Check out the new design

แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - ศูนย์การแปลรุว๊าด * - สารบัญ​คำแปล


แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: Al-A‘rāf   อายะฮ์:
إِنَّ وَلِـِّۧيَ ٱللَّهُ ٱلَّذِي نَزَّلَ ٱلۡكِتَٰبَۖ وَهُوَ يَتَوَلَّى ٱلصَّٰلِحِينَ
Hakika Mlinzi wangu ni Mwenyezi Mungu ambaye aliteremsha Kitabu. Naye ndiye anayewalinda walio wema.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱلَّذِينَ تَدۡعُونَ مِن دُونِهِۦ لَا يَسۡتَطِيعُونَ نَصۡرَكُمۡ وَلَآ أَنفُسَهُمۡ يَنصُرُونَ
Na wale mnaowaomba badala ya Mwenyezi hawawezi kuwanusuru, wala hawajinusuru wao wenyewe.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِن تَدۡعُوهُمۡ إِلَى ٱلۡهُدَىٰ لَا يَسۡمَعُواْۖ وَتَرَىٰهُمۡ يَنظُرُونَ إِلَيۡكَ وَهُمۡ لَا يُبۡصِرُونَ
Na mkiwaita kwenye uongofu, hawasikii. Na utawaona wanakutazama hali ya kuwa hawaoni.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
خُذِ ٱلۡعَفۡوَ وَأۡمُرۡ بِٱلۡعُرۡفِ وَأَعۡرِضۡ عَنِ ٱلۡجَٰهِلِينَ
Chukua yaliyo mepesi (katika matendo yao), na amrisha mema, na jitenge na majahili.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِمَّا يَنزَغَنَّكَ مِنَ ٱلشَّيۡطَٰنِ نَزۡغٞ فَٱسۡتَعِذۡ بِٱللَّهِۚ إِنَّهُۥ سَمِيعٌ عَلِيمٌ
Na kama uchochezi kutoka kwa Shetani utakuchochea, basi tafuta ulinzi wa Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ni Msikizi mzuri, Mwenye kujua vyema.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّ ٱلَّذِينَ ٱتَّقَوۡاْ إِذَا مَسَّهُمۡ طَٰٓئِفٞ مِّنَ ٱلشَّيۡطَٰنِ تَذَكَّرُواْ فَإِذَا هُم مُّبۡصِرُونَ
Hakika wale wamchao Mungu, zinapowagusa pepesi kutoka kwa Shetani, mara huzindukana na hapo huwa wenye kuiona haki.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِخۡوَٰنُهُمۡ يَمُدُّونَهُمۡ فِي ٱلۡغَيِّ ثُمَّ لَا يُقۡصِرُونَ
Na ndugu zao wanawavuta kwenye upotovu, kisha wao hawaachi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِذَا لَمۡ تَأۡتِهِم بِـَٔايَةٖ قَالُواْ لَوۡلَا ٱجۡتَبَيۡتَهَاۚ قُلۡ إِنَّمَآ أَتَّبِعُ مَا يُوحَىٰٓ إِلَيَّ مِن رَّبِّيۚ هَٰذَا بَصَآئِرُ مِن رَّبِّكُمۡ وَهُدٗى وَرَحۡمَةٞ لِّقَوۡمٖ يُؤۡمِنُونَ
Na usipowajia na Ishara, wanasema: Kwa nini hukuibuni? Sema: hakika mimi ninafuata tu yale yanayofunuliwa kwangu kutoka kwa Mola wangu Mlezi. Hii (Qur'ani) ni hoja zinazotoka kwa Mola wenu Mlezi, na uongofu, na rehema kwa kaumu wanaoamini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِذَا قُرِئَ ٱلۡقُرۡءَانُ فَٱسۡتَمِعُواْ لَهُۥ وَأَنصِتُواْ لَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ
Na inaposomwa Qur-ani, basi isikilizeni na mnyamaze ili mrehemewe.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱذۡكُر رَّبَّكَ فِي نَفۡسِكَ تَضَرُّعٗا وَخِيفَةٗ وَدُونَ ٱلۡجَهۡرِ مِنَ ٱلۡقَوۡلِ بِٱلۡغُدُوِّ وَٱلۡأٓصَالِ وَلَا تَكُن مِّنَ ٱلۡغَٰفِلِينَ
Na mkumbuke Mola wako Mlezi katika nafsi yako kwa unyenyekevu na hofu, na bila ya kuinua sauti juu kwa kauli, asubuhi na jioni, wala usiwe miongoni wa walioghafilika.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّ ٱلَّذِينَ عِندَ رَبِّكَ لَا يَسۡتَكۡبِرُونَ عَنۡ عِبَادَتِهِۦ وَيُسَبِّحُونَهُۥ وَلَهُۥ يَسۡجُدُونَۤ۩
Hakika wale walio kwa Mola wako Mlezi hawajivuni wakaacha kumuabudu, na wanamtakasa, na wanamsujudia Yeye.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
 
แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: Al-A‘rāf
สารบัญสูเราะฮ์ หมายเลข​หน้า​
 
แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - ศูนย์การแปลรุว๊าด - สารบัญ​คำแปล

แปลโดยทีมงานศูนย์แปลรุว๊าด ร่วมกับสมาคมการเผยแพร่ศาสนาอิสลามที่รอบวะฮ์ และสมาคมบริการเนื้อหาอิสลามด้วยภาษาต่าง ๆ

ปิด