Check out the new design

Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - Savahili Dili Tercüme - Rowad Tercüme Merkezi * - Mealler fihristi


Anlam tercümesi Sure: Sûratu'l-Bakarah   Ayet:

Al-Baqarah

الٓمٓ
Alif Lam Mim.[1]
[1] Ama herufi za mkato mwanzoni mwa sura mbalimbali. Lililo salama zaidi kuhusiana nazo ni kukaa kimya na kutoziingilia maana zake bila ya dalili ya Kisheria, pamoja na kuwa na yakini kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu hakuziteremsha bure, bali kwa hekima tusiyoijua. (Tafsir As-Sa'dii)
Arapça tefsirler:
ذَٰلِكَ ٱلۡكِتَٰبُ لَا رَيۡبَۛ فِيهِۛ هُدٗى لِّلۡمُتَّقِينَ
Hiki ni Kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake; ni uwongofu kwa wachamungu.[1]
[1] Na kwa sababu shaka ni kusitasita kati ya mambo, basi kitu chenye shaka hakiwezi kumuongoa mtu. Na kwa sababu sifa ya Qur-aani ni kwamba haina shaka yoyote, basi ikalazimu kwamba ni yenye kuongoa. Ndiyo maana Mwenyezi Mungu akasema: "Ni uwongofu kwa wachamungu" peke yao. Kwa sababu, wasiokuwa wachamungu na wakaidi hawakosi kuwa na shaka katika jambo hata kama halina shaka yoyote. (Tafsir Al-Baqa'ii)
Arapça tefsirler:
ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡغَيۡبِ وَيُقِيمُونَ ٱلصَّلَوٰةَ وَمِمَّا رَزَقۡنَٰهُمۡ يُنفِقُونَ
Ambao huyaamini ya ghaibu na hushika Sala, na hutoa katika[1] tuliyowapa (tuliyowaruzuku).
[1] Na alitumia neno “min (katika)” linalomaanisha baadhi (ya kitu), ili awatanabahishe kuwa yeye kwa hakika hakuta kutoka kwao isipokuwa sehemu ndogo kutoka kwa mali zao, ambayo haina madhara kwao wala uzito wowote, bali wao wanafaidika kwa kuitoa, na pia ndugu zao wanafaidika kwayo.
Arapça tefsirler:
وَٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِمَآ أُنزِلَ إِلَيۡكَ وَمَآ أُنزِلَ مِن قَبۡلِكَ وَبِٱلۡأٓخِرَةِ هُمۡ يُوقِنُونَ
Na ambao wanayaamini yaliyoteremshwa kwako, na yaliyoteremshwa kabla yako; na Akhera wana yakini nayo.
Arapça tefsirler:
أُوْلَٰٓئِكَ عَلَىٰ هُدٗى مِّن رَّبِّهِمۡۖ وَأُوْلَٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ
Hao wapo juu ya uwongofu utokao kwa Mola wao Mlezi, na hao ndio waliofaulu.[1]
[1] Kwa sababu Qur-ani ndio uwongofu wao, limetumika neno "juu" ili kuifananisha hali ya kuimarika kwa Waumini katika uwongofu na uthabiti wao juu yake; na kujaribu kwao kuuongeza na kutembea katika njia za heri. Na mwonekano wa (mtu) aliyepanda kipando (kama farasi) katika kuwa kwake juu ya kipando hicho, na uwezo wake wa kukiendesha na kukifanya kuwa kitiifu. (Tafsir At-Tahrir Wat-tanwiir cha Ibn 'Aashuur)
Arapça tefsirler:
 
Anlam tercümesi Sure: Sûratu'l-Bakarah
Surelerin fihristi Sayfa numarası
 
Kur'an-ı Kerim meal tercümesi - Savahili Dili Tercüme - Rowad Tercüme Merkezi - Mealler fihristi

Rowad Tercüme Merkezi Ekibi tarafından Rabvede'ki Tebliğ, İrşat ve Toplum Bilinçlendirme Derneği ve Dünya dillerinde İslami içerik ve hizmet cemiyeti işbirliğiyle tercüme edilmiştir.

Kapat