Check out the new design

Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili ng Sentro ng Rowad sa Pagsasalin * - Indise ng mga Salin


Salin ng mga Kahulugan Surah: Ad-Dukhān   Ayah:

Ad-Dukhan

حمٓ
Ha Mim.[1]
[1] Herufi hizi "Ha, Mim" na herufi nyinginezo za mkato zilizo mwanzoni mwa sura mbalimbali zinaonyesha hali ya ushindi wa Qur-ani. Kwani, washirikina walipewa changamoto kwayo, lakini wakashindwa na hawakuweza kuipinga, ilhali inajumuisha herufi hizi zinazounda lugha ya Kiarabu. Kwa hivyo, kutoweza kwa Waarabu kuleta kitu kama hicho - ingawa walikuwa ndio watu wenye ufasaha zaidi - kunaonyesha kwamba Qur-ani ni ufunuo (wahyi) kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ
Ninaapa kwa Kitabu kinachobainisha.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّآ أَنزَلۡنَٰهُ فِي لَيۡلَةٖ مُّبَٰرَكَةٍۚ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ
Hakika Sisi tumekiteremsha katika usiku uliobarikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فِيهَا يُفۡرَقُ كُلُّ أَمۡرٍ حَكِيمٍ
Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hekima.
Ang mga Tafsir na Arabe:
أَمۡرٗا مِّنۡ عِندِنَآۚ إِنَّا كُنَّا مُرۡسِلِينَ
Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.
Ang mga Tafsir na Arabe:
رَحۡمَةٗ مِّن رَّبِّكَۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ
Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.
Ang mga Tafsir na Arabe:
رَبِّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.
Ang mga Tafsir na Arabe:
لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ يُحۡيِۦ وَيُمِيتُۖ رَبُّكُمۡ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.
Ang mga Tafsir na Arabe:
بَلۡ هُمۡ فِي شَكّٖ يَلۡعَبُونَ
Lakini wao wanacheza katika shaka.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَٱرۡتَقِبۡ يَوۡمَ تَأۡتِي ٱلسَّمَآءُ بِدُخَانٖ مُّبِينٖ
Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapoleta moshi ulio dhahiri.
Ang mga Tafsir na Arabe:
يَغۡشَى ٱلنَّاسَۖ هَٰذَا عَذَابٌ أَلِيمٞ
Utakaowafunika watu. Hii ni adhabu chungu!
Ang mga Tafsir na Arabe:
رَّبَّنَا ٱكۡشِفۡ عَنَّا ٱلۡعَذَابَ إِنَّا مُؤۡمِنُونَ
Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.
Ang mga Tafsir na Arabe:
أَنَّىٰ لَهُمُ ٱلذِّكۡرَىٰ وَقَدۡ جَآءَهُمۡ رَسُولٞ مُّبِينٞ
Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.
Ang mga Tafsir na Arabe:
ثُمَّ تَوَلَّوۡاْ عَنۡهُ وَقَالُواْ مُعَلَّمٞ مَّجۡنُونٌ
Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: 'Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.'
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّا كَاشِفُواْ ٱلۡعَذَابِ قَلِيلًاۚ إِنَّكُمۡ عَآئِدُونَ
Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!
Ang mga Tafsir na Arabe:
يَوۡمَ نَبۡطِشُ ٱلۡبَطۡشَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰٓ إِنَّا مُنتَقِمُونَ
Siku tutakayoyashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
۞ وَلَقَدۡ فَتَنَّا قَبۡلَهُمۡ قَوۡمَ فِرۡعَوۡنَ وَجَآءَهُمۡ رَسُولٞ كَرِيمٌ
Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
أَنۡ أَدُّوٓاْ إِلَيَّ عِبَادَ ٱللَّهِۖ إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Akasema: 'Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَأَن لَّا تَعۡلُواْ عَلَى ٱللَّهِۖ إِنِّيٓ ءَاتِيكُم بِسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٖ
Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِنِّي عُذۡتُ بِرَبِّي وَرَبِّكُمۡ أَن تَرۡجُمُونِ
Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِن لَّمۡ تُؤۡمِنُواْ لِي فَٱعۡتَزِلُونِ
Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.'
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنَّ هَٰٓؤُلَآءِ قَوۡمٞ مُّجۡرِمُونَ
Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: 'Hakika watu hawa ni wakosefu.'
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَأَسۡرِ بِعِبَادِي لَيۡلًا إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
Mwenyezi Mungu akasema: 'Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱتۡرُكِ ٱلۡبَحۡرَ رَهۡوًاۖ إِنَّهُمۡ جُندٞ مُّغۡرَقُونَ
Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao ni jeshi litakalozamishwa.'
Ang mga Tafsir na Arabe:
كَمۡ تَرَكُواْ مِن جَنَّٰتٖ وَعُيُونٖ
Mabustani mangapi na chemchemi ngapi waliziacha!
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَزُرُوعٖ وَمَقَامٖ كَرِيمٖ
Na mimea na vyeo vitukufu!
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَنَعۡمَةٖ كَانُواْ فِيهَا فَٰكِهِينَ
Na neema walizokuwa wakijistareheshea!
Ang mga Tafsir na Arabe:
كَذَٰلِكَۖ وَأَوۡرَثۡنَٰهَا قَوۡمًا ءَاخَرِينَ
Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَمَا بَكَتۡ عَلَيۡهِمُ ٱلسَّمَآءُ وَٱلۡأَرۡضُ وَمَا كَانُواْ مُنظَرِينَ
Basi mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَلَقَدۡ نَجَّيۡنَا بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ مِنَ ٱلۡعَذَابِ ٱلۡمُهِينِ
Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,
Ang mga Tafsir na Arabe:
مِن فِرۡعَوۡنَۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَالِيٗا مِّنَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ
Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَلَقَدِ ٱخۡتَرۡنَٰهُمۡ عَلَىٰ عِلۡمٍ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَءَاتَيۡنَٰهُم مِّنَ ٱلۡأٓيَٰتِ مَا فِيهِ بَلَٰٓؤٞاْ مُّبِينٌ
Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَيَقُولُونَ
Hakika hawa wanasema:
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنۡ هِيَ إِلَّا مَوۡتَتُنَا ٱلۡأُولَىٰ وَمَا نَحۡنُ بِمُنشَرِينَ
Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَأۡتُواْ بِـَٔابَآئِنَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.'
Ang mga Tafsir na Arabe:
أَهُمۡ خَيۡرٌ أَمۡ قَوۡمُ تُبَّعٖ وَٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ أَهۡلَكۡنَٰهُمۡۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ مُجۡرِمِينَ
Je, ni wao bora au watu wa Tubbaa' na waliokuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَمَا خَلَقۡنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَا لَٰعِبِينَ
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo.
Ang mga Tafsir na Arabe:
مَا خَلَقۡنَٰهُمَآ إِلَّا بِٱلۡحَقِّ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ
Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّ يَوۡمَ ٱلۡفَصۡلِ مِيقَٰتُهُمۡ أَجۡمَعِينَ
Hakika siku ya Uamuzi ni wakati uliowekwa kwa wao wote.
Ang mga Tafsir na Arabe:
يَوۡمَ لَا يُغۡنِي مَوۡلًى عَن مَّوۡلٗى شَيۡـٔٗا وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ
Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِلَّا مَن رَّحِمَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Isipokuwa atakayemrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu mno.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّ شَجَرَتَ ٱلزَّقُّومِ
Hakika Mti wa Zaqqum
Ang mga Tafsir na Arabe:
طَعَامُ ٱلۡأَثِيمِ
Ni chakula cha mwenye dhambi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
كَٱلۡمُهۡلِ يَغۡلِي فِي ٱلۡبُطُونِ
Kama shaba iliyoyeyushwa, hutokota matumboni.
Ang mga Tafsir na Arabe:
كَغَلۡيِ ٱلۡحَمِيمِ
Kama kutokota kwa maji ya moto.
Ang mga Tafsir na Arabe:
خُذُوهُ فَٱعۡتِلُوهُ إِلَىٰ سَوَآءِ ٱلۡجَحِيمِ
(Itasemwa): 'Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!
Ang mga Tafsir na Arabe:
ثُمَّ صُبُّواْ فَوۡقَ رَأۡسِهِۦ مِنۡ عَذَابِ ٱلۡحَمِيمِ
Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayochemka.'
Ang mga Tafsir na Arabe:
ذُقۡ إِنَّكَ أَنتَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡكَرِيمُ
Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّ هَٰذَا مَا كُنتُم بِهِۦ تَمۡتَرُونَ
Hakika haya ndiyo mliyokuwa mkiyatilia shaka.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي مَقَامٍ أَمِينٖ
Hakika wacha Mungu watakuwa katika mahali pa amani.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فِي جَنَّٰتٖ وَعُيُونٖ
Katika mabustani na chemchemi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
يَلۡبَسُونَ مِن سُندُسٖ وَإِسۡتَبۡرَقٖ مُّتَقَٰبِلِينَ
Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana.
Ang mga Tafsir na Arabe:
كَذَٰلِكَ وَزَوَّجۡنَٰهُم بِحُورٍ عِينٖ
Hivi ndivyo itakavyokuwa, na tutawaoza mahurilaini.
Ang mga Tafsir na Arabe:
يَدۡعُونَ فِيهَا بِكُلِّ فَٰكِهَةٍ ءَامِنِينَ
Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani.
Ang mga Tafsir na Arabe:
لَا يَذُوقُونَ فِيهَا ٱلۡمَوۡتَ إِلَّا ٱلۡمَوۡتَةَ ٱلۡأُولَىٰۖ وَوَقَىٰهُمۡ عَذَابَ ٱلۡجَحِيمِ
Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda na adhabu ya Jahannamu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَضۡلٗا مِّن رَّبِّكَۚ ذَٰلِكَ هُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ
Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَإِنَّمَا يَسَّرۡنَٰهُ بِلِسَانِكَ لَعَلَّهُمۡ يَتَذَكَّرُونَ
Basi tumeifanya nyepesi hii Qur-ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَٱرۡتَقِبۡ إِنَّهُم مُّرۡتَقِبُونَ
Ngoja tu, na wao wangoje pia.
Ang mga Tafsir na Arabe:
 
Salin ng mga Kahulugan Surah: Ad-Dukhān
Indise ng mga Surah Numero ng Pahina
 
Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili ng Sentro ng Rowad sa Pagsasalin - Indise ng mga Salin

Isinalin ito ng isang pangkat ng Sentro ng Rowad sa Pagsasalin sa pakikipagtulungan ng Samahan ng Da‘wah sa Rabwah at Samahan ng Paglilingkod sa Nilalamang Islāmiko sa mga Wika.

Isara