Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Mealler fihristi


Anlam tercümesi Sure: Sûretu'l-Hakkâh   Ayet:

Surat Al-Haqqah

ٱلۡحَآقَّةُ
Kiyama chenye kutukia kikweli ambacho ndani yake inahakikika ahadi ya Mwenyezi Mungu na onyo Lake.
Arapça tefsirler:
مَا ٱلۡحَآقَّةُ
Kiyama chenye kutukia kikweli ni zipi sifa zake na hali zake?
Arapça tefsirler:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحَآقَّةُ
Na kitu gani kilichokujulisha wewe, ewe Mtume, na kukueleza uhakika wa Kiyama na kikakupa wewe picha ya janga lake na shida zake?
Arapça tefsirler:
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ وَعَادُۢ بِٱلۡقَارِعَةِ
Thamūd, nao ni watu wa Ṣāliḥ, na ‘Ād, nao ni watu wa Hūd, walikikanusha Kiyama ambacho kinagonga nyoyo kwa vituko janga lake.
Arapça tefsirler:
فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهۡلِكُواْ بِٱلطَّاغِيَةِ
Ama hao Thamūd waliangamizwa kwa ukelele mkubwa uliopita kiasi ukali wake,
Arapça tefsirler:
وَأَمَّا عَادٞ فَأُهۡلِكُواْ بِرِيحٖ صَرۡصَرٍ عَاتِيَةٖ
na ama‘Ād waliangamizwa kwa upepo baridi unaovuma kwa nguvu.
Arapça tefsirler:
سَخَّرَهَا عَلَيۡهِمۡ سَبۡعَ لَيَالٖ وَثَمَٰنِيَةَ أَيَّامٍ حُسُومٗاۖ فَتَرَى ٱلۡقَوۡمَ فِيهَا صَرۡعَىٰ كَأَنَّهُمۡ أَعۡجَازُ نَخۡلٍ خَاوِيَةٖ
Mwenyezi Mungu Aliwasaliti nao masiku saba na michana minane yenye kufuatana, isiyokatika wala kusimama. Utawaona watu katika masiku hayo na michana wamekufa, kama kwamba wao ni vigogo mitende iliyo mibovu iliyolika ndani.
Arapça tefsirler:
فَهَلۡ تَرَىٰ لَهُم مِّنۢ بَاقِيَةٖ
Basi je utamuona mtu yoyote miongoni mwao mwenye kusalia bila kuangamia?
Arapça tefsirler:
وَجَآءَ فِرۡعَوۡنُ وَمَن قَبۡلَهُۥ وَٱلۡمُؤۡتَفِكَٰتُ بِٱلۡخَاطِئَةِ
Na akaja mpita kiasi katika uasi Fir’awn na ummah waliomtangulia waliokanusha Mitume wao, na watu wakazi wa vijiji vya watu wa Lūṭ ambao majumba yao yaliwapindukia kwa sababu ya kitendo kibaya walichokifanya, cha ukafiri, ushirikina na mambo machafu.
Arapça tefsirler:
فَعَصَوۡاْ رَسُولَ رَبِّهِمۡ فَأَخَذَهُمۡ أَخۡذَةٗ رَّابِيَةً
Kila ummah kati yao walimuasi mjumbe wa Mola wao ambaye alitumwa kwao, basi Mwenyezi Mungu Akawashika mshiko mkali mno.
Arapça tefsirler:
إِنَّا لَمَّا طَغَا ٱلۡمَآءُ حَمَلۡنَٰكُمۡ فِي ٱلۡجَارِيَةِ
Sisi, maji yalipopita kipimo chake, mpaka yakawa juu na kuangatika juu ya kila kitu, tuliwabeba watu wa asili zenu pamoja na Nūḥ ndani ya jahazi ambayo ilikuwa ndio sababu ya kuokoka Waumini na kuzamishwa makafiri,
Arapça tefsirler:
لِنَجۡعَلَهَا لَكُمۡ تَذۡكِرَةٗ وَتَعِيَهَآ أُذُنٞ وَٰعِيَةٞ
hili likiwa ni mazingatio na mawaidha, na lipate kulihifadhi tukio hilo kila shikio ambalo kazi yake ni kuhifadhi, na lielewe kile ambacho limekisikia.
Arapça tefsirler:
فَإِذَا نُفِخَ فِي ٱلصُّورِ نَفۡخَةٞ وَٰحِدَةٞ
Pindi Malaika atakapopuliza kwenye barugumu mpulizo mmoja, nao ni mpulizo wa kwanza ambao hapo patapatikana maangamivu ya ulimwengu,.
Arapça tefsirler:
وَحُمِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ وَٱلۡجِبَالُ فَدُكَّتَا دَكَّةٗ وَٰحِدَةٗ
Na pindi ardhi na milima itakapoinuliwa kutoka mahali ilipo ikavunjwavunjwa na kugongwagongwa mara moja,
Arapça tefsirler:
فَيَوۡمَئِذٖ وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ
Wakati huo Kiyama kitasimama.
Arapça tefsirler:
وَٱنشَقَّتِ ٱلسَّمَآءُ فَهِيَ يَوۡمَئِذٖ وَاهِيَةٞ
Na mbingu zitafanya ufa na ziwe dhaifu na kulegea Siku hiyo, hazitakuwa na mshikamano wala ugumu.
Arapça tefsirler:
وَٱلۡمَلَكُ عَلَىٰٓ أَرۡجَآئِهَاۚ وَيَحۡمِلُ عَرۡشَ رَبِّكَ فَوۡقَهُمۡ يَوۡمَئِذٖ ثَمَٰنِيَةٞ
Na Malaika watakuwa kwenye pambizo na pande zake, na wataibeba «Arshi ya Mola wako juu yao Siku ya Kiyama Malaika wanane miongoni mwa Malaika wakubwa.
Arapça tefsirler:
يَوۡمَئِذٖ تُعۡرَضُونَ لَا تَخۡفَىٰ مِنكُمۡ خَافِيَةٞ
Katika Siku hiyo, mtaorodheshwa kwa Mwenyezi Mungu, enyi wat, ili mhesabiwe na mlipwe, hakuna chochote kitakachofichamana kwa Mwenyewzi Mungu miongoni mwa siri zenu.
Arapça tefsirler:
فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ فَيَقُولُ هَآؤُمُ ٱقۡرَءُواْ كِتَٰبِيَهۡ
Ama yule Atakayepewa kitabu cha matendo yake kwa mkono wake wa kulia, atasema akiwa katika hali ya ubashasha na furaha, ‘Chukueni kitabu changu mkisome!
Arapça tefsirler:
إِنِّي ظَنَنتُ أَنِّي مُلَٰقٍ حِسَابِيَهۡ
Mimi nilikuwa na yakini duniani kuwa nitapata malipo yangu Siku ya Kiyama, nikajiandalia nayo kwa matayarisho ya Imani na matendo mema.»
Arapça tefsirler:
فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ
Basi yeye atakuwa kwenye maisha ya furaha ya kumridhisha;
Arapça tefsirler:
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ
kwenye Pepo ya juu kimahali na daraja;
Arapça tefsirler:
قُطُوفُهَا دَانِيَةٞ
matunda yake yako karibu, anayachuma anayesimama, anayeketi na anayelala.
Arapça tefsirler:
كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَآ أَسۡلَفۡتُمۡ فِي ٱلۡأَيَّامِ ٱلۡخَالِيَةِ
Wataambiwa, «Kuleni na mnyweni kila aina ya vyakula na vinywaji, mkiwa mbali na kila kero, mkiwa mmesalimika na kila mnalolichukia, kwa sababu ya matendo mema mliyoyatanguliza siku za ulimwenguni.»
Arapça tefsirler:
وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِشِمَالِهِۦ فَيَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي لَمۡ أُوتَ كِتَٰبِيَهۡ
Na ama yule atakayepewa kitabu cha matendo yake kwa mkono wake wa kushoto,
Arapça tefsirler:
وَلَمۡ أَدۡرِ مَا حِسَابِيَهۡ
atasema akiwa katika hali ya kujuta na kupata hasara,
Arapça tefsirler:
يَٰلَيۡتَهَا كَانَتِ ٱلۡقَاضِيَةَ
«Natamani lau mimi sikupewa kitabu changu na sikujua malipo yangu! Natamani lau kile kifo nilichokufa duniani kilikuwa ndicho chenye kukata kabisa mambo yangu na nisifufuliwe baada yake!
Arapça tefsirler:
مَآ أَغۡنَىٰ عَنِّي مَالِيَهۡۜ
Mali yangu niliyoyakusanya hayakuninufaisha duniani!
Arapça tefsirler:
هَلَكَ عَنِّي سُلۡطَٰنِيَهۡ
Hoja zangu zote zimenionokea, na sina hoja tena ya kuitumia kama hoja.»
Arapça tefsirler:
خُذُوهُ فَغُلُّوهُ
Hapo waambiwe walinzi wa Moto wa Jahanamu, «Mchukueni mhalifu huyu mfanya dhambi, ikusanyeni mikono yake shingoni mwake muitie pingu,
Arapça tefsirler:
ثُمَّ ٱلۡجَحِيمَ صَلُّوهُ
kisha mtieni kwenye Moto unaowaka sana, apate kulihisi joto lake.
Arapça tefsirler:
ثُمَّ فِي سِلۡسِلَةٖ ذَرۡعُهَا سَبۡعُونَ ذِرَاعٗا فَٱسۡلُكُوهُ
Kisha mfungeni mnyororo wa chuma ambao urefu wake ni dhiraa sabini mumkokote nao na mumtie humo.
Arapça tefsirler:
إِنَّهُۥ كَانَ لَا يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ ٱلۡعَظِيمِ
Kwani yeye hakuwa akiamini kuwa Mwenyezi Mungu Ndiye Mola wa Haki, Peke Yake, Asiye na mshirika.
Arapça tefsirler:
وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ
Wala hakuwa akitenda matendo yanayoambatana na uongofu Wake, wala hakuwa akiwahimiza watu duniani kuwalisha wenye uhitaji miongoni mwa masikini na wengineo.
Arapça tefsirler:
فَلَيۡسَ لَهُ ٱلۡيَوۡمَ هَٰهُنَا حَمِيمٞ
basi kafiri huyu Siku ya Kiyama hatakuwa na jamaa wa karibu wa kumuepushia adhabu,
Arapça tefsirler:
وَلَا طَعَامٌ إِلَّا مِنۡ غِسۡلِينٖ
wala hatakuwa na chakula isipokuwa kile kinachotokana na usaa wa watu wa motoni,
Arapça tefsirler:
لَّا يَأۡكُلُهُۥٓ إِلَّا ٱلۡخَٰطِـُٔونَ
hakuna mwenye kukila isipokuwa wale wenye dhambi, wanaoshikilia kumkanusha Mwenyezi mungu.
Arapça tefsirler:
فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَا تُبۡصِرُونَ
Naapa kwa mnavyoviona miongoni mwa vitu vinavyooonekana,
Arapça tefsirler:
وَمَا لَا تُبۡصِرُونَ
na vile msivyoviona miongoni mwa vile vilivyoghibu kwenu., hakika Qur’ani ni maneno ya Mwenyezi Mungu.
Arapça tefsirler:
إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ
Inasomwa na mjumbe mkubwa wa cheo na utukufu.
Arapça tefsirler:
وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَاعِرٖۚ قَلِيلٗا مَّا تُؤۡمِنُونَ
Na si maneno ya mshairi kama mnavyodai, ni uchache mno mnavyoamini.
Arapça tefsirler:
وَلَا بِقَوۡلِ كَاهِنٖۚ قَلِيلٗا مَّا تَذَكَّرُونَ
Wala si tungo kama zile tungo za makuhani, ni kuchache mno kule kukumbuka kwenu na kutia akilini kuwa kuna tafauti baina ya mawili hayo.
Arapça tefsirler:
تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Lakini hiyo Qur’ani ni maneno ya Mola wa viumbe wote Aliyoyateremshia Mtume Wake Muhaammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Arapça tefsirler:
وَلَوۡ تَقَوَّلَ عَلَيۡنَا بَعۡضَ ٱلۡأَقَاوِيلِ
Na lau Muhammad angalitusingizia maneno tusiyoyanena
Arapça tefsirler:
لَأَخَذۡنَا مِنۡهُ بِٱلۡيَمِينِ
tungalimtesa na tungalimkamata kwa nguvu na uweza, kwani nguvu ya kila kitu iko kwenye upande wake wa kulia,
Arapça tefsirler:
ثُمَّ لَقَطَعۡنَا مِنۡهُ ٱلۡوَتِينَ
kisha tungalimkata mshipa wa moyo wake.,
Arapça tefsirler:
فَمَا مِنكُم مِّنۡ أَحَدٍ عَنۡهُ حَٰجِزِينَ
hataweza yoyote kuyazuia mateso yetu yasimpate.
Arapça tefsirler:
وَإِنَّهُۥ لَتَذۡكِرَةٞ لِّلۡمُتَّقِينَ
Na hii Qur’ani ni mawaidha kwa wachamungu wanaofuata amri za Mwenyezi Mungu na kuyaepuka makatazo yake.
Arapça tefsirler:
وَإِنَّا لَنَعۡلَمُ أَنَّ مِنكُم مُّكَذِّبِينَ
Na sisi kwa hakika tunajua kwamba miongoni mwenu kuna wanaoikanusha hii Qur’ani pamoja na kuwa dalili zake ziko wazi.
Arapça tefsirler:
وَإِنَّهُۥ لَحَسۡرَةٌ عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ
Na kwa hakika kuikanusha Qur’ani ni majuto makubwa kwa wenye kuikanusha pindi watakapoiona adhabu yao na kuona starehe za wenye kuiamini.
Arapça tefsirler:
وَإِنَّهُۥ لَحَقُّ ٱلۡيَقِينِ
Na kwa hakika hii Qur’ani ni haki iliyothibiti na yakini isiyo na shaka.
Arapça tefsirler:
فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ
Basi Mwepushie Mwenyezi Mungu, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, kila sifa isiyonasibiana na haiba Yake, na umtaje kwa jina Lake tukufu.
Arapça tefsirler:
 
Anlam tercümesi Sure: Sûretu'l-Hakkâh
Surelerin fihristi Sayfa numarası
 
Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Mealler fihristi

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Kapat