Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилча таржима, таржимонлар: Абдуллоҳ Муҳаммад ва Носир Хумайс * - Таржималар мундарижаси


Маънолар таржимаси Сура: Воқеъа сураси   Оят:

Surat Al-Waqi'ah

إِذَا وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ
Kitakaposimama Kiyama.
Арабча тафсирлар:
لَيۡسَ لِوَقۡعَتِهَا كَاذِبَةٌ
Hakutakuwa na yoyote mwenye kukanusha kusimama kwake.
Арабча тафсирлар:
خَافِضَةٞ رَّافِعَةٌ
Ni chenye kuwainamisha chini maadui wa Mwenyezi Mungu ndani ya Moto na ni chenye kuwainua juu Peponi wale wenye kumtegemea.
Арабча тафсирлар:
إِذَا رُجَّتِ ٱلۡأَرۡضُ رَجّٗا
Itakapotikiswa ardhi mtikiso wa nguvu.
Арабча тафсирлар:
وَبُسَّتِ ٱلۡجِبَالُ بَسّٗا
Na yakamumunyuliwa majabali mmumunyuo wa kina.
Арабча тафсирлар:
فَكَانَتۡ هَبَآءٗ مُّنۢبَثّٗا
Yakawa vumbi lenye kuruka angani lililosukumwa na upepo.
Арабча тафсирлар:
وَكُنتُمۡ أَزۡوَٰجٗا ثَلَٰثَةٗ
Na mkawa, enyi viumbe, makundi matatu:
Арабча тафсирлар:
فَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ
Kundi la watu wa upande wa kulia, wenye daraja kubwa. Ni kikubwa kilioje cheo chao!
Арабча тафсирлар:
وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ
Kuna na kundi la watu wa upande wa kushoto, wenye daraja duni. Ni mbaya iliyoje hali yao!
Арабча тафсирлар:
وَٱلسَّٰبِقُونَ ٱلسَّٰبِقُونَ
Na wale waliotangulia mbele kwenye kheri duniani ndio wenye kutangulia mbele kwenye daraja za juu huko Akhera.
Арабча тафсирлар:
أُوْلَٰٓئِكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ
Wao ndio walioletwa karibu kwa Mwenyezi Mungu,
Арабча тафсирлар:
فِي جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Mola wao Atawatia kwenye mabustani ya Pepo ya starehe.
Арабча тафсирлар:
ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ
Watayaingia watu wengi watu wa mwanzo wa ummah huu, na ummah wengineo wasiokuwa wao,
Арабча тафсирлар:
وَقَلِيلٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ
na wachache miongoni mwa watu mwisho wa ummah huu,
Арабча тафсирлар:
عَلَىٰ سُرُرٖ مَّوۡضُونَةٖ
wakiwa juu ya vitanda vilivyofumwa kwa dhahabu,
Арабча тафсирлар:
مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيۡهَا مُتَقَٰبِلِينَ
na wakiwa katika hali ya kuvitegemea na huku wanaelekeana na kukutana.
Арабча тафсирлар:
يَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ
Wanawazunguka wao kuwatumikia watumishi vijana wasiozeeka wala kufa,
Арабча тафсирлар:
بِأَكۡوَابٖ وَأَبَارِيقَ وَكَأۡسٖ مِّن مَّعِينٖ
wakiwa na vikombe, mabirika na gilasi kutoka kwenye chemchemi ya pombe yenye kupita ndani ya Pepo,
Арабча тафсирлар:
لَّا يُصَدَّعُونَ عَنۡهَا وَلَا يُنزِفُونَ
na hawaumwi na vichwa kutokana nayo wala hawarukwi na akili.
Арабча тафсирлар:
وَفَٰكِهَةٖ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ
Na watawazunguka wao watumishi vijana na kila kitu wanachokichagua miongoni mwa matunda,
Арабча тафсирлар:
وَلَحۡمِ طَيۡرٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ
nyama ya ndege ambayo nafsi zao inavutika nayo.
Арабча тафсирлар:
وَحُورٌ عِينٞ
Na watakuwa na wanawake wenye macho makubwa kama kwamba wao,
Арабча тафсирлар:
كَأَمۡثَٰلِ ٱللُّؤۡلُوِٕ ٱلۡمَكۡنُونِ
kwa usafi wao na uzuri wao, ni lulu iliyohifadhiwa ndani ya mashaza yake,
Арабча тафсирлар:
جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
hali hayo yakiwa ni malipo yao kwa yale waliokuwa wakiyafanya duniani.
Арабча тафсирлар:
لَا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا تَأۡثِيمًا
Hawatasikia humo Peponi ubatilifu wala yale ya kuwatia madhambini kuyasikia,
Арабча тафсирлар:
إِلَّا قِيلٗا سَلَٰمٗا سَلَٰمٗا
isipokuwa maneno yasiyokuwa na kasoro hizi na kusalimiana wao kwa wao.
Арабча тафсирлар:
وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ
Na watu wa upande wa kulia,
Арабча тафсирлар:
فِي سِدۡرٖ مَّخۡضُودٖ
ni kikubwa kilioje cheo chao na malipo yao!
Арабча тафсирлар:
وَطَلۡحٖ مَّنضُودٖ
Watakuwa kwenye mikunazi isiyo na miba, na ndizi zilizopandana na kupangika,
Арабча тафсирлар:
وَظِلّٖ مَّمۡدُودٖ
kila ndizi juu ya nyingine, na vivuli vya daima visivyoondoka,
Арабча тафсирлар:
وَمَآءٖ مَّسۡكُوبٖ
na maji yanayotembea yasiyokatika,
Арабча тафсирлар:
وَفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ
na matunda mengi
Арабча тафсирлар:
لَّا مَقۡطُوعَةٖ وَلَا مَمۡنُوعَةٖ
yasiyomalizika wala kuwaishia wala hakuna kizuizi chochote kinachowazuia wao kuyafikia,
Арабча тафсирлар:
وَفُرُشٖ مَّرۡفُوعَةٍ
na matandiko yaliyoinuliwa juu ya vitanda.
Арабча тафсирлар:
إِنَّآ أَنشَأۡنَٰهُنَّ إِنشَآءٗ
Sisi tumewaumba wanawake wa watu wa Peponi umbile ambalo silo lile umbile lililokuwa duniani, umbile lililokamilika lisilokubali kutoweka,
Арабча тафсирлар:
فَجَعَلۡنَٰهُنَّ أَبۡكَارًا
na tumewafanya ni wanawali wenye kujipendekeza kwa waume zao,
Арабча тафсирлар:
عُرُبًا أَتۡرَابٗا
hali ya kuwa ni marika na wao kimiaka.
Арабча тафсирлар:
لِّأَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ
Tumewaumbia wanawake hao watu wa upande wa kulia.
Арабча тафсирлар:
ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ
Nao ni kundi la watu wengi wa mwanzo
Арабча тафсирлар:
وَثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ
na kundi la watu wengi wa mwisho.
Арабча тафсирлар:
وَأَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ
Na watu wa upande wa kushoto, ni mbaya iliyoje hali yao na malipo yao!
Арабча тафсирлар:
فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ
Watakuwa kwenye upepo ulio moto utokanao na joto la Moto wa Jahanamu utakaozuia pumzi zao, na maji moto yanayochemka,
Арабча тафсирлар:
وَظِلّٖ مِّن يَحۡمُومٖ
na kivuli cha moshi mweusi sana,
Арабча тафсирлар:
لَّا بَارِدٖ وَلَا كَرِيمٍ
usio na mashukio baridi wala mandhari mazuri.
Арабча тафсирлар:
إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَبۡلَ ذَٰلِكَ مُتۡرَفِينَ
Kwani wao walikuwa duniani wakijistarehesha kwa vitu vya haramu wakijiepusha na yale ambayo Mitume walikuja nayo.
Арабча тафсирлар:
وَكَانُواْ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلۡحِنثِ ٱلۡعَظِيمِ
Na walikuwa wamesimama wima katika kumkanusha Mwenyezi Mungu na kumshirikisha na kumuasi, na hawakuwa na nia ya kutubia kwa hayo.
Арабча тафсирлар:
وَكَانُواْ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ
Na walikuwa wakisema hali ya kukanusha Ufufuzi, «Je hivi sisi tutafufuliwa tutakapokufa na tukawa mchanga na mifupa iliyochakaa?» Maneno yao hayo yanaonesha kuwa wao walikuwa wakiliona jambo hili la kufufuliwa kuwa liko mbali na ukweli na wakilikanusha.
Арабча тафсирлар:
أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ
«Je tutafufuliwa sisi na hali baba zetu waliotangulia wamekuwa mchanga uliotapakaa kwenye ardhi?»
Арабча тафсирлар:
قُلۡ إِنَّ ٱلۡأَوَّلِينَ وَٱلۡأٓخِرِينَ
Sema uwaambie, «Hakika wa mwanzo na wa mwisho miongoni mwa binadamu
Арабча тафсирлар:
لَمَجۡمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ
watakusanywa katika Siku iliyowekewa wakati maalumu, nayo ni Siku ya Kiyama.
Арабча тафсирлар:
ثُمَّ إِنَّكُمۡ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلۡمُكَذِّبُونَ
«Kisha nyinyi, enyi mliopotea njia ya uongofu mnaokanusha onyo la Mwenyezi Mungu na agizo Lake,
Арабча тафсирлар:
لَأٓكِلُونَ مِن شَجَرٖ مِّن زَقُّومٖ
ni wenye kula kutokana na mti wa zaqqūm,
Арабча тафсирлар:
فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ
nao ni katika miti mibaya zaidi, na ni wenye kujaza matumbo yenu kutokana nao kwa sababu ya ukali wa njaa,
Арабча тафсирлар:
فَشَٰرِبُونَ عَلَيۡهِ مِنَ ٱلۡحَمِيمِ
na ni wenye kunywa juu yake maji yaliyo moto hadi ya mwisho, yasiyomaliza kiu.
Арабча тафсирлар:
فَشَٰرِبُونَ شُرۡبَ ٱلۡهِيمِ
Mtayanywa maji hayo kwa wingi kama vile ngamia wenye kiu wasioshiba maji kwa ugonjwa uliowapata.»
Арабча тафсирлар:
هَٰذَا نُزُلُهُمۡ يَوۡمَ ٱلدِّينِ
Adhabu hii watakayoipata ndiyo zawadi Aliyowaandalia Siku ya Kiyama. Katika haya kuna kuwalaumu na kuwacheza shere.
Арабча тафсирлар:
نَحۡنُ خَلَقۡنَٰكُمۡ فَلَوۡلَا تُصَدِّقُونَ
Sisi tumewaumba, enyi watu, na hamkuwa kitu chochote. Basi si msadiki kuwa kuna kufufuliwa?
Арабча тафсирлар:
أَفَرَءَيۡتُم مَّا تُمۡنُونَ
Mnayaonaje maji ya manii mnayoyatupa ndani ya vizazi vya wake zenu,
Арабча тафсирлар:
ءَأَنتُمۡ تَخۡلُقُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡخَٰلِقُونَ
je nyinyi ndio mnaomuumba mwanadamu kutokana na hayo au ni sisi ndio wenye kuumba?
Арабча тафсирлар:
نَحۡنُ قَدَّرۡنَا بَيۡنَكُمُ ٱلۡمَوۡتَ وَمَا نَحۡنُ بِمَسۡبُوقِينَ
Sisi tumekadiria kifo kwenu,
Арабча тафсирлар:
عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ أَمۡثَٰلَكُمۡ وَنُنشِئَكُمۡ فِي مَا لَا تَعۡلَمُونَ
na sisi si wenye kushindwa kubadilisha umbo lenu Siku ya Kiyama na kuwaumba kwa sifa na namna msizozijua.
Арабча тафсирлар:
وَلَقَدۡ عَلِمۡتُمُ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُولَىٰ فَلَوۡلَا تَذَكَّرُونَ
Na hakika mlijua kuwa Mwenyezi Mungu Aliwaumba uumbaji wa kwanza na hamkuwa kitu chochote. Basi si mkumbuke uweza wa Mwenyezi Mungu wa kuwaumba mara nyingine?
Арабча тафсирлар:
أَفَرَءَيۡتُم مَّا تَحۡرُثُونَ
Mnazionaje mbegu mnazozipanda?
Арабча тафсирлар:
ءَأَنتُمۡ تَزۡرَعُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلزَّٰرِعُونَ
Je ni nyinyi mnaoziotesha kutoka ardhini? Sisi ndio tuaozituliza na kuziotesha ardhini.
Арабча тафсирлар:
لَوۡ نَشَآءُ لَجَعَلۡنَٰهُ حُطَٰمٗا فَظَلۡتُمۡ تَفَكَّهُونَ
Lau tungalitaka tungaliifanya mimea inayotokana na mbegu hizo kuwa mapepe, haimkiniki kunufaika nayo kwa kula,
Арабча тафсирлар:
إِنَّا لَمُغۡرَمُونَ
mkawa mnaona ajabu kwa kilichoshukia mimea yenu na mnasema, «Sisi tumepata hasara na ni wenye kuungulika.
Арабча тафсирлар:
بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ
Bali sisi tumekoseshwa riziki.»
Арабча тафсирлар:
أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلۡمَآءَ ٱلَّذِي تَشۡرَبُونَ
Mnayaonaje maji mnayokunywa ili mhuike kwayo?
Арабча тафсирлар:
ءَأَنتُمۡ أَنزَلۡتُمُوهُ مِنَ ٱلۡمُزۡنِ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنزِلُونَ
Je ni nyinyi mliyoyateremsha kutoka kwenye mawingu hadi kwenye kituo cha ardhi au ni sisi tuliyoyateremsha ili kuwarehemu nyinyi?
Арабча тафсирлар:
لَوۡ نَشَآءُ جَعَلۡنَٰهُ أُجَاجٗا فَلَوۡلَا تَشۡكُرُونَ
Lau tungalitaka tungaliyafanya maji haya yawe na chumvi sana, ikiwa haiwezekani kunufaika nayo kwa kunywa wala kwa mimea. Basi si mumshukuru Mola wenu kwa kuteremsha maji tamu kwa kuwanufaisha nyinyi.
Арабча тафсирлар:
أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلنَّارَ ٱلَّتِي تُورُونَ
Mnaouonaje moto mnaouwasha?
Арабча тафсирлар:
ءَأَنتُمۡ أَنشَأۡتُمۡ شَجَرَتَهَآ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنشِـُٔونَ
Je ni nyinyi mlioufanya mti wake, unaozalisha moto kwa kukwaruzwa, upatikane au ni sisi tulioufanya upatikane?
Арабча тафсирлар:
نَحۡنُ جَعَلۡنَٰهَا تَذۡكِرَةٗ وَمَتَٰعٗا لِّلۡمُقۡوِينَ
Sisi tumeufanya moto wenu mnaouwasha ni ukumbusho kwenu wa Moto wa Jahanamu na pia ni manufaa kwa wasafiri.
Арабча тафсирлар:
فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ
Basi mtakase Mola wako, ewe Nabii, Aliye mtukufu Mwenye ukamilifu wa majina na sifa, Mwingi wa wema na kheri.
Арабча тафсирлар:
۞ فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَوَٰقِعِ ٱلنُّجُومِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mapomoko ya nyota nyakati za kuzama kwake mbinguni.
Арабча тафсирлар:
وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٞ لَّوۡ تَعۡلَمُونَ عَظِيمٌ
Nacho ni kiapo kikubwa lau mnajua kadiri yake.
Арабча тафсирлар:
إِنَّهُۥ لَقُرۡءَانٞ كَرِيمٞ
Hakika hii Qur’ani iliyoteremshiwa Muhammad ni Qur’ani yenye manufaa makubwa, yenye kheri nyingi na yenye elimu tele,
Арабча тафсирлар:
فِي كِتَٰبٖ مَّكۡنُونٖ
iliyo ndani ya Kitabu kilichohifadhiwa, kilichofichwa na macho ya viumbe, nacho ni Kitabu ambacho kiko mikononi mwa Malaika.
Арабча тафсирлар:
لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُطَهَّرُونَ
Hawaigusi Qur’ani isipokuwa malaika watukufu ambao Mwenyezi Mungu Amewasafisha na aibu na madhambi. Na pia hawaigusi isipokuwa watu waliojitohirisha na ushirikina na janaba na ukosefu wa udhu.
Арабча тафсирлар:
تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na hii Qur’ani tukufu imeteremshwa kutoka kwa Mola wa viumbe vyote, kwani hiyo ndiyo haki isiyo na shaka ndani yake.
Арабча тафсирлар:
أَفَبِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ أَنتُم مُّدۡهِنُونَ
je hii Qur’ani, enyi washirikina, mnaikanusha?
Арабча тафсирлар:
وَتَجۡعَلُونَ رِزۡقَكُمۡ أَنَّكُمۡ تُكَذِّبُونَ
Na je mnaifanya shukrani yenu kwa neema za Mola wenu ni kuwa nyinyi mnazikanusha na kukufuru? Hapa pana makaripio kwa anayedharau amri za Qur’ani na kutojali mwito wake.
Арабча тафсирлар:
فَلَوۡلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلۡحُلۡقُومَ
Basi je mnaweza pindi roho ya mmoja wenu inapofika kwenye koo katika uchungu wa kifo,
Арабча тафсирлар:
وَأَنتُمۡ حِينَئِذٖ تَنظُرُونَ
na hali nyinyi mmehudhuria mnamtazama, kuizuia roho yake ndani ya mwili wake? Hamtaweza hilo!
Арабча тафсирлар:
وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنكُمۡ وَلَٰكِن لَّا تُبۡصِرُونَ
Na sisi tuko karibu na yeye zaidi, kupitia Malaika wetu, kuliko nyinyi, lakini nyinyi hamuwaoni.
Арабча тафсирлар:
فَلَوۡلَآ إِن كُنتُمۡ غَيۡرَ مَدِينِينَ
Na je mnaweza, iwapo nyinyi si wenye kuhesabiwa wala kulipwa kwa matendo yenu,
Арабча тафсирлар:
تَرۡجِعُونَهَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
kuirudisha roho kwenye mwili, iwapo nyinyi ni wakweli? Hamtaweza kuirudisha.
Арабча тафсирлар:
فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ
Basi iwapo yule anayekufa ni kati ya watu wa upande wa kulia, atapata rehema kunjufu na furaha,
Арабча тафсирлар:
فَرَوۡحٞ وَرَيۡحَانٞ وَجَنَّتُ نَعِيمٖ
wakati wa kufa kwake, na kila kinachoifurahisha nafsi yake, Na atapata Pepo ya starehe huko Akhera.
Арабча тафсирлар:
وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ
Na iwapo yule anayekufa ni kati ya watu wa upande wa kulia,
Арабча тафсирлар:
فَسَلَٰمٞ لَّكَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ
ataambiwa, «Umesalimika na kuwa kwenye amani, kwa kuwa wewe ni miongoni mwa watu wa upande wa kulia.»
Арабча тафсирлар:
وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُكَذِّبِينَ ٱلضَّآلِّينَ
Na iwapo yule anayekufa ni miongoni mwa wenye kukanusha kufufuliwa, waliopotoka na njia ya uongofu,
Арабча тафсирлар:
فَنُزُلٞ مِّنۡ حَمِيمٖ
basi atapata makaribisho ya kinywaji cha moto wa Jahanamu kilichochemshwa, kilicho na joto hadi ya mwisho,
Арабча тафсирлар:
وَتَصۡلِيَةُ جَحِيمٍ
na atachomwa na Moto na aungulike na adhabu yake kali.
Арабча тафсирлар:
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ ٱلۡيَقِينِ
Hakika habari hii tumezokuelezea, ewe Mtume, ni ukweli wa yakini usio na shaka.
Арабча тафсирлар:
فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ
Basi litakase jina la Mola wako Aliyetukuka na umtakase na yale ambayo madhalimu na wenye kukanusha wanayasema. Mwenyezi Mungu Yuko juu ya yale wanayoyasema ujuu mkubwa sana.
Арабча тафсирлар:
 
Маънолар таржимаси Сура: Воқеъа сураси
Суралар мундарижаси Бет рақами
 
Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилча таржима, таржимонлар: Абдуллоҳ Муҳаммад ва Носир Хумайс - Таржималар мундарижаси

Қуръон Карим маъноларининг савоҳилийча таржимаси, мутаржимлар: д. Абдуллоҳ Муҳаммад Абу Бакр, Шайх Носир Хумайс

Ёпиш