Check out the new design

Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis * - Indise ng mga Salin


Salin ng mga Kahulugan Surah: Fātir   Ayah:
وَمَا يَسۡتَوِي ٱلۡبَحۡرَانِ هَٰذَا عَذۡبٞ فُرَاتٞ سَآئِغٞ شَرَابُهُۥ وَهَٰذَا مِلۡحٌ أُجَاجٞۖ وَمِن كُلّٖ تَأۡكُلُونَ لَحۡمٗا طَرِيّٗا وَتَسۡتَخۡرِجُونَ حِلۡيَةٗ تَلۡبَسُونَهَاۖ وَتَرَى ٱلۡفُلۡكَ فِيهِ مَوَاخِرَ لِتَبۡتَغُواْ مِن فَضۡلِهِۦ وَلَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ
Na hazilingani bahari mbili: hii ni tamu yenye upeo wa utamu, ni laini kupita kooni, inaondosha kiu, na hii (nyingine) ni ya chumvi yenye uchumvi mkali. Na kutokana na kila mojawapo ya bahari mbili mnakula samaki wazuri wenye ladha ya kupendeza, na mnatoa pambo, ambalo ni lulu na marjani, la nyinyi kulivaa. Na utaviona vyombo ndani ya bahari hizo vinapasua maji, ili mkiwa mnatafuta kheri Zake katika biashara na megineyo. Katika haya kuna dalili ya uweza wa Mwenyezi Mungu na upweke Wake, na huenda nyinyi mkamshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema hizi ambazo Amewaneemesha nazo.
Ang mga Tafsir na Arabe:
يُولِجُ ٱلَّيۡلَ فِي ٱلنَّهَارِ وَيُولِجُ ٱلنَّهَارَ فِي ٱلَّيۡلِ وَسَخَّرَ ٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَۖ كُلّٞ يَجۡرِي لِأَجَلٖ مُّسَمّٗىۚ ذَٰلِكُمُ ٱللَّهُ رَبُّكُمۡ لَهُ ٱلۡمُلۡكُۚ وَٱلَّذِينَ تَدۡعُونَ مِن دُونِهِۦ مَا يَمۡلِكُونَ مِن قِطۡمِيرٍ
Na Mwenyezi Mungu Anazitia nyakati za usiku ndani mchana, hivyo basi mchana ukarefuka kwa kadiri ya usiku uliopungua; na Anazitia nyakati za mchana ndani ya usiku, hivyo basi usiku ukarefuka kwa kadiri ya mchana uliopungua. Na Amedhalilisha jua na mwezi vikawa vinatembea kwa wakati maaalumu. Huyo aliyefanya hili ndiye Mwenyezi Mungu Mola wenu. Ni Wake Yeye ufalme wote. Na wale mnaowaabudu badala ya Mwenyezi Mungu hawamiliki hata utandu mwembamba unaozunguka koko ya tende.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِن تَدۡعُوهُمۡ لَا يَسۡمَعُواْ دُعَآءَكُمۡ وَلَوۡ سَمِعُواْ مَا ٱسۡتَجَابُواْ لَكُمۡۖ وَيَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ يَكۡفُرُونَ بِشِرۡكِكُمۡۚ وَلَا يُنَبِّئُكَ مِثۡلُ خَبِيرٖ
Mnapowaomba, enyi watu, waabudiwa hawa badala ya Mwenyezi Mungu, hawasikii maombi yenu, na lau wangalisikia, kwa kukisia, hawangaliwaitikia nyinyi. Na Siku ya Kiyama, watajiepusha na nyinyi. Na hakuna yoyote wa kukupasha habari, ewe Mtume, mkweli zaidi kuliko Mwenyezi Mungu, Aliye Mjuzi, Aliye Mtambuzi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
۞ يَٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ أَنتُمُ ٱلۡفُقَرَآءُ إِلَى ٱللَّهِۖ وَٱللَّهُ هُوَ ٱلۡغَنِيُّ ٱلۡحَمِيدُ
Enyi watu! Nyinyi ndio wahitaji wa Mwenyezi Mungu katika kila kitu, hamjitoshelezi Naye hata kiasi cha kupepesa jicho. Na Yeye, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, Ndiye Mwenye kujitosheleza na watu na kila kitu miongoni mwa viumbe Vyake, Mwenye kushukuriwa kwa dhati Yake na majina Yake na sifa Zake, Anaeshukuriwa kwa neema Zake. Kwani kila neema waliyo nayo watu inatoka Kwake. Sifa njema zote ni Zake na shukrani kwa kila namna.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِن يَشَأۡ يُذۡهِبۡكُمۡ وَيَأۡتِ بِخَلۡقٖ جَدِيدٖ
Akitaka Mwenyezi Mungu Atawaangamiza nyinyi, enyi watu, na Awalete watu wengine Ambao watamtii na watamuabudu Peke Yake.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَمَا ذَٰلِكَ عَلَى ٱللَّهِ بِعَزِيزٖ
Na halikuwa hili la kuwaangamiza nyinyi na kuwaleta viumbe wasiokuwa nyinyi ni jambo lisiowezekana kwa Mwenyezi Mungu, bali hilo ni jambo jepesi na rahisi
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَلَا تَزِرُ وَازِرَةٞ وِزۡرَ أُخۡرَىٰۚ وَإِن تَدۡعُ مُثۡقَلَةٌ إِلَىٰ حِمۡلِهَا لَا يُحۡمَلۡ مِنۡهُ شَيۡءٞ وَلَوۡ كَانَ ذَا قُرۡبَىٰٓۗ إِنَّمَا تُنذِرُ ٱلَّذِينَ يَخۡشَوۡنَ رَبَّهُم بِٱلۡغَيۡبِ وَأَقَامُواْ ٱلصَّلَوٰةَۚ وَمَن تَزَكَّىٰ فَإِنَّمَا يَتَزَكَّىٰ لِنَفۡسِهِۦۚ وَإِلَى ٱللَّهِ ٱلۡمَصِيرُ
Na kiumbe yoyote Aliyefanya dhambi hatabeba dhambi za mtu mwingine. Na mtu yoyote aliyelemewa na dhambi, akiomba mwenye kumbebea dhambi zake, hatapata mwenye kumbebea chochote, hata kama yule aliyemuomba ana ujamaa wa karibu na yeye, kama baba au ndugu na mfano wao. Hakika ni kwamba wewe, ewe Mtume, unawaonya wale wanaoogopa adhabu ya Mola wao pamoja na kuwa wao hawaioni na wakatekeleza Swala inavyotakikana itekelezwe. Na mwenye kujisafisha na ushirikina na maasia mengine, basi yeye anajisafisha nafsi yake. Na kwa Mwenyezi Mungu, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, ndio marejeo ya viumbe wote na mwisho wao, hapo Amlipe kila mmoja kile anachostahiki.
Ang mga Tafsir na Arabe:
 
Salin ng mga Kahulugan Surah: Fātir
Indise ng mga Surah Numero ng Pahina
 
Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis - Indise ng mga Salin

Isinalin ito nina Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr at Sheikh Nasir Khamis.

Isara