Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis * - Indise ng mga Salin


Salin ng mga Kahulugan Ayah: (44) Surah: Fussilat
وَلَوۡ جَعَلۡنَٰهُ قُرۡءَانًا أَعۡجَمِيّٗا لَّقَالُواْ لَوۡلَا فُصِّلَتۡ ءَايَٰتُهُۥٓۖ ءَا۬عۡجَمِيّٞ وَعَرَبِيّٞۗ قُلۡ هُوَ لِلَّذِينَ ءَامَنُواْ هُدٗى وَشِفَآءٞۚ وَٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ فِيٓ ءَاذَانِهِمۡ وَقۡرٞ وَهُوَ عَلَيۡهِمۡ عَمًىۚ أُوْلَٰٓئِكَ يُنَادَوۡنَ مِن مَّكَانِۭ بَعِيدٖ
Na lau tungaliifanya hii Qur’ani tuliyokuteremshia, ewe Mtume, ni kwa lugha isiyokuwa ya Kiarabu, washirikina wangalisema, «Je, si zifafanuliwe aya zake tupate kuzifahamu na kuzijua? Ni vipi hii Qur’ani ni kwa lugha isiyokuwa ya Kiarabu na hali lugha ya huyu aliyeteremshiwa ni ya Kiarabu? Hili haliwi!» Waambie, ewe Mtume, «Hii Qur’ani, kwa wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, ni uongofu kutoka kwenye upotevu na ni ponyesho la yaliyomo vifuani ya shaka na magonjwa. Na wale wasioiamini Qur’ani kuna uziwi ndani ya mashikio yao unaowafanya wasiisikie na wasiizingatie; nayo (hiyo Qur’ani) ni upofu kwao wa nyoyo zao, hawaongoki kwayo.» Basi washirikina hao ni kama yule anayeitwa naye yuko mahali mbali, hamsikii mwenye kulingania wala hamuitiki mwenye kuita.
Ang mga Tafsir na Arabe:
 
Salin ng mga Kahulugan Ayah: (44) Surah: Fussilat
Indise ng mga Surah Numero ng Pahina
 
Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis - Indise ng mga Salin

Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an sa Wikang Swahili. Isinalin ito nina Doktor Abdullah Muhammad Abu Bakr at Shaykh Nasir Khamis. Inilathala ito ng King Fahd Glorious Quran Printing Complex sa Madinah Munawwarah, imprenta ng taong 1435 H.

Isara