Check out the new design

Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili ng Sentro ng Rowad sa Pagsasalin * - Indise ng mga Salin


Salin ng mga Kahulugan Surah: Al-Hāqqah   Ayah:
وَجَآءَ فِرۡعَوۡنُ وَمَن قَبۡلَهُۥ وَٱلۡمُؤۡتَفِكَٰتُ بِٱلۡخَاطِئَةِ
Na Firauni na waliomtangulia, na miji iliyopinduliwa chini juu, walileta khatia.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَعَصَوۡاْ رَسُولَ رَبِّهِمۡ فَأَخَذَهُمۡ أَخۡذَةٗ رَّابِيَةً
akamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato uliozidi nguvu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّا لَمَّا طَغَا ٱلۡمَآءُ حَمَلۡنَٰكُمۡ فِي ٱلۡجَارِيَةِ
Maji yalipofurika Sisi tulikupandisheni katika safina.
Ang mga Tafsir na Arabe:
لِنَجۡعَلَهَا لَكُمۡ تَذۡكِرَةٗ وَتَعِيَهَآ أُذُنٞ وَٰعِيَةٞ
Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalosikia liyahifadhi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَإِذَا نُفِخَ فِي ٱلصُّورِ نَفۡخَةٞ وَٰحِدَةٞ
Na litapopulizwa barugumu mpulizo mmoja tu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَحُمِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ وَٱلۡجِبَالُ فَدُكَّتَا دَكَّةٗ وَٰحِدَةٗ
Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَيَوۡمَئِذٖ وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ
Siku hiyo ndio Tukio litatukia.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱنشَقَّتِ ٱلسَّمَآءُ فَهِيَ يَوۡمَئِذٖ وَاهِيَةٞ
Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱلۡمَلَكُ عَلَىٰٓ أَرۡجَآئِهَاۚ وَيَحۡمِلُ عَرۡشَ رَبِّكَ فَوۡقَهُمۡ يَوۡمَئِذٖ ثَمَٰنِيَةٞ
Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
يَوۡمَئِذٖ تُعۡرَضُونَ لَا تَخۡفَىٰ مِنكُمۡ خَافِيَةٞ
Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ فَيَقُولُ هَآؤُمُ ٱقۡرَءُواْ كِتَٰبِيَهۡ
Basi ama atakayepewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنِّي ظَنَنتُ أَنِّي مُلَٰقٍ حِسَابِيَهۡ
Hakika nilijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ
Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ
Katika Bustani ya juu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
قُطُوفُهَا دَانِيَةٞ
Matunda yake ya karibu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَآ أَسۡلَفۡتُمۡ فِي ٱلۡأَيَّامِ ٱلۡخَالِيَةِ
Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyotanguliza katika siku zilizopita.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِشِمَالِهِۦ فَيَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي لَمۡ أُوتَ كِتَٰبِيَهۡ
Na ama atakayepewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingelipewa kitabu changu!
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَلَمۡ أَدۡرِ مَا حِسَابِيَهۡ
Wala nisingelijua nini hisabu yangu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
يَٰلَيۡتَهَا كَانَتِ ٱلۡقَاضِيَةَ
Laiti mauti ndiyo yangelikuwa ya kunimaliza kabisa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
مَآ أَغۡنَىٰ عَنِّي مَالِيَهۡۜ
Mali yangu hayakunifaa kitu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
هَلَكَ عَنِّي سُلۡطَٰنِيَهۡ
Madaraka yangu yamenipotea.
Ang mga Tafsir na Arabe:
خُذُوهُ فَغُلُّوهُ
(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!
Ang mga Tafsir na Arabe:
ثُمَّ ٱلۡجَحِيمَ صَلُّوهُ
Kisha mtupeni Motoni!
Ang mga Tafsir na Arabe:
ثُمَّ فِي سِلۡسِلَةٖ ذَرۡعُهَا سَبۡعُونَ ذِرَاعٗا فَٱسۡلُكُوهُ
Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabini!
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّهُۥ كَانَ لَا يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ ٱلۡعَظِيمِ
Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ
Wala hahimizi kulisha masikini.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَلَيۡسَ لَهُ ٱلۡيَوۡمَ هَٰهُنَا حَمِيمٞ
Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
 
Salin ng mga Kahulugan Surah: Al-Hāqqah
Indise ng mga Surah Numero ng Pahina
 
Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili ng Sentro ng Rowad sa Pagsasalin - Indise ng mga Salin

Isinalin ito ng isang pangkat ng Sentro ng Rowad sa Pagsasalin sa pakikipagtulungan ng Samahan ng Da‘wah sa Rabwah at Samahan ng Paglilingkod sa Nilalamang Islāmiko sa mga Wika.

Isara