Check out the new design

Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis * - Indise ng mga Salin


Salin ng mga Kahulugan Surah: Al-Mā’idah   Ayah:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا قُمۡتُمۡ إِلَى ٱلصَّلَوٰةِ فَٱغۡسِلُواْ وُجُوهَكُمۡ وَأَيۡدِيَكُمۡ إِلَى ٱلۡمَرَافِقِ وَٱمۡسَحُواْ بِرُءُوسِكُمۡ وَأَرۡجُلَكُمۡ إِلَى ٱلۡكَعۡبَيۡنِۚ وَإِن كُنتُمۡ جُنُبٗا فَٱطَّهَّرُواْۚ وَإِن كُنتُم مَّرۡضَىٰٓ أَوۡ عَلَىٰ سَفَرٍ أَوۡ جَآءَ أَحَدٞ مِّنكُم مِّنَ ٱلۡغَآئِطِ أَوۡ لَٰمَسۡتُمُ ٱلنِّسَآءَ فَلَمۡ تَجِدُواْ مَآءٗ فَتَيَمَّمُواْ صَعِيدٗا طَيِّبٗا فَٱمۡسَحُواْ بِوُجُوهِكُمۡ وَأَيۡدِيكُم مِّنۡهُۚ مَا يُرِيدُ ٱللَّهُ لِيَجۡعَلَ عَلَيۡكُم مِّنۡ حَرَجٖ وَلَٰكِن يُرِيدُ لِيُطَهِّرَكُمۡ وَلِيُتِمَّ نِعۡمَتَهُۥ عَلَيۡكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ
Enyi mlioamini! Mkitaka kuinuka ili kuswali, hali ya kuwa hamuna udhu, basi osheni nyuso zenu na mikono yenu mpaka kwenye visukusuku (Kisukusuku ni kiungo kilichoko kati ya mkono na nyoka-mkono). Na pakeni maji kwenye vichwa vyenu na muoshe miguu yenu pamoja na macho mawili ya miguu ( nayo ni mifupa miwili iliyojitokeza katika makutano ya muundi na nyayo). Na mtakapopatikana na tukiyo la hadathi kubwa ya kuondoa utohara, basi jitahirisheni kwa kuoga kabla ya kuswali. Na mkiwa ni wagonjwa au muko safarini katika hali ya afya, au iwapo mmoja wenu amemaliza haja yake, au amemuingilia mke wake, na mkawa hamkupata maji, basi ipigeni ardhi kwa mikono yenu na mupukuse nyuso zenu na mikono yenu kwayo. Mwenyezi Mungu Hataki kuwadhiki katika jambo la kujitoharisha, ndipo Akawatolea nafasi na kuwahurumia kwa kuwaruhusu kutayamamu (kutumia mchanga) badala ya kutumia maji katika kujitoharisha. Ruhusa ya kutayamamu ilikuwa ni katika kuzikamilisha neema ambazo zinapelekea kumshukuru Mneemeshaji kwa kumtii katika yale Aliyoyamrisha na kuyakataza.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱذۡكُرُواْ نِعۡمَةَ ٱللَّهِ عَلَيۡكُمۡ وَمِيثَٰقَهُ ٱلَّذِي وَاثَقَكُم بِهِۦٓ إِذۡ قُلۡتُمۡ سَمِعۡنَا وَأَطَعۡنَاۖ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلِيمُۢ بِذَاتِ ٱلصُّدُورِ
Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu kwenu katika sheria Yake Aliyowaekea na kumbukeni ahadi Yake Yeye Aliyetukuka, Aliyoichukua kwenu ya kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kuwasikiliza na kuwatii. Na mcheni Mwenyezi Mungu katika Aliyowaamrisha na Aliyowakataza. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa mnayoyaficha katika nafsi zenu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُونُواْ قَوَّٰمِينَ لِلَّهِ شُهَدَآءَ بِٱلۡقِسۡطِۖ وَلَا يَجۡرِمَنَّكُمۡ شَنَـَٔانُ قَوۡمٍ عَلَىٰٓ أَلَّا تَعۡدِلُواْۚ ٱعۡدِلُواْ هُوَ أَقۡرَبُ لِلتَّقۡوَىٰۖ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَۚ إِنَّ ٱللَّهَ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,, kuweni wasimamizi wa haki kwa ajili ya kuzitafuta radhi za Mwenyezi Mungu, muwe mashahidi kwa uadilifu. Wala kusiwapelekee nyinyi kuwachukia watu kuacha kufanya uadilifu. Fanyeni uadilifu baina ya maadui na vipenzi kwa daraja moja sawasawa. Kufanya uadilifu huko kuko karibu zaidi na kumuogopa Mwenyezi Mungu. Na jihadharini na kufanya udhalimu, hakika Mwenyezi Mungu ni Mtambuzi wa mnayoyafanya na Atawalipa kwa hayo.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَعَدَ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُم مَّغۡفِرَةٞ وَأَجۡرٌ عَظِيمٞ
Mwenyezi Mungu Amewapa ahadi, wale ambao wamemuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakatenda mema, kwamba Atawasamehe madhambi yao na Atawalipa Pepo kwa hilo. Na Mwenyezi Mungu Haendi kinyume na ahadi Yake.
Ang mga Tafsir na Arabe:
 
Salin ng mga Kahulugan Surah: Al-Mā’idah
Indise ng mga Surah Numero ng Pahina
 
Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis - Indise ng mga Salin

Isinalin ito nina Dr. Abdullah Muhammad Abu Bakr at Sheikh Nasir Khamis.

Isara