Check out the new design

《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 * - 译解目录

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

含义的翻译 章: 舍姆斯   段:

Ash-Shams

وَٱلشَّمۡسِ وَضُحَىٰهَا
Naapa kwa jua na mwangaza wake! [1]
[1] Naapa kwa jua na mwangaza wake na kuchomoza kwake na kwa joto lake!
阿拉伯语经注:
وَٱلۡقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا
Na kwa mwezi unapo lifuatia! [2]
[2] Na kwa mwezi unapo lifuata na likawa nyuma yake kwa kutoa mwangaza baada ya kuchwa jua,
阿拉伯语经注:
وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا
Na kwa mchana unapo lidhihirisha! [3]
[3] Na kwa mchana unapo lidhihirisha jua, likaonekana wazi halikufichikana.
阿拉伯语经注:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰهَا
Na kwa usiku unapo lifunika! [4]
[4] Na kwa usiku unapo lifunika jua, ukawa mwangaza wake hauonekani.
阿拉伯语经注:
وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا
Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga! [5]
[5] Na kwa mbingu na kwa Mweza Mtukufu aliye inyanyua na akaijenga kwa hikima yake.
阿拉伯语经注:
وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا طَحَىٰهَا
Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza! [6]
[6] Na kwa ardhi na kwa Mweza Mtukufu aliye ikunjua kwa kila upande, na akaitengeneza kwa ajili ya utulivu, na akaifanya kama tandiko.
阿拉伯语经注:
وَنَفۡسٖ وَمَا سَوَّىٰهَا
Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza! [7]
[7] Na kwa nafsi, na aliye iumba na akaiweka sawa, kwa kuipa nguvu,
阿拉伯语经注:
فَأَلۡهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقۡوَىٰهَا
Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake! [8]
[8] Akaifunza jema na baya, na akaipa uweza wa kutenda itakayo katika hayo,
阿拉伯语经注:
قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّىٰهَا
Hakika amefanikiwa aliye itakasa! [9]
[9] Hakika amefuzu mwenye kuisafisha nafsi yake kwa ut'iifu na vitendo vya kheri.
阿拉伯语经注:
وَقَدۡ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا
Na hakika amekhasiri aliye iviza. [10]
[10] Na hakika amekhasiri mwenye kuzificha fadhila zake, na akayaua matayarisho aliyo umbwa nayo ya kutenda kheri.
阿拉伯语经注:
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِطَغۡوَىٰهَآ
Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao, [11]
[11] Kina Thamudi walimkanusha Nabii wao kwa upotovu wao na jeuri zao,
阿拉伯语经注:
إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشۡقَىٰهَا
Alipo simama mwovu wao mkubwa, [12]
[12] Alipo gutuka mwovu wao mkubwa kabisa kutaka kumchinja ngamia.
阿拉伯语经注:
فَقَالَ لَهُمۡ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقۡيَٰهَا
Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake. [13]
[13] Saleh, Mtume wa Mwenyezi Mungu, akawaambia: Mwachilieni huyu ngamia wa Mwenyezi Mungu ale maridhawa katika ardhi ya Mwenyezi Mungu, na tahadharini msimzuie maji katika siku yake aliyo wekewa.
阿拉伯语经注:
فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمۡدَمَ عَلَيۡهِمۡ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمۡ فَسَوَّىٰهَا
Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa. [14]
[14] Wakamkadhibisha Mtume wao katika hilo onyo lake, wakamchinja. Mola wao Mlezi akazibomoa nyumba zao kwa sababu ya dhambi zao; akazisawazisha na ardhi!
阿拉伯语经注:
وَلَا يَخَافُ عُقۡبَٰهَا
Wala Yeye haogopi matokeo yake. [15]
[15] Wala Yeye Mwenyezi Mungu hakhofu matokeo ya adhabu hiyo, kwani hiyo ni malipo ya haki kwa yale waliyo yatenda.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 章: 舍姆斯
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 - 译解目录

阿里·穆哈森·伯瓦尼翻译。

关闭