Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Indise ng mga Salin

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Salin ng mga Kahulugan Surah: Ash-Shams   Ayah:

Surat Ash-Shams

وَٱلشَّمۡسِ وَضُحَىٰهَا
Naapa kwa jua na mwangaza wake!
Naapa kwa jua na mwangaza wake na kuchomoza kwake na kwa joto lake!
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱلۡقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا
Na kwa mwezi unapo lifuatia!
Na kwa mwezi unapo lifuata na likawa nyuma yake kwa kutoa mwangaza baada ya kuchwa jua,
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا
Na kwa mchana unapo lidhihirisha!
Na kwa mchana unapo lidhihirisha jua, likaonekana wazi halikufichikana.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰهَا
Na kwa usiku unapo lifunika!
Na kwa usiku unapo lifunika jua, ukawa mwangaza wake hauonekani.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا
Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!
Na kwa mbingu na kwa Mweza Mtukufu aliye inyanyua na akaijenga kwa hikima yake.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا طَحَىٰهَا
Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!
Na kwa ardhi na kwa Mweza Mtukufu aliye ikunjua kwa kila upande, na akaitengeneza kwa ajili ya utulivu, na akaifanya kama tandiko.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَنَفۡسٖ وَمَا سَوَّىٰهَا
Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!
Na kwa nafsi, na aliye iumba na akaiweka sawa, kwa kuipa nguvu,
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَأَلۡهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقۡوَىٰهَا
Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake!
Akaifunza jema na baya, na akaipa uweza wa kutenda itakayo katika hayo,
Ang mga Tafsir na Arabe:
قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّىٰهَا
Hakika amefanikiwa aliye itakasa!
Hakika amefuzu mwenye kuisafisha nafsi yake kwa ut'iifu na vitendo vya kheri.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَقَدۡ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا
Na hakika amekhasiri aliye iviza.
Na hakika amekhasiri mwenye kuzificha fadhila zake, na akayaua matayarisho aliyo umbwa nayo ya kutenda kheri.
Ang mga Tafsir na Arabe:
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِطَغۡوَىٰهَآ
Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,
Kina Thamudi walimkanusha Nabii wao kwa upotovu wao na jeuri zao,
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشۡقَىٰهَا
Alipo simama mwovu wao mkubwa,
Alipo gutuka mwovu wao mkubwa kabisa kutaka kumchinja ngamia.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَقَالَ لَهُمۡ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقۡيَٰهَا
Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.
Saleh, Mtume wa Mwenyezi Mungu, akawaambia: Mwachilieni huyu ngamia wa Mwenyezi Mungu ale maridhawa katika ardhi ya Mwenyezi Mungu, na tahadharini msimzuie maji katika siku yake aliyo wekewa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمۡدَمَ عَلَيۡهِمۡ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمۡ فَسَوَّىٰهَا
Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.
Wakamkadhibisha Mtume wao katika hilo onyo lake, wakamchinja. Mola wao Mlezi akazibomoa nyumba zao kwa sababu ya dhambi zao; akazisawazisha na ardhi!
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَلَا يَخَافُ عُقۡبَٰهَا
Wala Yeye haogopi matokeo yake.
Wala Yeye Mwenyezi Mungu hakhofu matokeo ya adhabu hiyo, kwani hiyo ni malipo ya haki kwa yale waliyo yatenda.
Ang mga Tafsir na Arabe:
 
Salin ng mga Kahulugan Surah: Ash-Shams
Indise ng mga Surah Numero ng Pahina
 
Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Indise ng mga Salin

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Isara