Check out the new design

Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - 斯瓦西里语翻译 - 阿卜杜拉·穆罕默德和纳索尔·胡麦斯 * - Mục lục các bản dịch


Ý nghĩa nội dung Chương: Sad   Câu:
ٱصۡبِرۡ عَلَىٰ مَا يَقُولُونَ وَٱذۡكُرۡ عَبۡدَنَا دَاوُۥدَ ذَا ٱلۡأَيۡدِۖ إِنَّهُۥٓ أَوَّابٌ
Vumilia, ewe Mtume, kwa unayoyachukia katika hayo wanayoyasema, na umtaje mja wetu Dāwūd, mwenye nguvu juu ya maadui wa Mwenyezi Mungu na uvumilivu juu ya kumtii Yeye. Hakika yeye ni mwingi wa kutubia, ni mwingi wa kurejea kufanya yale yanayomridhisha Mwenyezi Mungu. Katika haya pana kumliwaza Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنَّا سَخَّرۡنَا ٱلۡجِبَالَ مَعَهُۥ يُسَبِّحۡنَ بِٱلۡعَشِيِّ وَٱلۡإِشۡرَاقِ
Hakika sisi tuliyadhalilisha majabali pamoja na Dāwūd, yakawa yanamtakasa Mwenyezi Mungu kwa kumsabihi wakati anapomtakasa kwa kumsabihi mwanzo wa mchana na mwisho wake.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَٱلطَّيۡرَ مَحۡشُورَةٗۖ كُلّٞ لَّهُۥٓ أَوَّابٞ
Na tukawadhalilisha ndege pamoja naye, kwa mkusanyiko wao, wakawa wanatakasa kwa kusabihi na kuwa watiifu kwake
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَشَدَدۡنَا مُلۡكَهُۥ وَءَاتَيۡنَٰهُ ٱلۡحِكۡمَةَ وَفَصۡلَ ٱلۡخِطَابِ
Tukamtilia nguvu ufalme wake kwa haiba, uwezo na ushindi, na tukampa unabii na upambanuzi wa maneno na utoaji hukumu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
۞ وَهَلۡ أَتَىٰكَ نَبَؤُاْ ٱلۡخَصۡمِ إِذۡ تَسَوَّرُواْ ٱلۡمِحۡرَابَ
Na je, ilikujia, ewe Mtume, habari ya watesi wawili walioparaga ukuta wakamuingilia Dāwūd mahali pake pa kuabudu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِذۡ دَخَلُواْ عَلَىٰ دَاوُۥدَ فَفَزِعَ مِنۡهُمۡۖ قَالُواْ لَا تَخَفۡۖ خَصۡمَانِ بَغَىٰ بَعۡضُنَا عَلَىٰ بَعۡضٖ فَٱحۡكُم بَيۡنَنَا بِٱلۡحَقِّ وَلَا تُشۡطِطۡ وَٱهۡدِنَآ إِلَىٰ سَوَآءِ ٱلصِّرَٰطِ
Na Dāwūd akashutuka kwa wao kumuingilia? Walimwambia, «Usiogope! Sisi ni watesi, mmoja wetu amemdhulumu mwenzake. Basi hukumu baina yetu kwa uadilifu, wala usitoe hukumu ya maonevu juu yetu, na utuongoze kwenye njia ya sawa.»
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنَّ هَٰذَآ أَخِي لَهُۥ تِسۡعٞ وَتِسۡعُونَ نَعۡجَةٗ وَلِيَ نَعۡجَةٞ وَٰحِدَةٞ فَقَالَ أَكۡفِلۡنِيهَا وَعَزَّنِي فِي ٱلۡخِطَابِ
Mmoja wa wale wawili alisema, «Huyu ni ndugu yangu; ana kondoo tisini na tisa na mimi sina isipokuwa kondoo mmoja, akafanya tamaa kumtaka na akasema, ‘Nipe mimi!’ Na akanishinda kwa hoja.»
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
قَالَ لَقَدۡ ظَلَمَكَ بِسُؤَالِ نَعۡجَتِكَ إِلَىٰ نِعَاجِهِۦۖ وَإِنَّ كَثِيرٗا مِّنَ ٱلۡخُلَطَآءِ لَيَبۡغِي بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٍ إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ وَقَلِيلٞ مَّا هُمۡۗ وَظَنَّ دَاوُۥدُ أَنَّمَا فَتَنَّٰهُ فَٱسۡتَغۡفَرَ رَبَّهُۥ وَخَرَّۤ رَاكِعٗاۤ وَأَنَابَ۩
Dāwūd akasema, «Kwa hakika ndugu yako amekudhulumu kwa kutaka kwake kumchukua kondoo wako awe pamoja na kondoo wake. Na kwa hakika, wengi wa washirika, baadhi yao wanadhulumu wengine: wanawadhulumu kwa kuchukua haki zao na kukosa kuwa waadilifu wa nafsi zao. Isipokuwa watu wema walioamini, kwani wao hawadhulumiani, nao ni wachache.» Na Dāwūd akajua kwa yakini kuwa sisi tumemtahini kwa utesi huu, hivyo basi akamuomba msamaha Mola wake, akasujudu kwa kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu na akarejea Kwake na akatubia.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَغَفَرۡنَا لَهُۥ ذَٰلِكَۖ وَإِنَّ لَهُۥ عِندَنَا لَزُلۡفَىٰ وَحُسۡنَ مَـَٔابٖ
Tukamsamehe hilo na tukamfanya ni miongoni mwa watu waliosogezwa karibu na sisi, na tumemuandalia mwisho mwema huko Akhera.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
يَٰدَاوُۥدُ إِنَّا جَعَلۡنَٰكَ خَلِيفَةٗ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَٱحۡكُم بَيۡنَ ٱلنَّاسِ بِٱلۡحَقِّ وَلَا تَتَّبِعِ ٱلۡهَوَىٰ فَيُضِلَّكَ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِۚ إِنَّ ٱلَّذِينَ يَضِلُّونَ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ لَهُمۡ عَذَابٞ شَدِيدُۢ بِمَا نَسُواْ يَوۡمَ ٱلۡحِسَابِ
Ewe Dāwūd! Sisi tumekufanya ni msimamizi ardhini na tumekupa mamlaka huko, basi hukumu baina ya watu kwa uadilifu na uchungaji haki, na usifuate matamanio katika kuhukumu, kwani hilo litakupotosha na Dini ya Mwenyezi Mungu na Sheria Yake, hakika wale wanaopotea njia ya Mwenyezi Mungu watapata adhabu ya uchungu humo Motoni, kwa kughafilika kwao na Siku ya kulipwa na kuhesabiwa. Katika haya pana ushauri kwa viongozi wahukumu kwa haki iliyoteremshwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, wala wasipotoke nayo wakapotea njia Yake.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Chương: Sad
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - 斯瓦西里语翻译 - 阿卜杜拉·穆罕默德和纳索尔·胡麦斯 - Mục lục các bản dịch

阿卜杜拉·穆罕默德·艾布·比克尔和谢赫纳索尔·胡麦斯翻译

Đóng lại