Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилча таржима, таржимонлар: Абдуллоҳ Муҳаммад ва Носир Хумайс * - Таржималар мундарижаси


Маънолар таржимаси Сура: Қиёмат сураси   Оят:

Surat Al-Qiyamah

لَآ أُقۡسِمُ بِيَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ
Anaapa Mwenyezi Mungu kwa Siku ya Hesabu na Malipo,
Арабча тафсирлар:
وَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلنَّفۡسِ ٱللَّوَّامَةِ
na Anaapa kwa nafsi yenye kuamini na kuchamungu, inayomlaumu mwenyewe kwa kuacha matendo ya utiifu na kufanya matendo yenye kuangamiza, kwamba watu watafufuliwa.
Арабча тафсирлар:
أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَلَّن نَّجۡمَعَ عِظَامَهُۥ
Je anadhanihuyu binadamu kafiri kuwa sisi hatutaweza kuikusanya mifupa yake baada ya kuwa mbalimbali.?
Арабча тафсирлар:
بَلَىٰ قَٰدِرِينَ عَلَىٰٓ أَن نُّسَوِّيَ بَنَانَهُۥ
Ndio! Tutaikusanya na tunaweza kufanya vidole vyake au ncha za vidole vyake- baada ya kuvikusanya na kuzioanisha- viwe kwenye umbo la sawasawa, kama vilivyokuwa kabla ya kufa.
Арабча тафсирлар:
بَلۡ يُرِيدُ ٱلۡإِنسَٰنُ لِيَفۡجُرَ أَمَامَهُۥ
Bali binadamu anakanusha kufufuliwa, anataka asalie kwenye kufanya ubaya kwa siku za mbeleni za maisha yake.
Арабча тафсирлар:
يَسۡـَٔلُ أَيَّانَ يَوۡمُ ٱلۡقِيَٰمَةِ
Kafiri huyu huwa akiuliza, akiliona jambo la kusimama Kiyama kuwa liko mbali, «Ni lini Siku ya Kiyama?’
Арабча тафсирлар:
فَإِذَا بَرِقَ ٱلۡبَصَرُ
Basi macho yatakapoduwaa na yakashituka kwa kutishika na kile yalichokiona cha vituko vya Siku ya Kiyama,
Арабча тафсирлар:
وَخَسَفَ ٱلۡقَمَرُ
na ukafutika mwangaza wa mwezi,
Арабча тафсирлар:
وَجُمِعَ ٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ
na vikakusanywa jua na mwezi katika kukosa mwangaza, kikawa kila mojawapo ya hivyo viwili hakina mwangaza,
Арабча тафсирлар:
يَقُولُ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذٍ أَيۡنَ ٱلۡمَفَرُّ
wakati huo binadamu atasema, «Pa kukimbilia ni wapi kuiepuka adhabu?»
Арабча тафсирлар:
كَلَّا لَا وَزَرَ
Mambo sivyo kama unavyotamani yawe, ewe binadamu, ya kutaka kukimbia. Huna mahali pa kukimbilia wala pa kupata uokozinfsi yake.
Арабча тафсирлар:
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمُسۡتَقَرُّ
Kwa Mwenyezi Mungu Peke Yake ndio mwisho wa viumbe Siku ya Kiyama na ndipo mahali pao pa kutulia, na hapo Amlipe kila mtu kwa kile alichostahiki.
Арабча тафсирлар:
يُنَبَّؤُاْ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذِۭ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ
Atapashwa habari binadamu Siku hiyo kwa matendo yake yote, mema na mabaya, aliyoyatanguliza miongoni mwa hayo katika maisha yake na aliyoyachelewesha.
Арабча тафсирлар:
بَلِ ٱلۡإِنسَٰنُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ بَصِيرَةٞ
Bali binadamu ni hoja iliyo wazi juu ya nafsi yake, yenye kumfuata kwa alichokitenda na alichokiacha,
Арабча тафсирлар:
وَلَوۡ أَلۡقَىٰ مَعَاذِيرَهُۥ
hata kama atakuja na kila udhuru wa kuelezea sababu ya uhalifu wake, hilo halitamfaa.
Арабча тафсирлар:
لَا تُحَرِّكۡ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعۡجَلَ بِهِۦٓ
Usitikise, ewe Nabii, ulimi wako kwa Qur’ani wakati wahyi unapoteremka ili ufanye haraka kuihifadhi kwa kuogopa isikuponyoke.
Арабча тафсирлар:
إِنَّ عَلَيۡنَا جَمۡعَهُۥ وَقُرۡءَانَهُۥ
Kwani ni juu yetu sisi kuikusanya kwenye kifua chako kisha uisome kwa ulimi wako wakati utakapo. Mjumbe wetu Jibrili akikusomea,
Арабча тафсирлар:
فَإِذَا قَرَأۡنَٰهُ فَٱتَّبِعۡ قُرۡءَانَهُۥ
basi kisikilize kisomo chake na umpulikize. Kisha isome kama alivyokusomea,
Арабча тафсирлар:
ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا بَيَانَهُۥ
kisha ni juu yetu kukuelezea kilichokutatiza kukifahamu katika maana yake na hukumu zake.
Арабча тафсирлар:
كَلَّا بَلۡ تُحِبُّونَ ٱلۡعَاجِلَةَ
Mambo sivyo kama mlivyodai, enyi mkusanyiko wa washirikina, kuwa hakuna kufufuliwa wala kulipwa.
Арабча тафсирлар:
وَتَذَرُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ
Bali nyinyi ni watu mnaopenda dunia na pambo lake na mnaacha Akhera na starehe zake.
Арабча тафсирлар:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاضِرَةٌ
Nyuso za watu wema Siku ya Kiyama zitakuwa ni zenye kung’ara, nzuri na zenye furaha,
Арабча тафсирлар:
إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٞ
zitamuona Mola Aliyeziumba na Anayezimiliki, na zitastarehe kwa hilo.
Арабча тафсирлар:
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذِۭ بَاسِرَةٞ
Nyuso za watu wabaya Silku ya Kiyama zitakuwa ni zenye kukunjana na kusinyaa,
Арабча тафсирлар:
تَظُنُّ أَن يُفۡعَلَ بِهَا فَاقِرَةٞ
zinatazamia kushukiwa na msiba mkubwa wenye kuvunja.
Арабча тафсирлар:
كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِيَ
Ni kweli! Pindi roho itakapofika sehemu za juu za kifua,
Арабча тафсирлар:
وَقِيلَ مَنۡۜ رَاقٖ
na wakasema baadhi ya waliohudhuria kuwaambia wengine, «Je kuna mtu wa kumzungua na kumpoza kutokana na hali hii aliyonayo?»
Арабча тафсирлар:
وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلۡفِرَاقُ
Na yule ambaye yuko katika hali ya kufa akajua kwamba lile lililomshukia ni kuaga dunia, kwa kuwa anawaona Malaika wa mauti.
Арабча тафсирлар:
وَٱلۡتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ
Na ikashikana shida ya mwisho wa duniani na shida ya mwanzo wa Akhera. Kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka.
Арабча тафсирлар:
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمَسَاقُ
Watu watapelekwa Siku ya Kiyama: ima Peponi au Motoni.
Арабча тафсирлар:
فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ
Hakuwa kafiri ni mwenye kumuamini Mtume na Qur’ani, wala hakuwa ni mwenye kumtekelezea Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Swala za faradhi.
Арабча тафсирлар:
وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
Lakini aliikanusha Qur’ani na akaipa mgongo Imani,
Арабча тафсирлар:
ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ
kisha akaenda kwa watu wake akijiona hali ya kujigamba katika kutembea kwake. Basi maangamivu
Арабча тафсирлар:
أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰ
ni yako baada ya maangamivu!
Арабча тафсирлар:
ثُمَّ أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰٓ
Kisha maangamivu ni yako baada ya maangamivu!
Арабча тафсирлар:
أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَن يُتۡرَكَ سُدًى
Je anadhani huyu binadamu anayekanusha kufufuliwa kuwa ataachwa bure: haamrishwi wala hakatazwi, hahesabiwi wala hateswi?
Арабча тафсирлар:
أَلَمۡ يَكُ نُطۡفَةٗ مِّن مَّنِيّٖ يُمۡنَىٰ
Kwani hakuwa binadamu huyu ni tone la manii dhaifu linalotokana na maji matwevu yanayomwagwa na kumiminwa kwenye kizazi,
Арабча тафсирлар:
ثُمَّ كَانَ عَلَقَةٗ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ
kisha yakawa ni kipande cha damu iliyo kavu. Mwenyezi Mungu Akaliumba kwa uweza Wake na Akazilinganisha sura zake katika umbo la mwili lililo zuri kabisa?
Арабча тафсирлар:
فَجَعَلَ مِنۡهُ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ
Akafanya kutokana na binadamu huyu jinsi mbili: ya kiume na ya kike. Je kwani hakuwa Mola huyo Muumba wa vitu hivyo ni Muweza wa kuwarudisha viumbe wakiwa hai baada ya kutoweka kwao.
Арабча тафсирлар:
أَلَيۡسَ ذَٰلِكَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحۡـِۧيَ ٱلۡمَوۡتَىٰ
Ndio! Anaweza. Yeye, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, kwa hakika ni Muweza wa hilo.
Арабча тафсирлар:
 
Маънолар таржимаси Сура: Қиёмат сураси
Суралар мундарижаси Бет рақами
 
Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилча таржима, таржимонлар: Абдуллоҳ Муҳаммад ва Носир Хумайс - Таржималар мундарижаси

Қуръон Карим маъноларининг савоҳилийча таржимаси, мутаржимлар: д. Абдуллоҳ Муҳаммад Абу Бакр, Шайх Носир Хумайс

Ёпиш