti wa mkunazi ulio kwenye uwingu wa saba ambapo hapo kinakomea kinachopanda juu kutoka ardhini na kinakomea kinachoshuka chini kutoka juu yake.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
عِندَهَا جَنَّةُ ٱلۡمَأۡوَىٰٓ
Mbele ya mti huo kuna Pepo ya al- Ma’wā (Makazi ya Daima) ambayo waliahidiwa wachamungu.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
إِذۡ يَغۡشَى ٱلسِّدۡرَةَ مَا يَغۡشَىٰ
Pindi huo Mkunazi ulipofinikwa kutokana na amri ya Mwenyezi Mungu na kitu kikubwa hakuna ajuaye sifa zake isipokuwa Mwenyezi Mungu, Aliyeshinda na kutukuka.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
مَا زَاغَ ٱلۡبَصَرُ وَمَا طَغَىٰ
Na Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, alikuwa na sifa kubwa ya uthabiti na utiifu, hayakupotoka macho yake kuliani wala kushotoni, wala hakupitisha zaidi ya kile alichoamrishwa kukiona.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
لَقَدۡ رَأَىٰ مِنۡ ءَايَٰتِ رَبِّهِ ٱلۡكُبۡرَىٰٓ
Hakika Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, aliona, usiku wa Mi'rāj (kwenda mbinguni) alama kubwa zinazojulisha uweza wa Mwenyezi Mungu na ukubwa Wake miongoni mwa Pepo, Moto na vinginevyo.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
أَفَرَءَيۡتُمُ ٱللَّٰتَ وَٱلۡعُزَّىٰ
Mnawaonaje, enyi washirikina, waungu hawa mnaowaabudu: Lāta, 'Uzzā
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
وَمَنَوٰةَ ٱلثَّالِثَةَ ٱلۡأُخۡرَىٰٓ
na mwingine wa tatu ni Manātu, je hao wamenufaisha au kudhuru mpaka wawe ni washirika wa Mwenyezi Mungu?
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
أَلَكُمُ ٱلذَّكَرُ وَلَهُ ٱلۡأُنثَىٰ
Je huyu mwanamume mnamfanya ni wenu kwa kuwa mnaridhika naye, na mwanamke ambaye hamridhiki naye nyinyi wenyewe mnamfanya ni wa Mwenyezi Mungu?
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
تِلۡكَ إِذٗا قِسۡمَةٞ ضِيزَىٰٓ
Hiko ni kigawanyo cha kidhalimu. Hawakuwa hawa masanamu isipokuwa majina yasiyokuwa na sifa zozote za ukamilifu.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
إِنۡ هِيَ إِلَّآ أَسۡمَآءٞ سَمَّيۡتُمُوهَآ أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُم مَّآ أَنزَلَ ٱللَّهُ بِهَا مِن سُلۡطَٰنٍۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَمَا تَهۡوَى ٱلۡأَنفُسُۖ وَلَقَدۡ جَآءَهُم مِّن رَّبِّهِمُ ٱلۡهُدَىٰٓ
Hayo si chochote isipokuwa ni majina mliyoyaita nyinyi na baba zenu kulingana na matamanio yenu yaliyo batili, Mwenyezi Mungu hakuteremsha ushahidi wowote wa kusadikisha madai yenu juu ya hayo. Hawafuati hawa washirikina isipokuwa dhana na matamanio ya nafsi zao zilizopotoka zikawa kando na maumbile ya sawa. Na hakika yaliwajia wao kutoka kwa Mola wao, kwa ulimi wa Nabii, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, yale ambayo ndani yake pana uongofu wao, na wao hawakunufaika nao.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
أَمۡ لِلۡإِنسَٰنِ مَا تَمَنَّىٰ
Binadamu hatapata kile anachokitamani cha kuwa waabudiwa hawa au wasiokuwa hawa, katika vitu vinavyotamaniwa na nafsi yake, watamuombea.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
فَلِلَّهِ ٱلۡأٓخِرَةُ وَٱلۡأُولَىٰ
Basi ni ya Mwenyezi Mungu amri ya duniani na Akhera.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
۞ وَكَم مِّن مَّلَكٖ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ لَا تُغۡنِي شَفَٰعَتُهُمۡ شَيۡـًٔا إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ أَن يَأۡذَنَ ٱللَّهُ لِمَن يَشَآءُ وَيَرۡضَىٰٓ
Na kuna Malaika wengi huko mbinguni, pamoja na vyeo vyao vya juu, kuombea kwao hakunufaishi chochote isipokuwa baada ya Mwenyezi Mungu kuwapa idhini wao waombee na Aridhike na yule mwenye kuombewa.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
 
අර්ථ කථනය පරිච්ඡේදය: අන් නජ්ම්
සූරා පටුන පිටු අංක
 
ශුද්ධවූ අල් කුර්ආන් අර්ථ කථනය - ස්වහීලී පරිවර්තනය - අබ්දුල්ලා මුහම්මද් සහ නාසර් ඛමීස් - පරිවර්තන පටුන

මෙය ආචාර්ය අබ්දුල්ලාහ් මුහම්මද් අබූ බක්ර් සහ අෂ්-ෂෙයික් නාසර් කමීස් විසින් පරිවර්තනය කරන ලදී.

වසන්න