Check out the new design

Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - 斯瓦西里语翻译 - 阿卜杜拉·穆罕默德和纳索尔·胡麦斯 * - Mục lục các bản dịch


Ý nghĩa nội dung Chương: Yasin   Câu:
إِنَّ أَصۡحَٰبَ ٱلۡجَنَّةِ ٱلۡيَوۡمَ فِي شُغُلٖ فَٰكِهُونَ
Hakika watu wa Peponi Siku hiyo watakuwa wameshughulishwa kwa aina mbalimbali za neema za wao kustarehe nazo, hawawafikirii watu wengine.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
هُمۡ وَأَزۡوَٰجُهُمۡ فِي ظِلَٰلٍ عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِ مُتَّكِـُٔونَ
Wao na wake zao watakuwa wanajistarehesha juu ya vitanda vilivyopambwa , na chini ya vivuli vilivyoenea.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
لَهُمۡ فِيهَا فَٰكِهَةٞ وَلَهُم مَّا يَدَّعُونَ
Wao Peponi watakuwa na starehe ya matunda yenye ladha ya kila aina, na watakuwa na kila wanalolitaka.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
سَلَٰمٞ قَوۡلٗا مِّن رَّبّٖ رَّحِيمٖ
Watakuwa na starehe nyingine kubwa kabisa nayo ni Atakaposema nao Mola wao, Mwenye kuwarehemu kwa kuwasalimia, na hapo watapata amani iliyotimia kwa kila namna.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَٱمۡتَٰزُواْ ٱلۡيَوۡمَ أَيُّهَا ٱلۡمُجۡرِمُونَ
Na wataambiwa makafiri Siku hiyo, «Jitengeni na Waumini na mjiepushe nao.»
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
۞ أَلَمۡ أَعۡهَدۡ إِلَيۡكُمۡ يَٰبَنِيٓ ءَادَمَ أَن لَّا تَعۡبُدُواْ ٱلشَّيۡطَٰنَۖ إِنَّهُۥ لَكُمۡ عَدُوّٞ مُّبِينٞ
Na Mwenyezi Mungu Atawaambia kwa kuwalaumu na kuwakumbusha, «Kwani sikuwausia, kupitia ndimi za Mitume wetu kwamba msiabudu Shetani wala msimtii? Hakika yeye ni adui ambaye uadui wake umejitokeza wazi.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَأَنِ ٱعۡبُدُونِيۚ هَٰذَا صِرَٰطٞ مُّسۡتَقِيمٞ
«Na nikawaamrisha mniabudu mimi peke yangu, kwani kuniabudu mimi na kunitii na kumuasi Shetani ndiyo Dini iliyonyoka yenye kupelekea kupata radhi zangu na mabustani ya Pepo yangu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَلَقَدۡ أَضَلَّ مِنكُمۡ جِبِلّٗا كَثِيرًاۖ أَفَلَمۡ تَكُونُواْ تَعۡقِلُونَ
«Hakika Shetani amewapoteza na kuwatoa kwenye haki viumbe wengi kabla yenu. Basi kwani hamkuwa na akili, enyi washirikina, ya kuwakataza nyinyi kumfuata?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
هَٰذِهِۦ جَهَنَّمُ ٱلَّتِي كُنتُمۡ تُوعَدُونَ
«Huu ni moto wa Jahanamu ambao mlikuwa mkiahidiwa duniani kwa kumkufuru kwenu Mwenyezi Mungu na kukanusha kwenu Mitume Wake.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ٱصۡلَوۡهَا ٱلۡيَوۡمَ بِمَا كُنتُمۡ تَكۡفُرُونَ
«Basi uingieni leo na mteseke kwa joto lake, kwa sababu ya ukafiri wenu!
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ٱلۡيَوۡمَ نَخۡتِمُ عَلَىٰٓ أَفۡوَٰهِهِمۡ وَتُكَلِّمُنَآ أَيۡدِيهِمۡ وَتَشۡهَدُ أَرۡجُلُهُم بِمَا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ
Siku hiyo tutaipiga muhuri midomo ya washirikina hawatakuwa ni wenye kusema, na itasema na sisi mikono yao kwa yale iliyoyafanya ya maonevu, na itatoa ushahidi miguu yao kwa yale iliyoyaendea duniani na dhambi ilizozichuma.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَلَوۡ نَشَآءُ لَطَمَسۡنَا عَلَىٰٓ أَعۡيُنِهِمۡ فَٱسۡتَبَقُواْ ٱلصِّرَٰطَ فَأَنَّىٰ يُبۡصِرُونَ
Na lau tutataka tutayafuta macho yao na kuondoa maangalizi yao, kama tulivyoifunga midomo yao, hapo waikimbilie njia ya Ṣirāṭ ili waivuke. Basi vipi hilo litakuwa kwao na hali macho yao yamefutwa hayaoni?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَلَوۡ نَشَآءُ لَمَسَخۡنَٰهُمۡ عَلَىٰ مَكَانَتِهِمۡ فَمَا ٱسۡتَطَٰعُواْ مُضِيّٗا وَلَا يَرۡجِعُونَ
Na lau tunataka tutaligeuza umbo lao na kuwakalisha mahali pao, wasiweze kuenda mbele wala kurudi nyuma.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَمَن نُّعَمِّرۡهُ نُنَكِّسۡهُ فِي ٱلۡخَلۡقِۚ أَفَلَا يَعۡقِلُونَ
Na yoyote tutakayeurefusha umri wake mpaka awe mkongwe tunamrudisha kwenye hali ya udhaifu wa akili na udhaifu wa mwili. Basi hawatii akilini kwamba yule Aliyefanya hili ni mwenye uweza wa kuwafufua?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَمَا عَلَّمۡنَٰهُ ٱلشِّعۡرَ وَمَا يَنۢبَغِي لَهُۥٓۚ إِنۡ هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ وَقُرۡءَانٞ مُّبِينٞ
Na hatukumfundisha mjumbe wetu Muhammad mashairi, na haipasi kwake kuwa mshairi. Haikuwa hii aliokuja nayo isipokuwa ni Ukumbusho kwa wale wenye busara kujikumbusha nao na ni Qur’ani yenye kufafanua haki na batili, hukumu zake ziko wazi, na pia hekima zake na mawaidha yake,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
لِّيُنذِرَ مَن كَانَ حَيّٗا وَيَحِقَّ ٱلۡقَوۡلُ عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ
ili imuonye ambaye moyo wake uko hai na akili yake ina nuru, na ili ithibiti adhabu kwa wenye kumkanusha Mwenyezi Mungu, kwa kuwa wao, kwa hii Qur’ani, hoja ya Mwenyezi Mungu ya mkato imewasimamia.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Chương: Yasin
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - 斯瓦西里语翻译 - 阿卜杜拉·穆罕默德和纳索尔·胡麦斯 - Mục lục các bản dịch

阿卜杜拉·穆罕默德·艾布·比克尔和谢赫纳索尔·胡麦斯翻译

Đóng lại