Check out the new design

Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - 斯瓦西里语翻译 - 阿卜杜拉·穆罕默德和纳索尔·胡麦斯 * - Mục lục các bản dịch


Ý nghĩa nội dung Chương: Ali 'Imran   Câu:

Al-'Imran

الٓمٓ
«Alif, Lām, Mīm» Yametangulia maelezo kuhusu matamko haya katika mwanzo wa sura ya Al-Baqarah.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ ٱلۡحَيُّ ٱلۡقَيُّومُ
Yeye Ndiye Mwenyezi Mungu. Hapana muabudiwa kwa haki isipokuwa Yeye, Anayesifika kwa uhai mkamilifu unaonasibiana na utukufu Wake.Anayesimamia kila kitu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
نَزَّلَ عَلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّ مُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِ وَأَنزَلَ ٱلتَّوۡرَىٰةَ وَٱلۡإِنجِيلَ
Amekuteremshia wewe, ewe Mtume, Qur’ani kwa haki ambayo haina shaka, inayoshuhudia ukweli wa Vitabu na Mitume kabla yake. Na Aliiteremsha Taurati kwa Musa, amani imshukie, na Injili kwa Īsā, amani imshukie,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
مِن قَبۡلُ هُدٗى لِّلنَّاسِ وَأَنزَلَ ٱلۡفُرۡقَانَۗ إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ لَهُمۡ عَذَابٞ شَدِيدٞۗ وَٱللَّهُ عَزِيزٞ ذُو ٱنتِقَامٍ
kabla ya kuteremka Qur’ani, ili kuwaongoza Wacha-Mungu kwenye Imani na kutengeneza dini yao na dunia yao. Na Aliteremsha yenye kupambanua baina ya haki na batili. Na wale ambao wamekanusha aya za Mwenyezi Mungu zilizoteremshwa, wana adhabu kubwa. Na Mwenyezi Mungu ni Mshindi Asiyeshindwa, ni Mwenye kumtesa anayezikanusha hoja na dalili Zake na kupwekeka Kwake kwa uungu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَخۡفَىٰ عَلَيۡهِ شَيۡءٞ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَا فِي ٱلسَّمَآءِ
Hakika Mwenyezi Mungu, ujuzi Wake umewazunguka viumbe wote. Hakuna kitu chenye kufichika Kwake katika ardhi wala katika mbingu, kiwe kichache au kingi.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
هُوَ ٱلَّذِي يُصَوِّرُكُمۡ فِي ٱلۡأَرۡحَامِ كَيۡفَ يَشَآءُۚ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ
Yeye Peke Yake Ndiye Ambaye Anawaumba nyiyi katika zao za mamama zenu kama Atakavyo: wanaume, wanawake, wazuri, wabaya, waovu na wema. Hapana mwenye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Yeye, Mshindi Asiyeshindwa, Mwenye hekima katika amri Zake na uendeshaji mambo Wake.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
هُوَ ٱلَّذِيٓ أَنزَلَ عَلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ مِنۡهُ ءَايَٰتٞ مُّحۡكَمَٰتٌ هُنَّ أُمُّ ٱلۡكِتَٰبِ وَأُخَرُ مُتَشَٰبِهَٰتٞۖ فَأَمَّا ٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِمۡ زَيۡغٞ فَيَتَّبِعُونَ مَا تَشَٰبَهَ مِنۡهُ ٱبۡتِغَآءَ ٱلۡفِتۡنَةِ وَٱبۡتِغَآءَ تَأۡوِيلِهِۦۖ وَمَا يَعۡلَمُ تَأۡوِيلَهُۥٓ إِلَّا ٱللَّهُۗ وَٱلرَّٰسِخُونَ فِي ٱلۡعِلۡمِ يَقُولُونَ ءَامَنَّا بِهِۦ كُلّٞ مِّنۡ عِندِ رَبِّنَاۗ وَمَا يَذَّكَّرُ إِلَّآ أُوْلُواْ ٱلۡأَلۡبَٰبِ
Yeye Peke Yake Ndiye Ambaye Aliyekuteremshia Qur’ani ambayo katika hiyo kuna aya zenye maana yaliyo wazi; hizo ndizo msingi wa Kitabu ambao unategemewa ikitokea tashwishi, na ambao chochote kinachohalifiana nao kinarudishwa na kuoanishwa nao. Na katika hiyo kuna aya zingine mutashabihat: zinazoleta tashwishi kwa kuwa zinabeba zaidi ya maana mamoja, kwa namna ambayo haiwezekani kujuwa maana iliyokusudiwa isipokuwa kwa kuziambatanisha na muhkam: aya zenye maana yaliyo wazi. Basi wenye nyoyo zenye ugonjwa zilizopotoka, kwa ubaya wa nia zao, huzifuata hizi aya zenye tashwishi peke yake, ili kutia tashwishi kwa watu kwa lengo la kuwapoteza kwa kuzifasiri kuambatana na madhehebu yao yaliyo batili. Ilihali hakuna ajuwaye uhakika wa maana ya aya hizi isipokuwa Mwenyezi Mungu. Na wale waliovama kwenye elimu wanasema, «Tumeiamini hii Qur’ani, kwani yote imetujia kutoka kwa Mola wetu kwa ulimi wa Mtume Wake Muhammad , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,.» na wanairudisha yenye tashwishi katika Qur’ani na kuiyoanisha na iliyo wazi yake. Hakika ni kwamba wanaoyafahamu na kuyazingatia maana kama ilivyo sahihi ipasavyo ni wale wenye akili timamu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
رَبَّنَا لَا تُزِغۡ قُلُوبَنَا بَعۡدَ إِذۡ هَدَيۡتَنَا وَهَبۡ لَنَا مِن لَّدُنكَ رَحۡمَةًۚ إِنَّكَ أَنتَ ٱلۡوَهَّابُ
Na wanasema, «Ewe Mola wetu, usizipotoe nyoyo zetu na kukuamini Wewe, baada ya kutuneemesha kwa uongofu wa kufuata Dini Yako; na utupe miongoni mwa fadhila zako, rehema yenye kuenea. Kwani Wewe Ndiye Mpaji: Mwingi wa fadhila na vipaji vipaji., unampa unayemtaka bila ya hesabu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
رَبَّنَآ إِنَّكَ جَامِعُ ٱلنَّاسِ لِيَوۡمٖ لَّا رَيۡبَ فِيهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُخۡلِفُ ٱلۡمِيعَادَ
Ewe Mola Wetu, sisi tunakubali na kushuhudia kwamba Wewe utawakusanya watu Siku isiyo na shaka , nayo ni Siku ya Kiyama. Hakika Wewe huendi kinyume na ahadi uliyowapa waja Wako.»
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Chương: Ali 'Imran
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - 斯瓦西里语翻译 - 阿卜杜拉·穆罕默德和纳索尔·胡麦斯 - Mục lục các bản dịch

阿卜杜拉·穆罕默德·艾布·比克尔和谢赫纳索尔·胡麦斯翻译

Đóng lại