Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis * - Indise ng mga Salin


Salin ng mga Kahulugan Ayah: (170) Surah: An-Nisā’
يَٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ قَدۡ جَآءَكُمُ ٱلرَّسُولُ بِٱلۡحَقِّ مِن رَّبِّكُمۡ فَـَٔامِنُواْ خَيۡرٗا لَّكُمۡۚ وَإِن تَكۡفُرُواْ فَإِنَّ لِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلِيمًا حَكِيمٗا
Enyi watu, amewajia nyinyi Mjumbe wetu,Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na Uislamu, Dini ya haki, kutoka kwa Mola wenu, basi ikubalini na muifuate, kwani kuiyamini ni bora kwenu. Na iwapo mtaendelea na ukafiri wenu, basi Mwenyezi Mungu ni Mkwasi, Hana haja nanyi, na pia Hana haja ya kuamini kwenu, kwa kuwa Yeye ni Mmiliki wa vilivyo mbinguni na ardhini. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi mno wa maneno yenu na vitendo vyenu, ni Mwingi wa hekima katika uwekaji Sheria Wake na amri Zake. Na iwapo mbingu na ardhi zimemnenyekea Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, katika kuwa na kukadiriwa, kama viumbe vyingine vyote vilivyomnyenyekea, basi ni bora kwenu mumwamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, muiamini Qur’ani Aliyomteramshia na muifuate Dini hiyo kisheria hadi ulimwengu wote uwe ni wenye kumnyenyekea Mwenyezi Mungu kimpango uliokadiriwa na kisheria. Katika aya hii kuna dalili ya kuwa ujumbe wa Nabii wa Mwenyezi Mungu na Mtume Wake Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, unakusanya ulimwengu wote.
Ang mga Tafsir na Arabe:
 
Salin ng mga Kahulugan Ayah: (170) Surah: An-Nisā’
Indise ng mga Surah Numero ng Pahina
 
Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis - Indise ng mga Salin

Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an sa Wikang Swahili. Isinalin ito nina Doktor Abdullah Muhammad Abu Bakr at Shaykh Nasir Khamis. Inilathala ito ng King Fahd Glorious Quran Printing Complex sa Madinah Munawwarah, imprenta ng taong 1435 H.

Isara